Notifications
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (24)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NNETULIPOISHIA...Kwa kweli siku hiyo niliwaza sana na kutafakri vitu vingi. Wale wanachuo wenzangu wamenambia kuwa Msouth alikuwa kwa kimada mwingine na japo stori haikumalizikia ila ukweli ni kwamba alifumaniwa na kupigwa vibaya na huenda walimtupa mahali na ndio maana chanzo cha kifo chake hakieleweki.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijaribu kuijikontrol ili nisiwaze kitu…
  • MY DIARY (23)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TATUTULIPOISHIA...Alinisihi sana nisitoe niilee na yeye atatoa huduma zote lakini tuendelee kufanya siri ili tusije tukahatarisha ndoa yake na kusababisha familia yake kuyumba. Kwa kweli sikuweza maana ilikuwa ni kujipa tabu mimi na huyo mtoto atakayezaliwa. Bora ataa ingekuwa ni mimba ya ule mwalimu ambaye hajaoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilitamani nimchomekee hiyo mimba…
  • MY DIARY (22)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILITULIPOISHIA...Alitumia vizuri umbo lake la kimiss kutembea kimiss na kuweka mapozi ya maana. Na baada hapo alilala kwenye kile kigodoro na akachojoa vyote isipokuwa kufuli jeupe ambalo nalo alipewa hapo hapo kwa ajili ya kazi hiyo. IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi sikumpa nafasi Joyce niliingilia nafasi yake na kuchukua ule uume wa bandia nikamfuta yule dada.…
  • MY DIARY (21)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJATULIPOISHIA...Nilichomeka simu chaji na kuiweka hewani ili nione kama kutakuwa na sms yeyote iliyoingia.Hofu ilizidi kunitawala na wakati naendela kufikira simu yangu iliita niakzani labda ni Joyce na nilipoiangalia nilimkuta ni Msouth. Sikutaka kuipokea nikaiacha iite mpaka ikate yenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikajiuliza kwani amepatwa na nini usiku huo mpaka…
  • MY DIARY (20)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINITULIPOISHIA...Nikamwambia kuhusu namba zangu za simu amuombe aliyemtuma anisaidie na kuhusu hilo la pili je hatuwezi kufanya kesho kwa sababu kuna mahali nilikuwa nikienda? Alifikiria kwa sekunde kadhaa na kuniambia kuwa hapana anaomba nimsaidie leo kama yeye alivyonisaidia mimi kwa sababu ningekuwa kwenye foleni nisingeweza kuondoka kirahisi hivyo kama ninavyofikiria.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (19)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA TISATULIPOISHIA...Baada ya hapo niliendelea kumdadisi juu ya tukio lile lakini hakuwa tayari kufunguka zaidi ya kusema aliumia sana. Hapo nikaamua kuutafuta ukweli kwa kutumia mbinu za kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilimwekaa mikono begani na kumwambia pleaee dear naomba uniambie ukweli ili nijue nakusaidiaje? Basi Ramadhani akaanza kulalamika kuwa baba yake amekuwa akimwingilia…
  • MY DIARY (18)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA NANETULIPOISHIA...Halafu eti akawasha simu na kuonesha zile picha alizotupiga kweli huyu rafiki yangu alikuwa hamnazo sio picha tu alituchukua video kabisa na sauti. Akanambia ngoja ampigie paparazi mmoja hivi aje ili atengeneze habari tupate hela. Kauli hiyo ilinikosesha amani na kunikera sana akanmabia eti kuna namna ya kufanya ili sura yangu isitokee.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (17)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SABATULIPOISHIA...Nilijifikiria mara mbili nikajikuta namkubalia kwani alionekana ni mpole na mstaarabu sana.Basi tukaenda hadi kwake ambapo haikuwa mbali na hapo tulipokuwa na kweli alikuwa na chumba na sebule na sebuleni kwake niliona picha ya ukutani akiwe yeye na mke wake nahisi ilikuwa siku ya harusi yao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikasema huyu kijana atakuwa amefunga ndoa…
  • MY DIARY (16)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMI NA SITATULIPOISHIA...Mwanamke akaamua kuingia jikoni na kukarangiza viazi na nyama rosti na kilipoiva kililetwa mezani tukaendelea kujenga afya. Sikuaamini kama Joyce alikuwa anakumbuka hata kupika kwa sababu alibadilka sana na alikuwa akiishi maisha ya starehe.. Lakini aliniprovu wrong kwa kutoa rost ya hatari.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baada ya kula alinambia kuwa alikuwa amechoka…

SORRY MADAM (108)

SEHEMU YA MIA MOJA NA NANE
ILIPOISHIA...
"Ehee niambie zile damu ulizitoa wapi?"
"Tutazumgumza kitandani"
"Sawa"
Tukamaliza kuonysha vyombo na kuvipanga vizuri, tukawaaga watoto wetu na kuingia chumbani wao wakaendelea na mambo wanayo yafanya.

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
Phidaya akapitiliza bafuni kuoga, baada ya muda akarudi na kujirusha kitandani.
"Nasubiria hayo mazungumzo"
Nikashusha pumzu huku nikimtazama Phidaya anaye hitaji nimuambie ni nini kilicho nikuta.
"Nina tatizo mke wangu"
"Tatizo! Tatizo gani?"
"Kipindi fulani nilipo kua Afrika Kusini nilifanyiwa uchunguzi na kubainika nina ugonjwa wa hasira ambao, nikikasirika sana damu puani hua zinanitoka, pamoja na mwili kushikwa na kizungu zungu"
Nilimfinya Phidaya juu ya ugonjwa wa saratani(Canser), ambao niligundulika unaninyemelea.

"Mmmm leo ni nini kilicho kukasirisha?"
Nikamtazama Phidaya kwa macho ya kumdadisi kama anaweza kuhimili kile nitakacho kwenda kumuambia.
"Nilikumbuka, kitu licho nifanyia John. Nikajikuta nikiwa nimemasirika sana"
Ilinibidi nimdanganye tena kwani hakuwa jasira kwa lile nililo panga kumueleza kuhusiana na John

"Ni hilo tu au kuna jengine?"
"Hakuna jengine zaidi ya hilo"
"Ila baba Junio, kama ni huyo John, achana naye. Kikubwa umesha ipata furaha yako"
"Una uhakika na unalo lizungumza?"
"Kama mimi nimesha msamehe japo sihitaki kuonana naye. Kwa maana nikimuona nitatamani nimuue?"
Nikamchunguza Phidaya nikagundua ana usingizi unao mnyemelea, hata anacho kizungumza hakzingatii.

"Kwanza Junio alivyo zaliwa, aliwapeleka wapi. Hadi mukawa munazungumza na mimi?"
"Ni stori ndefu, kesho tutazungumza tukiwa tumetulia. Ila msamehe tuu"
"Siwezi kumsamehe, hadi nichukue kila kitu alicho nichukulia mikoni mwangu"
"Utavichukua vitu vipi?"
"Vingi tu"
"Mtu mwenyewe yupo huko Afrika kusini utampataje?"
"Nitampata tu"
Katikati ya mazungumzo Phidaya akapitiwa na usingizi, mzito ulio tokàna na uchovu wa kutwa nzima. Saa ya ukutani inaonyesha ni saa saba usiku.

Sikuwa na hata lepe la usinguzi, nikaibeba simu ya mezana na kwenda nayo sebleni, ambapo nikamkuta Shamsa akiwa amepitiwa na usingizi. Huku Junio akiwa amejilaza kwenye sofa.
"Shamsa amka ukalale"
Shamsa akanyanyuka kiuvivu, akaifunga laptop.
"Niachie laptop hiyo"
"Usiku mwema"
Shamsa alizungumza huku akipiga miyayo ya uchovu. Nikamnyua Junio na kumuingiza chumbani kwake, huku akiwa usingizini. Nikamlaza kitandani na kumfunika vizuri na shuka.

Nikarudi sebleni na kukaa kwenye kiti chenye meza iliyo na laptop. Nikaifungua na kukuta ikiwa bado ipo hewani kwenye mtandao wa Facebook. Nikatazana tamzama alicho weka Shamsa, Picha moja niliyo piga mimi, Junio na Phidaya inaonekana ikiwa na maoni mengi ya watu. Ikanivutia niyafungue. Kitu kilicho nistua ni baadhi ya maoni ya watu yakionyesha masikitiko yao juu ya kifo changu. Mapigo ya moyo yakaanza kunienda kasi huku wasiwasi ukinijaa. Nikataona maoni ya Blanka aliyo yaandika kwa herufi kubwa.

'MBONA SIELEWI NI NINI HICHI?"
Nikachukua simu na kumpigia Blanka tena, safari hii akapokea haraka.
"Blanka mimi ni Eddy"
"Ndio sauti yako nimeikumbuka, jana ulivyo piga nilikua usiku nimelala"
"Vipi kuna lipi jipya?"
"Jipya bwana, ni mhabari juu ya kifo chako"
"Kifo changu, kivipi?"
"Ndio, kitu kilicho nifanya nijue hujakufa ni picha nilizo ziona hii asubuhi facebook, ukiwa na familia yako. Hapo ndipo nikakumbuma uliniambia unakwenda kutafuta familia yako"
"Sasa kifo changu kipi?"

"Tumemzika majuzi juzi Eddy aliye uawa pamoja na dada Sheila"
"Fredy aneuawa?"
"Ndio, walitekwa kwenye arusi yeye na Sheila, ila hadi sasa mwili wa Sheila haujapatikana"
"Sasa nakuomba usimuambie mama kuhusiana na hii ishu."
"Eddy mama ana hali mbaya sana, amepararaizi baada ya kifo chako, hali, hanywi yupo yupo tu"
"Nini?"
"Ndio hivyo, dokta wake amesema tunaweza kumpoteza mama muda wowote kuanzia leo. Hapa nilipo nimechanganyikiwa"
Nikakata simu, mwili mzima nikawa kama umezizima, picha ya Jonh na Sheila zikanijia kichwani jinsi walivyo kua na furaha, nilipo waona kwenye mgahawa.

"John nilazima ulipe kwa hili. Nikatuua kwa mkono wangu mwenyewe, ole mama yangu afe, nitakufanya kama Derick"

Kila nilicho kifikiria juu ya adhabu nitakayo mpa John, sikupata jibu la uhakika. Nikazima kila kitu na kurudi chumbani kwetu. Nikajilaza kitandani taratibu huku mawazo yakiendelea kuniandama. Kikubwa nikawa ninamfikiria sana mama yangu. Sikulala hadi kunapambazuka.
"Umeamkaje baby?"
Phidaya alinisalimia mara baada ya yeye kuamka.

"Safi vipi?"
"Ahaaa poa, alafu nimeota ndoto mbaya kama nini?"
"Ndoto gani?"
"Nimeota John amekuja hapa tulipo, akiwa na wale watu wake, akatufunga kamba, sote wanne, kisha wakatuweka hapo sebleni. Wakamwaga mafuta ya petroli kila sehemu, na kuwasha moto wao wakaondoka. Ndio nikastuka"
"Mmmm hakuna kitu kama hicho"
Niliamua kumfariji Phidaya, kwani sikupenda apoteze amani asubuhi hii, ambayo tunaendelea kujiandaa na maandalizi ya sherehe ya kuzaliwa kwa Junio wetu.

"Hapa nilipo mapigo ya moyo yananienda mbio."
Nikamvuta karibu yangu na kumlaza kifuani mwangu, taratibu nikaanza kuzichezea nywele zake ndefu na laini.
"Tulia mke wangu"
"Eddy naogopa"
"Umaogopa nini mke wangu"
"Nahisi familia yangu, itapata shida tena. Tena hii itakua kubwa kuliko ya kwanza"
"No baby usiyape nguvu, mawazo hayo mimi nipo. Nitahakikisha hakuna kitakacho haribika wala mtu kunyanyua mkono wake juu ya familia yangu nipo tayari kwa lolote hata kufa ili mradi familia yangu iishi kwa amani"

"Kweli baby?"
"Ndio kama aliweza ile mara ya kwanza basi hii ya pili, hato weza kamwe"
Nilizungumza huku nikiwa na jazba ya hasira, kwani hadi hapa ninavyo zidi kumfariji mke wangu, tayari John amesha yaweka maisha ya mama yangu mashakani. Taratibu Phidaya akaanza uchokozi wa kitandani, sikuwa na hiyana zaidi ya kumpa haki yake anayo stahili kama mke wangu. Hadi tunamaliza kila mmoja akawa kwenye furaha isiyo simulika, kwani wote tulifika kwa wakati mmoja mwisho wa mechi yetu.

"Ngoja nikaandae kifungua kinywa"
"Sawa"
Phidaya akanyanyuka na kuingia bafuni, akaoga na kutoka. Akavaa nguo alizo amua kuvaa kwa siku hii yaleo na kwenda nje. Nikachukua simu ya mezani, nikaziingiza namba za Blanka na kumpigia. Simu ikaita baada ya muda ikapokelewa.
"Vipi hali ya mama?"
"Kuna mabadiliko kidogo?"
"Mazuri au mabaya?"

"Mazuri, nilimuonyesha mama picha yako ukiwa na mkeo na mwanao. Kidogo mama alianza kufungua kinywa huku akitabasamu"
"Hakusema chochote?"
"Hapana, alitabasamu tu na kutingisha kichwa kama mtu aliye furahi kwa kuiona hiyo picha"
"Poa nitakuja"
"Kwani upo wapi?"
"Nitakuambia siku nyingine. Kwaheri"
Nikakata simu, baada ya kumuona Junio akiingia chumbani huku akilia jambo lililo nistua sana.
"Mona unalia?"
"Mamy kanipiga"
Kidogo mapigo ya moyo yakanitulia.

"Kisa nini?"
"Eti hataki nimsaidie kupika chai"
"Ni hilo au kuna jengine"
"Nihilo dady"
"Mwanao ni muongo"
Phidaya aliingia huku akionekanana kukasirika.

"Amefanyaje?"
"Nimemuambia asicheze mpira ndani, likawa halinielewi. Mpaka akaipiha Tv ya ukutani ikaanguka"
"Imevunjika?"
"Hapana, haijavunjika. Tena huku nje usitoke ubaki humu humu na huyo baba yako. Sitaki kukuona huku nje sawa?"
Phidaya alizunguilmza na kutoka nje, nikamnyanyua Junio na kumtupia kitandani nilipo na kumfanya aanze kucheka na kufurahi.

"Huo uronaldo wako, uwe unaufanyia nje sawa mwangu?"
"Sawa dady, twende tukacheze nje"
Junio alizungumza huku akinivuta mkono, nikatizama saa ya ukutani inaonyesha ni saa tatu asubuhi.
"Nenda ukaningoje sebleni nioge mara moja"
"Ok dady"
Junio akatoka nikaingia bafuni na kuoga, kisha, nikavaa nguo za mazoezi na kutoka nje.

"Munaenda wapi?"
Phidaya alutuuliza baada ya kutuona tukitoka mlangoni bila ya kuaga.
"Ufukweni"
"Kifungua kinywa tayari"
"Anzeni tu sisi tunakuja"
"Eddy mbona unapenda kumuendekeza huyo mwanao, kila anacho taka unamfanyia"
Nikamfwata Phidaya na kumbusu mdomoni.

"Tunakuja baby, Shamsa yupo wapi?"
"Yupo jikoni anamalizia kupika"
"Ok tunakuja"
Tukatoka na Junio, tukaingia kwenye lifti na kushuka hadi chini, tukitokea gorofa ya saba, yalipo makazi yetu. Tukaelekea kwenye fukwe zilizopo pembezoni mwa hotel hii. Kitu kilicho nishangaza ni jinsi Junio alivyo maarufu kwa watoto wezake ambao tuliwakuta hapa ufweki. Wakaunda timu mbili huku nami nikiwa timu pinzani na Junio. Wakanichagua kua goli kipa na sikuwa na jinsi. Magoli ya viayu tuliyo yaweka hayakuzuia mechi kuanza, huku golikipa wa timu ya Junio, akiwa mzee mwenye mjukuu wake kwenye timu yangu.

Hapa ndipo nilipo pata fursa ya kumtazama Junio vizuri, nakugundua anakipaji kikubwa cha kucheza mpira. Mara kadhaa akawa anapiga mashuti mazito golini mwangu, ambayo niliweza kuyanyaka vizuri. Huku wachezaji wa timu yangu wakinisifia kwamba ninaweza kazi ya kulinda goli. Kitendo cha kuinyaka mipira, ndivyo jinsi Junio alivyo ongeza juhudi ya kucheza na kupiga mashuti mazito golini.

"Kumbe na wewe ni kipa mzuri?"
Mzee wa timu ya Junio ambayo hadi sasa hivi hakuna goli alilo fungwa, aliniuliza tulipokua tukibadilishana magoli, baada ya dakika kumi na tano alizo tuwekea refa wetu kuisha.
"Najaribu tuu"
"Hapana, kuna kitu nimekiona ndani yako na huyo mwanao"
"Kitu gani?"
"Muna vipaji vikubwa sana, hakikisha unamuendeleza mwanao katika fani hii, atafanikiwa sana na atakuwa mchezaji mkubwa sana duniani"
Sauti ya filimbi ikatustua mimi na huyu mzee, huki refa akituomba kila mmoja akakae kwenye goli lake, tukafanya kama alivyo tuelekeza.

Mpira ukaanza, japo kuna tifutifu jingi kwenye hii fukwe, ila Junio, anakimbia kuliko watoto wezake ambao mara kadhaa, walikua wakianguka anguka.
Shuti kali alilo lipiga Junio, akiwa karibu yangu, likanipita katikati ya miguu yangu na kwenda mbali kidogo na sehemu tunayo chezea mpira. Nakuwafanya Junio na timu yake kushangilia ushindi wa goli hilo walilo kua wakilitafuta kwa juhudi mara baada ya kipindi cha pili kuanza.

"Hahaaaa haaaaaa"
Nilimuona Phidaya akicheka, huku akiwa na kamera yetu. Nikatambua moja kwa moja anacheka goli, nililo fungwa na Junio.
"Junio kachukue mpira sijui umeenda wapi"
Nilimuambia Junio aufwate mpira wake ambao yeye ndio aliuona sehemu ulipo elekea. Junio akaongozana na wezake wawili kwenda kuutafuta.

"Unacheka nini?"
"Nakucheka wewe, ulivyo fungwa na huyo mwanao, njoo uone hili goli lilivyo ingia"
Nikamfwata Phidaya alipo, akanionyesha video aliyo rekodi, goli lililo pita katikati ya miguu yangu
"Mwanao amekupiga tobo"
"Huyu mtoto, ananguvu za miguu kama hadi ananiogopesha, skija golini"
"Ndio hivyo tumepata mchezaji, mzuri tusubirie atakaye kuja sijui atakuwaje"

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
39 Simulizi Sorry Madam
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni