SORRY MADAM (48)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA AROBAINI NA NANE
ILIPOISHIA...
“Sheila…..Sheila?”
Akaonekana kustustuka na akanikazima macho hadi akaanza kuniogopesha akajaribu kuzungumza ila akawa kama anashindwa.Aafuta vidoli vyake chini na kuandika maandishi yaliyo nistua zaidi
{MIMI SIWEZI KUZUNGUMZA NIPO SAWA SAWA NA BUBU}
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Maumivu makali yakapenya kwenye moyo wangu na kujikuta sura nzima ikitawaliwa machozi.Nikachukua kijiti chake na kumuandikia chini
{KWANINI HUWEZI KUONGEA?}
Sheila akanitazama kwa macho ya mshangao kwa jinsi ninavyo lia kisha akaniandikia chini
{SIWEZI TUU KWANI NILILISHWA MAKAA YA MAWE KWENYE MDOMO WANGU}
Sheila akaufungua mdomo wake na kuutoa ulimi wake nje na nikajikuta nikitetemekwa kwa woga kwani ulimi wake una majeraha makubwa yanayo onyesha vika ni kweli alilishwa makaa ya moto.Sheila akasimama gafla na ni mimi nikasimama na akaanza kutembea na kujikuta nikizidi kuumia kwani hata shepu lake la nyuma lilidhohofika sana.Tukaongozana hadi kwenye moja ukumbi ambao kuna kiwanja cha mpira wa kikapu(basketball) na akazidi kunipeleka hadi kwenye moja ya mabafu na akanitazama na kulivua gauni lake
Nikajikuta hata uwezo wa kuhema ukianza kuwa mdogo kutokana na mstuko nilio upata baada ya kuuna mwili wa Sheila ulivyo jaa majeraha makubwa ya kachanwa chwana na kutu chenye ncha kali.Akanigeukia mgongoni na kunionyesha kuvu kubwa la kutobolewa huku ngozi ya sehemu hiyo ikiwa imekunjamana na kujikuta nikizidi kuteswa na uchungu,Macho ya Sheila yakaanza kuvunjwa na machozi na akatazama tazama ndani ya bafu hili na sikujua anatafuta nini.Akafungua koki ya bomba la maji kisha akachovya kidole chake kimoja ndani ya maji na kuandika kwenye kiio kikubwa kilichopo ukutani
{MIMI SIO KICHAA ILA WATU WANANIISI KUWA MIMI NI KICHAA ILA UKWELI NI KWAMBA NINAAKILI ZANGU VIZURI NA HAYA YOTE YAMETOKANA NA MAUMIVU MAKALI NILIYO PEWA NA MZEE MMOJA AMBAYE NI MKUU WA JESHI NA NIBABA WA MPENZI WANGU EDDY}
Sheila akanigeukia na kuniuliza kwa ishara kama nimeelewa alicho kiandika na mimi nikatingisha kichwa nikimuashiria kuwa nimeelewa
“Unanikumbuka?”
Nilimuuliza Sheila na akabaki akinitazama kwa muda kisha akachovya kidole chake kwenye maji na kuandika kwenye kioo
{HAPANA ILA NINAKUFANANISHA NA EDDY WANGU ILA SIO WEWE KWANI YEYE ANAAKILI ZAKE TIMAMU NA SIO CHIZI KAMA ULIVYO WEWE}
Nikatulia kwa muda huku nikiyatafakari maneno ya Sheila aliyo toka kuniandikia muda mchache ulio pita.Nikamsogelea Sheila na kumkumbatia huku nikiwa ninamwagikwa na machozi.Mlango ukafunguliwa na wakaingia madaktari wawili wa kiume na walivyo tuona tumekumatiana wakanitoa mimi kwa nguvu na kuchomoa virungu vyao na kuanza kunipiga huku wakiniburuza na kunitoa nje
“Sheila….nisaidie ninakufa mimi”
Nilizungumza kwa sauti ya juu huku nikiwa ninalia kwa uchungu na kuzidi kuwaongezea hasira madaktari hawa na kuzidi kunipiga,Sheila kwa haraka akatoka huku akiwa na nguo ya ndani na akamsukuma dokta mmoja ana akajibamiza kichwa ukutani na akaanguka chini kisha akamshika kichwa cha gaktari na kunaza kukibamiza kwenye sakafu kwa nguvu hadi kipasukwa kwenye kisogo chake,Daktari aliye kuwa anaendelea kunipiga baada ya kumuona mwenzake akiwa anaaga dunia akaniacha na kwa nguvu zake zote akarusha kirungu chake na kikatua kichwani mwa Sheila na akadondoka chini na damu za puani zikaanza kumwagika
Taratiu nikaanza kujiburuza chini hadi sehemu aliyo angukia Sheila huku machozi yakinimwagika na kujikuta nikijilaza juu yake na kumfanya daktari aliye mpiga akanza kunipiga tena kwenye mgongo akinimrisha nimuechie Sheila ili aendelea kumshuhulikia kwa kipigo.Kila nilipo jaribu kumtingisha Sheila sikuweza kuona dalili yoyote ya kuishi kwake na kujikuta nikizidi kumkumbatia kwa uchungu.Nikaanza kusikia makelele yakija kwa nyuma yangu,nikageuza shingo yangu na kuona kundi kubwa la vichaa wakija kwa kasi na kumfanya daktari anaye nipiga kutimka mbio na sikujua ni wapi anapo elekea na wote wakanipita na kuendeleka kumkimbiza dakrari aliye kuwa akinipiga
Nikaona nikiendelea kujiliza haita saidi zaidi ya kumfanya Sheila kuzidi kuzidiwa na kipigo alicho kipata.Nikajikaza na kwabahati nzuri miguu yangu ina nguvu za kutosha nikanyanyuka na kujinyoosha japo nilijawa na maumivu makali ila sikuwa na jinsi.Nikanyanyua Sheila na kutokana na kudhohofika kwake kwa mwili haikuwa ngumu kwangu kumbeba hadi tukafika kwenye kwenye moja ya ofifisi na kuwakuta vichaa wakiwashambulia manesi waliomo ndani ya ofisi.Hali ya hospitali imechafuka kupita maelezo madaktari wanashambuliwa na vichaa ambao wamepandwa na hasira.Kwa bahati nzuri nikaona gari moja ya waogonjwa amayo imesimama nje kwenye maegesho huku dereva wake akichomolewa kwenye gari na kuanza kupewa kipigo kama ilivyo kwa wahudumu wengine wa hospitali ikiwemo walinzi
Hapa ndipo nikagundua kuwa vichaa tunafahamiana kwa maana kwa kila nilipo pita huku nikiwa nimembeba Sheila hapakuwa na anaye nigusa tofauti na wanapo muona muudumu wa hospitali hii.Nikafanikiwa kufika kwenye gari la wagonjwa nakumuingiza ndani ya gari Sheila na kwenda upande wa dereva na kuanza kutafuta fungua na sikuweza kuiona ikanibidi nishuke na kuunza kuupapasa mwili wa dereva ulio lala pembezoni mwa gari na kwabahati nzuri nikaiona funguo kwenye mfuko wake wa suruali.Nikawasha gari na kuondoka hukiwasaidia vichaa kutoka ndani ya hospitali hii baada ya kuligonga geti lililokuwa kimefungwa.Kutokana sikuwa ni mwenyeji sikujua ni wapi nielekee ili kumuwahisha Sheila hospitali.Nikasimamisha gari pembezoni mwa arabara huku likiwa linawaka ving’ora na kuichukua simu iliyopo ndani ya hospitali na kuanza kubuni namba ya baba
Kwa mara ya kwanza ikapokelewa na mwanamke ambaye hata lugha hatulewaa na nikajua nitakuwa nimekosea,nikajaribu kufikiria namba nyingi ambazo zinaweza kufanana na namba ya baba na pia namba niliyo ipiga ikapokelewa na kijana na akaanza kumwaga matusi alipoona sizungumzi kitu chochote baada ya kusema haloo.Nikajaribu zaidi ya mara saba nipo kumbukumbu ya namba za baba ziliponijia vizuri kichwani na nikaipiga ikaita kwa muda kisha ikapokelewa
“Nani mwenzangu?”
Ilikuwa ni sauti ya baba na kidogo tabasamu likanijia usoni
“Mimi Eddy”
“Eddy……!!”
“Ndio ni mimi baba ninaomba msaada wako”
Upo wapi mbona makelele ya king’ora?”
“Nipo kwenye gari ya wagonjwa nimetoroka hospitalini ila mimi sio kichaa kama ulivyo dhania”
“Ngoja kwanza umesema upo wapi?”
“Mimi hapa wala sipajui ila kuna magorofa mafupi mafupi hii na kuna magari mengi yamesimama pembeni”
“Umesema upo kwenye gari ya wagonjwa?”
“Ndio”
“Wewe ndio dereva ua kuna dereva?”
“Mimi ndio dereva”
“Sasa angalia kwenye upande wa kusoto kuna kijitivii kidogo….”
“Ndio nimekiona”
“Kiwashe kama hakija washwa na kwenye sehemu ya chini yake kuna batani nane umeziona”
“Ndio”
“Minya batani iliyo andikwa Map”
Nikaiiminya batani ambayo baba aliniambia na ndani ya sekunde kadhaa kukatokea ramani yenye mistari mingi mingi huku kukiwa na kialama chekundu kikiwa kina waka waka
“Inakisoma vipi hiyo ramani?”
“Inasoema Cape Town, Western Cape City”
“Subiri tunakuja sasa hivi”
Nikakata simu na kuzima gari na kufungua kijidirisha kilichopo nyuma ya siti yanga na kumuona Sheila akiwa amejilaza huku akipumua kwa shida kidogo nikapata matumaini.Ndani ya nusu saa gari mbili zikasimama mbele ya gari nililipo na mtu wa kwanza kushuka ni baba na moja kwa moja akafika kwenye gani na akaonekana kunishangaa jinsi damu zinavyo nivuja.Watu wake wakanitoa ndani ya gari
“Baba kuna mtu mwengine huku nyuma”
“Ni nani?”
“Rafiki yangu”
Nikahakikisha wamemshusha Sheila na kumuingiza ndani ya gari ndio na mimi nikaingia.Ndani ya gari nikajikausha kimya hadi tukafika kwenye moja ya hospitali.Madaktari wakanichukua na kuniingiza kwenye chumba kingine na Sheila akaingizwa kwenye chumba kingine kwa ajili ya matibabu.Matibabu yangu hayakuchukua muda sana japo nimeumia ila kidogo ninaafadhali ni tofauti na Sheila.
“Eddy ni kitu gani kilikupata?”
“Wapi?”
“Hadi ukawa kama umechanganyikiwa?”
“Baba kusema ukweli sijachanganyikiwa ila kuna kitu nilikuwa ninakiitaji kukifanya ili niweze kumpata mtu ambaye anaweza kumjua mama ni wapi alipo?”
“Una taka kuniambia kipindi chote hicho ulikuwa ukiigiza?”
“Ndio ila lengo langu limefanikiwa?”
“Kwanza mama anaendeleaje?”
“Mama yako hadi sasa hivi bado hajapatikana japo wale watu ambao niliwapa hiyo kazi wanasema kazi yao inaendelea vizuri”
“Sasa baba hivyo wanavyo sema kuwa inaendelea vizuri si uongo huo,mimi ninavyo jua kuwa kazi ikiendelea vizuri ni kwamba kuna majibu ya uhakika na wanacho kifanya…….Baba ninatambua fika kuwa wewe unamchukia sana mama kwa sababu ya aliyo kufanyia..ila kwangu mimi ni tofauti kabisa na wewe ninampenda mama yangu na yeye ndio kila kitu kwangu”
Nilizungumza kwa sauti ya ukali kidogo iliyo jaa uchungu kiasi kwamba baba akabaki akitazama chini pasipo kunijibu
“Baba….lengo langu kubwa ni wewe na mama mupatane,musameheane muwe kitu kimoja kumbuka kuwa mimi ndio mtoto wenu wa pekee.Mama hana mtoto mwengine…..wewe huna mtoto mwengine au unafurahia maisha ya manyanyaso na yule mwanake mwengine……baba simama kama baba uiokoe familia yako achana na nini kilitokea kati yako wewe na mama.Mimi peke yangu baba nitashindwa bado mimi ni mdogo nahitaji maelekezo kutoka kwenu kwanini baba inakuwa hivyo”
Nilizungumza kwa uchungu huku machozi yakinimwagika baba akainyanyua sura yake na nikashuhudia kwa mbali machozi yakimlenga lenga
“Eddy samahani mwanangu sikuweza kulifwatilia hilo swala la mama yako bado ninamchukia sana kupita kitu kingine chochote dunia…niangalie mimi leo hii nimekuwa ni kilema wa kila kitu maishani mwangu.Na kama sio pesa mimi leo hii nisinge weza kutembea…..”
“Baba baba kumbuka mama alikubebea damu yako miezi tisa…..”
“Alinitenga mbali na damu yangu.Alinifanya nisiione damu yangu na aliniulia damu yangu ni nini ambacho Eddy mwangu utaniambia nikakuelewa juu ya mama yako”
“Haya kama baba au wewe unafurahia kuishi maisha ya kuonewa yule mwanamke asiye na heshima anakazi ya kutembea na waanya kazi wako….?”
“Mama yako ndio chanzo wa hayo yote mwangu………Mimi sina nguvu za kumfurahisha mwanamke na sindano niliyo chomwa ndio imenipelekea kuwa hivi”
Nikabaki mdomo wazi huku nikimuangalia baba kwa macho ya mshangao hulu machozi yakinitiririka.
“Eddy anacho kifanya yule mwanamke ni haki yake…..tangu mimi nimchukue sijawahi kufanya naye chochote….Ndio maana mara ya kwanza nikakuambia kuwa mama yako ni katili sana na mimi ninajua kila kitua anacho kifanya mke wangu”
“Oohh baba kwanini eeehee umemchukua wa nini sasa yule mwanamke?”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni