SEHEMU YA MIA MOJA NA NNE
ILIPOISHIA...
Shamsa akanyanyuka, kitandani mwangu, akapiga hatua hadi mlangoni akafungua na kutoka. Nikabaki nikiwa nà msongo wa mawazo, nikiiwazia familia yangu. Kijiusingizi kikaanza kunipitia taratibu, kila nilipo jaribu kuitazama saa ya ukutani, masaa yalizidi kuyoyoma pasipo Madà m Mery kutokea.Mida ya saa sifa usiku, nikasikia mlango ukigongwa taratibu.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Nikanyanyuka, nikiwa nimeishika bastola yangu, iliyopo chini ya mto. Nikasimama pembeni ya mlango.
"Nani?"
Niliuliza kwa sauti ya chini, ambayo mtu aliyopo nje ya chumba ataisikia vizuri.
"Mery"
Ilikua nisauti ya Madam Mery nikashika funguo, iliyopo kwenye kitasa nikaizungusha tatatibu, huku nikiwa makini kwa lolote litakalo jitokeza. Nikaufungua mlango, nikakuta Madam Mery akiwa amevalia baibui jeusi, bila ya salamu kaingia ndani. Nikachungulia nje kwenye kordo, hapakuwa na mtu. Nikafunga mlango.
Madam Mery akanikumbatia kwa furaha, huku akihema mihemo yenye pumzi moto, iliyo katiza mara kadhaa kwenye shingo yangu.
"Mbona umeche......."
Madam Mery akaniwahi kuninyonya mdomo sangu, na kuikatisha sentensi yangu. Fukuto zito la mzhaba likatukamata miiili yetu. Nikalivua baibui la Madam Mery na kulitupa kando. Tukaendelea kunyonyà ña midomo yetu, nikamnyanyua na kumuweka kitandani, tukasndelea kupeana burudani za mwili.
Saa kumi alfajiri Madam Mery akastuka, kutoka usingizini, baada ya kupitiwa na uchovu wa penzi zito tulilo peana usiku mzima.
"Unakwenda wapi?"
"Nyumbani"
"Usiku wote huu?"
"Kuna kazi nakwenda kuifanya"
Madam Mery alizungumza kwa wasiwasi, huku akiingia bafuni, akaoga na kurudi chumbani, Akavaa haraka sana, akanifwata kitandani, akanipiga busu mdomoni.
"Kesho Eddy"
Madam Mery akatoka haraka, hadi nikabaki nikishangaa.Saa kumi na mbili Sahamsa akaingia chumbani.
"Eddy za kazi"
"Kazi?"
"Ndio kazi uliyo ifanya jana usiku na mtu wako?"
Nikastuka, Shamsa akatoa simu, niliyo mnunulia jana, akanirushia kitandani. Nikaona video ya jinsi madam Mery alivyo kuja, chumbani kwangu Nikichungulia na kuufunga mlango.
"Huyo ni mimi niliye rekodi hiyo video, pasipo nyinyi kujijua. Piga picha siku wakiwa ni watu wa huyo waziri, itakuaje?"
"Jibu unalo, siñà haja ya kukusimulia kitakacho tokea. Amka twende tulipo panga"
Nikajikuta nikianza kumuogopa Shamsa, sikukua kama atanifwatilia kwa ukaribu kiasi hichi. Nikajiandaa, tukalata kifungua kinywa na kuelekea ilipo kambi ya wakimbizi, huku Shamsa akiwa ndio dereva.
Gafla Shamsa akafunga breki kali, huku akijitahidi kumkwepa mtu aliye lazwa barabarani akionekana hajitabui. Gari, likafanikiwa kusimama.
"Eddy usishuke, hili eneo sio salama"
"Ngoka kwanza"
Nikavua koti langu la suti, pamoja na tai. Nikaichomoa bastola yangu na kuanza kutembea kwa tahadhari, kwenda alipo lala mtu huyo, huku macho yangu yakiwa makini kila sehemu. Nikafika sehemu alipo mtu huyo. Kwakutumia mguu nikamgeuza. ili niione sura yake, kutokana amelala kifudi fudi. Moyo ukanipasuka baada ya kukuta ni Amina rafiki wa Mnka, akiwa ameuawa kikatili, huku macho yake mawili yakiwa yameng'ofolewa
Huku yakitoka funza wadogo wadogo, harufu kali ya mwili wa Amina, haikunizuia kuchuchumaa kumtazama vizuri. Mwili wake tayari umeanza kuharibika kutokana na kujeruhiwa vibaya kwa mapanga, sikuweza kuusogeza pembeni ya barabara, kutokana na baadhi ya nyama za mwili wake, kushikamana na barabara hii ya lami. Nikajikuta machozi yakianza kunilenga lenga, nikatazama pande zote ya eneo tulilopo hapakuwa na dalili yoyote ya mtu kutokea zaidi ya Shamsa aliye simama, nje ya gari letu akinitazama kwa kitu ninacho kifanya.
Nikazidi kujihisi uchungu baada ya kukisogeza kichwa cha Amina kwa kutumia bastola yangu, na kukuta ubongo wote ukiwa nje. Huku sehemu ya pembeni, upande wa kushoto ikiwa imepasuliwa vibaya mno.
"Ahaaa"
Nikajikuta nikitoa sauti ya uchungu, huku nikisimama. Wasiwasi ukaanza kunijaa moyoni mwangu, wa kwanza kumfikiria ni mke wangu Phidaya, ambaye kwa mara ya mwisho alikua na Amina, ambaye ni huyu amelala hapa barabarani, akiwa tayari ni mfu. Nikaanza kupiga hatua za taratibu kurudi kwenye gari. Nikafungua mlango wa gari pasipo kumsemesha chochote Shamsa, ambaye naye aliingia ndani ya gari na kuliwasha. Akanitazama kwa muda jinsi machozi hanavyo nitiririka kwenye mashavu yangu pasipo kutoa mlio wowote wakulia. Akawasha gari na kuondoka eneo hili taratibu.
Mwendo wa takribani lisaa lizima, sikufungua kinywa changu kuzungumza na Shamsa, ambaye mara kwa mara aliniita pasipo kumjibu chochote. Akasimamisha gari kwenye moja ya sheli ya mafuta. Akashuka na kuzungumza na muuzaji wa mafuta kisha yeye akaingia kwenye duka lililopo hapa kwenye sheli. Picha kadhaaa, za Amina alivyo nisaidia kwenye tukio la kuiokoa familia yangu, zikaanza kunijia kichwani. Hadi picha ya mwisho ya mwili wake, ulio haribika ndio ikagota kwenye ubongo wangu, unao shuhulka na kumbukumbu. Nikaichomoa bastola yangu haraka na kuinyoshea kwa mtu aliye chungulia kwenye kioo cha upande wa Shamsa.
"Ohhhhhhhh"
Sauti ya dada, muhudumu wa sheli hii, niliisikia. Macho yake akawa meyatoa kwenye bastola niliyo mnyooshea. Nikamuona jinsi anavyo tetemeka kwa woga. Jasho jingi likaanza kunimwagika. Huku nikiyang'ata meno yangu kwa hasira kali, iliyo changanyika na uchungu wa kutamani kulipiza kisasi kwa yeye aliye muua Amina.
"Eddy unafanya nini?"
Shamsa alizungumza huku akiufungua mlango wa gari, akausogeza mkono wangu pembeni ulio shika bastola. Akaweka bidhaa alizo zinunua siti ya nyuma.
"Samahani dada, pesa yako hii hapa."
Shamsa alizungumza huku akimpa dada huyo, pesa anayo dai kwa mafuta aliyo tuwekea kwenye gari. Shamsa akafunga kioo, akawasha gari na tukaondoka.
"Eddy unatatizo gani, nji nzima unakazi ya kumwagikwa na machozi, nakuuliza hutaki kunijibu?"
Shamsa liniuliza kwa sauti ya ukali, huku akinikodolea macho. Nikairudisha bastola yangu nilipo ichomoa kwenye kiuno, ilipo kua imebanwa vizuri kwa mkanda wangu wa suruali.
"Geuza gari turudi, kwenye ule mwili"
"Nini, hivi Eddy umechanganyikiwa?"
Shamsa alizungumza huku, akifunga breki za gari na kulisimamisha kando ya barabara.
"Nimekuambia geuza gari turudi, kwenye ile maiti."
"Eddy tumia akili, mtu humjui, ya nini kujifanya msamaria mwema, kwa matatizo yasiyo yako. Tumebakisha kilomita moja tufike, wewe unataka turudi tena kilomita ishirini nyuma? Ahaaa siwezi kufanya ujinga kama huo."
Shamsa alizumgumza kwa kujiamini sana. Nikamtazama kwa macho makali yaliyo jaa hasira na uchungu. Nahisi atambui ni nini anazungumza.
"Tunarudi au haurudi?"
Ilinibidi na mimi kuzungumza kwa sauti ya hasira, iliyo mstua Shamsa, ambaye kwa kipindi kifupi nilicho kaa naye, amenizoea sana.
"Eddy, fikiria juu ya familia yako, fikiria juu ya mwanao na mkeo. Kwa nini unataka kufanya vitu vitakavyo kuhatarisha usalama wako, na kukutenga na familia yako?"
"Fikiria hilo, hii nchi haina usalama kama umavyo fikiria wewe, jiulize yule ni kwanini amuauwa na kutupwa pale barabarani, piga picha ni mimi au wewe ndio tumetupwa pale barabarani, utajihisi vipi?"
Shamasa alizungmza kwa sauti ya upole huku machozi yakimwagika, nikabaki niliwa ninafikiria ni nini cha kufanya. Sikuwa na uwezo wa kuhairisha safari ya kwenda kwenye kambi ya wakimbizi ilipo familia yangu, na kurudi kuuchukua mwili wa Amina ambao tayari umesha haribika vibaya mno, na hata niiuchukua nisingeweza kuuzika leo, pia endapo polisi watanikamata na mwili huu, wataniweka kuzuizini hadi watakapo fanya uchunguzi ambao sijajua utachukua muda gani kukamilika.
"Eddy, natambua wewe ni mtu mwema. Ila si kwa kila kitu unatakiwa kufanya wema, mengine inapo kupasa kufanya ukatili fanya hata kama mtu unamtambua. Ila kama atakuwa adui yako wewe fanya kwani ukimuacha atakudhuru wewe"
Shamsa alizungumza maneno yaliyo nifanya nianze kukata tamaa, juu ya mwili wa Amina, uliopo barabarani.
"Washa gari tuendelee na safari"
Shamsa akafanya kama nilivyo muagiza. Safari ikaendelea.
"Kwani unamtambua marehemu?"
"Ndio"
"Eheeee ni nani yako!?"
"Anaitwa Amina, ndio aliye nisaidia katika kuiokoa familia yangu, hadi ikachukuliwa na jeahi la umoja wa mataifa. Na wakapelekwa kwenye hiyo kambi ya wakimbizi kwa usalama wao zaidi"
"Mmmm, kuna kitu kinacho endelea hapa. Kuwa makini Eddy. Yaani hii nchi anaye kuua huwezi kumdhania kabisa. Laiti ningeamua kukuua mimi si ningekuua siku tulivyo kutana. Ila uliniacha kwasababu ni mtoto."
"Ndio"
"Ndio unatakiwa kuwa makini, na hata watoto wadogo, kwani huku watoto pia wamepandikizwa roho za chuki na ugaidi"
"Ile nyumba iliyo lipuka ni ya yule dada, aliye uwawa"
"Weee, acha utani!?"
"Utani wa nini sasa?"
"Ndio ukweli huo."
"Mungu ailaze mahali pema, roho ya marehemu"
"Amin"
Taratibu nikaanza kupata picha ya siku nilivyo rudi, nyumbani mwa Amina na kukuta mwili wa askari aliye kufa. Wasiwasi ukazidi kuongezeka baada ya kumkumbuka Manka, ambaye tulimuacha kwenye nyumba ya Amina na sikumkuta na hadi sasa hivi sifahamu ni wapi alipo.
"Ngoja niipate familia yangu kwanza"
Nilizungumza, huku Shamsa akisimamisha gari, kwenye megesho ya nje ya geti, la kuingilia katika kambi ya wakimbizi.
Tukaacha bastola zetu ndani ya gari, tukashuka na kwenda kwenye kijumba kidogo, kilicho jengwa kwa ajili ya ofisi ya wanajeshi wanao simama getini, kuangali ni nani anaye ingia na kutoka ndani ya kambi hii. Wakatukagua kabla ya kuingia kwenye ofisi hiyo. Kisha wakaturuhusu kuingia ndani ya ofisi, baada ya kuridhishwa na kutukagua kwetu.
"Mumesema nyinyi, niwatoaji misaada si ndio?"
Mwanajeshi mmoja, alituulizaa kwa lugha ya kifaransa, huku akitutizama machoni kwa umakini.
"Ndio"
Nilimjibu kwa kujiamini, huku nikizichunguza nguo alizo vaa, zikionyesha bendera ya nchi ya Ufaransa kwenye bega la mkono wake wa kushoto, huku mkono wa kulia kukiwa na kitambaa cheupe, kilicho andikwa kwa maandishi makubwa yenye rangi nyekundu 'MP'.
"Mumetokea wapi?"
"Ohhh Eddy karibu"
Kabla sijamjibu, aliingia mwanajeshi, mwenye nyota tatu begani, wanajeshi walio kuwemo ndani ya hii ofisi wakampigia saluti. Ikanibidi kuipokea salamu yake kwa tabasamu huku nikimpa mkono. Japo sifahamiani naye, na wala sina kumbukumbu ni wapi nilionana naye.
"Jamani huyu ndio yule jamaa aliye okoa familia ya balozi wa Marekani nchini Afrika kusini."
Wanajeshi wengine wakaanza kutabasamu na kunipa mikono ya pongezi hata wale walio nisemesha kwa kifaransa, wakazungumza kingereza japo, kifaransa ninakijua kidogo.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com