Mwandishi: Andrew Mhina
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“Nimekuelewa rafiki uko sawa kabisa. lakini nimekuuliza habari ya ndoa yenu mmepangaje naona bado hujanijibu vizuri.” Mary alikumbusha. “Ni kama nilivyokuambia rafiki yangu kuwa ndoa yenyewe ina mambo ya kuchanganya tu.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
“Unajua kwenye mahusiano kama hayo halafu kukiingizwa vipingamizi kibao inasumbua sana kichwa?” Alisema Irene kwa umakini sana. “Mvutano gani tena?” Si ulisema shida ilikuwa ni nyinyi kuamua mahali pa kufungia ndoa kati ya Kanisani au msikitini? Nikafikiri labda mmepata maamuzi watu waanze vikao vya maandalizi.” Alisema mary.“Bado hatujapata maamuzi ya maana rafiki yangu unajua swala la kubadili dini kwa upande wetu sio tatizo ila wazazi ndio wanaoleta vipingamizi.
Sijajua la kufanya na hata mwenzangu amechanganyikiwa kabisa.” Alisema Irene kwa masikitiko kidogo. “Sawa Irene lakini kama imeshindikana kufungia kanisani au Msikitini, fanyeni uamuzi wa kufungia bomani, kusudi kila mtu abaki na dini yake?” Alishauri Mary.“Mary unafikiri ni rahisi kufanya hivyo? Bado maamuzi yanabaki kwa wazazi wetu. Hakuna kati yetu aliyefikiria suala la kufungia ndoa Serikalini.
Ila wazo hili ni jema nitajaribu kulipenyeza kwa mwenzangu alipeleke kwa wazazi wake tuone kama linaweza kuleta matokeo.” Alisema Irene. “Basi rafiki yangu jaribu kumpa njia hiyo halafu tusikilizie kama itakubaliwa.” Alisema May huku akinyanyuka na kuaga kuwa anaondoka. “Mbona mapema sana Mary kwani unakimbilia nini?” Alisema Irene kwa mashangao kidogo.“Kuna mambo naenda kuyaweka sawa rafiki yangu. Nafikiri tuonane tu kesho mchana ili tuelekee Beach si ndivyo tumekubaliana?” Alisema Mary.
Sawa rafiki yangu Nitajiandaa kisha nitakujibu kama nitakuwa okay hiyo kesho kuhusu kwenda Ufukweni.” Alisema Irene wakati akinyanyuka kitini kwa ajili ya kumsindikiza rafiki yake.“Sawa naomba iwe hivyo ili tukazungumzie mambo yetu huko ninahitaji sana ushauri wako.” Alisema Mary huku akitabasamu.
“Ushauri kuhusu nini? Si nimekuambia kuwa sitashiriki kukushauri ikiwa unataka kupoteza ndoa yako, kwa ajili ya mtu wa ufukweni utajijua mwenyewe!” Wote walicheka na Mary alipanda kwenye gari. Hujajua nataka ushauri gani unarukia tu mambo,” alisema Mary huku akimpungia mkono rafiki yake na kuondoa gari taratibu na baadaye, akatoweka nje ya geti.
Haikuwa hiyari yake kabisa kuingia katika uhusiano huu! Moyo wake ulimuuma kila wakati, kwani hakuwahi kuwa na uhusiano na mwanamke yeyote tangu udogo wake. Sio kwamba alikuwa na tatizo la hasha. Alikuwa anajiepusha sana na mambo hayo ili ajiwekee malengo yake na kufikia ndoto zake. Aliwaona vijana wengi waliopoteza malengo yao, kwa kujihusisha na wanawake. Hakupenda kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi kabla ya ndoa.
Alikutana na vishawishi vingi sana, toka kwa wasichana na wanawake wenye ndoa zao. Wengi wakimsifia kuwa alikuwa na umbo zuri la kimazoezi na sura yake iliwavutia. Lakini kwake hakutoa nafasi ya kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi. Mazoezi na uchapakazi ni vitu vilivyoondoa kabisa hamu ya kujihusisha na mapenzi. mawazo yake aliyaelekeza kwenye ndoto zake za kimaendeleo na alifanya bidii sana ili azifikie ndoto hizo.
Leo ilikuwa tofauti kabisa, kwani ile nadhiri aliyojiwekea ilivunjika tena kwanjiaambayo kamwe hakuitarajia. Ilikuwa ni njia tofauti na ndoto zake. Njia mbaya ya kuingia katika uhusiano na mke wa mtu! Ramson alikuwa akijifikiria jinsi alivyoingia katika uhusiano huo mbaya. Alimfananisha Mrs.Doctor na Delila alivyomrubuni Samson, hata akaanguka katika mikono yake na kupoteza nguvu zake alizopewa na Mungu.
Ushawishi wa Mary juu ya anguko hilo, ulisababisha Ramson ajikute tayari ndani ya uhusiano huo. Uhusiano huu ulikuwa umeshafungua ukurasa mwingine kabisa katika moyo wake. Hakuwa tena na ujanja kila wakati akawa kama mtumwa wa mapenzi, kwani hisia zake zikawa zimetekwa mateka na mwanamke huyo. Lakini kila wakati alifikiria jinsi ya kujinasua kwenye uhusiano huo.
Ilikuwa siku ile aliyofika Mary na Mwenzake aitwaye Irene katika ufukwe huo, ndipo Mary alipomtamkia maneno ya kumtaka wawe na uhusiano wa kimapenzi. Kukataa kwake hakukuwa na nguvu mbele za mwanamke huyo. Alimwahidi kufika ufukweni hapo siku iliyofuata, ili wazungumze vizuri kuhusu hilo. Siku aliyoahidi kuja Mary ilikuwa ni siku ya katikati ya wiki. Kwa kawaida siku hizi huwa wateja hawaji ufukweni hapo na kama watakuja basi ni mmoja mmoja.
Siku aliyosema atakuja ilifika naye akaja. “Unajua Ramson vile nilivyokuambia jana ninamaanisha? Labda tu huelewi kuwa ninakupenda kwa kisi gani.” Alisema Mary kwa sauti ya kushawishi. “Mary hilo sahau kabisa dada yangu. kiukweli maisha yangu nayapenda na sihitaji kuyahatarisha na hatimaye kuyapoteza kijinga kiasi hicho.” Alisema Ramson kwa dhati huku akionyesha msimamo. “Ni hatari gani unayoizungumzia Ramson?” Aliuliza tena Mary.
“Hatari! Hujui kuwa wewe ni mke wa mtu? isitoshe huu sio wakati wake wa mimi kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi. Ninangojea wakati wangu ufike ili nioe na ndipo nitakapoingia rasmi kwenye mambo hayo.” Alisema Ramson. Lakini Mary alifanya kazi kubwa sana ya ubembelezi na kuahidi kuwa itakuwa ni siri kubwa kati yao. na mwisho wake Ramson akaingia kwenye mahusiano hayo.
Ilikuwa ni hali ngeni kwake kwani kila wakati alisumbuliwa na kichefu chefu na hali ya uchomvu usio na sababu. vipimo mbalimbali vya kidaktari havikubaini lolote katika mwili wake. Hiyo ni hali mpya kwake naye aliamua kuikubali kuwa ni sehemu ya tatizo lake maana haikutibika. Siku moja asubuhi alimpigia simu rafiki yake Irene: “Halo rafiki yangu nimevumilia kukuambia lakini naona haina maana kukuficha maana unaweza kunisaidia.” Alisema Mary kwa unyonge.
“Una nini rafiki yangu.” Aliuliza Irene kwa mashaka kidogo. “Unajua nina mwezi sasa ninasumbuliwa na kichefuchefu, uchomvu na wakati mwingine ninatapika. Nimekwenda kupima kwa Daktari lakini bado hakujaonekana ugonjwa wowote.” Alisema Mary kwa sauti ya kukata tamaa. “Hiyo inaweza kuwa ni habari njema rafiki yangu ila umakini unahitajika hapo ili usije ukapoteza ndoa yako.
”Alisema Irene kwa uchangamfu. “Unamaanisha nini rafiki yangu? yaani kuumwa kwangu ni habari njema?” Alisema Mary kwa hamaki. “Mary hiyo ni mimba rafiki yangu, amini usiamini na kama bado hujanielewa nenda tena kwa Daktari umwambie akupime ujauzito utakuja kuniambia.” Alisema Irene kwa uhakika.
“Sawa rafiki yangu nitakwenda leo kupima mapema sana kuanzia wakati huu.” Alijibu Mary kisha akakata simu. Hakuchukuwa muda mrefu sana alikwenda kwenye Zahanati iliyokuwepo jirani katika mtaa wao na kumwomba nesi aliyemkuta ampime ujauzito. Majibu yaliyotoka karibu yamtie kichaa kwa furaha. Alifurahi sana kwa sababu aliishi katika ndoa yake kwa muda wa miaka minne bila mafanikio.
Masimango na kejeli za mawifi vilimchosha na kumtia aibu. Kila wakati alijihisi kama alikuwa sio mwanamke aliyekamilika, kwa kukosa mtoto katika ndoa yake. Mume wake mara chache sana alilalamika kuhusu hilo, lakini baadaye alinyamaza kimya na kumtia moyo, kuwa kila kitu kingeenda sawa kwani Mungu ana wakati wake.
Maneno ya mume wake hayakumfanya ajisikie huru kwa kuwa huo ulibaki kuwa ukweli na kilema katika familia. Mawifi nao hawakukoma kupiga vijembe vya masimango kuhusu tatizo lake. Kupata kwake ujauzito kulimfanya ampende zaidi Ramson na kumwona wa maana kuliko mume wake.
Suala hilo lilisababisha ampigie simu kwa haraka baada ya kurudi kutoka kwenye vipimo vyake. Ramson alipokea habari hizo kwa hofu kidogo, akihofia usalama wa maisha yake kwa kuingia katika uhusiano na mke wa mtu. Kwakweli haikuwa habari njema kwake kama ilivyokuwa kwa Mary. Ilimtia mashaka na kuona wazi kuwa tayari maisha yake yamekuwa hatarini. Baada ya kumjulisha Ramson akampigia rafiki yake Irene simu na kumwambia kuwa ameshapima na kwamba tayari yeye ni mjamzito kama alivyotangulia kumwambia.
“Kweli mwenzangu wewe ni mtaalamu! Vile ulivyoniambia ni kweli kabisa.” Alisema kwa furaha sana Mary. “Sawa rafiki lakini umeshamjulisha mumeo kuwa umepata ujauzito?” Irene alimwuliza kwa shauku. “Hilo nimelisahau mwenzangu, kwa furaha nimeishia kumjulisha Ramson badala ya mume wangu.” Alisema Mary kizembe, baada ya kukumbushwa kuwa ingekuwa bora amwambie mumewe kuwa alimwacha na ujauzito.
“Kumwambia Ramson ni kosa kubwa litakalokugharimu mambo mengi sana.” Alikohoa kidogo Irene kisha akaendelea. “Suala la mimba hakupaswa kuambiwa kabisa huyo jamaa, badala yake ungembambikizia mumeo kwa ajili ya kulinda ndoa yako. Ila hujachelewa bado hebu mpigie mumeo , kwa sababu tangu aondoke mpaka sasa ni miezi miwili tu mjulishe kuhusu hali yako.”Alishauri Irene na kukata simu.
Hii hali ilimchanganya sana baada ya kupewa mbinu hii na rafiki yake. Tayari alishajiona amefanya jambo la kijinga na litakalomgharimu sana, katika kulinda siri hii isivuje na kumfikia mumewe. Jioni ya siku hii ilibidi apige simu kwa mumewe na kumwelezea kuhusu hali yake. “Dear nina jambo la furaha sana nataka kukujulisha” Alisema Mary baada ya kuongea machache na mumewe ya kujuliana hali na maendeleo ya masomo pamoja na biashara baina yao. “Ni jambo gani hilo mke wangu?” Aliuliza Dr. Jackson kwa shauku.
Tangu uondoke nimekuwa nikisumbuliwa sana na kichefu chefu na wakati mwingine ninachoka sana mwili wangu.” Alisema Mary na kutulia kidogo. “Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa habari njema ndio huko kutapika na kuchoka mwili? Acha utani kama hakuna maelezo mengine hebu kapime upate dawa huenda ni malaria.” Alisema Dr. Jackson kwa bashasha. “Kwani mimi sijui habari njema?” Alihamaki Mary.
“Kama ungenisikiliza vizuri ningekujulisha habari yenyewe lakini unaonekana una haraka.” Alisema Mary… kisha akaendelea. “Nilikwenda Hospitali na kupimwa vipimo vyote lakini haikuonekana malaria wala ugonjwa wowote. Nikawa sina la kufanya kwa muda mrefu kidogo. Ila nilivyomjulisha rafiki yangu Irene akanishauri nikapime ujauzito, ndipo vipimo vilipobaini kuwa nina ujauzito wa kama miezi miwili hivi.
Kwa hiyo nina habari njema kuwa hatimae umeniachia ujauzito.” Alisema Mary kwa hamasa. “Woooow!!! unasema kweli mke wangu?” Alisema Dr. Jackson kwa furahakubwa sana. “Ni ukweli kabisa nina ujauzito na hatimaye aibu itakuwa imekwisha ya kuonekana kuwa mimi ni mgumba!”…. “Achana nayo hayo mke wangu hebu tuangalie mambo yetu.
Nafurahi kusikia habari hizo endelea na vipimo kuhusu afya yako na kufuata masharti ya madaktari kuhusu kujitunza na mtoto aliyeko tumboni sawa mke wangu?” Alisema Dr. Jackson.. “Sawa Mume wangu nitafanya hivyo.” Kisha simu ikakatika.
USIKOSE SEHEMU IYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi