NISAMEHE LATIFAH (20)

0
Mwandishi: Nyemo Chilongani

SEHEMU YA ISHIRINI
ILIPOISHIA...
Kila mtu alitaka kumsikiliza, kila mtu alitaka kusikia historia ya maisha yake kwamba alianzia wapi, alipitia wapi na wapi mpaka kuwa vile alivyokuwa kipindi hicho. Kila kona, stori ilikuwa moja tu kuhusu Latifa, matangazo yakatangazwa sana, watu wakashikwa na hamu kubwa ya kumsikiliza msichana huyo mrembo.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

SASA ENDELEA...
Kwa kuwa alikuwa amekwishamwambia mzee Deo kuhusu Latifa, alichokifanya ni kumwambia kwamba msichana yule aliyekuwa amemkataa alitarajiwa kuhojiwa katika televisheni, hivyo akawa na hamu ya kutaka kumuona.

Siku hiyo ambayo ndiyo ilitakiwa kuonyeshwa kwa kipindi hicho, Ibrahim akaamua kumchukua mzee huyo na kumpeleka nyumbani kwake, hakumuhofia mke wake, alijua kwamba mwanamke huyo alikuwa mkorofi lakini kwenye suala la Latifa, hakutaka kusikia chochote kile.

“Umemleta kufanya nini humu?” aliuliza Nusrat huku akionekana kuwa na hasira, mbaya zaidi akaziba hata pua yake kumaanisha kwamba alikuwa akisikia harufu mbaya.

“Nimemleta, nataka kumuonyeshea yule msichana aliyenipenda, nikaamua kumuacha kwa ajili yako shetani,” alisema Ibrahim kwa kiburi.

“Ndani ya nyumba yangu?”

“Wewe mjinga nini, hebu tupishe, na ole wako ulete za kuleta, ndugu zako watakuta maiti tu humu ndani,” alisema Ibrahim, hata Nusrat alipomwangalia mumewe, alijua kwamba siku hiyo alikuwa tofauti, kama ni ng’ombe basi aliota mapembe.

Ibrahim akamchukua mzee Deo na kwenda kutulia naye kochini, akachukua rimoti ya televisheni na kisha kuiawasha. Mzee Deo alikaa kitini, hakujisikia kuangalia, hakuwa na amani kabisa kwani jinsi alivyokuwa akimwangalia Nusrat ambaye alikaa pembeni kabisa, alionekana kuwa na hasira mno.

Latifa alivyoonyeshwa kwenye televisheni, Ibrahim akajikuta akianza kububujikwa na machozi, moyo wake uliumia, kila alipokuwa akimwangalia msichana yule, akagundua kwamba aliitupa almasi jangwani na kuokota bati.

Msichana huyo mrembo, mwenye muonekano wa fedha akaanza kusimulia historia ya maisha yake. Kila mmoja akabaki kimya akimsikiliza, alianza kusimulia kuanzia mbali, tangu mama yake alipofukuzwa nyumbani kwao, alipokwenda nyumbani kwa mpenzi wake, Deo kisha kumfukuza, alionekana kuumia mno.

Mzee Deo aliposikia historia aliyokuwa akiisimulia Latifa, akashtuka, akaanza kumwangalia Latifa, akasimama kutoka katika kochi lile na kuisogelea televisheni, kila mmoja mule ndani akabaki akimshangaa.

“Ibrahim….” aliita mzee Deo, machozi yakaanza kumtoka.

“Nipo mzee….”

“Latifa ni binti yangu!” alisema mzee Deo huku akionekana kushangaa, Ibrahim akashtuka, si yeye tu, hata Nusratakashtuka.

“Unasemaje?”

“Kumbe Latifa ndiye mtoto wangu aliyezaliwa na Nahra,” alisema mzee Deo.

Hapo ndipo Ibrahim alipoanza kukumbuka mahojiano yale, alikumbuka Latifa alimtaja mtu aliyeitwa Nahra na Deo, wazazi wake waliokuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi mpaka baba yake alipomfukuza mama yake.

Mahojiano yale akayaunganisha na historia aliyowahi kusimuliwa na mzee huyo kwamba zamani alikuwa na mwanamke wa Kihindi, alimpa ujauzito lakini baadaye akafukuzwa nyumbani kwao, na alipokuja kwake, naye alimfukuza ila ni kwa sababu tu alitishiwa kuuawa na ndugu zake Nahra kwa kutumiwa watu waliokuwa na bunduki, na kama asingemfukuza basi angeuawa yeye.

“Ni mtoto wangu! Kumbe Latifa ni mtoto wangu!” alisema mzee Deo huku akijifuta machozi.

Ibrahim alishindwa kuamini, wakati mwingine alifikiri kwamba alikuwa ndotoni, katika kipindi chote alichokuwa akiishi na huyo mzee, alivyokuwa akizungumza naye kumbe alikuwa mzazi wa msichana aliyekuwa amemuacha, Latifa.

Latifa hakuwa na kipindi kirefu katika kituo kile, alichokifanya Ibrahim ni kumwambia kwamba ilikuwa ni lazima kumfuata Latifa huko na kumwambia ukweli kwamba alikuwa na baba yake nyumbani kwake.

“Ngoja nikamlete uzungumze naye,” alisema Latifa.

“Atakubali kuja?”

“Atakuja tu. Subiri,” alisema Ibrahim huku akionekana kuchanganyikiwa, hakutaka kuchelewa, akaondoka kuelekea huko, tena alikuwa akikimbia kwa kasi ajabu.

Jina la Ibrahim lilimchanganya, hakuamini kama kweli aliitwa na msichana yule kwa kuwa alikuwa akihitajika na mtu aliyejitambulisha kwa jina hilo. Huku akionekana kuwa na hasira, akatoka pamoja na ndugu zake kuonana na huyo mtu.

Alipofika, alipomwangalia Ibrahim, akajikuta akiingiwa na huruma, aliyesimama mbele yake alikuwa Ibrahim, yuleyule kijana aliyekuwa amemtesa na kumkataa kipindi cha nyuma, ila hali aliyokuwa nayo, ilimtia huruma mno.

“Ibarhim,” alijikuta akimuita kijana huyo aliyeonekana kupigwa na maisha.

“Latifa…” aliita Ibrahim, tayari machozi yakaanza kumbubujika, hata naye kumbukumbu za nyuma zikaanza kujirudia kichwani mwake.

“Umefuata nini?” aliuliza Latifa huku akiwa amesiamam.

“Kwanza naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea, dunia imeniadhibu kwa kile nilichokufanyia,” alisema Ibrahim.

Japokuwa alijiahidi kwamba asingeweza kumsamehe mwanaume huyo lakini hakuwa na jinsi, kwa namna ambavyo alionekana mahali hapo, ilionyesha kabisa kwamba maisha yalimpiga, hivyo hakutaka kumwadhibu tena, alichokifanya ni kuukunjua moyo wake na kumsamehe kwa kila kitu kilichotokea.

“Nimekusamehe Ibrahim, dunia imekufunza,” alisema Latifa.

“Kuna kitu ninahitaji kutoka kwako.”

“Kitu gani?”

“Baba yako anateseka Latifa, kila ulichoambiwa ni kweli kilitokea, ila naye ana historia ya tofauti na hiyo uliyokuwa nayo,” alisema Ibrahim, alikuwa amemsogelea kidogo, kila mtu akashtuka.

“Baba yangu?”

“Ndiyo!”

“Nani?”

“Mzee Deo!”

“Hapana! Baba yangu kashakufa!”

“Una uhakika? Ulionyeshewa kaburi lake? Au hata picha yake unayo”

“Ibrahim, baba yangu! Haiwezekani!”

“Latifa, huu ndiyo muda wa kuusikia ukweli, twende ukamuone baba yako, ameteseka sana, kansa ya mguu ilisababisha kukatwa mguu wake, twende ukamuone, atafurahi kama akikuona,” alisema Ibrahim.

“Baba yangu……” alisema Latifa, sauti ya kilio chake ikaanza kusikika.

“Ni kweli, yupo hai, hana pa kuishi, amekuwa akiteseka miaka yote, alikuwa ombaomba mitaani, alifukuzwa kila sehemu. Nimekuwa nikiishi naye kwa kipindi kirefu pasipo kujua kwamba ni baba yako, historia aliyonisimulia, ni hiyohiyo ambayo umesimulia japokuwa kuna kitu ambacho haukukifahamu, si wewe tu bali hata marehemu mama yako hakukifahamu, nimemsaidia sana mpaka kufikia kipindi hiki. Naomba twende ukamuone, tuwahi, namjua mke wangu, anaweza hata kumuua,” alisema Ibrahim.

“Kumuua! Amuue baba yangu!”

“Ni mwanamke mwenye roho mbaya! Twende Latifa,” alisema Ibrahim, hawakutaka kusubiri, waliposikia kwamba mke wa Ibrahim angeweza kumuua mzee Deo, wote wakaingia ndani ya gari na kuanza kuelekea huko.

Garini, bado Ibrahim aliendelea kumuomba msamaha msichana huyo, alijutia matendo aliyoyafanya, hakuomba msamaha kwa kuwa Latifa alikuwa msichana bilionea, aliomba msamaha kwa kuwa alihitaji kusamehewa kwa yote aliyoyafanya.

“Ibrahi…nime…kus…ame..he..” alisema Latifa huku akilia.

Walichukua dakika kumi njiani ndipo walipofika alipokuwa akiishi Ibrahim. Kwa kuwa nyumba ilizungushiwa ukuta huku ikiwa na geti kubwa, Ibrahim akateremka na kwenda kulifungua geti lile ili gari liingizwe ndani.

Kitu cha ajabu alipofika katika eneo la nyumba hiyo, akapiga uyowe mkubwa, mbele yake alikuwepo mzee Deo, alikuwa hoi chini, kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, muda huo napo damu zilikuwa zikimtoka katika kipande cha mguu wake, Nusrat alikuwa amemtoa ndani ya nyumba yake.

Latifa na watu wengine waliposikia uyowe huo, wakahomoka kutoka garini, wakajua kwamba kulikuwa na kitu ndani ya nyumba hiyo, walipolifungua geti dogo na kuingia ndani, wakamkuta Ibrahim akiwa amemshika mzee Deo aliyekuwa chini huku akilia, mzee huyo alikuwa hoi, damu ziliendelea kumtoka katika kipande chake cha mguu na alikuwa akilia kwa maumivu makali.

Wote wakamfuata, kila mtu aliyemwangalia, sura yake ilifanana na Latifa kwa mbali, hakukuwa na mtu aliyekuwa na ubishi kwamba mzee yule alikuwa mzazi wa Latifa.

Latifa akajikuta akianza kulia, hasira ikamkaba kooni dhidi ya Nusrat, alionekana kuwa na hasira mno.

“Hanijui, yaani pamoja na kuniumiza bado ananiumizia baba yangu! Atanitambua mimi ni nani,” alisema Latifa huku kwa kumwangalia tu ungegundua ni jinsi gani alikuwa na hasira.

Walichokifanya ni kumchukua na kumpeleka hospitalini huku Latifa akiahidi kwamba ni lazima angemuonyesha Nusrat yeye alikuwa nani.

Latifa alikuwa akilia tu, kila alipomwangalia baba yake, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama alikuwa kwenye hali ile. Watu wengine walimbembeleza anyamaze lakini hakunyamaza, hasira kali dhidi ya Nusrat ilimkamata mpaka kufikia kiasi cha kukunya ngumi.

Kitendo cha kupigwa baba yake na kuumizwa namna ile kulimuongezea hasira ya kumchukia Nusrat ambaye miaka michache nyuma alimuumiza kwa kumchukulia mwanaume wake, hakuonekana kuridhika, leo hii alimpigia baba yake.

“Nitamuonyesha,” alisema Latifa huku akionekana kuwa na hasira kali.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Japokuwa kipindi cha nyuma alisema kwamba baba yake alikuwa miongoni mwa watu aliokuwa akiwachukia kwa kuwa tu alkimfukuza mama yake lakini wakati alipokuwa akimwangalia, mateso aliyoyapata, chuki yote dhidi yake aliyokuwa nayo ikaondoka na huruma kumuingia.

Manesi waliokuwa na machela wakasogea lilipokuwa gari lile na kumpajndisha mzee Deo juu ya machela ile na kuanza kusukumwa kwenda kwenye chumba kimoja kilichoandikwa Theatre. Walipofika nje ya chumba kile, wakazuiliwa.

Watu waliokuwa wamegundua kwamba msichana aliyekuwa mbele yao alikuwa Latifa walibaki wakishangaa, hawakuamini kama kweli yule aliyesimama mbele yao alikuwa ndiye au alikuwa msichana mwingine aliyefanana naye.

“Inawezekana ndiyo yeye,” alisema jamaa mmoja huku akimwangalia Latifa ambaye machozi yalikuwa yakimbubujika tu.

“Labda! Ila awe hapa anafanya nini?”

“Sijui, hebu tusogee karibu zaidi tumuone.”

Kila aliyepita, hakuacha kumshangaa Latifa aliyekuwa akilia tu. Ibrahim alikuwa kimya, moyo wake ulimuuma, alimzoea sana mzee Deo, alikuwa rafiki yake mkubwa, alimpenda pasipo kujua kwamba mzee huyo alikuwa mzazi wa msichana aliyemuacha kipindi cha nyuma, Latifa.

Madaktari wakawa wanapishana mlangoni, wengine waliingia na wengine kutoka. Mgonjwa aliyeletwa kwao alionekana kuwa wa maana sana, ilikuwa ni bora kuleta utani kwa mgonjwa mwingine lakini baba yake Latifa.

Baada ya msaa mawili, mlango ukafunguliwa na daktari kutoka, akawaita watu hao ofisini kwake kwa lengo la kuzungumza nao. Walipofika huko, akawaweka chini.

USIKOSE SEHEMU IYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)