Mwandishi: Nyemo Chilongani
SEHEMU YA MBILI
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Deo alikuwa kimya chumbani kwake, machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake, hakuamini kile kilichotokea, kumfukuza Nahra nyumbani kwake kilikuwa moja ya vitendo kilichomuuma mno.
Alimpenda Nahra kwa mapenzi ya dhati, hakuwa tayari kumuona msichana huyo akipata shida yoyote ile, japokuwa alikuwa msichana wa Kihindi, kwake haikuwa tatizo, alikuwa akimpenda hivyohivyo.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
Wazazi wa Nahra walionekana kuwa tatizo kwake. Mara baada ya kumpa mimba msichana huyo na kuhamia kwake kwa kuwa wazazi wake walimfukuza, wazazi hao wakawatuma wanaume wawili waliokuwa na bunduki, walichokuwa wakikitaka ni kuona Deo akimfukuza Nahra nyumbani hapo, vinginevyo, wangemuua.
Huo ulikuwa mtihani mkubwa maishani mwake, alimpenda Nahra, hakutaka apate tabu yoyote ile, kitendo cha kuambiwa amfukuze msichana huyo kilikuwa kigumu, akakataa.
Watu hao walipoona kwamba kitu hicho hakikufanyika, wakarudi kwa mara ya pili, wakati huu walionekana kuwa na hasira zaidi, kila walipomwangalia Deo usoni, waliyakumbuka maneno ya mzee Patel ambaye aliwaambia wamuue tu.
“Kijana, fanya tunachokwambia. Tumeagizwa tuje kukuua, hatuwezi, tunakuonea huruma. Fanya hivyo, tunakupa siku moja ya ziada, kesho tukija, tunakuja na sura tofauti na hizi,” alisema mwanaume mmoja huku akimwangalia Deo usoni.
Kwa jinsi walivyoonekana, kwa maneno yao yaliyowatoka midomoni mwao ilionyesha kabisa watu hao walimaanisha kile walichokiongea, Deo akakubaliana nao kishingo upande.
Siku hiyo usiku ndiyo ilikuwa siku ya kumfukuza Nahra nyumbani hapo. Alifanya hivyo huku moyo ukimuuma mno, kila alipomwangalia msichana huyo, alijisikia huruma, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali.
“Nahra, naomba unisamehe, sikutaka kukufukuza, wazazi wako ndiyo waliolazimisha kufanya hivi, ninakupenda Nahra,” alisema Deo huku akimuona Nahra akikimbia, machozi yalikuwa yakimmbubujika msichana huyo, baada ya hapo, hakujua Nahra alikimbilia wapi, usiku huo, kwake ukawa usiku wenye mateso mengi.
“Nitamtafuta tu,” alisema Deo huku akijipa uhakika kwamba angeweza kumuona tena Nahra aliyekuwa na mimba yake.
Nahra alikuja kupata fahamu asubuhi, alikuwa katika majani yenye unyevuunyevu, mwili wake ulikuwa ukimuwasha. Pamoja na kuwashwa huko, alikuwa akisikia maumivu makali chini ya kitovu.
Akaanza kujiuliza sababu ya yeye kuwa mahali hapo, hakukumbuka kitu chochote kile, alibaki akishangaa mpaka kumbukumbu zilipokaa sawa na kuanza kukumbuka kila kitu kilichotokea usiku uliopita, Nahra akaanza kulia, akajiangalia, sehemu zake za siri zilikuwa zimeharibiwa vibaya, akaendelea kulia mfululizo huku akijiinua kuelekea barabarani.
Kila mtu alibaki akimshangaa, alionekana msichana mrembo mno lakini muonekano wake ulikuwa tofauti kabisa, alikuwa msichana mchafu mno, kwa jinsi uzuri wake ulivyokuwa, hakutakiwa kuwa kama alivyokuwa.
“Hata kama nimechafuka na hata kama nimebakwa, bado ninahitaji kumuona Mithun, ni lazima nimfuate na anisaidie, sina kimbilio jingine zaidi yake,” alisema Nahra.
Kila alipopita, watu walimshangaa, hakuwa akitembea kawaida, alikuwa akichechemea kama mtu aliyekanyaga mwiba. Alitembea hivyohivyo mpaka alipofika maeneo ya Fire ambapo akaunganisha mpaka Mtaa wa Twiga, mtaa uliokuwa na maghorofa mengi, huko ndipo alipokuwa akiishi Mithun.
“Mungu, naomba Mithun anikubalie, anisamehe kwa kila kitu niweze kuwa naye, asahau kila kitu kilichotokea maishani mwetu,” alisema Nahra, tayari alikuwa amefika katika mlango wa nyumba ya kina Mithun, akaanza kugonga mlango, moyo wake ulijawa hofu.
Wala hazikupita dakika nyingi, mlango ukafunguliwa, mtu aliyekuwa akimuhitaji ndiye aliyefungua mlango, alikuwa Mithun.
Mwanaume huyo alibaki akimwangalia Nahra huku uso wake ukiwa kwenye mshangao mkubwa. Hakuamini kama yule aliyesimama mbele yake alikuwa Nahra yule aliyekuwa akimfahamu au alikuwa mtu mwingine.
Alikuwa mchafu mno, nguo zake zilikusanya majanimajani huku zikiwa zimetapakaa tope, kwa kumwangalia tu, Mithun alijisikia kinyaa.
“Nikusaidie nini?” aliuliza Mithun huku akijitahidi kujizuia kupumua kupitia pua yake, maji yaliyokuwa yameilowanisha nguo ya Nahra, yalikuwa yakinuka.
“Naomba unisamehe,” alisema Nahra huku akijitahidi kupiga magoti chini.
Alikuwa akilia kwa maumivu makali, alijua kwamba alifanya makosa kumkataa mwanaume huyo aliyekuwa na lengo la kumuoa na kumkubali Deo aliyekuwa amemfukuza kama mbwa.
Macho yake yalionyesha kila kitu, alikuwa akiomba msamaha lakini Mithun hakujali. Alikumbuka vema kila kitu kilichotokea katika maisha yake ya nyuma na binti huyo.
Alimpenda Nahra na kuahidi kumuoa lakini maamuzi ya msichana huyo yalikuwa kwa Deo, mwanaume mweusi aliyempa mimba na kumtimua.
“Unanuka Nahra,” alisema Mithun maneno yaliyomuumiza mno Nahra, ila kwa kuwa alikuwa na uhitaji, akavumilia.
“Naomba unisamehe Mithun.”
“Nikusamehe ili iweje? Na hicho kitumbo ukipeleke wapi? Nikusamehe wewe? Ulivyonikataa kwa maneno ya dhihaka! Nahisi umepotea njia. Kwanza unanuka sana, hivi ulioga jana?” alisema Mithun na kuuliza kwa dharau.
Kilio cha Nahra kikaongezeka zaidi, hakuamini kama maneno yale yote yalitoka Mithun. Alijitahidi kuomba msamaha lakini matokeo yale aliambulia maneno ya kejeli tu, hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, akaondoka zake huku akilia.
“Nitakwenda wapi mimi? Nitaishi vipi mimi? Bora nikajiue tu, siwezi kuendelea kuishi,” alijisemea Nahra na huku akipiga hatua kuelekea nje ya ghorofa hilo.
Huo ndiyo ulikuwa uamuzi alioufikia, hakutaka kuendelea kuishi tena, mateso na maumivu aliyoyapitia yalitosha kabisa kumfunza, hivyo alitaka kujiua kwa kuamini kwamba angekwenda kupumzika.
Akaanza kukimbia kuelekea Kariakoo Relini huku lengo lake kubwa ni kwenda Mivinjeni. Hakukuwa na kitu alichokifikiria zaidi ya kujiua tu, alitaka kuiondoa roho yake kwa kulala kwenye reli na treni kupita juu yake.
Mara baada ya kufika Kariakoo Relini, akachukua Barabara ya Kilwa na kunyoosha nayo kama alikuwa akienda Bandarini. Alipofika Mivinjeni, akaanza kuelekea katika reli iliyokuwa chini ya daraja ambako kulikuwa na vyumba vingi vya reli ya kati.
“Nitajiua tu,” alijisemea Nahra na kujibanza sehemu huku akisubiria treni ipitie na yeye kulala relini. Aliyachoka maisha yake hiyo ndiyo sababu iliyompelekea kutaka kujiua siku hiyo. Hakutaka kuendelea kuishi na wakati watu wote aliokuwa amewaamini hawakutaka kuishi na yeye.
Moyo wake ulimuuma, hakukuwa na kitu kingine alichokiona kuwa suluhisho la maisha yake zaidi ya kujiua tu. Alidhamiria kufanya hivyo kwa kuamini kwamba asingeweza kuumizwa tena, asingeweza kulia tena, huko atakapokuwa, angeishi maisha matamu milele na kuepuka ghadhabu za dunia hii.
“Pooooooo,” ilisikika honi ya treni ya mizigo, alipoisikia honi hiyo, akachungulia kwa jicho moja kutoka pale ukutani alipojibanza. Treni ile ya mizigo ilikuwa ikija kwa kasi.
Ilikuwa imetoka kituoni na kuanza safari yake, alipoiona treni hiyo kwa mbali, Nahra akasubiri mpaka ikaribie na ndiyo aende kujilaza relini na hatimaye aweze kufa na kuyaepuka mateso aliyokuwa akiyapata.
“Nisamehe Mungu! Mateso yamezidi, acha tu nijiue ili wazazi wangu wapumzike, wasinichukie tena. Pia nisamehe kwa kukiua hiki kiumbe unachokitengeneza tumboni mwangu. Mungu, sifanyi hivi kwa kupenda, najua unayajua maisha ninayopitia,” alisema Nahra huku treni ile ikiendelea kusogea zaidi.
Nahra aliendelea kuisubiria,treni ilibakisha kama hatua mia mbili kabla ya kufika pale alipotaka kujilaza. Kichwa chake kilitawaliwa na mawazo tele, alikuwa tayari kujiua lakini si kuendea kuishi kwa mateso kama aliyokuwa akiishi.
“Bora nife tu, sina haja ya kuendelea kuishi,” alisema Nahra.
Baada ya sekunde kadhaa, treni ilikuwa mbali kama hatua mia moja, alichokifanya Nahra, akakimbilia relini na kujilaza. Machozi yalimbubujika mashavuni mwake, hakuamini kama maisha yake yote aliyokuwa akiishi, mwisho wa siku alikuwa amefikia hatua ya kujiua.
“Nisamehe Mungu, sikupenda kujiua, ila sina jinsi. Acha nife na mwanangu aliyepo tumboni,” alisema Nahra, treni ya mizigo ilikuwa ikija kwa kasi, na ilibakisha hatua arobaini tu za miguu ya binadamu kabla ya kumkanyaga pale relini alipokuwa amelala. Muda wote treni ilikuwa ikipiga honi lakini Nahra hakutoka relini, alidhamiria kujiua kwa kukanyagwa na treni hiyo.
Huku treni ikiwa imebakiza kama hatua thelathini za miguu ya binadamu huku Nahra akiendelea kulala relini pale na macho yake yakiwa yamefumba, ghafla akashtuka akishikwa mikono na kuanza kuvutwa.
Hapo, akayafumbua macho yake kuangalia ni nani aliyekuwa akimvuta. Macho yake yakatua kwa kijana mmoja mchafumchafu, aliyevalia pensi ya jinzi chakavu huku mdomoni mwake akiwa na sigara.
“Toka hapo, njoo huku,” alisema kijana yule huku akimvuta Nahra kutoka katika reli ile.
Kwa kuwa kijana yule alikuwa na nguvu Nahra akajikuta akitolewa katika reli ile na treni kupita kwa kasi kubwa.
“Unataka kujiua?” aliuliza jamaa yule huku akimwangalia Nahra machoni, alikuwa akimshangaa tu.
“Ungeniacha nife, sitaki kuishi, naomba uniache nife,” alisema Nahra huku akilia kama mtoto.
“Hapana. Kwani kuna nini? Mbona msichana mrembo unataka kujiua, hebu nieleze, kuna nini,” alisema kijana yule huku akimwangalia Nahra usoni.
Kwake, Nahra alikuwa msichana mrembo kuliko mwanamke yeyote aliyewahi kumuona machoni mwake, kitendo cha binti huyo kutaka kujiua kilimshtua mno.
Nahra hakusema kitu, alibaki akilia tu. Bado moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, kiu ya kutaka kujiua iliendelea kumkamata moyoni mwake. Lawama zake zote zilikuwa kwa mwanaume huyo aliyemtoa relini, hakujua ni aina gani ya maisha aliyokuwa akiyapitia, hakujua ni jinsi gani moyo wake ulikuwa kwenye chuki kubwa dhidi ya wazazi wake na hata ndugu zake.
“Kuna nini Mhindi wewe?” aliuliza mwanaume yule.
“Nataka kufa.”
“Kwa nini? Umechoka kula ugali?”
“Hapana kaka, nataka kufa tu.”
“Hebu kwanza tutoke hapa, unaweza kuniletea msala,” alisema mwanaume yule na kuanza kuondoka mahali pale.
Wakatoka sehemu ile karibu na reli ile na kwenda juu kulipokuwa na daraja ambapo wakavuka na kuanza kutembea pembezoni mwa Barabara ya Kilwa huku wakielekea Kariakoo Relini.
Nahra alikuwa akilia tu, alikitamani mno kifo kuliko kitu chochote kile, hakuamini kama kweli mwanaume huyo alikuwa amemuokoa na wakati alidhamiri kujiua.
Alikasirika, alimkasirikia kijana huyo. Hakutaka kuzungumza chochote kile, machozi yaliendelea kumbubujika tu mashavuni mwake.
“Nini kinaendelea?” aliuliza mwanaume yule.
Hapo ndipo Nahra alipoanza kusimulia kile kilichokuwa kimetokea maishani mwake tangu alipoanza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Deo, alipopata mimba iliyompe
USIKOSE SEHEMU IYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi