SORRY MADAM (98)

0
SEHEMU YA TISINI NA NANE
ILIPOISHIA...
"Vipi Eddy mbona kama una wasiwasi?"
"Kaka nina matatizo makubwa sana"
Nikanza kumuadisia Smith, tukio moja baada ya jengine, sikumficha kitu cha aina yoyote.
"Eddy nakuahidi hakuna kitakacho haribika, nitakusaidia kaka yangu"

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
"Pesa yote hiyo utaitoa wapi Smith, wakati bado upo Tanzania?"
"Njoo uone"
Tukaingia ña Smith kwenye moja ya chumba, ambapo tukakuta Mtu anaye fanana na mimi kila kitu.
"Huyu nane ni nani?"
"Tumemtafuta mtu wa kufanana na wewe, ili aweze kurekebisha baadhi ya vipande, tulijaribu kukupigia simu ila hatukukupata"
Hapa ndipo nilipo amini duniani watu ni wawili wawili, Jamaa hadi kuzungumza anafanana na mimi.

"Umaitwa nani?"
"Fred"
"Duuu jamaa anafanana na mimi"
Nilizungumza huku nikiwa ninacheka kwani sikuamini kukutana na mtu anaye fanana na mimi, kwa asilimia zaidi ya tisini.
"Eddy huyu umnaonaje kakakusaidia katika swala zima la wewe kuoa"
"Apo Smith umenena jambo la maana"
"Alafu una bahati kwa maana ndio amemaliza kushooti vipande tulivyo vikosea"
Nikaanza kumuelezea fredy historia yangu yote kuanzia mwanzo hadi mwisho, nikamuelezea mazingira yate ya nyumbani, pamoja na mtafaruku uliopo kati yangu na mama

"Nimekuelewa Eddy, ila huoni kwamba itakua hatati siku wakigundua kwamba mimi sio wewe?"
"Hawawezi kugundua, kikubwa ni weww kuwa karibu sana na mimi, kila jambo ambalo utaona linakutatiza nijulishe kwa njia ya meseji"
"Ila kuna kitu kingine ambacho ni kigumu"
"Kitu gani?"
"Na mimi nina mke, ila bado sijamuoa"
"Ahaaaa Fredy, hii ni ishu kati yangu mimi na wewe, pia nitakupa kiasi chochote cha pesa"
"Utachukua muda gani kurudi, kutoka kuko Somalia?"

"Haitazidi mwezi mmoja"
"Ahaa kaka, huoni nitampoteza mke wangu"
"Mkeo anaishi wapi?"
"Mbagala rangi tatu"
"Ndipo ulipo kua ukiishi wewe?"
"Ndio ninapo ishi"
"Fanya hivi, mimi ninakupeleka nyumbani kwetu, mimi nielekeze kwako, nitazungumza na mkeo"
Fredy akajifikiria kwa dakika kadhaa, akakakubali kuufanya mchezo wa hatari, uliopo mbele yetu. Ikanilazimu kumnunulia Fredy kama nilizo vaa, pamoja na simu inayo fanana na mimi. Nikatafuta laini mpya ya kuwasiliana na Fredy tu, kwani ya kwangu imeunganishwa na namba ya mama.

"Bado nini hapa"
"Sweta ulilo vaa wewe"
"Twende nitakupa mbele ya safari"
Tukaingia kwenye gari ya Smith, tukaelekea nyumbani kwetu, ambapo nikakuta basi kubwa, lililo toka kuwachukua ndugu kutoka stendi ya ubungo, walio toka mikoa tofauti kuja kushuhudia harusi yangu, wakishuka na kuingia ndani, huku wengine wakicheza kwa furaha.
Nikampa Fredy sweta langu na kujifunika kichwa chake, akajichanganya na wanandugu hao, walio landuka kwa kucheza kwa furaha, wengine wakionekana kulewa chakari. Fredy akafanikiwa kuingia ndani pasipo kustukiwa. Nikampigia simu

"Sasa chumba chako ni kipi?"
"Si umeona kuna nyumba tatu?"
"Ndio"
"Sasa wewe, pandisha kwenye hilo gorofa lenye rangi ya pinki, achana na hayo majengo mawili yenye ghorofa mbili mbili"
"Mbona zote zina rangi sawa"
"Hilo jengo la katikati, ndio upande, si umeliona?"
"Ndio naelekea"
Smith akawasha gari, tukaondoka, huku simu yangu ikiwa hewani
"Nipo ndani"
"Pandisha ngazi hizo utakuta kirdo ndefu, nyoosha hadi mwisho chumba cha mwisho kushoto ndio changu"
Japo ni jambo la hatari tunalo lifanya mimi na Fredy ila hapakuwa na njia nyingine zaidi ya kufanya hivyo.

"Nimesha ingia chumbani kaka, nipazuri sana"
"Sasa kazi kwako, ila hakikisha huwi muongeaji sana, usije ukachapia baadhi ya vitu"
"Nimekupata, demu anaitwa Sheila?"
"Ndio"
"Poa, kaka kukiwa na shida nitakueleza"
"Sawa"
Moja kwa moja tukaelekea Mbagala, hadi nyumbani kwa Fredy, kutokana Smith anapafahamu haikuwa shida kwangu kupajua. Tayari yaamekatika masaa manne yamesalia masaa kumi na moja kabla sijapeleka pesa ya kumkomboa Phidaya na mwanangu Junio.

Kitendo cha kushuka kwenye gari, nakastukia nikiguswa kwa nyuma, kugeuka nikakutana na Manaka akiwa amejitanda kanga mbili mwilini mwake
"Karibu sana mume wangu"
Nikasita kidogo kuitikia salamu yake, ila Smith akanikonyeza kuaahiria kwamba huyo ndio mke wa Fredy
"Safi"
Nilijibu kwa kifupi, kwani ukweli ni kwamba Manka ni dada yangu, niliye potezana naye muda mrefu sana. Mara ya mwisho kukutana naye ni ile siku, nilipo kua nimetekwa na Mzee Godwin, na kupelekwa kwenye ngome yake, iliyokuwa milimani.

"Mbona hivyo mume wangu, umechoka nini?"
"Yaa nimechoka sana"
"Ahaaa pole sana"
Manka akauleta mdomo wake, kwangu. Ikanilazimu kuupokea japo kiroho ngumu, japo kuwa tulisha wahi kupeana penzi, hadi akapata ujauzito ulio toka kwa kupata ajali.
"Twendd ndani, Smith karibu ndani"
Manka akatagulia huku, tukifwata nyuma. Tukaingia kwenye chumba kimoja tu wanacho ishi yeye na Fredy, ambapo kimekosa nafasi kutokana na ukubwa wa kitanda pamoja na ndoo za maji, vistuli viwili.

"Mume wangu, umekuja hata kunipigia simu, au ulidhani utanifumamia?"
"Ndio, nilitaka kukufumania"
"Mmmm jiamini mume wangu, acha wivu"
"Wivu lazima, kila mtu na chake"
"Sikuwezi"
"Shem, tumekuja kukuchukua kukupeleka kwenye makazi mapya, ambayo tumekubaliana na bwana mkubwa hapa"

"Wee"
"Ndio"
"Jamani, kweli Mungu ni mwema, nahisi vicheko vya wapangaji dhidi yetu vitakwisha"
"Usijali, wewe chukua nguo tu, tuondoke usiku huu huu"
"Hata kula"
"Kula tutakula mbele ya safari"
Manka akachukua nguo zake chache na kuziweka kwenye mkoba wake, hadi hapa sikujua Smith anatupeleka wapi, tukatangulia kutoka nje na kumuacha Manka akiagana na wapangaji wezake

"Smith hivi jamaa alikua akifanya kazi gani?"
"Alikua akiuza maji baranarani, ndipo nilipo muona. Mara ya kwanza nilijua ni wewe ila baada ya kumuhoji ndipo nilipo gundua kwamba sio wewe. Ndio tukaamua kufanya naye kazi"
Sikutaka kumueleza Smith kuhusiana na Manka, tukaingia kwenye gari na kwenda maeneo ya Mbezi kwa Msuguri, ambapo kampuni ilimnunulia Fredy nyumba kubwa, na yakupendeza. Manka akaonekana kama kuchanganyikiwa kuiona nyumba hii, ambayo ni mpya kabisa.

"Ohhh Fredy nakupenda sana"
Manka alizungumza huku, akinibusu mdomoni mwangu, tukaingia ndani, tukakuta kila kitu kinacho paswa kuwepo ndani ya nyumba nzuri kipo. Manka akawa kama mtu aliye changanyikiwa, kila chumba akaanza kuingia.
"Kaka hapa nitaondokaje?"
"Usijali tutaondoka tuu, niachie mimi kila kitu"
Simu yangu, ikaita na kukuta ni Fredy anaye piga, ikanilazimu kutoka nje kwenda kuipokea

"Vipi?"
"Kaka nimeulizwa, pete za ndoa zipo wapi?"
"Nani kakuuliza?"
"Mama"
"Kwenye droo ya kitanda hapo, fungua utaziona"
"Poa, ila mama hajastuka"
"Hawawezi kustuka, hembu kata simu kuna simu kwangu inaingia"
"Poa"
Fredy akakata simu, nikapokea simu inayo ingia kupitia laini nyingine ya simu iliyopo ndani ya simu, yangu inayo ingia laini mbili

"Utatuletea utani si ndio?"
Sautii ya mwanaume anaye zungumza lafudhi ya kisomali, niliisikia kupitia simu yangu
"Ninawatania kivipi?"
"Tunataka hizo pesa, sasa nakuongezea masaa mengine ishirini na nne, ole walo usilete pesa nakata kichwa cha mkeo"
"Nitawapatia tu hizo pesa"
Simu ikakatwa, nakujikuta nikishusha pumzi
"Unaongea na nani?"
Sauti ya Manka ikaniatua, nikageuka nyuma, nikamkuta akiwa amesimama akinitazama

"Kuna jamaa zangu, niliwakopa pesa yao ndio wanayo ihitaji"
"Ahaa tena ufanye ukamlipe baba mwenye nyumba pesa yake kwa maana ananisumbua"
"Sawa nitakupa asubuhi, ukamlipe"
"Na kesho unakwenda Marekani, mbona hujaniambia?"
"Kwani mke wangu, tumekaa tukaongea"
"Sasa Fredy, umeacha hadi Smith ndio aniambie"
"Kwani shem, nikizungumza mimi ni sawa amezungumza yeye, kama nilivyo kuambia kuna mikataba anakwenda kusaini, akirudi utamsahau kwamba alikua ni muuza maji wako"
Hapa ndipo nikaamini, Smith anaakili kubwa ya kutengeneza matukio makubwa pasipo mtu mwengine kustuka kwa haraka.

"Kaka Fredy, mimi ngoja niwaache nitakuja kukuchukua saa kumi na moja alfajiri, ili kuwahi ndege"
"Sawa kaka"
Smith akanishika mkono, tukatoka nje ya geti, ambapo tulimuacha Manka akirudi ndani.
"Eddy kwa leo hapa tumefanikiwa, sasa ni hapo kukipambazuka tuifikirie familia yako"
"Nakushukuru sana kaka, yaani nilikua nimechanganyikiwa kabisa"
"Tupo pamoja, kesho nitakuja na pesa ya kumuachia huyu mkeo mpya, ili imsaidie kwa kipindi chote utakapo kua nje ya nchi"
"Asante sana kaka"
Smith akapanda gari, na kuondoka, nikarudi ndani, nikamkuta Manka akimalizia kupanga sahani mezani, kwa ajili ya chakula alicho kikuta kimesha pikwa na dada wa kazi ambaye, kipindi tukiingia ndani, yeye alikua amelala.

Tukala msosi, na kuelekea katika chumba ambacho tayari Manka alisha ingiaza nguo zake. Manka kwa haraka akavua nguo zake na kuingia bafuni
"Mmmmm leo kazi ninayo"
Nilijisemea huku nikisikilizia maji yanayo mwagika bafuni. Manka akatoka bafuni, pasipo kua na kitu chochote mwilini mwake. Akajirusha kitandani jilipo lala. Akaanza kufanya uchokozi kama wafanyao wanawake walio shikika na hamu nzito ya kukutana kimwili na mwanaume.

Manka akaanza kunivua nguo moja baada ya nyngine, nilipo baki na boksa akaonekana kustuka kodogo
"Vipi?"
"Fredy umekula nini?"
"Kwa nini?"
"Mbona, nanilou yako imekua kubwa, tofauti na siku zote?"

"Ahhh kuna... kuna videngo Smith alinipa, ndio vimeifanya iongezeke kua hivi"
"Mmmmm, vidonge gani hivyo?"
"Ahaaa mimi sijui."
"Hujui, na ilikuaje akakupa?"
"Manka, mambo mengine ni yakiume"
"Fredy umeniitaje?"
"Si Manka"
Manka akaonekana kunitazama vizuri, usoni mwangu kwa macho yaliyo jaa umakini mkubwa. Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio, macho yake yakatua kwenye kifua changu, akanitazama vizuri kwa umakini.

Akaipeleka mkono wake kwenye kifua changu, nakuanza kukipitisha kiganja chake kutoka eneo moja la kifua changu kwenda eneo jingine la kifua changu.
"Hizi alama umezitoa wapi?"
Nikajitazama na kujikuta na makovu, ya risasi nilizo wahi kupigwa siku za nyuma kwenye kifua changu, kovu moja likiwa limetokana na yeye kunipiga risasi kipindi cha nyuma.
Sikuweza kumjibu kitu chochote, Manka kwani nikijikanyaga zaidi, naweza kuharibu kila kitu.

"Mbona hunijibu?"
"Sijui hata nikujibu nini, kwani hujawahi kuliona hili kovu?"
"Fredy leo hii, unataka kunuliona mimi ji mgeni wa mwili wako?"
"Labda siku zote, hukuwa makini na kunitazama"
"Ftedy, ni mara ngapi ninakunyonya kifua chako?"
"Nahisi leo huna hamu na mimi"
Nikanyanyuka kitandani, huku nikijifanya nimekasirika, kumbe ni njia ya kukimbia kikaangio cha maswali ambayo jimeanza kufeli kwa asilimia sifuri.

"Na huku mgongoni umefanyaje?"
Manka akanitandika swali jengine, nikiwa naingia mlango wa bafuni. Nikaingia haraka haraka kuepuka kujibu, hata hamu ya kuoga ikaanza kuniishia.
'Nikimueleza ukweli, nitaharibu kila kitu'

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)