NISAMEHE LATIFAH (19)

0
Mwandishi: Nyemo Chilongani

SEHEMU YA KUMI NA TISA
ILIPOISHIA...
Ratiba ilikuwa imekwishapangwa, Latifa alitakiwa kukaa hapo hotelini mpaka kesho yake ambapo angechukuliwa na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, huko, angefanya ziara ya kuzungukazunguka kwa wagonjwa kisha baadaye kupelekwa katika Hospitali ya Mwananyamala na mwisho kabisa kuitwa katika Kituo cha Televisheni cha Global.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

SASA ENDELEA...
Mawazo juu ya Dominick hayakuisha, picha ya mtu huyo ilikuwa ikimjia kichwani, alimpenda mno, hakutaka kumwambia ukweli kwani alikumbuka maneno aliyomwambia nchini Senegal kwamba asije siku akamwambia kwamba alikuwa akimpenda.

Usiku ulikuwa mrefu, alibaki akiwa amekumbatia mto tu huku mwili wake ukianza kumtetemeka, hakuwa na hamu ya kuwa na mwanaume mwingine, aliyekuwa akimtaka kipindi hicho alikuwa Dominick tu.

Baada ya kukaa mpaka saa saba usiku, Latifa akashindwa kuvumilia, alichokifanya ni kuchukua simu yake na kwenda sehemu ya majina, akaanza kulitafuta jina la Dominick.

“Mungu! Naomba anielewe,” alisema Latifa.

Alipoliona jina la Dominick, hapohapo akapiga namba hiyo na simu kuanza kuita. Wakati ikiwa inaita, mwili wake ukaanza kumtetemeka, japokuwa kulikuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikifanya kazi lakini kijasho chembemba kikaanza kumtoka.

“Hallo!” aliita Dominick kwenye simu.

“Hallo Dominick, naomba uje chumbani,” alisema Latifa kwa sauti ndogo.

“Kuna nini?”

“Wewe njoo tu!”

“Kuna amani lakini?”

“Ipo, tena nyingi tu, naomba uje,” alisema Latifa.

“Sawa!” alijibu Dominick na kukata simu.

Moyo wake ukapoa, akajisikia amani moyoni mwake, muda huo, usiku huo ulitulia alikuwa akimsubiri mwanaume aliyekuwa na mapenzi naye, Dominick afike chumbani humo.

Mara akasikia mlago ukigongwa, akashusha pumzi ndefu, akasimama na kuanza kuufuata mlango, alivalia nguo laini ya kulalia iliyoyafanya maungo yake kuonekana vilivyo, akaufuata mlango na kuufungua, alipomuona Dominick tu, mapigo ya moyo wake yakaanza kuongeza kasi, akahisi kama moyo ungeweza kuchomoka.

“Karibu,” Latifa alimkaribishaDominick.

“Ahsante.”

Dominick akaingia ndani, yeye mwenyewe alichanganyikiwa, vazi alilovaa msichana huyo lilimuweka kwenye wakati mgumu, kila kitu maungoni mwake kilionekana wazi, wazimu ukampanda, kila alipojitahidi kujikaza kiume, akashindwa kabisa.

“Umependeza,” alisema Dominick, alishindwa kuvumilia, japokuwa lilikuwa ni vazi la kulalia tu lakini akakosa maneno, akaona bora asifie hivyohivyo tu.

“Na hili vazi?” aliuliza Latifa.

“Ndiyo! Koh koh koh…u mzuri sana Latifa,” alisema Dominick na kujikoholesha, akili yake ilihama, alichokuwa akikifikiria ni mapenzi tu.

“Nashukuru!”

Latifa alifikiri kazi ingekuwa kubwa, alijipanga vilivyo lakini mara baada ya Dominick kuingia humo ndani, akagundua kwamba kazi ilikuwa nyepesi mno, hata kumsukuma mlevi katika mteremko wa mlima ilikuwa ngumu.

Alichokifanya Latifa ni kumsogelea Dominick pale alipokaa, kabla mwanaume huyo hajajiandaa, akashtukia akivamiwa na Latifa, mwisho wa siku wakajikuta wakiangukia kitandani, kilichoendelea, kilichotokea, hakukuwa kingine zaidi ya sauti ya kitanda na mihemo ya mahaba kusikika tu.

Asubuhi kila mtu alikuwa hoi, hawakulala usiku kucha, walikesha huku wakibusiana huku na kule. Baada ya kuamka, ilipofika saa moja na nusu wakaletewa kifungua kinywa na kuanza kunywa.

Walifanyiana mapenzi ya njiwa, walilishana, walibusiana na kukumbatiana, muda mwingi Dominick alikuwa akimpakata Latifa na kumbusu kadiri alivyoweza.

“Siamini,” alisema Dominick.

“Huamini nini?”

“Eti na mimi nimelala na bilionea!”

“Haha! Hebu acha maneno yako kipenzi, niite Latifa tu jamani, hilo bilionea, wala silipendi kuitwa na mtu kama wewe,” alisema Latifa kwa sauti laini, ya mahaba, yenye kumtoa nyoka pangoni, sauti iliyozitetemesha ngoma za masikio ya Dominick.

Ilipofika saa mbili na nusu wakapigiwa simu na kuambiwa kwamba muda ulikuwa umefika hivyo walitakiwa kuanza ziara ya kuelekea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Wakajiandaa na walipomaliza wakatoka ndani na kuelekea mapokezi ambapo huko wakakutana na dereva wa waziri ambaye akawachukua na kuanza kwenda huko huku wakitangulizana na Waziri Kibonde ambaye walimkuta garini.

Hawakuchukua muda mrefu, wakafika katika hospitali hiyo na moja kwa moja kuanza kile kilichokuwa kimempeleka nchini Tanzania. Kila alichokifanya, Dominick alikuwa akikichukua kwa kamera yake, bado alikuwa kwenye utengenezaji wa makala yake.

Baada ya kuzunguka huku na kule, kuwaona wagonjwa waliokuwa wakiteseka vitandani, Latifa akatoa msaada wa kiasi cha shilingi milioni mia tano ili kisaidie katika ununuaji wa dawa na kujenga maabara nyingine hospitalini hapo. Walipomaliza, wakaelekea katika Hospitali ya Mwananyamala, huko, alifanya kama alivyofanya Muhimbili na kuahidi kutoa kiasi kama kile kwa ajili ya utengenezaji wa maabara na kunua dawa kwa ajili ya wagonjwa katika hospitali hiyo.

“Tunashukuru kwa kila kitu. Nini kinafuata?” alisema Waziri Kibonde na kuuliza.

“Ahsante kwa kila kitu pia, tunatakiwa kwenda kwenye Kituo cha Televisheni cha Global kwa ajili ya mahojiano, baada ya hapo, nadhani tutakwenda kupumzika,” alisema Latifa.

“Sawa! Ila kuna kitu.”

“Kipi?”

“Rais amenipigia simu, amesema kwamba umealikwa ikulu kwenye chakula cha usiku na familia yako,” alisema waziri.

“Unasemaje?”

“Ndiyo hivyohivyo! Umealikwa.”

“Kweli?”

“Ndiyo!”

“Ikulu?”

“Hapohapo mjengoni.”

Latifa hakuamini, kile alichokuwa ameambiwa hakutarajia kukisikia. Leo hii aliambiwa kwamba alihitajika kwenda ikulu, hakuamini, msichana aliyekulia kwenye maisha ya kimasikini, leo hii alikaribishwa ikulu, kwake ilikuwa ni faraja tele.

“Nimefurahi, nitakuja,” alisema Latifa

Bi Rachel alikuwa na furaha tele, kila alipomwangalia Latifa ambaye alifika nchini Tanzania kwa ajili ya ziara yake ya kuwatembelea Watanzania wengine, moyo wake ukafarijika mno.

Kila wakati alikuwa akitazama televisheni, alimkumbuka msichana huyo, aliishi naye, yeye ndiye aliyempeleka nchini Marekani ambapo huko alisoma na binti yake, Dorcas, leo hii, yule Latifa masikini, mtoto aliyezaliwa na mwanamke mnywa gongo alikuwa maarufu duniani, tena mwenye fedha nyingi.

Baada ya Latifa kutembelea hospitali hizo, akapigiwa simu na msichana huyo na kumwambia kwamba alitakiwa kujiandaa kwani walitakiwa kuonana katika Ofisi za Kituo cha Televisheni cha Global kwa ajili ya kuzungumza mengi.

Bi Rachel alifurahi kusikia hivyo, akahisi kuthaminiwa zaidi ya mtu yeyote yule. Alichokifanya ni kuwasiliana na mzee Issa, na bi Semeni ambao hao ndiyo waliomlea Latifa kule Manzese, ila katika kipindi hicho, hata nao maisha yao yalikuwa mazuri hasa mara baada ya Latifa kuwa bilionea.

Wakafika katika jengo la kituo hicho cha televisheni na kuanza kumsubiria. Wafanyakazi wa kampuni hiyo walipoambiwa kwamba watu hao waliokuja walikuwa ndegu zake na Latifa, walijisikia wivu sana kwa kuona walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na bahati kubwa maishani mwao.

Ilipofika saa sita mchana, gari la kifahari likaanza kuingia katika eneo la kituo hicho, mlango ukafunguliwa na Latifa kuteremka, akaanza kutembea kuelekea ndani ya jengo hilo. Alipoingia ndani na kuwaona ndugu zake, kwa futaha akawakimbilia na kuwakumbatia, machozi ya furaha yakaanza kumtoka.

“Nashukuru sana mama, nashukuru sana mama kwa msaada wako, bila wewe, nisingekuwa hapa,” alisema Latifa huku akiwa amemkumbatia bi Rachel.

“Usijali Latifa, nilifanya yote kwa kuwa nilihisi kukusaidia,” alisema bi Rachel.

Wafanyakazi wote waliokuwa mahali hapo wakaanza kuwaangalia watu hao, kumuona Latifa katika ofisi zao walijisikia fahari sana, wengine wakachukua nafasi hiyo kupiga naye picha na kuzirusha mitandaoni.

Baada ya kumaliza ishu ya kupiga picha na wafanyakazi, akaitwa katika chumba kimoja ambacho kilikuwa maalumu kwa ajili ya kufanya interview ambayo ingerushwa moja kwa moja kwenye televisheni.

“Karibu Latifa,” alikaribishwa.

Akaanza kufanyiwa maandalizi kwa ajili ya uchukuaji video, muda huo, ndugu zake walikuwa pembeni wakifuatilia kila kitu, walionekana kuwa na furaha mno. Dominick hakuacha kuchukua kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo, bado aliendelea na mchakato wake wa kumtengenezea makala msichana huyo. Baada ya kumaliza, akaitwa mbele ya kamera na kuanza kuhojiwa.

Latifa akaanza kusimulia historia ya maisha yake tangu alipofukuzwa mama yake ambayo historia yake alisimuliwa na mzee Issa, alisimulia kila kitu, baada ya kutimuliwa nyumbani kwa mama yake kisa alikuwa na mimba ya mtu mweusi, akakimbilia kwa mwanaume aliyempa ujauzito ule ambaye naye huyo aliamua kumtimua nyumbani kwake.

Ilikuwa simulizi yenye kuhuzinisha, wakati mwingine alipokuwa akisimulia, alitabasamu, kuna kipindi alifika, alibubujikwa na machozi na kuendelea mbele. Hakutaka kuacha kitu, alimzungumzia Ibrahim, jinsi alivyoutesa moyo wake, alivyomuacha mbele ya msichana mmoja wa Kiarabu, aliumia, alikosa raha, akakata tamaa ya kupenda hivyo kurudi nchini Marekani.

Alipofika huko, akasimulia kuhusu Liban, kila alipokuwa akiwazungumzia watu hao wawili, machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake, aliumia mno, aliteseka moyoni mwake mpaka kipindi kingine alitamani kufa, afe ili asiweze kuteseka tena.

“Pole sana Latifa,” alisema mtangazaji aliyekuwa akimhoji.

“Ahsante sana, ila ni maisha, Mungu anaporuhusu jambo fulani litokee, huwa anakupa na mlango wa kutokea,” alisema msichana huyo.

Kipindi hicho kilichukua saa moja, alipomaliza, akasimama na kumfuata mzee Issa, akamkumbatia huku akibubujikwa na machozi mashavuni mwake, alipotoka mikononi mwake, akamfuata bi Semeni na kumkumbatia pia.

“Samahani Latifa,” alisema msichana mmoja, alikuwa mfanyakazi wa hapo.

“Bila samahani.”

“Kuna mtu anakuulizia hapo getini.”

“Nani?”

“Anaitwa Ibrahim, amesema kwamba unamfahamu,” alijibu msichana yule.

Latifa alipolisikia jina hilo, moyo wake ukapiga paaaa, akakunja uso wa hasira, machozi yakaanza kumbubujika tena, kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma kama mkanda wa filamu.

Kwa mara ya kwanza Kituo cha Televisheni cha Global kilitangaza kwa kusema kwamba siku ya Ijumaa kungekuwa na mahojiano maalumu na msichana bilionea mwenye asili ya Kitanzania ambaye alikuwa akiishi nchini Marekani, Latifa Issa kama alivyojulikana.

Kila mtu akatamani kukiangalia kipindi hicho kilichotarajia kuruka majira ya saa tisa alasiri. Watu wakaambiana, wakasambaziana taarifa kwamba msichana huyo bilionea, aliyeleta tumaini kubwa duniani hasa kwa wagonjwa wa kansa angehojiwa moja kwa moja kwenye televisheni.

Kila mtu alitaka kumsikiliza, kila mtu alitaka kusikia historia ya maisha yake kwamba alianzia wapi, alipitia wapi na wapi mpaka kuwa vile alivyokuwa kipindi hicho. Kila kona, stori ilikuwa moja tu kuhusu Latifa, matangazo yakatangazwa sana, watu wakashikwa na hamu kubwa ya kumsikiliza msichana huyo mrembo.

USIKOSE SEHEMU IYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)