NISAMEHE LATIFAH (1)

0
Mwandishi: Nyemo Chilongani

SEHEMU YA KWANZA
Msichana mrembo mwenye asili ya Kihindi, Nahra Patel alikuwa akilia huku akikimbia kwa kasi kuelekea sehemu kulipokuwa barabara ya lami. Jasho lilimtoka, alikuwa akihema kwa nguvu, japokuwa alionekana kuchoka lakini hakutaka kusimama.

Miguuni mwake hakuwa na viatu na alikimbia katika sehemu zilizokuwa na mibamiba, lakini Nahra hakusimama, aliendelea kusonga mbele, cha ajabu hata miba haikumchoma, na kama ilimchoma, hakusikia maumivu yoyote yale.

Machozi yalitiririka mashavuni mwake, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hakuamini msichana mrembo kama yeye, aliyesifiwa na wanaume kwamba alikuwa mithili ya malaika, leo hii alikuwa amefukuzwa kama mbwa na mwanaume ambaye kila siku alimuona kuwa ndoto ya maisha yake.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

“Deo, mimi? Hapana! Kwa nini? Nimekufanya nini?” aliuliza maswali mfululizo lakini hakupata jibu, wakati huo alikuwa akikaribia barabara ya lami.

Alipofika barabarani, akatulia chini, pembezoni kabisa mwa barabara hiyo na kuanza kulia huku akiwa amekiingiza kichwa chake katikati ya mapaja yake. Machozi yaliendelea kumtoka, kila alipokumbuka namna alivyokimbizwa na mwanaume aliyemchukulia kama mume wake wa baadaye, moyo wake ulimuuma mno.

Hakuwa na sehemu ya kwenda na wala hakuwa na fedha. Wazazi wake hawakutaka kumuona kabisa kwa sababu alikuwa amebeba mimba ya kijana mwenye ngozi nyeusi na wakati yeye alikuwa Mhindi.

Mapenzi yake ya dhati, kung’ang’ania kwake kuwa na Deo ndiyo kulimfanya leo kuwa katika hali hiyo. Hapo barabarani, alikuwa mtu wa kujuta tu, kila alipokumbuka maisha aliyopitia, alibaki akimlaani Deo.

“Ubungo buku…Ubungo buku,” ilisikika sauti ya kondakta wa daladala moja iliyokuwa ikipita mahali hapo.

Nahra akauinua uso wake na kuiangalia daladala iliyosimama mbele yake, akasimama na kuanza kuifuata, alipoifikia akaingia ndani na kuondoka.

Ndani ya daladala, kila mwanaume alikuwa akimwangalia kwa matamanio, alikuwa msichana mrembo wa Kihindi mwenye sifa zote za kuitwa Malkia Cleopatra. Kwa sababu ilikuwa ni usiku na gari halikuwa na taa ndani, hakukuwa na mtu aliyeyaona machozi yake japokuwa uzuri wake ulionekana.

“Unalia nini tena Kajool?” aliuliza mwanaume aliyekaa naye, alimuita jina la muigizaji maarufu wa kike wa filamu za Kihindi, Nahra hakujibu swali hilo, bado kilio cha kwikwi kiliendelea kusikika.

Kuanzia hapo Kibaha mpaka anaingia Dar es Salaam, alikuwa mtu wa kulia tu, kumbukumbu za maisha aliyokuwa akiishi na Deo zilijirudia kama mkanda wa filamu kitu kilichomuumiza na kumliza zaidi.

Mpaka daladala inaingia Ubungo, tayari ilikuwa saa mbili usiku, Nahra akateremka na kusimama kituoni pamoja na watu waliokuwa wakisubiri usafiri.

“Niende wapi?” alijiuliza Nahra, jibu lililokuja ni kwamba alitakiwa kwenda kwa wazazi wake waliokuwa wakiishi Masaki.

Baada ya dakika kumi, akapanda daladala iliyokuwa ikielekea Masaki na safari ya kuelekea nyumbani kwao kuanza. Kama kawaida, bado alikuwa mtu wa kulia tu, kilio chake cha kwikwi hakikuisha, baada ya dakika thelathini, akafika nje ya geti la nyumba yao, akaanza kugonga.

“Nahra, umefuata nini, baba yako ataniua,” aliuliza mlinzi aliyefungua geti, hakuamini kumuona Nahra mahali hapo tena.

“Naomba niingie, nataka kuonana na baba,” alisema Nahra.

“Hapana. Naogopa Nahra. Siku ile alitaka kunipiga risasi, siwezi kukuruhusu,” alisema mlinzi huyo huku akianza kulifunga geti hilo.

“Ninataka kuingia ndani Chichi, niache niingie nikaongee na baba yangu,” alisema Nahra huku akianza kulia tena, akaanza kulisukuma geti ili mlinzi asilifunge.

Msimamo wa mlinzi ulikuwa uleule, hakutaka kumruhusu Nahra kuingia ndani. Baada ya kulazimisha sana tena kwa kusukumana, Nahra akafanikiwa kuingia ndani ya eneo la nyumba yao. Akaanza kuufuata mlango wa kuingilia sebuleni na kuanza kuugonga.

Baada ya dakika tano, mlango ukafunguliwa na wazazi wake wote wawili kutoka ndani. Macho yao yalipotua kwa binti yao aliyekuwa akilia huku akiomba msamaha, baba yake, mzee Patel akabadilika, akakunja uso kwa hasira.

“Umefuata nini hapa? Umefuata nini wewe mbwa?” aliuliza mzee Patel huku akionekana kuwa na hasira kali, Nahra hakujibu kitu, alichokifanya mzee huyo ni kurudi ndani, kama kawaida yake alikuwa ameikumbuka bunduki yake.

Mama yake, bi Aishani alimtaka Nahra aondoke kwani alijua fika mumewe alifuata bunduki lakini Nahra hakutaka kuondoka, alikuwa tayari kupigwa risasi na kufa, ila si kuondoka nyumbani hapo.

Msimamo wa Nahra ulikuwa palepale, hakutaka kuondoka mahali hapo, alikuwa radhi kumuona baba yake akimpiga risasi na kufa lakini si kukubali kirahisi kuondoka nyumbani hapo.

Alikuwa akilia, alijiona kunyanyaswa kwa kile kilichotokea, kitendo cha kutengwa na ndugu zake kisa alikuwa na mimba ya mtu mweusi kilimuumiza mno.

Hakukuwa na mtu aliyemuelewa, hata mama yake, mtu pekee aliyekuwa akimuonyeshea mapenzi ya dhati siku za nyuma, katika suala hilo alikuwa tofauti naye.

Mlango ukafunguliwa, mzee Patel kutoka huku mkononi akiwa na gobole, alichokifanya, huku akionekana kutetemeka kwa hasira, akamnyooshea Nahra gobole lile tayari kwa kumfyatulia risasi.

“Niue tu, we niue baba, ila jua kwamba nilimpenda Deo na nisingeweza kumuacha, kama mnaona nilifanya makosa, wewe niue tu kwani hata wewe utakufa tu,” alisema Nahra, alikuwa amepiga magoti huku akilia kama mtoto.

Bila bi Aishani kulipiga gobole lile, basi risasi iliyotoka ingeweza kumpiga Nahra kifuani. Mdomo wa gobole ukaenda pembeni, risasi ikatoka na kupiga ukutani. Japokuwa mtoto wao alikuwa amefanya makosa yaliyoonekana kuwa makubwa kwa kuzaa na mtu mweusi lakini hakuwa radhi kumuona Nahra akipigwa risasi na kufa.

“Punguza jazba,” alisema bi Aishani huku akimsihi mume wake asimuue Nahra.

“Usinizuie, niache nimuue huyu malaya, ametuzalilisha sana, acha nimuue,” alisema mzee Patel huku akionekana kuwa na hasira mno.

Bado Nahra aling’ang’ania kubaki mahali hapo, hakuwa na pa kwenda usiku huo, kama walivyokuwa wazazi wake, hata ndugu zake wa Kihindi walikuwa wamemtenga, sababu ilikuwa ni ileile ya kuwa na mimba ya mwanaume mweusi.

Mbali na ndugu zake, mwanaume aliyekuwa amempa mimba, Deo alikuwa amemfukuza nyumbani kwake. Hakutaka kuondoka, kama kuuawa, alikuwa tayari kufa lakini si kuondoka nyumbani hapo.

“Chichi, mtoe huyu mbwa mara moja,” alisema mzee Patel, mlinzi akasogea Nahra na kumshika Nahra, akaanza kumbeba juujuu.

Japokuwa hakupendezwa na jambo lile lakini hakuwa na jinsi, alitekeleza amri ya bosi wake kwamba Nahra alitakiwa kutolewa ndani kinguvu.

“Niacheeee, nimesema niacheeee, nimesema sitokiiiiiiiii,” alisema Nahra huku akipiga kelele.

Hiyo wala halikusaidia, Chichi akafanikiwa kumtoa Nahra ndani ya nyumba hiyo. Kwa sababu mvua ilianza kunyesha na ardhi kuanza kulowanishwa na maji, Nahra hakujali, akakaa chini na kuendelea kulia.

Katika maisha yake yote, hicho kilikuwa kipindi kigumu kuliko vyote, hakuamini kama kweli wazazi wake walimfukuza kama mbwa kisa tu alizaa na mwanaume mweusi. Hata kama alikuwa Muhindi, akajikuta akianza kuwachukia Wahindi wote kwa kile alichokuwa amefanyiwa.

“Sitorudi tena nyumbani na sitorudi tena kwa Deo, acha niendelee na maisha yangu,” alisema Nahra na kisha kusimama, akaanza kuondoka.

Alitembea kwa mwendo wa taratibu, mvua kubwa iliendelea kunyesha na kumlowanisha mno lakini hakusimama sehemu kwani nyumba zote za Masaki zilikuwa za kifahari zilizokuwa na uzio mkubwa.

Wakati mwingine alijuta kupewa mimba na Deo kwa kuwa tu jamii yake ilimtenga lakini kuna kipindi aliona kwamba hakutakiwa kujilaumu, kile kilichokuwa kimetokea, kilitokea hivyo alitakiwa kusonga mbele.

Dakika ziliendelea kusonga mbele, mpaka anafika kituoni, tayari ilikuwa ni saa tano usiku, akakaa hapo na kuanza kusubiri daladala japokuwa mkononi hakuwa na fedha yoyote ile. Baada ya dakika thelathini, daladala ndogo (hiace) ikasimama hapo na kupanda.

Safari ya kuelekea Magomeni ikaanza, hakuwa na ndugu yeyote lakini kitu pekee alichokitaka ni kufika huko tu. Mawazo yalimtawala, hakujua ni sehemu gani alitakiwa kwenda kuishi. Huku akifikiria ni wapi alitakiwa kwenda, kichwani mwake likaja jina la mwanaume mmoja, huyu aliitwa Mithun, mwanaume wa Kihindi ambaye alimpenda lakini alimkataa kwa sababu alikuwa na Deo.

“Nitakwenda Kariakoo kwa Mithun, nitamuomba anisaide,” alijisemea Nahra.

Alipofika Magomeni, akadaiwa nauli lakini hakuwa nayo. Kondakta hakuwa mkorofi, kwa muonekano wa Nahra alionekana kuwa na matatizo, akamruhusu kuondoka, safari ya Kariakoo ikaanza huku ikiwa ni saa nne usiku.

Akaanza kutembea kwa miguu, sehemu pekee aliyokuwa akiihofia ilikuwa ni Jangwani tu. Huku akiwa amefika maeneo hayo ya hatari, mbele yake akawaona vijana wawili wakiwa wamesimama, naye akasimama, ila kabla hajafanya kitu chochote, akashtukiwa akipigwa kofi moja zito kwa nyuma.

Wakati anaugulia maumivu, akajikuta akibebwa msobemsobe na kuingizwa vichakani, wanaume wengine wanne waliokuwa na pensi walikuwa wakimsubiri huku wakionekana kuwa na tamaa ya ngono, walitaka kumbaka Nahra. Alijaribu kupiga kelele ili asaidiwe lakini hakukuwa na msaada wowote ule.

Nahra aliendelea kupiga kelele, wanaume wanne waliokuwa wamesimama mbele yake walikuwa wakihangaika kufungua bukta zao huku wakizichana nguo zake. Hakukuwa na mtu yeyote aliyesikia kelele hizo alizokuwa akipiga japokuwa zilitoka kwa sauti ya juu.

“Naanza mimi,” alisema mwanaume mmoja.

“Fastafasta, usinogewe na mtoto wa Kihindi,” alisema jamaa mwingine.

Usiku huo ulikuwa ni usiku wa kuumiza mno maishani mwake, wanaume hao wanne wakaanza kumuingilia kinguvu tena kwa zamu. Alipomaliza huyu, alikuja yule.

Nahra alisikia maumivu makali, kiuno chake kikaanza kukaza, kelele alizokuwa akizipiga, zikaanza kupungua kwani kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo alivyokuwa akiumia zaidi.

Hakuchukua muda mrefu, huku akiendelea kuingiliwa kichakani pale, mbele yake akaanza kuona giza, akajitahidi kuyafumbua macho yake, haikuwezekana, hapohapo akapoteza fahamu huku wanaume wale wakiendelea kumuingilia kama kawaida, tena kwa zamu.

Deo alikuwa kimya chumbani kwake, machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake, hakuamini kile kilichotokea, kumfukuza Nahra nyumbani kwake kilikuwa moja ya vitendo kilichomuuma mno.

Alimpenda Nahra kwa mapenzi ya dhati, hakuwa tayari kumuona msichana huyo akipata shida yoyote ile, japokuwa alikuwa msichana wa Kihindi, kwake haikuwa tatizo, alikuwa akimpenda hivyohivyo.

USIKOSE SEHEMU IYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)