Mwandishi: Andrew Mhina
SEHEMU YA KUMI NA NNE
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Alinyanyuka na kwenda kumlaza kwenye kitanda chake. Waliongea mambo mengi sana wakiulizana hiki na kile kwa zamu. Baada ya muda mrefu wote walijikuta wamepitiwa na usingizi. Kwa Jackson furaha ilikuwa kubwa sana kwa kuungana na mke na Mtoto wake. Aliyafurahia maisha kwa namna ya ajabu sana.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
Ila kwa mkewe alikuwa na siri moyoni mwake. siri nzito ambayo kama ikifichuka na kujulikana kwa Mumewe Italeta adhari kubwa sana katika maisha yake. Siri hii ilikuwa ni kama bomu. Bomu linaloweza kuangamiza kabisa familia yake iwapo litalipuka. Moyo wake haukuwa na raha hata pale ambapo mumewe alionyesha furaha yeye alikuwa akifanya maigizo tu.
Roho yake ilikuwa inamsuta kila saa anapomwangalia mtoto wake na kumwangalia mumewe jinsi alivyokuwa akimfurahia. Kwa namna Alivyokuwa haikuchukuwa muda mrefu Dr. Jakson alimgundua mkewe kuwa hakuwa na furaha sana ila alichukulia tu kuwa labda ni hali ya uchovu, au alikuwa huenda hajisikii vizuri. Zawadi alizompa zilimfurahisha sana Mary hivyo kumfanya asahau ile hali ya mwanzoni.
Kesho yake walifunga safari kurudi uwanja wa ndege tayari kwa safari ya Tanga ambako ndipo walipoweka makaazi yao ya kudumu. Walifurahia sana kuwepo Tanga baada ya dakika arobaini kuwepo angani wakielekea katika mji huo. Kwakuwa walifika mapema Siku yao ilikuwa ni njema sana na wakati wa jioni ulipofika waliamua kwenda kupunga upepo baharini. Mwahako ndiko walikojichagulia maana walipapenda sana. Walipofika walikuwa na wakati mzuri sana wa kupumzika ufukweni hapo, huku wakizungumza hili na lile kwa furaha. Mazungumzo yao kati yake na Mudy yalihusu masomo.
Walikumbushana mengi baada ya hapo hasa walipokuwa wakisomea nchini India miaka kumi iliyopita. Ramson aliwahudumia kama kawaida kwa vinywaji huku akimtupia Mary jicho la wizi. Mary alikuwa mtulivu sana jioni hii. Baadaye waliondoka na kurudi mjini wenye furaha kubwa. Kwa Ramson alikuwa na kidonda moyoni cha wivu, ambacho hakufikiria hapo mwanzo kuwa mapenzi yalikuwa yamebeba vitu kama hivyo.
Kwake kumwona Mary amekaa na mumewe na kukumbatiwa, moyo wake ulipata tabu sana kwa wivu wa kimapenzi. Tangu akiwa mdogo hakuwahi kushiriki mapenzi na mwanamke yeyote, kwa hiyo hakujua kuwa ndani ya mapenzi kuna kitu kibaya sana kiitwacho wivu. Alikuwa anasikia tu kwa watu kuhusu mambo ya wivu wa kimapenzi, kwake aliona ni ujinga wa hali ya juu sana kumwonea mwanamke wivu. Leo imekuwa zaidi ya kituko kwa kumwonea wivu mke ambaye hakuwa wa kwake. Alipotaka kupotezea hali hiyo iliibuka kama moto! Ilikuwa haiepukiki.
Kingine kilikuwa ni mtoto wake Lameck. Hakupenda kumwona yuko mikononi mwa baba mwingine, wakati yeye yupo. Hali ile ilimsukuma aone heri kuhamia mahali pengine ili awe salama. Aliona kwamba ikiwa ataendelea kuwepo mahali hapo iko siku kingetokea kitu cha ajabu. Hizo zilikuwa ni fikra tu zilizopita kichwani kwake na kumpa namna ya kuondokana na shari.
Alijua atakapokuwa nje ya Tanga atasahau taabu hizo, zinazosababishwa na wivu kwa Mary na Uchungu wa mtoto wake.“Lakini huyu mwanamke atakaponipatia hela zilizobaki kwake sitapata taabu kuwa mbali na ufukwe huu.” Alijisemea…“Kumwachia mtu mahali hapa apaendeleze na mimi kwenda mbali kwa miaka miwili ama mitatu kutanipa nafasi ya kusahau kila kitu.” Aliendelea kujipa ushauri ambao kwake ulikuwa wa busara sana.
Ramson aliendelea na shughuli zake akiwa tayari katika kujipanga kuondoka, maana aliamini kuwa Mary hatakawia kumkabidhi kiasi cha shilingi millioni kumi zilizobaki kwenye mapatano yao. Kichwani kwake aliwafikiria marafiki zake na kuangalia japo ampate mmoja atakayemwamini ili amwachie biashara zake ufukweni hapo. Alipanga akipata hela zake kutoka kwa Mary na kuchanganya na nyingine zilizoko Bank, aweze kwenda kuanzisha biashara eneo jingine ndani ya nchi hii, au nje ya nchi ikibidi.
Mawazo yake yaliendelea hadi alipokuwa kitandani usiku. Kutokana na mawazo mengi usiku huo aliotandoto nyingi sana za kutisha na zisizoeleweka vizuri. Ilimradi alikuwa katika changamoto ya pekee juu ya tatizo lake jipya. Hata ilipofika asubuhi hakuwa na raha hasa kwa kukosa japo simu kutoka kwa Mary ya kumjulisha kuhusu fedha zake kuwa atamletea lini. Kujitenga kwa Mary kulimpa mtihani mkubwa sana kwani alizoea ukaribu wake. Jambo jingine lililokuwa linampa shida ni juu ya Patano lao kuhusu kiasi cha fedha za malipo ya mwisho.
Mary hakumjulisha hata juu ya mumewe kuwa alikuwa amerudi hivyo ilimpa shida kujua kuwa Dr.Jackson ameingia lini nchini. Mawazo yaliendelea kupandana kichwani kwake na kumfanya aone kuwa Mary anataka kumgeuka juu ya mpango waliopatana. Lililomtatiza ni kukosa mawasiliano na Mary, hasa kwa kujulishwa tu juu ya mpango wao baada ya mumewe kurudi.
Kwa siku nzima alikosa rahasana na akashindwa kufanya jambo lolote la maana. Muda wote alikuwa akiguna tu na kukosa mwelekeo wa kufanya hata kazi zake kwa umakini. kazi muhimu alimpatia kijana wake azisimamie na kuwaongoza wafanyakazi wenzie wachache, kufanya usafi na kuweka eneo lile katika hali ya kuvutia wateja. Moyo wake ulikuwa ukimwuma sana kila alipokuwa akifikiria habari ya Mary na mtoto wake.
Ulikuwa ni usiku wa saa sita simu ya Mary ilipoita. Alikuwa kitandani, Mumewe alikuwa amelala fofofo! Mary alipoangalia kwenye kioo cha simu, alikutana na Jina Ramson! Haraka sana aliondoka kitandani hapo na kuelekea sebuleni na kuipokea simu ile. “Ramson unasemaje usiku huu wote? Aliuliza Mary kwa hamaki.
“Unanilazimisha wewe Mary kufanya hiv,i sio makusudio yangu! Tangu mumeo amerudi huonyeshi hata dalili ya kutimiza ahadi tuliyowekeana, hupigi simu wala ujumbe mfupi hutumi.” Alisema Ramson kwa kulalamika. “Samahani sana Ramson kwa hilo lakini kumbuka kuwa simu na ujumbe mfupi kwangu ni hatari sana. Dr. anakuwa na simu yangu kila wakati. Sipati mpenyo mwingine wowote.” Alijibu Mary kwa kujitetea.
“Kwa hapo Mary huwezi kunidanganya! ikiwa anakuwa na simu yako kila saa mbona umepokea wewe wakati huu? Potelea mbali kuhusu hayo yote, la msingi nahitaji uniambie ni lini utanipa hela zangu zilizobaki?” Aliuliza Ramson bila mzaha. “Naomba Ramson nivumilie ili nilifanyie kazi jambo hilo.” Alisema Mary kwa kubembeleza. “Siwezi kuvumilia zaidi ya hapa!” Alisema Ramson kwa hasira. “Ramson nitakuja kesho tutaongea vizuri sawa?”
Mary alisema maneno hayo kwa kunong’ona baada ya kusikia sauti ya mumewe kutoka chumbani akikohoa; kisha akakata simu. Ramson aliduwaa lakini ahadi ya kwamba Mary atakuja ufukwenikesho yake, ilimvutia japo bado kuna hatari alikuwa anaihisi katika jambo hilo. Alikuwa hana hamu tena kuendelea kuwepo mahali hapo, kutokana na matatizo yaliyopo.
Alihofia maisha yake kukatizwa kutokana na uhusiano huo mbaya uliozaa matunda ya mtoto. Alijua kuwa kwa vyovyote Dr. Jackson anaweza kufanya vipimo vya DNA ikiwa tu atashtukia jambo fulani kwa mtoto. Baada ya kugundua lazima hatari ingefuata maana asingevumilia. Kwa mawazo hayo Ramson alikusudia apewe hela zake ili aondoke kabisa katika mji huo.
Kuhusu biashara zake na mradi wake kwa ujumla ufukweni hapo, angeuacha kwa marafiki zake. Kuchelewa kwa Mary kumpatia hela zake ni kumfanya akaribie kwenye mdomo wa mamba; kitu ambacho ni hatari kubwa sana kwake. Alisubiri siku ya pili yake aone uaminifu wa Mary juu ya ahadi yake.
Mapambazuko ya siku hii yaliambatana na hamu ya kumwona Mary. Kila wakati alikuwa anaangalia njia, kuona labda Mary angekuja wakati huo. Kila aliposikia muungurumo wa gari aligeuka upesi akifikiri ni Mary amekuja. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu sana, mpaka kufikia mchana wa siku hiyo. Kuna muda alifikia kukata tamaa kabisa juu ya ujio wake ufukweni hapo.
Usiku kabla ya kulala Dr. Jackson alimwambia mkewe ajiandaye kwa safari ya kesho yake. “Mke wangu ni siku nyingi sana nimekuwa nje ya nchi. Alisema Dr. Jackson akakohoa kidogo kisha akaendelea.. “Natamani kesho twende Lushoto, Tukaangalie Hotel zetu na maendeleo yake. utakuwa wakati wetu mzuri sana wakwenda kupumzika, baada ya kutengana kwa muda mrefu.”
Alitoa wazo Dr. Jackson.“Mume wangu nashukuru kwa wazo lako zuri, nadhani hilo halina tatizo kabisa nitajiandaa.” Alijibu Mary kisha akaenda kabatini kuandaa nguo chache za kwake na za mumewe. Baada ya kuzifunga vizuri kwenye mabegi alirudi kitandani na kuungana na mumewe. Waliongea mengi na hatimaye wote walipitiwa na usingizi.
kilichomwamsha Mary ilikuwa ni simu iliyopigwa na Ramson. Alijua kuwa kama atayachukulia kimzaha malalamiko ya Ramson yangemharibia. Jambo aliloona ni la lazima ni kutafuta kisingizio cha kutokwenda Lushoto na mumewe. Mwisho wa yote akaona kujifanya mgonjwa ndiyo njia pekee itakayompa mwanya wa kubaki.
Baada ya muda alianza kujiliza akijifanya anaumwa na Tumbo. Hata mumewe alipoamka alimkuta mkewe katika hali hiyo.Alipohoji tatizo Mary alisema kuwa anaumwa na tumbo. “Kama linakuuma sana basi nikupeleke ukapimwe Hospital ijulikane kuwa ni nini?” Alisema mumewe kwa msisitizo akimhimiza mkewe ajiandae waende Hospitali. “Usiwe na wasiwasi mume wangu hali hii sio ya kwenda Hospital.” Ni majira yake na halitadumu kwa muda mrefu zaidi ya siku mbili tu ya tatu linatulia kabisa. Alisema Mary na mumewe alimwelewa.
“Sawa mke wangu nimekuelewa sasa itabidi basi Lushoto niende peke yangu? Nitakuja baada ya siku mbili kwa kuwa Hoteli zote mbili kuzikagua ni kazi kubwa.” Alisema Dr. Jackson. Sawa mume wangu ila siku mbili nitakukosa sana! Japo pia kuna umuhimu mkubwa wa kutembelea Hotel zetu, maana kwakweli taarifa za kupewa tu hazitoshi.” Mary aliongea hivyo na baada ya muda alimwandalia mumewe chai mezani. Baada ya kuoga na kunywa chai hiyo alipakiza begi lake kwenye gari na kumuaga mkewe na kumbusu mtoto kisha akaondoka zake.
Asubuhi baada ya mumewe kuondoka, Mary alimpigia Ramson Simu kuwa anakuja. Ramson alifurahi kuwa hatimaye atapewa fedha zake. Mnamo saa tano za asubuhi Mary alikuwa barabarani kwenda Mwahako Beach. Mwendo wake ulikuwa wa kasi sana lakini alipofika mwakidila alikutana na ajali ya pikipiki na baiskeli watu wengi walikusanyika mahali hapo kwa wingi.
Kwakuwa waliogongana walikuwa wamelala barabarani aliteremka ili aone majeruhi hao. Baada ya muda majeruhi wale waliondolewa na kuruhusu magari kupita. Dr. Mudy aliyekuwa akitoka Pangani alipita mahali pale kwa kasi lakini macho yake yalimwona Mary Mke wa rafiki yake. Kwanza alianza kuiona gari yake na kisha baada ya kuangalia sana akamwona Mary akielekea iliko gari yake.
Alipopita kidogo alisimamisha gari kando ya barabara na kuangalia mwelekeo wa shemeji yake. Alipomwona akipinda kushoto mahali ilipo Mwakidila sokoni alijua kuwa alikuwa akielekea Mwahako Beach. Baada ya kuona hivyo ilimsikitisha sana maana alijua kuwa rafiki yake Dr. Jackson alikuwa akiibiwa na Beach Man. Hali hiyo ilimtia uchungu kutokana na taarifa aliyopewa na rafiki yake Jackson, kuwa alikuwa aende Lushoto na mkewe lakini tatizo ni kwamba mkewe alikuwa akiumwa.
USIKOSE SEHEMU IYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi