Mwandishi: Andrew Mhina
SEHEMU YA KUMI NA SITA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“Unaona sasa! Kwenye kitabu cha kupokea wageni kinaonyesha kuwa ni zaidi ya mara ishirini tumeingia mkataba na wageni toka nje ya nchi wa kukaa kwa muda mrefu. Wengine walikaa wiki mbili wengine walichukuwa Hoteli nzima kwa miezi mitatu.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
Hawa hapa walikaa kwa miezi miwili. waliokaa kwa muda wa miezi miwili miwili walikuwa watalii kutoka Nchini Marekani. Watalii hawa walikuja kuendesha semina za mambo ya ukimwi. Walichukuwa Hoteli nzima kwa muda wote huo. Wengine walitoka Austaralia hawa walikuja kufanya utafiti wa wadudu wanaoeneza magonjwa, kwa wanyama kama vile Ng’ombe, mbuzi na kondoo.
Hawa walikuwa watu mia moja na kumi, hivyo iliwalazimu kuchukuwa Hotel nzima waliobaki tuliwapeleka kwenye Hotel yetu nyingine. Kwa ujumla Bosi hao ndio wageni wetu waliotutembelea katika kipindi chote hicho.” Alisema Meneja huku akimalizia kuweka idadi kamili, katika karatasi moja na kumkabidhi bosi wake.
Kiasi cha fedha kwenye akaunt kimefikia shilingi ngapi kulingana na kazi zilizofanyika?” Aliuliza Dr. Jackson. Fedha zote zilizoko Bank nimekuwa nimeorodhesha kwenye kitabu cha mahesabu. Nimejitahidi kuhifadhi risiti za manunuzi ya vitu vya matumizi, faida nimeweka kwenye Akaunti. Kumbukumbu nimeweka kwenye kitabu hiki.” Alionyesha kitabu kikubwa cheusi. Alisema Meneja. Kiasi chote cha akiba iliyoko Bank ni hii hapa. Alimwonyesha kila kitu jinsi alivyotunza mahesabu.
Baada ya kumpa kitabu cha akiba iliyopo, alimpa kitabu kingine cha mchanganuo wa mapato na matumizi. Mwisho wa yote Dr. Alimpongeza sana Meneja wake kwa kufanya kazi nzuri sana. “Kazi yako ni nzuri sana. Endelea na shughuli mimi ninataka nikamilishe kuangalia Hotel ile nyingine. Nahitajika nirudi mjini Tanga maana nahitajiwa kazini.” Alisema Dr. Jackson. “
Ila bosi nimekuwa nikijiuliza kila siku mambo mengi sana ninakosa majibu. Wewe ni tajiri sana mwenye Miradi mingi kiasi hiki, lakini bado unafanya kazi ya kuajiriwa! Kwanini usitulie ukaangalia miradi yako?” Samahani bosi kama nitakuwa nimeingilia maisha yako binafsi.” Alisema Meneja wakati wanaagana.
“Bila samahani ni watu wengi wananiuliza swali hilo sio wewe tu. Unajua kazi ya Udaktari ni sehemu ya wito kwa ajili ya kuwasaidia binadamu wenzetu? Aliuliza kisha akaendelea. “Wito ni kitu cha ajabu sana, humuendesha mtu kwa ndani ya nafsi yake na mtu huyo akakosa maamuzi sahihi zaidi ya kuutimiza wito huo. Ndani yangu ninasukumwa na huruma kwa watu wanaoteseka kwa magonjwa.
Nikiwa nje ya kazi hii ninajiona kama sijakamilika, ikiwa tu sijafanya jukumu langu la kuwasaidia watu wanaoteseka. Hilo ndilo linalonisumbua na kunifanya niendelee kuwepo kazini. Hata kama ningekuwa na utajiri kiasi gani hauwezi kunifanya nikaacha kufanya kazi yangu ya Udaktari.” Alisema Dr. Jackson na kumalizia kwa kumpa mkono wa kwaheri Meneja wake. Asante mzee kwa kunijibu. Una moyo wa ajabu sana Bosi wangu.”
Alimaliziakuzungumza wakati Dr. akifunga mkanda na kuliwasha gari kisha kuliondoa kwa mwendo wa taratibu. Njiani aliwapungia mkono wafanya kazi wake waliokuwa wakifanya usafi na kuendelea na safari yake. Ukaguzi wa hoteli yake nyingine, ulikuwa ni hali kadhalika na baada ya kumaliza kukagua kila kitu aliondoka jioni ya siku ya pili tangu afike Wilayani hapo.
Fedha zilikuwa ni nyingi za faida alizozipata kwa kipindi chote hicho kiasi kwamba alifikiri kuanzisha mradi mwingine mkubwa sana. Alijaribu kufikiri akiwa kwenye gari lake, huku akipiga mluzi taratibu kufuatisha mziki uliokuwa ukipigwa na Mwanamuziki Mbiliabel.
Mary baada ya kurudi kutoka ufukweni alijipanga na kumpigia rafiki yake Irene simu kusudi waonane. “Kwani una haraka sana ya kuonana na mimi sasa hivi? Kama unaweza kusubiri niende mara moja Bank maana kuna Fedha zinatakiwa za marejesho Pride.” Alisema Irene baada ya Mary kumwambia anataka waonane ndani ya muda huo. “Mazungumzo yangu ni marefu na yanahitaji tuyaongee mapema sijui utafanyaje?” Aliuliza Mary kwa sauti ya chini yenye dalili kuwa amebanwa sana na jambo.
Irene kwa kuzingatia uzito huo aliouonyesha rafiki yake akamwambia: “Kwani kuna tatizo gani rafiki yangu? au mambo yameharibika?” Alisema Irene akisukumia na utani ambao ulifanana na ukweli. “Ninashukuru kama umekubali tuonane mengine tutaongea tukikutana.” Alisema Mary na kukata simu. Baada ya hapo aliingia kwenye gari lake na kuanza safari kuelekea kwa Irene.
Alienda kwa mwendo wa kasi kusudi amwahi rafiki yake. muda haukuwa mrefu sana alifika nyumbani kwake na kumkuta Irene Sebulen akiwa kakaa mkao wa kutaka kuondoka. “Wooooow Mary” Alisema Irene na kumkubatia rafiki yake… “Karibu sana naona leo huko kwenye hali yako ya ucheshi unanini” Alisema Irene baada ya kumkaribisha Mary kwenye moja ya sofa.
“Sio hali mbaya sana, ilibidi tu nikuone japo tupeane maarifa. Alisema Mary kwa unyonge. “Kuhusu nini sasa?” Aliuliza Irene akiwa na shauku ya kujua. “Rafiki yangu sasa hivi niko njia panda na sijui ni njia gani nitapita ili niokoke! Mpaka sasa Ramson ananidai kile kiasi cha shilingi millioni kumi, na amenikalia kooni kwelikweli hana utani kabisa. Lengo la Ramson anataka akimbie mji maana hana uhakika na maisha yake kama anavyodai mwenyewe. Nimempa siku tatu za kumlipa hela hizo, lakini mpaka sasa bado sijajua nitaanzia wapi kumwomba Mume wangu kiasi chote hicho.”
Alisema Mary katika hali ya majonzi akihitaji ushauri kutoka kwa Irene rafiki yake. “Pole sana Mary! Labda utakuwa unakumbuka maneno yangu, nilikuambia tangu mwanzo kuwa hukupaswa kumwambia Ramson kuwa una mimba yake. Ungezingatia yote haya yasingelitokea.” Irene alimwambia Mary kwa masikitiko.
“Ni kweli rafiki yangu lakini Waswahili wanasema: “Maji yakishamwagika hayazoleki.” Nimejuta sana juu ya hilo na kila wakati ninakumbuka ushauri wako, lakini majuto yangu hayawezi kubadilisha lolote kwa sasa. Kinachotakiwa ni kupata njia mpya ya jinsi ya kujikwamua kutokana na matatizo haya, nishauri ndugu yangu!” Alisema Mary kwa uchomvu wa mawazo. “Sawa rafiki yangu labda twende katika Pointi yenyewe.
Jioni Mr. wako atakaporudi ongea naye umwambie kuwa, kuna biashara tumeamua kuifanya ya kuleta vipodozi na kuviuza kwa jumla. Na kwamba bidhaa hizo tunazitoa nchini China. Mpe mchanganuo mzima wa mtaji unaohitajika na faida zitakazopatikana kutokana na biashara hizo. Kwa sasa tuandae mchanganuo huo, kisha nitauprint na kukupatia ili ukampe mumeo.”… Alisema Irene kisha akameza mate wakati huo Mary alikuwa amemtazama tu usoni.
“Kwenye huo mchanganuo nitaweka kiasi cha mtaji kama milioni Thelathini na tiketi itakuwa ni shilingi million tano. Mpaka kufikia hapo mimi hela zangu nitakuwa nazo tayari, kwa hiyo utamwambia kuwa ulikuwa unamsubiri kusudi umweleze jinsi tulivyopatana.” Alisema Ireni huku akimwangalia Mary usoni kuona kwamba maneno yale yamemwingia.
“Hapo umenipa njia. Kweli ninavyomjua ni kwamba hawezi kugoma, ila anachotaka mara nyingi ni kupewa mchanganuo wa kile kinachohitajika kufanywa. Unanishauri baada ya kupewa hela hizo nifanyeje?” Aliuliza Mary. “Ufanyeje tena!?” Alisema Irene kwa kushangaa!…“Lengo la yote haya ni ili upate hela za kumlipa Ramson!
Ninavyofahamu ni kwamba mumeo hakufuatilii katika miradi yako wala biashara zako. Kwa hiyo kwako ni njia nzuri sana ya kuondoa tatizo lililopo la huyu Ramson.Si ndiyo shida iliyopo kwa sasa?” Alisema Irene huku akitabasamu. “Hapo mwenzangu umenisaidia sana rafiki yangu.”
Alisema Mary huku akiungana na rafiki yake katika kutabasamu. Wewe ni Mbunifu sana wa mambo! Hiyo ni mbinu kabambe ambayo itanisaidia kuniondoa kwenye matatizo, Asante sana rafiki yangu.” Alisema Mary huku akionyesha uso wa matumaini. Irene alinyanyuka na kuingia ofisini kwake.“Jichukulie mwenyewe juisi hapo Frijini wakati nikiandaa Mchanganuo sawa?” Alisema kabla hajaingia na baadaye akatokomea ndani.
Ilikuwa ni ujumbe mfupi uliomshtua kwenye mawazo yake. Mawazo muhimu sana ya kupangilia namna ya kuanza mradi mkubwa, kulingana na fedha nyingi alizopata. Wimbo wa Mbiliabeli uliendelea kujirudia kweye Redio huku Dr. Jackson akiutolea kibwagizo kwa mluzi!Alichukuwa simu yake huku akiwa amekasirika kidogo. Baada ya kuifungua simu yake akakuta ujumbe mfupi kutoka kwa Dr.Mudy.
Ujumbe wenyewe ulikuwa na maneno machache sana, yaliyosomeka hivi: “Rafiki yangu kama umerudi fanya kila njia tuonane kwenye Hoteli ya Mkonge jioni hii, kuna habari nyeti sana nikuambie. Zingatia kuwa ni muhimu.”
Baada ya kusoma akairudisha simu mahali pake huku akiwaza ninini anachoitiwa na rafiki yake? “Ni jambo gani hilo la Muhimu tena?” Alijiuliza Dr. Jackson huku akikerwa na wito huo bila kujua kuwa unahusu nini.” Alifika nyumbani alasiri akiwa na uchomvu wa safari. Jioni hii alimkuta mkewe amechangamka sana. Lakini hakutaka kukaa sana maana wakati alioambiwa wakutane na Mudy ulikuwa umefika.
“Mbona unaondoka mapema kiasi hiki hata hujapumzika? halafu nina mazungumzo mazuri sana ambayo ungeyafurahia mume wangu.” Alisema Mary kwa hali ya deko.“Sawa Honey nitakaporudi baadaye tutakaa tuongee sawa? Kwa sasa nimeitwa na rafiki yangu Mudy amesema kuwa ana mambo muhimu sana ya kuzungumza na mimi.” Dr.Jackson alisema kwa kusihi ili apate nafasi ya kwenda kumwona Mudy.
“Mtoto yuko wapi?” Aliuliza kwa kumalizia akitaka kutoka. “Yuko chumba cha michezo anacheza.” Alijibu Mary. Mara hiyo Dr. Jackson akarudi na kuingia chumba cha michezo, alimkuta Lameck anachezea magari yake ya kitoto. Jambo Lameck? Alisema Dr. Jackson na Lameck akaitika na kumsalimia baba yake. Jackson alimbeba na kumpa zawadi alizomnunulia, kisha akatoka na kuingia kwenye gari kisha, akaiondoa kwa mwendo wa kasi kidogo.
Alifika mkonge baada ya muda mfupi maana kutoka mahali alipoishi na Hotelini hapo sio mbali sana. Baada ya kupaki gari mahali pake aliondoka na kwenda kwenye bustani iliyopo nyuma ya Hoteli hiyo kubwa. Kufika hapo alimkuta rafiki yake akiwa anamsubiri. “Kumbe umeshafika!” Jackson aliuliza huku akishangaa. “Zamani sana mbona?” Alisema Mudy huku akinyanyuka kwenye kiti na kumsalimia rafiki yake.
Baada ya kupeana mikono walikaa na wakati huo huo mhudumu alikuwa ameshafika kutaka kuwahudumia. “Niletee Malta Guiness ile isiyo na kilevi sawa?” Alisema Dr. Jackson. “Na mimi vilevile aliagizia Mudy na mara hiyo mhudumu akaenda kuwachukulia vinywaji. “Habari za Lushoto rafiki yangu?” Mudy aliuliza wakati akijiweka sawa kwenye kiti. “Habari sio mbaya ni nzuri sana rafiki yangu.Lushoto ni kuzuri sana baridi ya kule kama Uingereza nilikotoka.
USIKOSE SEHEMU IYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi