SORRY MADAM (56)
Zephiline F Ezekiel
5 min read
SEHEMU YA HAMSINI NA SITA
ILIPOISHIA...
Nikamtazama machoni kwa macho ya dharau,kisha nikaupitisha katikati ya miguu yangu na akabaki akinitazama, Nikaizungusha miguu yangu na kuusababisha mkono kutoa mlio wa kuvunjika mifupa iliyopo kwenye mkono wake.NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Dericka akaendelea kulia huku akigaragara chini.Nikaibaeba sahani yenye vidole hadi jikoni,nikaweka kikaangio kwenye jiko la gesi na kuliwasha,nikamimina mafuta mengi ya kula kisha nikavidumbukiza vidole vyote kwenye kikaangio na kuongeza moto ili viive haraka na kurusi sebleni.
Sheila akanitazama huku machozi yakimwagika,Mlio wa simu kutoka kweney mfuko wa suruali ya Derick ukaanza kusikika.Nikaitoa simu yake ikiita na kukuta ni madam Mery ndio anapiga simu kwani imeandikwa ‘wife’ na pembeni kuna picha yake.Nikamtazama Sheila na kumfwata,nikamshika nywele za kichwa chake
“Sikia wewe Malaya,zungumza na huyu mjinga mwenzako.Jitambulishe kuwa wewe ni mke mwenzake sawa?”
Sheila akatingisha kichwa,simu ikakata na baada ya muda ikaanza kuita tena,Nikamtoa Sheila vitambaa mdomoni.
“Zungumza naye”
Nikaminya kitufe cha kupokea na kuiweka simu iwe kwa sauti kubwa(Laudspeker) na kuisikia sauti ya madam Mery ikaanza kuzungumza
“Haloo mume wangu”
“Wewe mshenzi nimekuambia achana na mpenzi wangu.”
“Kwani wewe ni nani na namba ya mume wangu umeipataje?”
“ Hadi hapo ujaelewa tuu,mimi ni mke mwezio”
“Jamani kwa nini uanifanyia hivyo wewe dada kumbe wewe ndio umeficha mume wangu wiki nzima harudi nyumbana”
“Mjini hapa”
Nikaikata simu na kuizima huku nikijiuliza maswali ni kwanini Madam Mery aliamua kurudia na mume wake baada ya tukio la kuuawa kwa mwanangu
“NA YEYE LAZIMA AFE”
Nilizungumza kwa sauti ya hasira huku nikimtazama Sheila,nikamdumbukiza tena Sheila vitambaa vya mdomoni.Nikakimbilia jikoni na kukuta vidole vya Derick vikiungulia kwenye mafuta,Nikazima jiko na kuvitoa kwenye vikaangio na kuviweka kwenye sahani,Nikaona nyanya mbili juu ya friji,nikazikataka kata vizuri na kurudi sebleni nikiwa nimeishika sahani,Nikaviweka juu ya meza na kumgeuza Derick aliye lala kifudi fudi akiugulia maumivu.
“Derick nimekukangia miskaki iliyonona,karibu ule”
Derick akanitazama kwa macho ya hasira,nikamuitamia na kuvitoa vitambaa mdomoni mwake kisha nikachukua kidole kimoja na kukikandamiza mdomoni mwake,Gafla akanitemea kidole usoni na kuzidi kunipandisha hasira na nikaanza kumshindilia ngumi za pua hadi ikatepereka na kumwaga damu nyingi.
Nikajibwaga kwenye sofa huku nikimtazama Derick nikifikiria nini cha kumfanya ili apate uchungu kama nilio upata mimi kipindi alipo muua mwanangu.Nikapata wazo ambalo likanifanya nisimame na kumburuza Derick hadi nje kisha nikarudi ndani na kumchukua Sheila na kumbeba begani,Nikafungua mlango wa gari na kumuingiza upande wa dereva huku mikono na miguu yake nikiwa bado nimeifunga kwa kamba.Nikaaingia ndani na kuchukua kishoka changu na kurudi nje nikamchukua Derick na kumlaza chini ya gari,nikaingia ndani ya gari na kuifungua mikono ya Sheila
“Washa gari lako”
Nilizungumza huku kishoka nikiwa nimekiweka kwenye shingo yake.Sheila akaanza kutetemeka na akafanya kama nilivyo muagiza
“Endesha gari lako umkanyage huyo mwehu wako”
Sheila akatingisha kichwa,akiashiria kukataa.Nikamtoa vitambaa ambavyo nilimsokomeza mdomoni
“Endesha gari”
“Huoni tutamuua”
Nikamzaba Sheila kofi la shavu,na kumfanya kuweweseka na akakanyaga mafuta na gari ikasogea mbele na kupanda kwenye mwili wa Derick kama imepata kwenye matuta yaliyo tengenezwa barabarani.Nikashuka kwenye gari na kumkuta Derick akiwa yupo katika hali mbaya,kwa kutumia kishoka changu nikamkata Derick kichwa chake na kukirusha ndani ya gari alipo Sheila na kumfaya akarupuke kwa woga
“Sheila Sali sala yako ya mwisho,unamfwata mwehu wako kuzimu”
Nilizungumza kwa sauti nzito isiyo na huruma hata kidogo
“Eddy ni nini kimekupata unakuwa naroho mbaya kiasi hicho”
Sheila alizungumza kwa woga huku akitetemeka,Nikapiga hatua za taratibu hadi sehemu aliyo simama pembezoni mwa gari,
“Wewe ni mtu wa kunisaliti mimi?”
Swali langu likamfanya Sheila kutingisha kichwani,Nikamshika mkono na kuanza kumburuza hadi tukaingia ndani na kumsukumia kwenye sofa
“Eddy,kumbuka mimi na wewe tumetoka mbali........nilikuwa nipo radhi kufa kwa ajili yako.Leo hii huioni dhamani yangu kwanini lakini Eddy”
Sheila alizungumza huku akiendelea kumwagikwa na machozi mengi,Hasiri ikazidi kunipanda kila nilipo kumbuka tukio la wao kukumbatia na Derick
“Eddy mimi nilijua kuwa wewe umeniacha,Tazama nilikuokoa kwenye ndege nikawa nipo tayari mimi kufa ili wewe upone,Ila hata siku moja sijakuona hospitalini.Niliiungua kwa ajili yako wewe.Ila dhamani yangu ipo wapi au kwa sababu mimi ni mwanamke ndio unaamua kuninyanyasa?”
Sheila alizidi kuzungumza kwa uchungu na kunifanya niwe kimya nikimtazama huku asira ikinishuka
“Eddy nipo tayari kufa,Nichinje kama ulivyo mchinja Derick,NICHINJE”
Sheila alinamisha kichwa chake mbele ya miguu yangu na kujikuta nikikinyanyua kishoka changu juu kwa hasira machozi yakinimwagika taratibu
“Eddy ,najua nitakwenda kuzimu kwa maana nimekukosea sana.Ila sistahili kuendelea kuishi mip tayari uniue.”
Nikakitupa kishoka kwa nguvu kwenye meza ya kioo hadi meza ikavunjika.Taratibu nikakaa chini huku nikimwagikwa na machozi,Sheila akainyanyua sura yake iliyo lowana machozi na kuniangalia kwa uchungu
“Eddy kwa nini umeua,ulishwa kutuambia kiustarabu”
Kiganja cha mkono wangu wa kulia kwa haraka kikatua shingoni mwa Sheila na kuanza kuibana kwa nguvu,mikono ya Sheila ikawa na kazi ya kuuzuia mkono wangu usiendelee kuibana shingo yake
“UNAMAJUA DERICK VIZURI WEWE?”
“Mm..mmmmmmmm.....?”
Nikaiachia Shingo ya Sheila na kumfanya asogee mbali kidogo na nilipo mimi.Ukimya ukatawala kati yetu huku ikisikika mihemo yangu ya hasira jinsi inavyo panda na kushuka.
“Eddy ninakupenda sana,tena sana.Maishani mwangu nilikuambia kuwa sijawahi kupenda mwanaume yoyote kama wewe.Umenifundisha mengi Eddy,Upendo,Ujasiri,Huruma......Ila mimi sio kosa langu kuwa na Derick”
“Ila?”
“Derick mimi alinisaidia sana kipindi nipo Kenya,Sikuwa na mtu wa kunilipia hata pesa ya hospitali ambayo nilikuwa ninatibiwa.Aliweza kunihudumia kwa kila jambo,alininunulia dawa za gharama kuwa zilizo nisaidia ngozi yangu kurudi katika hali ya kawaida kama awali.Nilikuwa nimebabuka mwili mzima mimi,nilikuwa sitamaniki na......”
“Ukaamua kumpa mwili wako?”
“Sio kama niliamua kumpa mwili wangu,Aliweza kunishawishi na wewe sikujua ni wapi ulipo.Nilijariu kukuulizia shule ambayo ulikuwa unasoma ila sikupata jibu”
Nikaachia tabasamu la dharau lililo jaa hasira nzito inayo ifanya royo yangu kutamani niyanyofoe masikio ya Sheila,nikawa ninajikaza nisifanye kitu ninacho kiwaza
“Tangu tupoteane,imepita kipindi gani?”
“Miezi mitatu”
“Ulishindwa kuzizuia hisia zako hadi utakapo niona?”
Sheila akaa kimya huku macho yake akiyakwepesha kukutana na macho yangu yalio jaa ukali kama chui aliye jeruhiwa mwili wake kwa risasi.
“Dawa yako ipo jikoni”
Nilizungumza huku nikinyanyuka na kwenda njee,Nikauvuta mwili wa Derick na kuutoa chini ya gari,Nikaurudi ndani na kumkuta Sheila akiwa amejinamia chini akilia
“Funguo ya handaki lako iko wapi?”
“Ndani?”
“Wapi?”
“Kwenye dreasing table yangu”
Nikamtazama Sheila kwa muda,nikafunga mlango wa kutokea nje kwa funguo zilizokuwa zikining’inia ndani ila kumfanya Sheila asikimbie kwenda sehemu yoyote.Nikaingia chumbani kwake na kuiona rimoti ndogoi iliyopo juu ya kakabati kake kadogo kalicho jaa vipodozi.Nikaichukua kabla sijaondoka kwa bahati mbaya nikaangusha kichupa cha mafuta,nikakiokota na kukirudisha juu sehemu kilipo kuwa ambapo chini yake kuna karatasi iliyo geuzwa upande wa pili ambao hauna maandishi yoyote,Nikaichukua karatasi na kuigeuza upande wa pili
Nikaanza kusoma maandishi yaliyo andikwa kwa muandiko wa kulala na juu yake kuna jina la hospitali ambayo dokta huyo ndio ameandika vipimo vilivyo anza kuufanya mwili wangu kurudi katika hali ya hasira kali.Vipimo alivyo viandika daktari vinaonyesha Sheila ni mjamzito wa mimba ya wiki mbili na kwa pembeni yake baba wa mtoto ni Derick Malki
“ANAMIMBA YA DERICK....?”
Nilijiuliza swali ambalo jibu lake ninalo kichwani,Nikiwa ninaendelea kuitazama karatasi yangu ni kama Mungu aliye niambia nitazame kwenye kioo,Nikauona mkono wa Sheila akiwa ameunyanyua juu huku akiwa ameshika kishoka nilicho kuwa nacho mimi.Nikakikwepa na kuruka pembeni,Sheila akakirusha kishoka,nikainama na kikanikosa na kutua kitandani.Kama gari iliyo poteza breki zake,nikajirusha na kwakutumia bega langu la mkono wa kulia,likatua tumboni mwa Sheila na sote tukaanguka chini,Sheila akaanza kutoa kilio cha maumivu.Nikainyanyua ngumi yangu na kushusha kwa kasi na kabla haijafika usoni mwake nikaisimamisha na kumtazama jinsi alivyo fumba macho akiogopa mzigo utakao shuka kwenye uso wake
“UNATAKA KUNIUA WEWE MALAYA SI NDIO?”
Sheila hakunijibu chochote zaidi ya kuwa kimya.Nikampiga vibao vinne vya mashavu ili kuiweka akili yake sawa.
“Upendo wangu kwako usije ukageuka ukawa kifo chako,Sheila....nimezaliwa siku moja nia nitakufa siku moja,Hakuna kama mimi Eddy na hatotokea kama mimi.PUMBAVU”
Nikamalizia na kibao cha tano kilicho mfanya azidi kuwagikwa na machozi.Nikamnyanyua na kumuweka begani nikakichukua kishoka changu na tukatoka nje.Nikambwaga kwenye sofa kama zigo wa kuni na kabla sijatoka nje Sheila akaniita
“Nini?”
“Naomba unisamehe,haikuwa akili zangu”
“Zilikuwa akili za nani?”
“Ni shetani amenipitia,nikatamani kukuua”
Sheila alizungumza huku akiwa amejishika tumbo lake.
“Sheila mimi sina roho mbaya,ila inapobidi niwe na roho mbaya itakuwa.Mimi siwezi kumuua mtoto wa Derick uliye naye tumboni kama yeye alivyo fanya kwa mwanangu”
Sheila akakosa la kuzungumza na mimi,nikaufungua mlango na nikatoka nje,Kwa kutumia kirimoti nikaufungua mlango wa handaki na kisha nikabeba mwili wa Derick hadi ndani.Nikarudi juu na kuchukua kicha chake na kuingia nacho ndani.Nikalichunguza handaki na kugundua lina majiko mengi ya umeme ambayo yana sehemu ya kuwokea mikate.Nikaisogeza meza kubwa iliyipo pembeni yangu na nikauweka mwili wa Derick juu
“Eddy”
Sauti ya Sheila ikanifanya nimgeukie,Akainisogelea karibu na kunishika mkono wenye kishoka
“Hii roho ya kikatili umeitoa wapi?”
“Kwenye kazi zangu huwa sihitaji kuingiliwa,Ondoka kabla sijafanya maamuzi mabaya kwako”
“Eddy,mimi ndio nilikuwa ninakupunguza hasira zako.Hakuna mwanamke ambaye aliweza kufanya hivyo kama si mimi au mama yako”
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni