USALITI WA KIAPO (2)

0
Mwandishi: Nea Makala

SEHEMU YA PILI
ILIPOISHIA...
“Karibuni sana,” akawakaribisha.

“Asante,” Darmy akaitikia.

“Mambo zenu warembo,” Yassir akawasalimu.

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

SASA ENDELEA...
Tedy na Van nao wakaitikia na kwa pamoja wakakaa na vinywaji vikaongezwa wakaendelea kunywa na kuongea hili na lile.

Darmy akaendelea kufikiri juu ya mchezo alioucheza Tony asipate jibu akatamani kujua nini kilijili lakini hakuweza kuuliza kwa wakati ule. Ikamlazimu avute subira Zaidi hadi warembo wale watakapoondoka, matamanio yake yalitimia baada ya muda mfupi pale Vanessa na Tedy walivyoaga kwa pamoja kuwa muda umeenda na wanahitaji kurejea majumbani mwao. Tony alihofia mno kwa wasichana wale kama wangeongozana peke yao lolote lingetokea katika maongezi yao, akafikiri kitu kidogo kisha akasema,

“Vanessa Subiri kidogo acha nimsindikize Tedy”

“Kweli Van endelea kubaki nasi kidogo, kwanza mama hana shida alafu nyumbani ni hapo tuu karibu, acha Tony amsindikize Mgeni sisi tuendelee kupiga soga,”alisema Yassir.

Van bila kipingamizi akakubali, Darmy akamuangalia Tony na kumuonesha ishara ya dole gumba kuashiria kuwa asihofu kila kitu kiko sawa.

Tony akatoka na kimwana yule na kuwasha gari tayari kwa safari ya kumrudisha kwao,

“Asante mpenzi nimefurahi sana kuwa na wewe leo, hata wale rafiki zako na yule wifi yangu kwakweli ni wachechi mno,” Tedy alisema.

“Usijali mpenzi, nafanya yote kuhakikisha unafurahi”

Jibu lile liliiburudisha nafsi ya Tedy pasipo kujua kuwa ana wenzake wengi tuu, safari iliendelea hatimaye wakafika, Tedy akamtazama Tony kisha akambusu na kushuka kwenye gari.

Tony akamsindikiza kwa macho hadi alipoingia ndani akageuza gari na kurejea kwake ambapo akamchukua vanessa na kumfikisha nyumbani kisha akawasindikiza na maswahiba zake,

“Ebhana eenh leo umewezaje kuwa na wanawake wawili kwa wakati mmoja na wasifahamiane?” Yassir akafungua maongezi maana ya kimya kifupi kupita.

“Nilicheza tuu na saikolojia zao, nikaizuia hofu kwangu na kumfanya kila mmoja afurahi kwa nafasi yake,” akajibu Tony.

“Ila uoni kama ni hatari kuendelea kuwachanganya hivi, kwanini usichague mmoja ukatulia naye,” Yassir akaendelea kusema.

Kauli ile ilimfanya Tony afunge breki ya ghafla ambayo iliwashtua wote, kisha akapiga piga usukani kwa hasira na kumgeukia Yassir,

“Lini umekuwa na kichwa cha panzi kiasi cha kusahau yote ndani ya muda mfupi, leo hii wewe umekuwa wa kuniambia nitulie na msichana mmoja,” Tony aliongea kwa hasira mno.

“Kweli Tony wakati umefika lazima ufanye maamuzi magumu, chagua yule unayeona unampenda kuliko wengine,” Darmy naye akaongozea.

“Kupenda! Mnajua nini nyinyi kuhusu kupenda, mmesahau kisa cha mpendwa kupenda asipopendwa akatendwa na kwenda, lakini kule alikopendwa hakupenda!”.

Tony akashusha pumzi ndefu kisha akaendelea kuongea,

“Ninyi ni marafiki zangu wa muda mrefu sana, najua mna nia njema kwangu lakini kwa hili naomba mniache tu”

“Kweli sisi ni rafiki zako lakini unatupa wakati mgumu sana, hivi hao wanawake wakija kugundua kuwa unawachezea watatufikilia vipi sisi. muda ndio huu funika yaliyopita na usonge mbele, binafsi leo ndio mara ya mwisho siwezi tena kujiingiza kwenye ujinga wako,” aliongea Yassir kisha akafungua mlango na kushuka kwenye gari na kuondoka, Darmy nae akafanya vile vile na kumuacha Tony akiwa mwenye kuwaza sana.

Tony ni mmoja kati ya waongozaji wa filamu wenye mafanikio na upekee katika kazi zake, ubunifu, umakini na kujituma kwake kukaifanya kampuni ya STUDIO 7 MEDIA LTD. kukua na kutambulika ndani na nje ya mipaka ya Tanzania, mbali na mtazamo hasi juu ya wanawake lakini hakuwanyima fursa ya kufanya kazi walau kwa majukumu machache.

Upekee wa kampuni hiyo ndio uliosaidia kupata nafasi ya kuingia ubia na kampuni moja ya kikorea iliyofahamika kwa jina la TAE XHIANG SUNG GROUP, kampuni hii imejikita Zaidi katika maonesho ya mitindo na matangazo mbalimbali hivyo kwa kampuni ya Tony ilikuwa nafasi muhimu sana ya kuzidi kutanua wigo wa kazi yake.

Ni asubuhi moja tulivu yenye mawingu mepesi yaliyofanya siku hiyo kuwa na baridi kiasi, Tony akiwa kitandani akashtushwa na mlio wa simu yake, akaamka na kuangalia akagundua kuwa ni alarm aliyoitega ili imuamshe. Siku hiyo alikuwa na kikao cha muhimu sana, kitakachotoa mpango kazi kati ya kampuni yake na ile kampuni ya kikorea iliyofungua tawi hapa nchini, hivyo ikabidi ajiandae haraka tayari kwa ajili ya safari ya kwenda Ubungo plaza ambapo kikao kimepangwa kufanyika. Alipojaribu kuwasha gari likakataa kuwaka, hakupoteza muda kujua tatizo ni nini akaamua atumie usafiri wa umma kwa siku hiyo. Gari lilisimama karibu kila kituo jambo ambalo lilimkera Tony na akaanza kuona dalili za kuchelewa kikao.

Walipofika maeneo ya makongo wakakuta kuna foleni kubwa uliyoenda hadi mwenge na alivyotazama saa yake akaona amebakiwa na nusu saa kabla ya kikao kuanza, ikabidi ashuke na kupanda pikipiki. Akamuhimiza dereva wa pikipiki ile aongeze mwendo ili aweze kuwahi. Nausifu ujanja wa dereva yule kwani alijitahidi kupenyapenya kukwepa foleni ile lakini walipofika maeneo ya mawasiliano dereva alipoteza umakini kidogo na kujikuta akielekea kuivaa gari ndogo aina ya Ferrari akajitahidi kufunga breki lakini akuweza na kujikuta akiigonga kwa nyuma. Wote wakaanguka na kwa bahati nzuri hakuna aliyeumia zaidi ya ile pikipiki na gari, ndani ya sekunde kadhaa watu wakawa wamezunguka eneo lile, ugomvi ukazuka na wote wakataka kumpiga dereva wa pikipiki kwa kutokuwa makini.

“Jamani msimfanye chochote huyu dereva, kosa ni langu mimi ndiye niliyekuwa nikimchochea aongeze mwendo kwani nina kikao cha muhimu nahitaji kuwahi,” Tony alitoa utetezi wake.

“Mpumbavu wee! kikao ni muhimu kuliko usalama wako?” akasema mwananchi mmoja ambaye sikumfahamu Jina Lake.

“Naweza kusema hivyo ila tafadhalini sana msifanye lolote na naomba kuongea na mwenye gari sina muda zaidi wa kukaa hapa,” alisema Tony.

Mzozo uliendelea na ndani ya muda mfupi akatokea msichana ambaye kuwepo kwake tuu, kulifanya watu wote wakae kimya na kila mmoja aliduwazwa na uzuri wake. Akasogea akaliangalia lile gari kisha akamuangalia dereva wa pikipiki na kisha kumtazama Tony, ama kwa hakika ukimuangalia analipsi za kuvutia, kidevu ndio sisemi kitu jamani, macho yake ang’avu yalifanya nyoyo za vidume wengi kukimbia zaidi ya kawaida, umbo namba nane na mwenye mvuto zaidi ya maua wanaume wengi wakajikuta wakitaka kuonesha ubavu wao kumsaidia mrembo yule,

“Samahani sana dada yangu ni bahati mbaya tuu,” aliongea dereva wa pikipiki.

Yule mwanadada akamuangalia kwa dharau sana kisha akasonya,

“Unajua thamani ya hii gari? Unajua ni kiasi gani cha pesa unachotakiwa kulipa kwa ajili ya hii gari, nafikiria kukuweka polisi kwa muda hadi utakapolipa pesa yangu,” aliongea mrembo kwa dharau na hasira kidogo.

“Naomba nilipe mimi gharama za kutengeneza gari lako, haya yote yametokea kwa sababu yangu” Tony akazungumza.

Yule msichana akamuangalia Tony kisha akacheka kwa dharau sana, Tony alivyoangalia saa yake akagundua kuwa zimebaki dakika 5 kikao kuanza akakosa Amani na akahofu zaidi nini kitatokea endapo atakikosa kikao kile muhimu.

“Tafadhali dada yangu nina haraka mno, naomba tusifanye mambo kuwa makubwa binafsi nitalipa deni hili”

“Lipa sasa hivi! Asiondoke bila kulipa huyo! Wamezoea hao!” yalikuwa maneno ya baadhi ya watu waliokuwa eneo lile.

Tony akamshika mkono mrembo yule na kumsogeza pembeni lakini kitendo kile kikamchukiza mara dufu msichana yule, akanyanyua mkono wake na kumzaba kofi Tony, asee nafsi ilimuuma mno akatamani ajibu mapigo lakini akajiona mjinga endapo atafanya tukio lile, akajitahidi kujizua kisha akamuangalia usoni mwanadada yule,

“Huna hadhi ya kuhushika mkono huu masikini wewe na usirudie tena kunigusa, kwa kuwa umenianza mimi namaliza lazima ulale kituo cha polisi leo, unajua mimi ni nani?” msichana aliendelea kuongea kwa vitisho.

Tony alizidi kuumia nafsini kwani hata siku moja hakukubali kudhalilishwa na mwanadamu hasa wa kike, hasira zikampanda akamwangalia mwanadada yule kisha akajikuta anacheka mno,

“Sawa fanya unalojisikia ila huyu dereva muache aende,” Tony akasema na kumpa kiasi kidogo cha fedha dereva yule wa pikipiki ambaye alishangaa sana ukarimu wa Tony kwani toka aanze kufanya kazi ile hakuwahi kukutana na mteja wa namna ile akashukuru na kuondoka.

Mrembo bado akawa na nia ya kumdhalilisha Tony mbele ya watu ambao wengi walishaanza kupiga picha na kurekodi kwa simu zao tayari kwa kuziachia kwenye mitandao ya kijamii, Tony akatoa kitambulisho chake cha taifa na akatoa namba zake za simu na kumkabidhi yule msichana,

“Nakuamini na naomba uniamini, peleka gari yako gereji yeyote kisha baada tu ya kikao kuisha nitakuja hapo kulipa gharama zote, nitumie ujumbe wenye malekezo ya hiyo gereji kwa sasa naomba uniache niende”

Tony akusubili kuambiwa nenda akaanza safari baada tu ya msichana yule kuipokea ile dhamana, ya kitambulisho.

Kikao kikaanza bila hata ya Tony kuwasili, wadau wakaanza kujadili mambo mbalimbali juu ya uendeshwaji wa kampuni izo mbili ilipofika zamu ya STUDIO 7 MEDIA LTD kuelezea namna kazi itakavyoenda kila mmoja akashangaa kutokumuona mkurugenzi wa kampuni hiyo, ikabidi mkurugenzi wa kampuni ya kikorea asimame na kuongea kwanza,

“Nasikitika katika kikao cha kwanza mshirika mwenzetu kushindwa kufika, hii inanipa wasiwasi kidogo mimi kama mwakilishi na msimamizi wa kampuni hii ya TAE XHIANG SUNG GROUP kwa hapa Tanzania, japo sijajua ni sababu gani zilizomfanya hadi muda huu asiweze kufika lakini huu naweza kuuita uzembe usiweza kuvumilika,” aliongea Martha ambaye ni msimamizi wa kampuni ile.

Martha ni msichana anayejiamini mno katika kila analolifanya, yeye asili yake ni mtanzania japo kwa muda mrefu sana alikuwa nchini Korea kimasomo na kubahatika kufanya kazi huko huko ivyo kampuni aliyokuwa akiifanyia kazi kufungua tawi hapa nchini ilitokana na juhudi zake binafsi,

“Tumeipa nafasi kampuni ya STUDIO 7 MEDIA LTD kwa kuwa tuliamini ni kampuni yenye watu makini na ubunifu mwingi katika kazi lakini huu uzembe…………” kabla hajaendelea kuongea akajikuta anaduaa kumuona Tony akiingia huku akihema sana, Martha akajikuta anashindwa kuendelea kusema alichokusudia kusema,

“Lakini huu uzembe…lakini…..lakini….!” akajikuta anarudia maneno huku macho yake yakishindwa kutoka alipo Tony.

Tony aliposikia mwanadada yule anashindwa kumalizia sentensi zake akanyanyua kichwa na kutazama ili afahamu japo kwa kinaga ubaga nini tatizo, daah naye akashikwa na bumbuazi kukuta ni Mtu ambaye anamfahamu, mapigo ya moyo yakaenda mbio zaidi, akageuka kwa jirani yake na kumuuliza,

USIKOSE SEHEMU IYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)