SEHEMU YA TISINI NA TISA
ILIPOISHIA...
"Na huku mgongoni umefanyaje?"
Manka akanitandika swali jengine, nikiwa naingia mlango wa bafuni. Nikaingia haraka haraka kuepuka kujibu, hata hamu ya kuoga ikaanza kuniishia.
'Nikimueleza ukweli, nitaharibu kila kitu'
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
'Sasa leo nitamuepuka vipi huyu Manka?'
'Kwenye jina, nahisi nimevuruga, au sio Manka?'
'Ndio yeye bwana, isije nao wakawa wawili kama mimi na Fredy?'
Niliendelea kujiuliza maswali, mengi pasipo kujipatia jibu. Huku maji ya bomba la mvua yakiendelea kushuka mwilini mwangu, yakiitotesha boksa yangu ninayo ogopa kuivua.
"Yameanza lini kuoga na boksa?"
Sauti ya Manka, ikazidi kumistua, kwani hata alivyo ingia humu bafuni sikuweza kumsikia, kutokana na msongo mkubwa wa mawazo.
"Eheee"
"Fredy, mbona leo sikuewi. Nimekuuliza maswali yangu, hukanijibu nakuja huku nakukuta umeegemea ukuta, nini tatizo?"
"Ahaa naifikiria safari ya kesho"
"Mmmm haya mwaya, ila mmmmm"
Manka akatoka, bafuni nakujikuta nikishusha pumzi nyingi.
"Asiniumize kichwa mimi, ninamambo mengi ya kufanya"
Nilizumgumza kwa hasira huku, nikijipaka sabuni, na kuivu bosa yangu. Nikamaliza kuoga na kurudi ndani, nilamkuta Manka amesha jifunika kwa shuka, macho yake akiwa amenikodolea mimi.
Kiunyonge kikapanda kitandani, nikajilaza taratibu.
"Fredy, natambua kila siku ulikua unahitaji kujua historia yangu ya nyuma, ila nikawa ninakuficha."
"Leo nimeona uwe ni muda muafaka, wa kuzungumza na wewe, ili kama utaniacha uniache kwa amani."
Manka alizungumza kwa sauti ya untinfe iliyoa anza kumpeleka kwenye hisia ya kulia.
"Natambua umenifwatilia sana, hadi kulifahamu jina la Manka"
"Fredy, mimi siitwi Maria kama, unavyo nijua. Jina langu halisi ni Manka Godwin"
Manka alizungumza, huku machozi yakianza kumwagika.
"Fredy, niliweza kukupenda, japo hukua na uwezo kunifanya chochote kama wafanyavyo wanaume wengine kwa wapenzi wao."
Hapa ndipo nilipo anza kupata picha halisi kwamba Fredy hana nguvu za kiume.
"Yote ni kwasababu ya kumpenda mwanaume, aliye fanana na wewe, samahani kwa kile nitakacho zidi kukizumgumza, ila natambua utakwenda Matekani, labda Mungu anaweza kukufungulia milango yako zaidi na kuwa suprestar"
'Laiti angejua, nakwenda Somalia, wala asinge kuzungumza haya'
Manka taratibu, akajivuta na kukaa kitako kitandani.
"Huyo mwanaume, niliweza kumjeruhi, kwa risasi."
"Lakini baby hayo yote yametokea wapi, njoo tulale"
Manka akanigeukia, akanitazama kwa macho makali, hafla akanikalia kiunoni mwangu na kuanza kuninyonya midomo yangu. Akawa kama mithili ya mbogo, aliye jeruhiwa kwa rusasi, hakutaka kunipa nafasi ya kumuandaa, alainike ili iwe rahisi kufurahia mchezo huu, unao pendwa na watu wengi sana duniani.
Manka akawa kama mtu aliye kaa, kwa kipindi kirefu pasipo kukutana kimwili na mwanaume. Kwani kelele zake zilitawala chumba kizima. Hadi tunamaliza akabaki akiwa amenikalia kiunoni, huku jasho likimwagika.
"Your not a Fredy"(Wewe sio Fredy)
Manka alizungumza, huku akinitazama machoni, jasho likimdondoka.
"Wewe ni Eddy, kwani penzi hili ulinipa miaka mingi ya nyuma"
"Eddy! nani mimi?"
Nilibabaika, kwani tayari Manka ameutambua ukweli wa mambo.
"Eddy, nilijua umekufa"
"Mimi sio Eddy"
"Wewe ni Eddy, risasi niliyo kupiga ilitua hapa"
Manka akaniminya sehemu aliyo wahi kunipiga risasi kwa bahati mbaya.
"Mwili wako, ninaujua Eddy. Harufu yako haiwezi kuniondoka puani mwamgu, nilikutafuta miaka mingi, nikakukosa, nilimuona Fredy nikawa naye kama faraja ya kunikumbusha uwepo wako"
Manka alizungumza huku, akinitazama kila mahala.
Sikua na lakuzungumza zaidi ya kukaa kimya, kwani kitu anacho kizungumza Manka ni ukweli, kabisa na hajakosea sehemu yoyote ya mazungumzo yake.
"Manka nahitaji kujua ukweli?"
Sikuona sababu yà kuendelea kuminyana na Manka, kubisha kwamba mimi si Eddy, bali ni Fredy, ambaye hadi sasa hivi nimeguñdua kwamba ana idhaifu mkubwa, kitandani.
"Kwahiyo mama, hataki kumuona huyo Juñio na mama yake?"
"Ndio hapa, ninakazi ya kuwaokoa wao"
"Nitakusaidia kama, kaka yangu. Tusahau mambo ya kitandani, kwani yameshapita"
Uamuzi wa Manka, ukanishangà za kiasi cha kunifanya niaze kufarijika moyoni mwangu, kwani ukombozi wa familia yangu, unaweza kua wa asilimia mià . Kitu kilicho nitatoza ni kujua wapo Somalia sehemu gani.
Kama Smith alivyo ahidi, alfajiri na mapema, honi ya dari lake tukaisikia, ikipiga nje ya geti. Kutokana tulisha jiandaa, tukatoka na kuelekea nje ya geti
"Shem naye anakwenda MÃ rekani?"
Smith mimi, nakwenda Somalia hakuna cha Marekani hapa"
Smith akabaki akishangaa, kwani hakutarajia kusikia anacho kisikia. Nilamueleza Smith, historia kati yangu na Manka.
"Haya bwana nyinyi wajanja, sasa nitawapitisha Arusha, mutaingia Kenye, kisha Somalia"
"Sawa"
"Kenya kuna rafiki yangu, anafamya kazi kwenye shirika la mdege, mitawakabizi kwale naye atawafanyia mchà kato wa kuingia Somalia"
"Sawa"
Tukatumia takribani masaa, sota kufika Arusha, kitu cha kwanza baada ya kufika Arusha, tukaitafuta namba ya Phidaya kupitia 'Caller Tracker' ambayo, iliweza kutusaidia kuijua sehemu, alipo Phidà ya
Tukajatibu namba ya mtekaji, aliye nipigia kwa mara ya kwanza, nayo tukakuta inapatikana katika eneo hilo hilo, alipo Phidaya.
Tulafanikiwa kuingia nchini Kenya, kwa kuwahonga askari wa mpakà ni. Tukafika jijini Nairobi, ambapo Smith akatukabidhi kwa rafiki yake, akatuachia pesa ya kutosha, kiasi kipatacho milioni ishirini, za kitanzania.
Tukanunua baadhi ya nguo, zakitusaidia katika kazi iliyopo mbele yetu.
Hatukuweza kutumia usafiri wa gari, kuhofia kuchelewa, tukakodi boti ndogo ya kwenda kwa mwendo kasi, kila sehemu zilizo na vizuizi vya askari, tuliweza kuwapa chochote kitu, na kufanikiwa kupita pasipo tatizo. Tumaingia nchini Somalia, majira ya saa nane usiku
Manka akanipeleka kwà rafiki yake ambaye siku za nyuma, alikua akifañya kazi ya kigaidi, katika kundi la mzee Godwin, lililo sambaratishwa, baada ya kiongozi wao Mzee Godwin, kutiwa nguvuni, na jesi la Tanzania, na kufungwa kwenye gereza, lisilo julikana.
Manka akasalimiana na dada huyu mrefu kwenda juu, mwili wake umejengeka, na anaonyesha ni mtu wa mazoezi.
"Umemtoa wapi huyu?"
Dada huyu alizungumza huku akiwa ameninyooshea bastola yake, ambayo sikujua hata ameichomolea wapi, kwenye mwili wake
"Amina tulia bwana, huyu nahisi unamjua?"
"Ndio maana nikakuuliza, umemtolea wapi?"
Manka akamuelezea rafiki yake huyo kila kitu, kuhusiana na kutekwa kwa familia yangu, Amina akahitaji kiasi cha shilingi milioni mbili katika kuifañya kazi yetu.
Nikampa milioni moja na nusu, kwa makubaliano ya kazi ikikamilila ninampa laki tano, iliyo salia.
"Ahaaa, hiyo sehemu, ninaijua. Kwanza walio mteka pia nahisi ninawajua"
Amina alizungumza baada ya kumuelezea sehemu, sehemu walipo Phidaya na Junio.
"Ngoja kupambazuke, tutakwenda kupachunguza, usiku tukapige ambushi ya kufa mtu. Kama zile tulizo kua tukizifanya tukiwa na mzee G"
"Amina hapo umenena"
Manka alizungumza huku, akinyanyuka akielekea sehemu ilipo tv kubwa. Akaiwasha ila haikuwaka
"Hii tv yako vipi?"
"Ipige kwa juu hà po itawaka"
Manka akafanya kama alivyo elekezwa, na kweli ikawaka
"Mmmm, hii tv yako kiboko, hadi makofi ndio inawaka"
"Hiyo tv ya kibabe, hapo mwizi akiiba ataumbuka"
"Haaaaa, king'amuzi chako ni kipi"
"DSTv"
"Ngoja nitafute movie za ngumi, nikikumbushie"
Manka akaanza kubadilisha chaneli moja kwenda nyiñgine.
"Manka hembu weka chanel yoyote ya Tanzania"
Manka akaanza kutafuta chanel za Tanzania, na kufanikiwa kupata chaneli ya shirika la utangazaji Tanzania TBC1. Tukakuta kipindi cha kumekucha, ambapo kuna baadhi ya magazeti yanasomwa.
"Katika gazeti la burudani, ukurasa wake wa mbele linakicha cha habari kinachosema, NDOA YA MTOTO WA WAZIRI MKUU YA....."
Tukajikuta tukikitazama kioo cheusi cha Tv hii, kwani ilizima gafla
"Wanesha kata umeme wao,"
Amina alizungumza huku akinyanyuka kwenye sofa. Kwa hataka nikawasha simu yangu, niliyo kua nimeizima, nikajaribu kuingia kwenye mitandao ya kijamii, ila kukawa na tatizo la internet. Tukastushwa na sauti ya Tv, kwani umeme umerudi gafla na hatukuwa tumeizima.
"Watatuunguzia, vitu ahaaaa"
Amina alizungumza huku macho urmetu yakielekea kwenye Tv, tukitazama kipindi cha magazeti kilionyesha, picha moja iliyopo kweñye gazeti, likiwa limetobolewa sana kwa risasi.
"Hiyo ni picha ya ukurasa wa mbele katika gazeti hili la Jambo leo, ikibebwa na kichwa chà habari kisemacho, MTOTO WA WAZIRI MKUU NA MKEWE WATEKWA NA WATU WASIO JULIKANA, NA RISASI ZARINDIMA ENEO ZIMA LA KANISA"
Mtangazaji alizungumzà , huku akifunua kurasa ya ndani, akidai kwenda kuisoma taarifa hiyo kwa urefu zaidi.
Manka akazima tv, na kuiweka rimoti mezani, akionekana kupatwa na mawazo ya gafla.
"Mbona umezima"
Nilimuuliza kwa sauti ya upole sana
"Eddy, hichi ni nini ulicho kifanya kwa Fredy wangu?"
"Nisikili......"
"Eddy hapa hakuna cha kusikiliza, umemsababishia mwenzako matatizo makubwa sana"
"Ndio nalitambua hilo, ila natambua kwamba hajauliwa, lazima atakua hai"
"Una uhakika gani, hata kama Fredy hajiwezi kitandani, lakini nimempenda hivyo hivyo."
Manka alizungumza huku akiwa amekasirika sana, machozi yakaanza kulowanisha uso wake.
"Oya mboma mimi siwaelewi?"
Amina alituuliza baada ya tukio lililo tokea, kushindwa kulielewa. Nilamuelezea kwa ufupi, akanielewa vizuri
"Sasa wewe, Manka huo ni unafki sasa. Tangu lini ukamlilia mwanaume?"
"Amina hujui tu maumivu, niliyo kua nayo nampenda Fredy tena sana"
"Hembu sikia, ishu hapa ipo hivi. Tunakwenda kwa hao mafala walio teka mke wa bro, tukimaliza tunakwenda kwa hao mafala wengine walio teka Fredy"
Amina alizungumza huku akiwasha sigara yake kwa kiberiti cha kutumia gesi.
"Yaani hapa nguvu zote zimeniishia"
"Zimekuishia kisa mwanaume. Mbona umekua fala sana mtu wangu?"
"Manka niliye kua namjua mimi ni yule wakazi, sasa Manka wewe wa kulia lia kisa mwanaume sijui umetokea dunia gani. Hembu nyanyuka tukafanye kazi"
"Siendi popote"
”Nini wewe, sasa maana ya kuja hapa ni nini?"
"Siendi"
Mgomo wa Manka ukaañza kunipa wasiwasi mkubwa, dalili mbaya ya mpango nilio upanga mbele yangu nikaanza kuuona ukianza kuharibika.
"Manka nini unafanya, nini uliniahidi kulifanya juu ya familia yangu?"
"Sawa Eddy ila elewa siendi popote"
"Sikia Eddy asikuchanganye, mziki wako nauelewa vizuri. Twende tukapige job"
Manka akanyanyuka na kuingia ndani, kwa Amina. Amina akamfwata kwa nyuma kwenda kuzungumza naye. Nikawasha Tv, ila nikaikuta tarifa hiyo ikiwa imekwisha, nikajaribu kuitafuta kwenye chanel tofauti, pia sikuipata.
"Oya mtu wako amekataa bwana, tujiandae twende tukapachunguze, kisha usiku twende"
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com