Mwandishi: Andrew Mhina
SEHEMU YA KUMI NA TANO
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Baada ya kuona hivyo ilimsikitisha sana maana alijua kuwa rafiki yake Dr. Jackson alikuwa akiibiwa na Beach Man. Hali hiyo ilimtia uchungu kutokana na taarifa aliyopewa na rafiki yake Jackson, kuwa alikuwa aende Lushoto na mkewe lakini tatizo ni kwamba mkewe alikuwa akiumwa.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
Hali hii hakuivumilia badala yake alipiga simu ya Dr. Jackson. Halo ndugu yangu mambo vipi? Alisalimia Mudy baada ya simu kupokelewa. “Aisee ni nzuri sana kwema Pangani?” Aliuliza Dr. Jackson. “Pangani ni kwema nimeshamaliza shughuli zangu ila sasa niko hapa Mwang’ombe napita mahakamani hapa narudi Mjini.” Alisema Mudy.
“Sawa ndugu yangu mimi nilishafika Lushoto kitambo ninapitia mahesabu na kukagua mazingira ya Hoteli zangu.“Jackson alisema na mara hiyo simu ikakatika. Alijaribu kuipiga lakini alikutana na ujumbe ukisema: “Asante kwa kutumia mtandao wa voda com. Namba unayopiga kwa sasa haipatikani tafadhali jaribu tena baadaye.”
Dr. Mudy alitaka kuwakilisha ujumbe wake wa kimbea kuhusu kukutana na mke wa rafiki yake akielekea Beach. Ni mazungumzo mengi ya Jackson yaliyosababisha chaji yake iliyokuwa kidogo kwenye simu yake kwisha. Simu yake ilizima kabla hajawakilisha ujumbe huo. Aliendelea mbele akipania kuwa baada ya kuweka chaji kwenye simu yake basi angemweleza rafiki yake mambo yote.
Mary alifika ufukweni na Ramson alimpa mapokezi ya aina yake kwani walijumuika katika kukumbushia uhusiano wao. Baada ya zoezi lao Ramson aliuliza juu ya mpango wao waliopatana. “Mary uvumilivu unanishinda siwezi kuvumilia kukuona uko na mumeo na mtoto wangu. Ninachotaka kuanzia sasa nipate ule mzigo uliobaki nijue cha kufanya. Hiyo peke yake itakuwa ndio dawa ya kustiri siri yetu.” Alisema Ramson kwa Msisitizo.
“Ramson nimekuelewa mpenzi wangu lakini nimekuja kukuambia kuwa naomba usubiri kidogo tu kuna mambo nayarekebisha kusudi nikupe ule uzigo tuliopatana.” Mary alisema kwa upole. “Lakini Mary kumbuka kuwa ulisema jamaa akija tu utanipatia na sasa tangu aje ni wiki imeshaisha sio mapatano yetu. ila kama unavyosema ni muda mfupi naombaufanye hivyo kabla mambo hayajawa mabaya.
Nataka niondoke katika mji huu kwa muda usiojulikana.” Alisema Ramson.” “Usiwe na wasiwasi nitatimiza kila tulichoongea, nipe siku tatu tu tangu leo.” Alisema Mary kwa uhakika. “Kwa sababu umesema mwenyewe kuwa ni baada tu ya siku tatu naomba isivuke hapo. Kwa sababu sina amani moyoni mwangu juu ya maisha yangu.
Utanielewa vibaya ikiwa hutatimiza ahadi yako ndani ya siku hizo. Najua niko hatarini kwa sababu nawaelewa madaktari walivyo! Iko siku atashtuka kuwa mtoto sio wa kwake na kama akienda kwenye vipimo vya vinasaba kitakakachotokea ni siri kuwa wazi.” Alisema Ramson huku akionyesha hofu katika macho yake. “Ramson nitajitahidi nifanikiwe ndani ya siku hizo.” Alisema Mary huku akinyanyuka na kuaga kuwa anarudi nyumbani.”
“Zingatia hayo na uwe makini sana kwa kila jambo. usifanye papara katika kila pointi. Kosa moja tu litaifanya siri yetu kuwa hadharani.” Alitahadharisha Ramsoni. “Hakuna wasi wasi niko makini Ramson.” Alijibu Mary huku akiishilia ndani ya gari lake, baadaye akaliwasha na kuliondoa taratibu Ufukweni hapo. Mawazo yalipandana kwa Mary na kumsababisha kuwa na huzuni, iliyochanganyika na majuto.
Siri hii imekuwa kikwazo sana ndani ya maisha yake. Hakuwa tena na raha katika maisha kama ilivyokuwa hapo mwanzo.Hitaji la kupata mtoto na tamaa ya kimapenzi, imemwingiza katika hatari kubwa katika maisha yake. Nisawa kabisa kuwa alimpenda sana Ramson, lakini haikuwa zaidi ya mapenzi tu aliyoyataka kwake. Ndoa yake hakutaka kuipoteza kabisa hivyo alitamani kuilinda, kwa namna yoyote ile ya gharama.
Lakini dalili zinavyoonyesha mpaka hapo ni kwamba kuna dalili za siri hiyo kuvuja, kutokana na uharaka wa Ramson katika madai yake. Alijuta sana kumwambia Ramson kuwa alikuwa na mimba yake. Alikumbuka jinsi alivyopata furaha ya ghafla baada ya kupewa majibu ya vipimo na Daktari. Furaha yake ilimnyima simile hivyo akajikuta anaropoka na kumpa nafasi ya utawala Ramson, katika nafsi yake na maisha yake kwa ujumla.
“Umefanya kosa kubwa sana rafiki yangu kumwambia Ramson kuhusu huo ujauzito. Hiyo inaweza kukugharimu mambo mengi katika kuilinda siri hii.”
Alikumbuka maneno ya rafiki yake Irene, pindi tu alipomwambia kuwa amemjulisha Ramson juu ya ujauzito ule kuwa ni wake. Mpaka sasa kengele za tahadhari zilikuwa zikipigwa masaa ishirini na nne! Hali ya mashaka ilitawala kila wakati pindi tu anapofikiria jinsi ya kucheza katika pande zote mbili, kwa Ramson na mumewe.
Alijikuta yuko njia panda kwa ujumla. “Zingatia hayo na uwe makini kwa kila jambo, Usifanye papara katika kila pointi! Kosa moja tu litaifanya siri yetu kuwa hadharani!” Aliyakumbuka maneno ya Ramson ya mwisho wakati wanaachana. Hakuwa na hakika kuwa hatafanya kosa katika harakati zake za kuihifadhi siri hii; hasa ukizingatia kuwa pande zote alikuwa anawindwa!
Alikuwa na majukumu ya kawaida kwa mumewe na kwa Ramson. Kutoa Shilingi milioni kumi na kumpa Ramson halikuwa jambo kubwa sana wakati mumewe akiwa yuko masomoni. Lakini kutoa kiasi hicho cha fedha wakati mumewe akiwepo ni mtihani mkubwa sana, ambao umebeba hatari kubwa sana, kama hautafanywa kwa uangalifu.
Ubaya wenyewe ni kwamba pande zote mbili zitamwangukia kwa hasira kubwa sana bila huruma. Hayo yalikuwa ni mawazo ya kweli yaliyokuwa yakipita katika kichwa cha Mary. Kwakweli hakuwa na nafuu wala faraja kwa yote hayo; bali yalimtaka kuwa macho sana katika pande zote mbili. Kwa wakati huu Presha ilikuwa kwenye kulilipa deni la Ramson. Baada ya hapo abaki salama akiyalea mapenzi yake kwa mumewe. Tatizo kubwa lilikuwa ni Ramson na deni lake peke yake. Mawazo yake yalikuwa juu sana kutafuta jinsi ya kutatua tatizo hilo kwa busara.
Dr. Mudy alipofika nyumbani jambo la kwanza alikimbilia kwenye soketi ya umeme, ili kuchaji simu yake kusudi aweze kumpa rafiki yake habari juu ya Shemeji yake. Moyo wake ulikuwa na dukuduku bayasana, ambalo lilihitajika kutolewa mahali husika ili apate nafuu. Jamaa huyu huwa hawezi kuvumilia anapoona neno. Rafiki zake wengi walikuwa wakimshauri aachane na kazi ya udaktari, badala yake awe mwandishi wa habari wa magazeti ya udaku! Pendekezo hilo la rafiki zake lilikuwa sahihi, kwa sababu Dr. Mudy alikuwa hakai na jambo.
Anapoona jambo ambalo sio zuri, hulisimamia na kulitolea habari zake mahali husika. Mara tatu aliweza kutoa taarifa kuhusu Madaktari wenzake, waliokuwa wakijihusisha na kutoa mimba za wanafunzi. Madaktari hao walikamatwa na kufungwa kifungo cha miaka ishirini kila mmoja baada ya kubainika wakifanya tendo hilo. Leo hii yupo nyumbani kwake akiwa na harakati za kuchomeka simu kwenye chaji, lakini hali haikuruhusu kwani umeme ulikuwa umekatika.
Kidogo alitahayari kutokana na zoezi lake kukwamishwa na kukosekana kwa umeme. “Lakini ni kwa muda tu, umeme ukirudi nitachaji na kumwambia rafiki yangu habari hizi.” Alijisemea kimoyomoyo huku akielekea chumbani kwake na kuingia bafuni ili ajimwagie maji kuondoa uchomvu wa safari.
Baada ya kumaliza kuoga aliporudi chumbani kwake ili kuvaa nguo alikuta umeme umesharudi. Kwa haraka alichukuwa simu yake na kuiweka kwenye chaji. Baada ya hapo alirudi na kumalizia kuvaa, kisha akarudi na kuwasha simu ikiwa kwenye chaja na kutafuta namba ya Dr. Jackson.
Hata hivyo bahati haikuwa upande wake, kwa sababu simu ilikuwa haipatikani alijaribu tena ikawa vile vile. “Mmmmmh! huu umbea utachacha sasa! kama angepokea ningempasha habari zikiwa bado za motomoto, lakini inavyoonekana leo sikulalia mkono mzuri. Jamaa tunapishana tu nikitaka kufikisha umbea wangu kunatokea vikwazo!” Alilalamika Dr. Mudy huku akijaribu kupiga kwa mara nyingine ambayo ilijibiwa vilevile kuwa namba haipatikani labda ajaribu tena baadaye! “Hakuna neno ataifungua tu simu yake.
Na mimi sitaki kumtumia ujumbe mfupi wala nini! Nataka nimpigie na kumwambia kila kitu neno kwa neno.” Aliendelea kusema peke yake mawazoni huku akiwa ameshushuka kwa kukosa nafasi ya kubwagiza habari zile. Habari ambazo alizitunza kwa muda mrefu sana ila tu alikuwa akizitafutia ushahidi wa kutosha.
Alitayarisha ushahidi wa namna zote na kupata vigezo mbalimbali vya kuusema umbea ule kwa Jackson. Uchunguzi wake wa kina na ufuatiliaji wa mambo na kuhifadhi ushahidi ni sehemu ya kipaji chake. Hii ndio maana baadhi ya marafiki zake walimpendekeza kuwa alifaa sana kuwa mwandishi wa habari.
Kwa upande wa Mary aliweka ushahidi wa siku nyingi, hivyo kuifanya habari kamili juu ya kuibiwa kwa rafiki yakeiwe imeiva. Hii ndiyo sababu iliyopelekea kuhangaika sana ili kumpata Dr. Jackson, kusudi ampe habari kamili. Mahangaiko yake hayakufua dafu kwa siku ile, hivyo alilala nayo tena bila mafanikio.
Dr. Jackson alifika salama Lushoto na ukaguzi wa Hotel zake ulifanyika mara tu baada ya kufika. “Inaonekana mnafanya vizuri kazi zenu au sio Meneja?” Alisema Dr.Jackson baada tu ya kuingia kwenye Ofisi ya meneja wa Hotel mojawapo kati ya mbili alizonazo. Ni kweli Mzee tunajitahidi kufanya vizuri.” Alijibu Meneja kwa unyenyekevu. “Nimeona mazingira ya nje ni mazuri watu wa kukatia majani kwenye bustani wamefanya vizuri bwawa la kuogelea liko katika hali ya usafi, kadhalika bwawa la samaki pia naona linatunzwa vema, maana naona samaki wamekuwa wengi sana.
Hayo ni machache ya mambo niliyoyaona mazuri. Hongera sana Meneja kwa kazi yako nzuri.” Alisema Dr. Jackson huku akimpa mkono Meneja kusindikiza pongezi zake. “Asante Bosi kwa kuyaona hayo. Tunajitahidi kufanya vizuri kwa sababu wageni ni wengi kutoka Ulaya; wanakuja kulala hapa wengine wanakaa kwa mkataba, wa mwezi mpaka miezi mitatu.
Wanapokuja watu hawa kinachowavutia ni mazingira kwanza ya Hotel. Bwawa la kuogelea bwawa la samaki na vivutio vinginevyo, ikiwepo bustani ya mboga mboga na bustani ya matunda. Mpangilio wa vitu hivyo huwafanya waje hapa na kutaka kuishi hapa, ikiwa muda wao wa kukaa hapa ni mrefu.” Alisema Meneja kwa kirefu akielezea jinsi biashara zinavyoenda vizuri.
“Unataka kuniambia kuwa tangu niondoke nchini wamekuja watalii mara ngapi kwenye Hotel zetu?” Aliuliza Dr. Jackson. “Unajua mzee miaka mitatu sio mchezo! Inabidi niangalie kwenye kitabu kusudi nikupe idadi hasa za wageni wetu.” Alisema Meneja na huku akifungua kabati la vitabu vya wageni na taarifa za kila siku. Kisha akaendelea… “Unaona sasa! Kwenye kitabu cha kupokea wageni kinaonyesha kuwa ni zaidi ya mara ishirini tumeingia mkataba na wageni toka nje ya nchi wa kukaa kwa muda mrefu. Wengine walikaa wiki mbili wengine walichukuwa Hoteli nzima kwa miezi mitatu.
USIKOSE SEHEMU IYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi