SORRY MADAM (107)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA MIA MOJA NA SABA
ILIPOISHIA...
Nikasubiri kama dakika tano, mwili kidogo ukapata nguvu za kutembe. Nikamshukuru mlinzi, nikavuka barabara na kwenda kwenye duka nilipo waagiza Phidaya awachagulie wanae viatu. Nikawakuta wakiendelea kuchagua chagua viatu wanavyo vipenda.
"Mbona umelowa kichwani?"
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Phidaya aliniuliza huku akinigusa gusa kichwani mwangu.
"Kichwa kidogo kilikua kinaniuma, ndio nikanawa kichwani"
Ilinibidi kumdanganya Phidaya kwa maana vita yangu na John, nitaka niimalize mimi nwenyewe japo Phidaya naye alihusika katika mateso yote tuliyo sababishiwa na John.
"Hiii damu nayo imetoka wapi?"
Aliniuliza huku akinishika kwenye kifua changu akinionyesha matone kadhaa ya damu.
"Dady hapo je, nimependeza?"
Junio alisimama mbele yetu, huku akiwa amevalia viatu aina ya Supra, huku akiwa ameshika miwani iliyo endana na viatu alivyo vivaa, ikanilazimu kumjibu Junio kwanza na kulikwepa swali la Phidaya.
"Yeah umetokelezea mwanangu."
"Je nikivaa hii miwani?"
"Umekua kama Michael Jackson"
Junio akanifwata nilipo simama, tukagonganisha mikono, akaondoka akiwa amefurahi sana.
"Huo ubishoo mwanao ameridhi kwa nani?"
"Nikuulize wewe baba mtu, mtoto anapenda kuvaa vitu vizuri kama anajua kuvinunua"
"Muache bwana ndio muda wake huu wa kupendeza"
"Sawa tuachane na hayo, nijibu hizo damu umetoa wapi?"
"Tutazungumza nyumbani"
"Eddy umetoka kupigana?"
"Hapana mke wangu"
"Ila ni nini?"
"Sijapigana mke wangu. Hembu nenda ukawaambie hao wanao wafanye haraka turudi hotelini. Sijisikii vizuri"
Phidaya akanitazama machoni kwa umakini, kisha akawafwata Shamsa na Junio, sehemu walipo.
Nikasimama kwenye ukuta wa vioo wa hili duka ulio elekea sehemu ulipo mgahawa, nilipo waacha John na Sheila. Dakika kama tatu, nikamuona John na Sheila wakitoka kwenye duka hilo. Wakaingia kwenye gari moja yakifahari iliyo simama baada ya wao kusimama nje.
Nikastukia nikiguswa kwa nyuma, nikageuka na kumkuta Phidaya akiwa amesimama nyuma yangu, huku macho yake yakielekea lilipo gari walilo panda Jonh na Sheila.
"Unashangaa nini?"
Phidaya aliniuliza.
"Nashangaa magari"
"Alafu ile gari nimeipenda"
"Iipi?"
"Ile lililo ondoka nje ya mgahawa"
Nikagundua Phidaya hajamuona John, laiti angemuona asinge zungumza maneno kama haya.
"Nitakununulia"
"Mmmm ila inaonyesha ni gari la gharama sana"
"Hakuna shida, tutatafuta tununue na sisi, lakwetu"
"Haya njoo uwalipie hawa wanao viatu vyao walivyo vichagua"
Nikafika sehemu ya kulipia nikakuta viatu vya Junio na Shamsa vikiwa vimepangwa kwenye meza moja kubwa na kila mmoja amechagua pea ya viatu zaidi ya kumi.
"Eheee vyote hivi munakwenda kuvaa au kuweka mapambo?"
"Kuvaa"
Shamsa alinijibu huku akitabasamu.
"Mmm haya bwana"
"Ila kaka ndio watoto hao, usilalamike"
Jamaa muhudumu alizungumza kiswahili nakutufanya sote tushangae.
"Unajua kiswahili?"
"Ndio kaka, nilikulia Nairobi Kenya. Ila kaka familia yako ipo vizuri sana"
"Asante"
"Huyo mwanao wa kike amefanana sana na mama yake na huyo wa kiume ni chata yako kabisa."
"Etieer ehee"
"Ndio, hongera sana, umejua kuchagua."
Jamaa, alikua mzungumzaji sana, ila kusema ukweli Shansa anafanana sana na Phidaya, kuanzia rangi za mwili hadi sura zao. Japo mara kadhaa, Phidaya alikua akikataa hajafanana na Shamsa.
"Ni kiasi gani nadaiwa?"
Janaa akaminya batani ya mashine iliyo mbele yetu. Ikatoa bei ya pamoja ya viatu vyote.
"Hembu weka hiyo miwani kwenye meza"
Junio akaweka miwani kwenye meza, vilipo viatu. Mashine ikaongeza bei.
"Ni dola elfu moja na miatano"
Nikatoa pochi yangu, nikatoa dola mia mia kumi na tano na kumkabidhi muhudumu. Wafanyakazi wengine wakachukua viatu na kuviweka kwenye mifuko.
"Jamani kuuliza si ushamba. Hivi hiyo meza ndio inahesabu bei za vitu vinavyo wekwa juu yake?"
Nilimuuliza muhudumu baada ya kuona tukio hilo, lililo nishangaza sana.
"Ndio, inarahisisha kazi na kutoa shida ya wateja kulalamika kwamba tunawazidishia bei wateja. Ukiweka hapo kitu chochote kinacho uzwa humu ndani ya duka letu, basi bei inatoka kama hapa mulivyo ona, kwahiyo hakuna mabishano."
"Haki ya Mungu, hii mashine ikiwekwa kwenye maduka ya wachaga watafilisika"
"Wachaga wa Tanzania?"
"Ndio"
"Ahaaa kwa nini?"
"Unajua kitu kama cha dola tano, watakuanzia kukuuzia dola kumi, ukiwa mjinga wana kula ila ukiwa mjanja utashuka nao hadi bei halisi"
"Haaaaa, kwani wewe kaka kabila gani?"
"Ahaa kabila hapo...."
"Hapo nini si ujibu, kigugumizi cha nini?"
Phidaya alidakia kwenye mada niliyo kua nikizungumza na muhudumu.
"Mimi mwenyewe ni mchaga ila nimechanganyia na mpare"
"Mungu wangu, hayo makabila nasikia ni wabaili sana kwa nchi ya Tanzania?"
"Waongo hao, hukuna kitu kama hicho, tena ndio makabila yanayo ongoza kwa kutumia pesa bila kuijutia."
"Mmmmm"
"Usigune si unaniona mimi haoa ninavyo wapapendesha wanangu. Ngoja tuondoke kaka tumezunguka sana"
"Sawa kaka ninaitwa Salim"
"Mimi ni Eddy, huyu mke wangu na hawa ni wanangu"
"Karibuni sana"
"Asante"
Kwa uchangamfu wa jamaa huyu, ukanifanya mwili wangu kurudi katika hali ya kawaida hata, hasira niliyo kua nayo dhidi ya John ilanipotea. Tukatoka nje ya duka. Tukakodisha taksi hadi Hotelini, moja kwa moja nikaingia chumbani kwetu, nikawaacha Phidaya na wanae wakiendelea na kujipima pima nguo na viatu walivyo nunua. Nikachukua simu iliyopo mezani, nikaipakata mapajani, nikaingiza namba za simu ya Blanka mdogo wa Sheila. Kwa bahati nzuri simu ikaanza kuita. Ikaita kwa muda hadi ikakata. Nikajaribu kuipiga tena ikaita kwa muda mrefu, kabla haijakata ikapokelewa.
"Haloo"
Nilizungumza, ila Blanka hakuitikia.
"Blanka"
"Wewe nani?"
Blanka alizungumza kwa sauti yaupole, iliyo jaa wasiwasi mkubwa.
"Upo sehemu gani?"
"Wewe nani kwanza?"
"Eddy"
"Eddy gani?"
Nikaanza kupata wasiwasi dhidi ya Blanka nikahisi nimekosea namba, kwani hata namba yenyewe sikuwa naikumbuka kivile.
"Kwani wewe upo nchi gani?"
"Tanzania, kwani wewe ni Eddy gani au ndio hii mimamba ya Fremasoon? Hata kama munanichukua hamuwezi kunichukja damu ya Yesu imenifunika, washenzi nyinyi"
Simu ikakatwa nikabaki nikiwa ninashangaa, sikujua maneno yote hayo yametokea wapi.
"Labda nimekosea, ila sauti mbona niyake?"
Nilizungumza huku nikiirudisha simu mezani nilipo itoa, nikaingia bafuni, nikaoga na kurudi chumbani. Nikakuta simu ikimalizia kuita na kukatika. Nikafungua kabati lenye nguo zetu, nikiwa ninaendelea kuchagua chagua nguo ya kuvaa, simu ikaita tena. Nikaipokea na kuiweka sikioni. Huku nikisubidia kuisiki sauti ya Blanka
"Eddy toka uje kuwaona wanao walivyo pendeza"
Haikuwa sauti ya Blanka bali ni Phidaya ndio alizungumza.
"Sawa nakuja"
Nikakata simu, nikamaliza kuva na kutoka sebleni. Nikawakuta Shamsa na Junio wakiwa wanapigwa pigwa picha na mama yao, kusema ukweli wamependeza sana.
"Kaa na wewe hapo niwapige picha"
Phidaya alizungumza, akiniomba nikae kwenye sofa walilo kaa Junio na Shamsa. Huku akiwa ameshika camera aina ya Cannon D7 tuliyo inunua kwa ajili ya kuchukua matukio baadhi katika siku ya kuzaliwa kwa Junio.
"Nitapigaje picha na nguo hizi?"
"Kwani zina nini, hembu kaa bwana"
"Haya mwaya mamyto"
Nikakaa katikati ya Shamsa na Junio. Phidaya akawa na kazi ya kutupiga picha huku, tukiwa tunabadilisha mikao tofauti tofauti.
"Hizi picha tunazitupia facebook"
Phidaya alizungumza huku akitufwata kwenye sofa tulilo kaa akituonyesha picha tulizo piga.
"Zimependeza"
Shamsa alizungumza huku akiwa na furaha sana, kwani nimeamua kuifanya familia hii kuishi kwa amani, chochote watakacho hitaji kutoka kwangu, wakipate kwa muda muafaka.
"Haya na wewe mamyto kaa niwapige picha"
Phidaya akakaa katikati yao, na mimi nikaanza kuwapiga picha huku nao wakibadilisha miako tofauti tofauti.
"Nizamu ya baba na mama"
Shamsa alizungumza huku, akinifwata nilipo simama.
"Ile laptop mumeifungua kwenye boksi lake"
"Bado"
"Itoe"
"Ngoja nikaichukue ipo chumbani kwa Junio"
Shamsa akaingia chumba cha Junio, akarudi akiwa na boksi lenye laptop tuliyo nunua. Akaitoa na kuiweka mezani. Nikampa kamera, tukapiga piçha kadhaa nikiwa na Phidaya kisha tukapiga tukiwa na mtoto wetu Junio.
"Yaani facebook leo watakoma"
"Kwà nza muna account ya hiyo facebook au unasema tu watawakoma"
"Nitafungua, mimi Eddy, nifungulie kwa jina gani?"
"Mr and Mrs Eddy"
"Jina gani hilo? Mwaya Shamsa fungua kwa jina la Eddy family"
Phidaya alipendekeza jina lake, lililo nilazimu mimi kulikubali tu kishingo upande. Tukamaliza kupiga piga picha, nikaingia ndani kujipumzisha huku nikiwaacha wao wakifanya shughuli zao.
***
Jioni Phidaya akaniamsha kwa ajili ya kupata chakula cha jioni. Nikatoka na kukuta Shamsa akichezea chezea laptop huku Junio akicheza game ya mpira kwa kutumia deki ya 'Play station 4' niliyo mnunulia kama moja ya njia ya kukuza kipaji chake cha kucheza mpira.
"Eddy njoo uone"
Shamsa aliniita kuangalia anacho kifanya kwenye laptop.
"Cheki hadi sasa hivi nina marafiki mia tano"
"Ahaaa mimi nilijua una kitu cha cha maana kumbe ni hao marafiki"
"Ndio wanaendelea kuniomba urafiki na kukoment kwenye picha zetu."
"Acheni munacho fanya ni muda wa msosi"
Nilizungumza huku nikiwatazama Junio na Shamsa.
"Huyo Junio wako hataki kubanduka kwenye hiyo tv na migemu yake"
"Junio, Junio"
Wala Junio hakunisikia ninavyo muita, nikatazama jinsi anavyo wachezesha wachezaji wa timu aliyo ichagua kwenye game hiyo. Nikamtazama mchezaji wake anayekwenda kufunga goli, kabla hajafika golini nikachukua rimoti ya tv na kuizima
"Dadyyyyyyyy"
"Ni muda wa kula"
"Nifainali dady"
"Eheee ni muda wa kula, utaendelea baadaye"
Ilibidi nimfokee kidogo Junio, taratibu akanyanyuka na kukaa kwenye meza ya chakula huku akiwa na sura ya kukasirika.
"Junio ukinuna unatisha"
Shamsa alimtania Junio na kumnya azidi kununa huku machozi yakimlenga lenga.
"Eddy umeniharibia mtoto"
"Kwa nini?"
"Amechukua hasira zako zote, japo ni mdogo ila kanajifanyaga kababe. Kalikua nakazi ya kupigana na wezake kule kambini"
"Kwangu atanyooka. Tena Junio ukiendea kununa, sikufanyii sherehe na vitu vyote navirudisha madukani tulipo vinunua"
"Am sorry dady"(Samahani baba)
"Nime kusamehee"
Furaha ya Junio ikarudi kama kawaida, Tukamaliza kula chakula.
"Asante dady"
"Asante Eddy na Mama"
Shamsa na Junio wakamaliza kula na kutushukuru, kila mmoja akarudi katika shuhuli yake. Tukasaidia na Phidaya kutoa vyombo tulivyo kula na kuvipekeka jikoni. Uzuri wa hotel hii, unaweza kujipikia chakula chako ukiwa unahitaji kufanya hivyo. Tukasaidiana kuviosha vyombo.
"Ehee niambie zile damu ulizitoa wapi?"
"Tutazumgumza kitandani"
"Sawa"
Tukamaliza kuonysha vyombo na kuvipanga vizuri, tukawaaga watoto wetu na kuingia chumbani wao wakaendelea na mambo wanayo yafanya.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni