SORRY MADAM (57)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA HAMSINI NA SABA
ILIPOISHIA...
“Hii roho ya kikatili umeitoa wapi?”
“Kwenye kazi zangu huwa sihitaji kuingiliwa,Ondoka kabla sijafanya maamuzi mabaya kwako”
“Eddy,mimi ndio nilikuwa ninakupunguza hasira zako.Hakuna mwanamke ambaye aliweza kufanya hivyo kama si mimi au mama yako”
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
“Mama anakutaka uende nyumbani,amekutafuta kwa kipindi pasipo mafanikio yoyote.Nakuomba twende sote kwa mama leo”
Nikayatazama macho ya Sheila na kuyaona yanamaanisha kitu anacho kizungumza.
“Rudi ndani?”
“Unataka kuufanya nini huo mwili?”
“Rudi ndani usiniulize chochote”
Sheila taratibu akasogea pembeni yangu.Pasipo kuwa na haruma nikaanza kuucharanga kwa kishoka mwili wa Derick,Nikaufanya mwili wa Derick kuwa katika vipande vipande.Nikaliwasha jiko kubwa lenye visahani vinne vya kupikia.Nikaviingiza vipande vya mwili wa Derick.
“MUNGU ninaomba unisamehe katika hili”
Niliomba sala ya msamaha kwa Mungu wangu,Nikaifanya kazi yangu ya kuvikausha vipande vya mwili wa Derick hadi nikamalizia na kichwa chake kwa kukipasua.Nikaviweka kwenye turubai kubwa la kufunikia gari la Sheila kisha nikatoka nje,Nikamkuta Sheila kusafisha sehemu zote zenye damu.Macho ya Sheila yamevimba kidogo kwa kulia huku mashavu yake yakiwa na alama za vidole vyangu
“EDDY,hii ni siri kati yangu mimi na wewe.”
“Ukiitoa nikufanye nini?”
“Nifanye chochote upendacho”
“Sawa”
Tukasaidia kufamya usafi,Nilipo hakikisha hakuna uchafu wa ina yoyote tukarudi ndani na Sheila akawa wa kanza kuoga kisha nikafwatia na mimi,nikavaa suruali ya Sheila ambayo inanitosha na tisheti yake hii ni kutokana na kutokuwa na nguo.Mida ya saa mbili usiku tukafunga safari hadi nyumbani kwa mama,Sheila akapiga honi na geti la nyumba likafungulia na akaingiza gari hadi sehemu ambayo kuna magari yetu mengine.Nikashuka ndani ya gari ila Sheila akaniomba atangulie.Akaufungua mlango na kuanza kumuita mama ambaye niliisikia sauti yake akiitika.
“Ohoo karibu mwanangu”
Nikawachungulia ndani na kumuona Sheila akikumbatiana na mama.Nikaingia na kumfanya mama kunishangaa kwa muda huku akionekana kama kuto amini kwa kile anacho kiona mbele yake.Kwa Furaha mama akanikumbatia na sote machozi yakaanza kunimwagika.Mama akanikaribisha ndani huku akiwa na furaha kubwa
“Mwanangu Eddy ndio umevaa nini?”
Mama alinitazama kuanzia juu hadi chini na kumfanya Sheila kucheka
“Nimempisha pamba zangu zimemtoa chikopa kama nini?”
“Mwanangu ungekuwa mwanamke ungevutia kama nini”
“Mama.....!!”
“Ndio....ila ndio hivyo umezaliwa dume la mbegu”
Mama akatukaribisha mezani na kutakapa chakula cha usiku.Kutokana na mawazo mengi sikuweza kuzungumza sana na mama.Nikapanda gorofani kulala,nikajitupa kitandani ila usingizi haukunichukua kabisa.Tukio la uuwaji wangu wa kikatilii ulianza kunisumbua sana akilini mwangu.Taswira ya madam Mery ikaanza kukisumbua kichwa changu,Nikanyanyuka na kwenda cumbani kwa mama.Niifungua droo yake ambayo anahifadhia astola yeke.Kwa bahati nzuri nikaikuta.
Nikaitazama na kuikuta na risasi za kutosha,Nikafungua droo nyingine na kukuta pesa za kutosha,Nikachukua kibunda kimoja na sikujua idadi ya pesa iliyopo.Nikashusha pumzi vya kutosha,nikatoka chumbani kwa mama nikiwa ninakatiza kwenye kordo nikirudi chumbani kwangu nikayasikia mzungumzo ya mama na Sheila
“Wee unataka kuniambia kuwa mwangu amekuwa na roho mbaya kiasi hicho?”
“Ndio mama,Mbele ya macho yangu amemuua mwanaume mmoja ambaye anadai kuwa alimuulia mtoto wake”
“Mtoto?”
“Ndio mtoto ila sijajua huyo mtoto amezaa na mwanamke gani?”
“Ina maana Eddy alikuwa na manamke mwengine zaidi yako?”
“Ndio mama,Imeniuma sana mama yangu”
“Ila mama chonde chonde ninakuomba usimuambie Eddy chochote kwa maana,amekuwa kama mtu aliye changanyikiwa”
“NANI KACHANGANYIKIWA”
Nilishindwa kuvumilia ikanibudi nizungumze,taratibu nikiwa ninashuka kwenye ngazi na mkononi nikiwa nimeshika bastola na kuwafanya mama na Sheila kustuka
Sheila kwa haraka akarudi nyuma ya mama na kujificha,Mama akanitazama kwa macho yaliyo jaa mshangao
“Eddy mwanangu unataka kufanya nini?”
“Nataka kujua huyu mwanamke kwa nini amesema kuwa mimi nimechanganyikiwa”
“Hujachanganyikiwa mwanangu,tulikuwa tunazungumza kuhusiana na baba yako mzee Godwin kwamba amechanganyikiwa”
“Mama na wewe unashiriki zambi ya uongo?”
“Kweli mwanangu,aliniambia kuwa amemuona sehemu fulani katikati ya jiji akiwa anaruka ruka”
Nikamtazama mama kisha nikakaa kwenye sofa na kuiweka bastola pembeni yangu.Sheila akabaki akinitazama huku akiwa hana la kuzungumza.Wote wakaka na kunitazama,ukimya ukatawala ndani ya dakika kadhaa mama akaamua kuuvunja ukimya.
“Eddy na hiyo bastola yangu unakwenda nayo wapi?”
“Kuna kazi ninataka kwenda kuifanya”
“Eddy mwanangu,hembu niambie ni nini tatizo linalo pelekea kuwa na roho kama hiyo kwa maana umerudi hujazungumza na mimi vitu vingi zaidi ya kwenda kulala?”
“Mama bado mimi nipo,tutazaungumza kila kitu”
“Sawa,ila kwanini ume......”
Nikauona mguu wa Rahma ukiukanyaga mguu wa mama na kumfanya asiimalizie sentesi yake.
“Kwa nini umekaa huko mbali pasipo kuwa kunijulisha?”
“Huyo hajakuambia?”
“Yeye atajuaje mtoto wa watu?”
“Ahaa mama hiyo mada tutazungumza kesho.Oya ninaomba funguo”
“Za nini?”
Sheila alizungumza kwa sauti ya upole na yenye unyeyekevu mkubwa
“Funguo za gari na nyumba yako.”
Sheila akafungua pochi yake na kunipa.
“Mbona umevaa nguo hizo hizo ulizo kuja nazo?”
Nikajitazama kuanzia chini hadi juu,nikarudi chumbani kwangu na kuvaa nguo zangu vizuri,nikaichomeka bastola kiunoni mwangu na kuifunika na tisheti nyeusi niliyo ivaa,nikurudi sebleni.
“Wewe twende basi home”
Sheila akatazama na mama kisha akanitazama na mimi
“Mmmm nitalala na mama”
“Hutaki au?”
“Eddy muache mwenzako alale hapa,kwani huku kwake unakwenda kufanya nini?”
“Kulala”
Nikataka kutoka na mama akaniita
“Bastola yangu ipo wapi?”
“Nimeirudisha”
“Wapi?”
“Kwani mama ilikuwa wapi?”
“Basi baba nenda salama”
Nikatoka na kuufunga mlango vizuri.Nikasimama pembeni ya dirisha na kusikilizia ni nini mama na Sheila watakizungumza,kwa kupitia uwazi ulioachwa na dirisha nikawaona wakikaa kwenye sofa
“Mbona mwanangu amebadilika namna hii?”
“Mama wee acha tuu,Eddy mimi ninampenda ila kwa hapa alipo fikia ninamuogopa mama”
“Mmmm usimuogope”
“Mama Eddy kuna kipindi alipokuwa na hasira mimi nilikuwa nikimtuliza na kumsogelea,ila sasa hivi mmmmmm ni bora nimtoroke toroke hadi atakapo kaa sawa”
“Itabidi nitafute madaktari watakao muhudumia”
“Ni kweli mama,yaani mtu anazungumza kwa sauti nzito kama simba dume”
“Ila mwanangu huyu anaugonjwa wa asira,mimi wala simshangai sana kwani kuna kipindi akiwa mdogo alisha wahi kumuua mwenzake shule kwa kumpiga na chupa ya soda kichwani”
“Weeeee?”
“Ooohhh ilikuwa ni kesi kubwa kilicho muokoa ni udogo wake kwa alikuwa na miaka mitano”
“Mama ina maana Eddy kuua hakuanza leo?”
“Eddy mwangu akiwa na hasira si mtu wa kumsogelea,nilisha mpeleka hadi kwa wachungaji wamuombee ila wapii.Nilijaribu kutafuta wana saikology labda wakae nao ila imeshindikana.Kila dawa ambayo niliambiwa inafaa kwa kipindi hicho kuwa kama kitulizo cha ugonjwa wake ila wapi?”
“Mmmm”
“Yaani na haya matatizo yaliyo tokea hichi kipindi cha hivi karibuni naona pia yanachangia sana”
Nikataka kuondoka niwahi ninapotaka kwenda ila swali la Sheila likanifanya nipige hatua kadhaa kurudi dirishani
“Kweli mama,Hivi mzee Godwin yupo wapi?”
“Hadi leo sijamuona,Mimi mwenyewe ninafanya uchunguzi nije kumuona ila hadi sasa hivi sijapata jibu”
“Mama tutasaidiana katika hilo,yule mzee ni muuaji sana”
Sikuona haja ya kuendelea kusikiliza mazungumzo yao zaidi ya mimi kuondoka,Nikaingia ndani ya gari na mlinzi akanifungulia geti na kuondoka,Nikafika kwenye kituo cha kuongeza mafuta.Nikajaza tanki la gari na kulipa kiasi ambacho kimegharimu kiasi hicho cha mafuta.Njia nzima nikawa ninafikiria ni wapi alipo Mzee Godwin.Nikafika nyumbani kwa Sheila na kushuka kwenye gari na kufungua geti,nikaliingiza gari ndani na kufunga geti.Nikafungua ndani na kuchukua kirimoti cha kufungulia sehemu ya kuifadhia gari,Nikaingia na kuchukua turubai lenye mwili wa Derick ambao niliubanika vizuri
Nikauingiza ndani ya buti la gari na kulifunga vizuri,nikafunga kila sehemu kama nilivyo iacha,kabla sijatoka nikakumbuka simu ya Derick niliiacha sofa nikiwa nimeizima,Nikaingia ndani na kuichukua ila sikuiwasha,Nikafungua geti na kutoa gari.Nikarudi kulifunga na safari ya kuelekea Arusha ikaanza,Kutokana ni usiku sana hapana magari mengi zaidi ya maroli ya mizig ambayo yanakwenda kwa kasi na usipo kuwa makini utajikuta ukigongwa.Nikazidi kuongeza mwendo na kimoyo moyo nikawa na kazi ya kumuomba Mungu nisipate ajali kwani mwendo ninao tembea nao endapo nitakubwa hata na baiskeli basi kitakaocho endelea kwenye kuanguka nahisi kitakuwa ni kifo tu.Kwa hofu nikapunguza mwendo kutoka spidi 250 hadi mia moja japo gari bado ipo kwenye mwendo mkali sana.
Mwanga mkali wa gari linalokuja nyuma yangu ukaanza kuniumiza macho,Nikapunguza mwendo na kumuwashia taa nikimuashiria apite kwani sikuweza kuendesha kwa jinsi taa zake zinavyo niumiza macho kupitia vioo vya pembeni.Nikashuhudia gari aina ya ‘HAMMER’ yenye rangi nyeusi na vioo vyake vyote vikiwa ni vyeusi na limefungwa likinipita,Haikuwa ni moja zikapita nyingine mbili zikiwa katika kwendo kama ilivyo gari ya kwanza
“Mmmmmm ni kina nani hawa?”
Nilijiuliza maswali,Na mimi nikaanza kuongeza mwendo wa gari langu.Jinsigari hizi zinavyozidi kwenda ndivyo nami nilivyodidi kuongeza mwendo,Nikaanza kuzikaribia kwa karibu.Nikawasha taa zote za gari langu ili na mimi nimtese dereva wa gari la nyuma.Nikashanga kuona gari mbili za nyuma zikitanda barabarani na kunizuia kupita.Nikaanza kupatwa na mashaka baada ya madereva hao kuanza mtindo wa kupunguza punguza mwendo gafla gafla na usipo kuwa makini unazigonga kwa nyuma.
Kwa mbele likawa linakuja lori ikatulazimu sote kubana upande mmoja kuliacha lipite na mchezo ukarudi na kuwa wa kuzuiana kupita.Hadi tunafika daraja la wami ndio gari hizo zikapunguza mwendo kulikwepa fuso lililo haribika pembezoni mwa barabara
Tukalimaliza daraja,nikaona jamaa wananichelewesha nikamuomba dereva wa nyuma kuweza kupita akaniruhusu,Nikiwa ninamaliza kuliacha gari la nyuma gari la pili kutoka mbele likatanda barabarani na kuongeza mwendo.Dereva wa gari la nyuma akaongeza kasi zaid na kutanda kwa nyuma wakawa wameniweka katikati.Kwenye kioo kidogo kilichopo pembeni ya mskani kwenye gari langu nikaanza kuwaka taa nyekundu na kutoa maandishi yaliyo andikwa kwa herufi kubwa.
{HABARI YAKO BWANA EDDY, GARI YAKO IPO KWENYE WAKATI MGUMU WA USALAMA.KAMA UNATAKA ULINZI MINYA HAPA AU UNAWEZA KUKATA}
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni