Mwandishi: Nea Makala
SEHEMU YA TATU
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Tony aliposikia mwanadada yule anashindwa kumalizia sentensi zake akanyanyua kichwa na kutazama ili afahamu japo kwa kinaga ubaga nini tatizo, daah naye akashikwa na bumbuazi kukuta ni Mtu ambaye anamfahamu, mapigo ya moyo yakaenda mbio zaidi, akageuka kwa jirani yake na kumuuliza,
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
Huyu msichana ana cheo gani?”
“Huyu ndie mkurugenzi wa kampuni uliyoingia nayo ubia”
Fikra zikaenda mbali zaidi, kila mmoja akawa anashangaa juu ya tukio lile, Tony akawa anapiga piga meza kuonesha mfadhaiko.Martha akakohoa na kikao kikaendelea, Tony akaomba radhi kwa kuchelewa, wadau wakaelewa na wakafikia makubaliano namna ya kuanza kazi. Kikao kilifungwa na wakapena mikono ishara ya umoja lakini ilipofika zamu ya Tony kupeana mkono na Martha, Tony akakwepa na kuanza kuondoka lakini kabla hajatoka akasikia anaitwa,
“Mr. Tony nakuomba mara moja,” ilikuwa ni sauti ya mmoja ya wadau wa ile kampuni ya kikorea akihitaji kuzungumza machache.
Tony akasogea alipo yule mdau ili kusikiliza nini alichoitiwa,
“Mimi ni msaidizi wa bibie hapa, hivyo natumai utatupa ushirikiano wa kutosha katika kila jambo,” alisema yule mdau.
“Shaka ondoa” Tony akajibu.
“Kwa kuwa wakurugenzi wote mpo mimi nafikiri mngepata muda wa kukaa na kuona jambo gani lianze kufanyiwa kazi”
“Ni kweli ukizingatia muda unazidi kwenda na upinzani wa kibiashara ni mkubwa,” Martha akaongezea.
“Lolote mtakaloamua nipo tayari ila kwa sasa kuna mahali nawahi tutaonana wakati mwingine” akasema Tony na kuanza kuondoka.
Ukweli Tony hakufuraishwa kabisa kufanya kazi na mrembo yule alitamani hata avunje mkataba ila kila alivyofikiria kuhusu mafanikio atakayoyapata kutokana na ubia ule ikabidi avumulie.
Akaangalia simu yake na kukuta ujumbe mfupi uliomuelekeza mahali Fulani ambapo alitakiwa afike, bila kuchelewa akaanza safari na ndani ya dakika 45 akawa amefika. Ilikuwa ni gereji moja kubwa na ya kisasa iliyopo maeneo ya sinza iliyotambulika kwa jina la Mdidi Auto Garage. Alipoangaza huku na kule akakutana na sura ya mwanadada yule ambaye asubuhi alikuwa na ugomvi nae, akasogea hadi alipo na kumwambia,
“Nimerudi kulipa deni langu”
“Kaka naomba uniletee hiyo lisiti ya malipo” akasema yule msichana na ndani ya dakika lisiti ikaletwa Tony akashtuka alipoisoma, akakuta anatakiwa kulipa laki saba na nusu pesa za kitanzania (Tsh. 750,000).
“Mbona pesa nyingi kiasi hiki, na nikiangalia gari lilivyoumia haviendani” Tony akasema.
“Usitake nikuabishe lipa pesa kama huna sema,”
“Sawa nitalipa nipe dakika 15”
“Poa kila la kheri”
Tony hakuwa na pesa hizo mfukoni ikabidi aombe msaada kwa rafiki zake ambao jana yake tuu walikorofishana ila haikusumbua kitu kwani waliweza kumsaidia kwa kutumia mitandao ya simu. Tony akasogea hadi zilipo huduma za kutolea pesa kwa njia ya mtandao na akafanikisha hilo. Akarudi na kukabidhi zile pesa kisha akasogea kwa yule msichana na kumwambia,
“Samahani sana kwa usumbufu ila ulichonifanyia leo usikisahau”
“Una maana gani”
“Ya kawaida tuu, naomba unikabidhi kinachonistahili”
Msichana akapekua pochi yake kuangalia kitambulisho alichokabidhiwa na Tony kama dhamana ya uaminifu lakini hakukiona, akatoa kila kitu pembeni na kupekua kila mahala lakini hakufanikiwa kukipata. Akakaa chini na kuanza kutafakari wapi alipokiacha kitambulisho kile, akakumbuka kuwa amekiacha nyumbani kwao, ugumu ukaja ataanza vipi kumwambia Tony kuwa amesahau kitambulisho,
“Vipi ujakiona kitambulisho! Nina mambo mengi ya kufanya, nimeshalipa deni lako nikabidhi istahiki yangu niende,” akasema Tony.
“Samahani kaka yangu nimekisahau kitambulisho chako nyumbani”
Tony akamtazama sana msichana yule akajikuta hajui amfanye nini,
“Ila kama hutojali nitakuletea popote ulipo jioni hii” aliendelea kuongea mwanadada yule huku hofu kidogo ikimtawala.
Tony akatabasamu na kuanza kuondoka bila kutoa jibu lolote, wakati anaondoka akafikiri vingi sana na akajikuta akiongea kimoyo moyo,
“Kwa kuwa umenianza, hakika sitokuacha, unawezaje kunidhalilisha kiasi kile”.
Jioni ya siku hiyo ilikuwa ngumu sana kwa Tony akajikuta akizama katika dimbwi la mawazo akiyafikilia zaidi matukio ya siku hiyo kuanzia yule mrembo ambaye hakulifahamu jina lake na yule mkurugenzi mwenza aliyemfahamu kwa jina la Martha. Kila alivyofikiri kuhusu kuwa karibu na Martha ndivyo moyo wake ukajikuta ukijawa na hasira hasa baada ya kukumbuka miaka kadhaa iliyopita.
“Martha kwanini umekuja katika katika maisha yangu, japo si rahisi ila natamani uende mbali nami, kwa muda mrefu hakutokea mwanamke ambaye angeusimamisha moyo wangu walau kwa dakika na kunifanya nimfikirie yeye tuu, lakini wewe umeweza hilo, nakuchukia na lazima ulipie hili,” alisema Tony huku akinywa mvinyo wake taratibu.
“Nitayafanya maisha yako kuwa magumu kuliko kawaida, niko radhi kufanya lolote, liwe la kielevu au la kipumbavu, nitahakikisha unashuka na kuwa mtu wa chini.”
Wakati akiendelea kufikiri hayo simu yake ikaita kuangalia ilikuwa namba ngeni ikabidi aipokee,
“Hallo”
“Hallo! Naongea na Tony”
“Ndio! Nani mwenzangu?”
“Mimi ni Jamilah”
“Jamilah wa wapi?”
“Ooh! Tony unamaswali mengi nipo maeneo ya Bunju kwa sasa, niambie nikuone wapi ili nikukabidhi kitambulisho chako”
“Njoo Mapinga”
“Sawa dakika 15 nitakuwa huko”
Simu ikakatwa na mawazo juu ya Martha yakakata ghafla, Tony akajiandaa haraka huku akinuia kuwa lazima mrembo yule alipie ule uzalilishaji alioufanya juu yake, akapanga kufanya kila aliwezalo amnase mwanamke yule kimapenzi.
Baada ya dakika 15 Jamilah akawa ameshafika maeneo ya Mapinga na kabla hajampigia simu kujua alipo, Tony nae akawa ameshafika maeneo hayo. Tony alitumia takribani dakika moja kuuangalia uzuri wa msichana yule hakika alikubali kweli Jamilah ameumbwa akaumbika. Mrembo yule naye akabaki ameduwaa kwani alimuona Tony tofauti na alivyokuwa asubuhi na kadri alivyozidi kusogelewa na Tony ndivyo alivyozidi kuchanganyikiwa kwa utanashati wake, akajikuta anababaika kuongea asijue aseme nini,
“Siwezi kukupa kitambulisho chako hapa, tutafute sehemu iliyotulia tukae walau tuzungumze kidogo,” alisema Jamilah.
“Sawa twende ukapaki gari yako pale alafu tutaenda huko”
Jamilah akaenda kupaki gari yake sehemu aliyoelekezwa na Tony kisha wakasogea katika mgahawa uliyo karibu akaagiza kinywaji lakini tony akakataa na kusema kuwa alishakunywa alipotoka ivyo hajisikii kunywa chochote, jibu hilo lilimfanya Jamilah nae kughairi kuagiza kinywaji,
“Tony samahani sana kwa kile kilichotokea leo”
“Huna haja ya kuomba msamaha ila mimi ndio natakiwa kuomba radhi”
“Hapana Tony ukweli kila nikifikiria niliyokufanyia leo, moyo wangu unauma sana na sikujua kuwa wewe ni mtu mwema na mkarimu kiasi hiki, nilijisikia aibu pale niliposahau kitambulisho chako nyumbani na nilitegemea utanifanyia kama niliyokufanyia ila uko tofauti mno”
“Yameisha hayo mimi nishasahau”.
Tony alijibu japo moyoni alikuwa na hasira sana juu ya huyo msichana ila akaamua kuigiza mwema hili atomize lile analolitaka.
Jamilah akatoa kitambulisho na kumkabidhi Tony, nae akakipokea na kushukuru, wakaongea mengi na taratibu mazoea yakaanza, usiku ukaingia na wakaagana huku wakiahidiana kuonana tena siku zijazo. Uchangamfu na vituko vya Tony vilitosha kumloga Jamilah na kujikuta kutamani kuwa karibu na mkaka huyo tena na tena.
BAADA YA MIEZI MITATU
Ushirika wa kampuni mbili ukawa mkubwa na maarufu katika macho na masikio ya watanzania wengi, umaarufu huu haukuishia Tanzania tuu ulivuka mipaka na kuenea katika nchi nyingi za Asia hasa zilizo karibu na Korea. Tony alijitahidi kutengeneza Makala mbalimbali zilizoonesha mitindo yenye utamaduni wa kiafrika na kiasia, Kama utafatilia vizuri mpenzi msomaji Afrika na Asia tamaduni zao zinafanana kwa kiasi kikubwa tofauti na zile tamaduni za Ulaya na Amerika. Kila mmoja alifurahia mafanikio hayo na kukaandaliwa na sherehe maalumu kwa ajili ya kupongezana. Sherehe hiyo ikapangwa kufanyika katika moja ya hoteli za kitalii zilizopo katika fukwe za bahari ya Hindi katika mji mdogo wa Bagamoyo. Wafanyakazi wote wakataalifiwa hivyo kila mmoja akawa akiisubiri siku hiyo kwa hamu zote.
Siku ya siku ikafika Tony akiambata na maswahiba zake Darmy na Yassir ambapo kila mmoja alikuwa katika suti moja matata sana, Siku hiyo iliwafanya waonekane wa tofauti sana,
“Tangulieni ndani kuna mtu namsubili,” akasema Tony.
“Duuh! Kama kawaida yako,” Yassir akadakia.
“Haya nani huyo anayekuja leo, Vanessa au Tedy?” Darmy akauliza.
“Si Tedy wala si Van, ila ni…..acha iwe surprise mtamuona akifika”
Darmy na Yassir wakatazamana kisha wakaingia ndani bila kuongeza neno, Tony akaendelea kusubili na ndani ya muda mfupi mwanadada mwenye urembo wa asili akawasili. Tony alitumia dakika moja kuthibitisha kuwa yule ni binadamu au malaika,
“Hakika mwanamke ni sawa na waridi lenye kuvutia na kunukia vizuri, kama ilivyo kazi ya waridi kupendezesha nyumba ndivyo ilivyo kazi ya mtu mke kumburudisha na kumstarehesha mtu mume,” Tony akasema hayo maneno moyoni, akaachia tabasamu zito na akuweza kuzuia mikono yake kumkumbatia mwanadada yule pindi alipomkaribia.
Kwa pamoja wakaongozana ndani wakaangaza huku na huko wakakuta kuna meza tupu, wakajongea na kukaa hapo, Uzuri wa binti yule ulizua gumzo kubwa kwa wageni wote waliolikwa kwenye sherehe hiyo. Darmian na Yassir wakashindwa kuvumilia kule walipokaa,
“Ebhana eenh! Umeona kule,” Darmy akasema.
“Wapi tena?” Yassir akauliza.
“Kule kwenye meza ile”
“Wee! Yule mtoto mzuri vile Tony kamtolea wapi”
“Mhmh! Kwani wewe ndio umemfahamu leo?”
“Daah! Yule jamaa sijui anauchawi gani, yeye tuu kila siku anaibua wapya”
“Ila usifikirie sana labda anaweza kuwa rafiki tuu”
“Aah! Kama ni rafiki yake tuu, nitaomba aniachie mie yule mtoto”
“Wewe mjinga si umeoa acha tamaa nitakusemea mie”
“Daah! Vunga jamaa yangu ila twende palepale walipo”
Wakati wakiinuka kuelekea alipo Tony, Mshehereshaji akashika kipaza sauti na kuomba wageni waalikwa wote wasogee katika viti vya mbele hili sherehe iweze kuanza. Darmy na Yassir wakafika alipo Tony wakatabasamu na kukaa, ikabidi utambulisho mfupi ufanyike hili kuwafanya wawe huru zaidi katika maongezi yao,
“Jamilah hawa ni rafiki zangu wa karibu sana, huyu ni Darmian na huyu ni Yassir,” akawageukia rafiki zake na kuendelea utambulisho.
“Oyah ni shemeji yenu”
“Eenh! Shemeji!” Yassir akajikuta akiuliza kwa mshangao zaidi.
“Kwani ujasikia au ndio mbwembwe,” akasema Darmy.
“Nafurahi kuwafahamu,” Jamilah akasema huku akiwapa mikono wale maswaiba wa Tony.
Sherehe ikaanza kwa watu mbalimbali kuongea na kuonesha wazi kufurahishwa na juhudi za kampuni hiyo katika kukuza utamaduni wa Nchi, ikafika zamu ya mgeni rasmi ambaye pia ni naibu waziri wa Utamaduni, Habari na Michezo. Waziri alifuraishwa sana na hatua ya kampuni ya Korea kuja kuwekeza nchini kwetu, na hii imesaidia sana kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wengi aidha Waziri alishukuru pia kwa kuutangaza utamaduni wa nchi yetu.
USIKOSE SEHEMU IYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi