Notifications
  • MY DIARY (10)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KUMITULIPOISHIA...Nikamwambia Joyce ndo maana mimi nakupendaga. Nikamwambia “nitakuapa feedback ngoja nimpigie asije akaja na makufuli yake leo hii. Nikampigia baba mwenye nyumba eti kwa kujiamini kabisa akapokea nakusema “ Halow mrembo” Nikamwambia Yes mpenzi kitu ambacho kilimfurahisha sana..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Kuokoa hela ya vocha nikamwambia nimekubali ombi lako alafu nikakata…
  • MY DIARY (9)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TISATULIPOISHIA...Basi Dj wangu aliendelea na mautundu yake akaniwekea mambo ya pwani na hapo ndipo uvumilivu ulipomshinda akaja kunibambia na mimi sikuona haja ya kumbania kwa kuwa ni mali zake mwenyewe. Nilizungusha nyonga na kiuno mpaka nikachoka nikajitupa kitandani ili nipumzike. Nafsi yake ilikuwa imeridhika kwani hakutka tena penzi bali alichukua lap top yake na kuanza kunionesha picha na vitu vingine ambavyo vilinipa raha.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA…
  • MY DIARY (8)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NANETULIPOISHIA...Sijui hata haya maneno yalitoka wapi, fahamu zilinitoka na Ticha aliamua kuninyanyasa maana nilishajikojolea zaidi ya mara tano. Basi na yeye kwa kutafuta mbwembwe alianza yale mambo yao ya katerero, siunajua tena mwalimu John alitokea pande za Bukoba.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinichezea sana na baadaye nilishangaa kukuta jamaa ameshaingiza kunako. Sikujielewa kwa…
  • MY DIARY (7)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SABATULIPOISHIA...Kwaito zilivyonoga uzalendo ulinishinda nikajikuta na mimi nashuka ngazi kuelekea chini sehemu ya kuchezea.Nilizijua kwani shuleni tulikuwa tunazicheza sana hasa kwenye yale madisco yetu ya mwisho wa mwezi.John wangu alibaki juuu akiniangalia jinsi nilivyokuwa nikicheza vizuri.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Yeye alishindwa kushuka akiofika kile kitu kukaliwa na watu…
  • MY DIARY (6)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA SITATULIPOISHIA...Akanambia kuwa wamemwambia wapo East Africa Pub na tayari wamaeshaagiza mkuu wa mbuzi. Mmmmhhhh kusikia mguu wa mbuzi mate yalinijaa mdomoni. Basi kwa harakaharaka nikamwambia naomba niende niende nyumbani nikachukue viwalo vya club kisha nitawakuta hapo.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alinambia mbona hizo nguo ulizofaa zipo poa tu wewe twende hivyo bhana si upo na…
  • MY DIARY (5)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TANOTULIPOISHIA...Akanisimamisha na kuanza kuiuliza maswali mengi yasiyo na maana huko akionekana kutojiamini. “samahani dada, sijui unaelekea wapi”? Nikamjibu dukani. Akavuta pumzi ndefu na kuniambia ok, nisaidie namba zako za simu. Nikamwangalia juu na chini nikwambaia nimezisahau na simu nimeiacha ndani nikirudi ndani nitakuletea..IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Akaishiwa pozi akanambia,…
  • MY DIARY (4)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA NNETULIPOISHIA...Uchambuzi huu ulinigusa sana kwani hata mimi nilijihisi kuwa sikuwa na utando huo yaani bikira japo nilikuwa sijawahi kujamiana na mwanaume wa aina yeyote zaidi ya ile michezo ya utotoni ya kula mbakishie baba au ile ya kibabababa na kimamamama. Alianza kunishika mapajani na kunifanya nianze kusisimuka ajabu kwani japo alikuwa ni mwanaume mikono yake likuwa ni milani sana kama ya mtoto wa kike.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media…
  • MY DIARY (3)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA TATUTULIPOISHIA...Nazani sasa unanielewa ninaposema nilikuwa sina ndugu kwani baba yangu hakuwa na ndugu yeyeote zaidi ya marafiki ambao na wao kwa sasa ndio hao wameshagawana mali zote. Nimebaki mimi na dunia yangu hivyo basi nilimwomba rafiki yangu wa kufa na kuzikana kwa jina Joyce anisaidie kunisitiri nyumbani kwao.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Likizo ilipoisha tulirusi shuleni na…
  • MY DIARY (2)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA PILITULIPOISHIA...Kwa ufupi japo sitaki kueleza historia yake ila kwa sasa ni shoga na teja. Baba yetu alitupenda sana na alihakikisha tunapata elimu nzuri na bora. Mimi na kaka yangu wote tulisoma International school ya hapo Moshi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baadaye kaka yangu alianza kuvuta bangi kitu ambacho kilimtia hofu baba yangu na kuamua kumpeleka kusoma nje ya nchi.Alikosea sana…
  • MY DIARY (1)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA KWANZANilikuwa juu ya jukwaaa nikifanya vitu vyangu ili hali nikijua kabisa watu wote waliokuwa wakinitizama walikuwa wanaumia roho kutokana na mvuto wa umbo langu niliokuwa nao. Nilisikia mijibaba miwili ikiulizana hivi lile wowoo ni la kwake au ni la mchina? Mmoja wao akaropoka “wee kitu original hicho,kwani umemsaahau huyu binti tulishakutana nae kule Arusha mpaka tukambatiza jina la soda kubwa tena ya fanta yaani BAMBUCHA.?” Yeah nimekumbuka alidakia…

SORRY MADAM (57)

SEHEMU YA HAMSINI NA SABA
ILIPOISHIA...
“Hii roho ya kikatili umeitoa wapi?”
“Kwenye kazi zangu huwa sihitaji kuingiliwa,Ondoka kabla sijafanya maamuzi mabaya kwako”
“Eddy,mimi ndio nilikuwa ninakupunguza hasira zako.Hakuna mwanamke ambaye aliweza kufanya hivyo kama si mimi au mama yako”

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
“Mama anakutaka uende nyumbani,amekutafuta kwa kipindi pasipo mafanikio yoyote.Nakuomba twende sote kwa mama leo”
Nikayatazama macho ya Sheila na kuyaona yanamaanisha kitu anacho kizungumza.
“Rudi ndani?”
“Unataka kuufanya nini huo mwili?”
“Rudi ndani usiniulize chochote”

Sheila taratibu akasogea pembeni yangu.Pasipo kuwa na haruma nikaanza kuucharanga kwa kishoka mwili wa Derick,Nikaufanya mwili wa Derick kuwa katika vipande vipande.Nikaliwasha jiko kubwa lenye visahani vinne vya kupikia.Nikaviingiza vipande vya mwili wa Derick.
“MUNGU ninaomba unisamehe katika hili”

Niliomba sala ya msamaha kwa Mungu wangu,Nikaifanya kazi yangu ya kuvikausha vipande vya mwili wa Derick hadi nikamalizia na kichwa chake kwa kukipasua.Nikaviweka kwenye turubai kubwa la kufunikia gari la Sheila kisha nikatoka nje,Nikamkuta Sheila kusafisha sehemu zote zenye damu.Macho ya Sheila yamevimba kidogo kwa kulia huku mashavu yake yakiwa na alama za vidole vyangu
“EDDY,hii ni siri kati yangu mimi na wewe.”
“Ukiitoa nikufanye nini?”
“Nifanye chochote upendacho”
“Sawa”

Tukasaidia kufamya usafi,Nilipo hakikisha hakuna uchafu wa ina yoyote tukarudi ndani na Sheila akawa wa kanza kuoga kisha nikafwatia na mimi,nikavaa suruali ya Sheila ambayo inanitosha na tisheti yake hii ni kutokana na kutokuwa na nguo.Mida ya saa mbili usiku tukafunga safari hadi nyumbani kwa mama,Sheila akapiga honi na geti la nyumba likafungulia na akaingiza gari hadi sehemu ambayo kuna magari yetu mengine.Nikashuka ndani ya gari ila Sheila akaniomba atangulie.Akaufungua mlango na kuanza kumuita mama ambaye niliisikia sauti yake akiitika.
“Ohoo karibu mwanangu”

Nikawachungulia ndani na kumuona Sheila akikumbatiana na mama.Nikaingia na kumfanya mama kunishangaa kwa muda huku akionekana kama kuto amini kwa kile anacho kiona mbele yake.Kwa Furaha mama akanikumbatia na sote machozi yakaanza kunimwagika.Mama akanikaribisha ndani huku akiwa na furaha kubwa
“Mwanangu Eddy ndio umevaa nini?”
Mama alinitazama kuanzia juu hadi chini na kumfanya Sheila kucheka
“Nimempisha pamba zangu zimemtoa chikopa kama nini?”
“Mwanangu ungekuwa mwanamke ungevutia kama nini”
“Mama.....!!”
“Ndio....ila ndio hivyo umezaliwa dume la mbegu”

Mama akatukaribisha mezani na kutakapa chakula cha usiku.Kutokana na mawazo mengi sikuweza kuzungumza sana na mama.Nikapanda gorofani kulala,nikajitupa kitandani ila usingizi haukunichukua kabisa.Tukio la uuwaji wangu wa kikatilii ulianza kunisumbua sana akilini mwangu.Taswira ya madam Mery ikaanza kukisumbua kichwa changu,Nikanyanyuka na kwenda cumbani kwa mama.Niifungua droo yake ambayo anahifadhia astola yeke.Kwa bahati nzuri nikaikuta.
Nikaitazama na kuikuta na risasi za kutosha,Nikafungua droo nyingine na kukuta pesa za kutosha,Nikachukua kibunda kimoja na sikujua idadi ya pesa iliyopo.Nikashusha pumzi vya kutosha,nikatoka chumbani kwa mama nikiwa ninakatiza kwenye kordo nikirudi chumbani kwangu nikayasikia mzungumzo ya mama na Sheila

“Wee unataka kuniambia kuwa mwangu amekuwa na roho mbaya kiasi hicho?”
“Ndio mama,Mbele ya macho yangu amemuua mwanaume mmoja ambaye anadai kuwa alimuulia mtoto wake”
“Mtoto?”
“Ndio mtoto ila sijajua huyo mtoto amezaa na mwanamke gani?”
“Ina maana Eddy alikuwa na manamke mwengine zaidi yako?”
“Ndio mama,Imeniuma sana mama yangu”
“Ila mama chonde chonde ninakuomba usimuambie Eddy chochote kwa maana,amekuwa kama mtu aliye changanyikiwa”
“NANI KACHANGANYIKIWA”
Nilishindwa kuvumilia ikanibudi nizungumze,taratibu nikiwa ninashuka kwenye ngazi na mkononi nikiwa nimeshika bastola na kuwafanya mama na Sheila kustuka

Sheila kwa haraka akarudi nyuma ya mama na kujificha,Mama akanitazama kwa macho yaliyo jaa mshangao
“Eddy mwanangu unataka kufanya nini?”
“Nataka kujua huyu mwanamke kwa nini amesema kuwa mimi nimechanganyikiwa”
“Hujachanganyikiwa mwanangu,tulikuwa tunazungumza kuhusiana na baba yako mzee Godwin kwamba amechanganyikiwa”
“Mama na wewe unashiriki zambi ya uongo?”
“Kweli mwanangu,aliniambia kuwa amemuona sehemu fulani katikati ya jiji akiwa anaruka ruka”

Nikamtazama mama kisha nikakaa kwenye sofa na kuiweka bastola pembeni yangu.Sheila akabaki akinitazama huku akiwa hana la kuzungumza.Wote wakaka na kunitazama,ukimya ukatawala ndani ya dakika kadhaa mama akaamua kuuvunja ukimya.
“Eddy na hiyo bastola yangu unakwenda nayo wapi?”
“Kuna kazi ninataka kwenda kuifanya”
“Eddy mwanangu,hembu niambie ni nini tatizo linalo pelekea kuwa na roho kama hiyo kwa maana umerudi hujazungumza na mimi vitu vingi zaidi ya kwenda kulala?”
“Mama bado mimi nipo,tutazaungumza kila kitu”
“Sawa,ila kwanini ume......”

Nikauona mguu wa Rahma ukiukanyaga mguu wa mama na kumfanya asiimalizie sentesi yake.
“Kwa nini umekaa huko mbali pasipo kuwa kunijulisha?”
“Huyo hajakuambia?”
“Yeye atajuaje mtoto wa watu?”
“Ahaa mama hiyo mada tutazungumza kesho.Oya ninaomba funguo”
“Za nini?”

Sheila alizungumza kwa sauti ya upole na yenye unyeyekevu mkubwa
“Funguo za gari na nyumba yako.”
Sheila akafungua pochi yake na kunipa.
“Mbona umevaa nguo hizo hizo ulizo kuja nazo?”
Nikajitazama kuanzia chini hadi juu,nikarudi chumbani kwangu na kuvaa nguo zangu vizuri,nikaichomeka bastola kiunoni mwangu na kuifunika na tisheti nyeusi niliyo ivaa,nikurudi sebleni.
“Wewe twende basi home”

Sheila akatazama na mama kisha akanitazama na mimi
“Mmmm nitalala na mama”
“Hutaki au?”
“Eddy muache mwenzako alale hapa,kwani huku kwake unakwenda kufanya nini?”
“Kulala”
Nikataka kutoka na mama akaniita
“Bastola yangu ipo wapi?”
“Nimeirudisha”
“Wapi?”
“Kwani mama ilikuwa wapi?”
“Basi baba nenda salama”

Nikatoka na kuufunga mlango vizuri.Nikasimama pembeni ya dirisha na kusikilizia ni nini mama na Sheila watakizungumza,kwa kupitia uwazi ulioachwa na dirisha nikawaona wakikaa kwenye sofa
“Mbona mwanangu amebadilika namna hii?”
“Mama wee acha tuu,Eddy mimi ninampenda ila kwa hapa alipo fikia ninamuogopa mama”
“Mmmm usimuogope”
“Mama Eddy kuna kipindi alipokuwa na hasira mimi nilikuwa nikimtuliza na kumsogelea,ila sasa hivi mmmmmm ni bora nimtoroke toroke hadi atakapo kaa sawa”
“Itabidi nitafute madaktari watakao muhudumia”
“Ni kweli mama,yaani mtu anazungumza kwa sauti nzito kama simba dume”
“Ila mwanangu huyu anaugonjwa wa asira,mimi wala simshangai sana kwani kuna kipindi akiwa mdogo alisha wahi kumuua mwenzake shule kwa kumpiga na chupa ya soda kichwani”
“Weeeee?”
“Ooohhh ilikuwa ni kesi kubwa kilicho muokoa ni udogo wake kwa alikuwa na miaka mitano”
“Mama ina maana Eddy kuua hakuanza leo?”
“Eddy mwangu akiwa na hasira si mtu wa kumsogelea,nilisha mpeleka hadi kwa wachungaji wamuombee ila wapii.Nilijaribu kutafuta wana saikology labda wakae nao ila imeshindikana.Kila dawa ambayo niliambiwa inafaa kwa kipindi hicho kuwa kama kitulizo cha ugonjwa wake ila wapi?”
“Mmmm”
“Yaani na haya matatizo yaliyo tokea hichi kipindi cha hivi karibuni naona pia yanachangia sana”

Nikataka kuondoka niwahi ninapotaka kwenda ila swali la Sheila likanifanya nipige hatua kadhaa kurudi dirishani
“Kweli mama,Hivi mzee Godwin yupo wapi?”
“Hadi leo sijamuona,Mimi mwenyewe ninafanya uchunguzi nije kumuona ila hadi sasa hivi sijapata jibu”
“Mama tutasaidiana katika hilo,yule mzee ni muuaji sana”

Sikuona haja ya kuendelea kusikiliza mazungumzo yao zaidi ya mimi kuondoka,Nikaingia ndani ya gari na mlinzi akanifungulia geti na kuondoka,Nikafika kwenye kituo cha kuongeza mafuta.Nikajaza tanki la gari na kulipa kiasi ambacho kimegharimu kiasi hicho cha mafuta.Njia nzima nikawa ninafikiria ni wapi alipo Mzee Godwin.Nikafika nyumbani kwa Sheila na kushuka kwenye gari na kufungua geti,nikaliingiza gari ndani na kufunga geti.Nikafungua ndani na kuchukua kirimoti cha kufungulia sehemu ya kuifadhia gari,Nikaingia na kuchukua turubai lenye mwili wa Derick ambao niliubanika vizuri

Nikauingiza ndani ya buti la gari na kulifunga vizuri,nikafunga kila sehemu kama nilivyo iacha,kabla sijatoka nikakumbuka simu ya Derick niliiacha sofa nikiwa nimeizima,Nikaingia ndani na kuichukua ila sikuiwasha,Nikafungua geti na kutoa gari.Nikarudi kulifunga na safari ya kuelekea Arusha ikaanza,Kutokana ni usiku sana hapana magari mengi zaidi ya maroli ya mizig ambayo yanakwenda kwa kasi na usipo kuwa makini utajikuta ukigongwa.Nikazidi kuongeza mwendo na kimoyo moyo nikawa na kazi ya kumuomba Mungu nisipate ajali kwani mwendo ninao tembea nao endapo nitakubwa hata na baiskeli basi kitakaocho endelea kwenye kuanguka nahisi kitakuwa ni kifo tu.Kwa hofu nikapunguza mwendo kutoka spidi 250 hadi mia moja japo gari bado ipo kwenye mwendo mkali sana.

Mwanga mkali wa gari linalokuja nyuma yangu ukaanza kuniumiza macho,Nikapunguza mwendo na kumuwashia taa nikimuashiria apite kwani sikuweza kuendesha kwa jinsi taa zake zinavyo niumiza macho kupitia vioo vya pembeni.Nikashuhudia gari aina ya ‘HAMMER’ yenye rangi nyeusi na vioo vyake vyote vikiwa ni vyeusi na limefungwa likinipita,Haikuwa ni moja zikapita nyingine mbili zikiwa katika kwendo kama ilivyo gari ya kwanza
“Mmmmmm ni kina nani hawa?”

Nilijiuliza maswali,Na mimi nikaanza kuongeza mwendo wa gari langu.Jinsigari hizi zinavyozidi kwenda ndivyo nami nilivyodidi kuongeza mwendo,Nikaanza kuzikaribia kwa karibu.Nikawasha taa zote za gari langu ili na mimi nimtese dereva wa gari la nyuma.Nikashanga kuona gari mbili za nyuma zikitanda barabarani na kunizuia kupita.Nikaanza kupatwa na mashaka baada ya madereva hao kuanza mtindo wa kupunguza punguza mwendo gafla gafla na usipo kuwa makini unazigonga kwa nyuma.
Kwa mbele likawa linakuja lori ikatulazimu sote kubana upande mmoja kuliacha lipite na mchezo ukarudi na kuwa wa kuzuiana kupita.Hadi tunafika daraja la wami ndio gari hizo zikapunguza mwendo kulikwepa fuso lililo haribika pembezoni mwa barabara

Tukalimaliza daraja,nikaona jamaa wananichelewesha nikamuomba dereva wa nyuma kuweza kupita akaniruhusu,Nikiwa ninamaliza kuliacha gari la nyuma gari la pili kutoka mbele likatanda barabarani na kuongeza mwendo.Dereva wa gari la nyuma akaongeza kasi zaid na kutanda kwa nyuma wakawa wameniweka katikati.Kwenye kioo kidogo kilichopo pembeni ya mskani kwenye gari langu nikaanza kuwaka taa nyekundu na kutoa maandishi yaliyo andikwa kwa herufi kubwa.

{HABARI YAKO BWANA EDDY, GARI YAKO IPO KWENYE WAKATI MGUMU WA USALAMA.KAMA UNATAKA ULINZI MINYA HAPA AU UNAWEZA KUKATA}


KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
37 Simulizi Sorry Madam
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni