Mwandishi: Nea Makala
SEHEMU YA NNE
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Sherehe ikaanza kwa watu mbalimbali kuongea na kuonesha wazi kufurahishwa na juhudi za kampuni hiyo katika kukuza utamaduni wa Nchi, ikafika zamu ya mgeni rasmi ambaye pia ni naibu waziri wa Utamaduni, Habari na Michezo. Waziri alifuraishwa sana na hatua ya kampuni ya Korea kuja kuwekeza nchini kwetu, na hii imesaidia sana kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wengi aidha Waziri alishukuru pia kwa kuutangaza utamaduni wa nchi yetu.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI
SASA ENDELEA...
Ikafika hatua ya utoaji Tuzo kwa viongozi wa kampuni zote mbili, TAE XHIANG SUNG GROUP ikawa ya kwanza kuitwa kupokea Tuzo ya heshima. Taa zikazimwa na macho ya wote yakawa katika zulia jekundu ambapo kwa mwendo wa madaha kabisa mwanadada ambaye naweza kusema yeye ni zaidi ya mrembo akawa akitembea kueleka jukwaani, Darmy na Yassir wakashtuka mno wote kwa pamoja wakajikuta wakisema,
“Martha…!”
Jina lile lilivyopenya kwenye masikio ya Tony akajikuta akiangusha glasi aliyoishikiria mkononi mwake, taratibu akanyanyua shingo yake na kutazama kwenye zulia jekundu. Moyo ukamuenda mbio zaidi, Jamilah akabaki kuwashangaa asijue lolote, wakati akiendelea kushangaa Martha akawa ameshafika jukwaani na kupokea Tuzo ile. watu wakampongeza kwa makofi mengi kisha akasogea pembeni, Waziri akaendelea tena kwa kutoa tuzo kwa kampuni zalendo, jina la Tony likaitwa naye bila kuchelewa akamshika mkono Jamilah na kuongozana naye lakini kabla hajaenda Yassir akataka kumzuia kwa sababu aliona hatari ya kufanya vile. Waandishi wa habari walikuwa wengi eneo hilo hivyo kila tukio lilinaswa na kamera zao, Darmy na Yassir walifikiri itakuaje kwa Vanessa na Tedy ambao bila shaka watafatilia habari juu ya tukio hilo. Tony hakujali akaongozana na Jamilah, muonekano wao usiku huo ni kama maharusi, watu walishangilia mno, hali ilikuwa tofauti kwa Martha, alionesha wazi kuchukizwa na tukio hilo nafsi yake ilikaangika mno akapaona pale mbele pachungu. Wakafika jukwaani na Waziri mwenye zamana akatoa Tuzo ile.
Mshehereshaji akampa Martha kipaza sauti walau aongee machache, lakini hakuweza kusema kitu zaidi ya machozi kumtiririka, Tony alipoona vile akafurahi mno na kujisemea moyoni,
“Pole sana Martha, huu ni mwanzo tuu, picha kamili linakuja”
Mshehereshaji alivyoona Martha anashindwa kuongea akaamishia kipaza sauti kwa Tony, naye akakipokea na kuvuta pumzi ndefu kisha akasema,
“Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mungu kwanza, ambaye naamini kwa nguvu zangu nisingeweza kuwa hivi nilivyo leo. Pia shukrani kwa rafiki zangu wa karibu sana, Darmy na Yassir, Shukrani pia kwa wafanyakazi na uongozi mzima wa TAE XHIANG SUNG GROUP na shukrani za kipekee kwa Martha”.
Alipolitaja hilo jina kila mmoja akashangaa, watu wakawa kama wanaangalia picha la kihindi hasa baada ya Tony kugeuza shingo na kumtazama mrembo yule ambaye hatukujua kilio chake ni cha furaha au huzuni, japo alijitahidi kwa kiasi kikubwa kujenga tabasamu usoni mwake.
“Martha, nimejifunza mengi kupitia wewe, tamu na chungu vyote nimevijua asante sana,”
Akarudisha kipaza sauti na kumshika mkono Jamilah tayari kwa kuelekea kwenye nafasi yake.
Sherehe ikaisha na safari ya kurudi majumbani ikaanza Tony akaambata na marafiki zake pamoja na Jamilah, njia nzima kila mmoja akawa kimya hamna aliyejaribu kuuliza kitu. Tony alionekana mwenye mawazo mengi jambo lilimpa wakati mgumu Jamilah kuelewa nini kinazunguka vichwani mwao, wakafika Mapinga Darmy na Yassir wakashuka na Kuelekea makwao, Tony akageuka na kumtazama Jamilah,
“I want to spend this night with you, (nataka kuwa nawe usiku huu)”
“Its ok, am yours (sawa mimi ni wako tuu),” akajibu Jamilah huku akiupapasa mkono wa Tony kuashiria amekubali mualiko ule.
Safari ikaendelea na hatimaye wakafika nyumbani kwa Tony, Jamilah alishangazwa na ukubwa wa nyumba ile,
“Ina maana nyumba yote hii unaishi mwenyewe?”
“Ndio, naishi peke yangu”
“Mhmh! Umewezaje kuishi upweke kiasi hiki?”
“Aah! siwezi kuona upweke wakati wewe upo hapa”
“Wazazi au ndugu zako wako wapi?”
Jamilah akajikuta anauliza maswali mengi ambayo hayakuwa na umuhimu sana kwa wakati ule, Tony alivyoona Maswali yanazidi kuwa mengi akamsogelea Jamilah na kumshika kiuno kisha akamsogelea karibu zaidi na kumtazama usoni,
“Sasa nani…… anaye….ku…..pi….kia,” Jamilah akajikuta akihema kwa kasi mno na kushindwa kumalizia sentensi yake. Tony akamuangushia tabasamu zito na kumwambia,
“Acha nyoyo zetu zizungumze sasa, unachokihisi au ninachofikiri ni vigumu kukielewa, nataka usiku huu uwe wa kihistoria katika maisha yetu,”
“Tony nashindwa kujizuia kusema kuwa nakupenda sana, nifanye niwe wako siku zote”
“Shiiiii! Usiseme kitu”
Tony alizidi kumkoleza mrembo yule kwa maneno yaliyopenya moja kwa moja mtimani, aliugundua udhaifu wa Jamilah mapema sana hivyo akakoleza chumvi na ndani ya muda mfupi mwanadada yule akawa anahisi kama yupo dunia nyingine.
“Samahani sana Jamilah,”
Tony akasema japo kwa hali aliyokuwa nayo Jamilah muda huo akuelewa kitu, Tony akatumia nafasi hiyo kutimiza matakwa ya mwili wake.
Asubuhi na mapema Tony akaamka baada ya kuchangamsha mwili kwa mazoezi mepesi na kuweka mwili safi bafuni akaingia jikoni walau kuandaa kifungua kinywa kwa ajili ya mgeni wake ambaye hadi muda huo alikuwa bado amelala. Wakati Tony yupo jikoni simu yake ikawa inaita na mlio wa simu ukasababisha Jamilah aamke, akaiangalia ile simu akakuta Jina ni Tedy, akaiacha hadi ikakata, baada ya muda mfupi ukaingia ujumbe mfupi,
“Hello mpenzi! Bado umelala tuu”.
Ujumbe ule ukamshtua sana Jamilah, uvumilivu ukamshinda akaamua apekue zaidi simu ya Tony ili kujua zaidi habari za huyo Tedy, wakati akiendelea kupekua ukaingia ujumbe mwingine mfupi toka kwa Vanessa,
“Jamani bae, toka jana umenichunia shida nini, alafu mwenzio nimekumiss sana nataka nije kwako leo”
Jamilah akahisi kama anaota vile hakuamini yale aliyoyashuhudia, ikabidi ajifinye ili aone kama alikuwa ndotoni au la, japo hiyo haikubadili ukweli juu ya aliyoyashuhudia, akajikuta akitokwa na machozi kama mtoto mdogo,
“Siamini kama penzi langu la kwanza laweza kuwa chungu kiasi hiki, kwanini nimekuwa mpumbavu kumuamini mtu kirahisi hivi, kumbe hivi ndivyo maumivu ya mapenzi yalivyo,” aliendelea kusema Jamilah huku akilia, hakika hakuwa na nguvu hata ya kutoka pale kitandani hakutaka kuyakubali yale anayoyashuhudia.
Tony akamaliza kuandaa kifungua kinywa na akaingia chumbani kumuita Jamilah akaribie mezani, alipoingia hakika naye alishikwa na bumbuazi. Alikuta Jamilah akilia mithiri ya mtu aliyepata msiba wa mtu wake wa karibu, akasogea kujua kulikoni lakini Jamilah hakuongea kitu zaidi ya kumpa ile simu. Tony akaishiwa nguvu akajua tayari amesababisha ajali, Jamilah akamkunja Tony na kumpiga piga kifuani,
“Kwanini umenifanyia hivi Tony, katika siku yangu ya kwanza ya kujuana na mwanaume wewe umenifanyia ukatili huu, hakika sitokusamehe,” Jamilah akaongea kwa uchungu mno.
“Kwani nimekufanyia kipi kibaya?” Tony akauliza.
“Kwanini umenilaghai na kunifanya nikupende hadi kufikia hatua ya kulala na wewe wakati una mpenzi mwingine mbaya zaidi sio mmoja wawili Tony”
“Mhmh! Jamilah sasa mimi kuwa na wapenzi inahusiana nini na kilichotokea kati yetu?”
“Kwa iyo unanifanya mimi mtoto kunichanganya na wanawake wengine”
“Binafsi sikumbuki kama ulishawahi kuniuliza kama nina mpenzi au la, pia katika kinywa changu sijawahi kutamka neno nakupenda kwako”
“Tony..!”
Jamilah alijikuta akikosa neno la kuzungumza, hakuamini kama Tony angeweza kucheza na akili yake kiasi kile.
“Twende tukapate kifungua kinywa,” Tony alisema.
Jamilah akamuangalia Tony kwa hasira sana, hakujua nini afanye Zaidi ya machozi kumbubujika, hakuwa na nguvu hata ya kuinuka pale kitandani,
“Tony niambie kuwa niliyoyaona na niliyoyasikia kuwa si kweli”
“Unataka nikuambie nini Jamilah?”
“Niambie kuwa unanipenda na utaachana na hao wapenzi wako”
“Hahahahahahaha! You can’t be seriously! How could I do that? (Unamasihara wewe! Nawezaje kufanya hivyo)”
Jamilah akanyanyuka kitandani bila kusema neno, akaingia bafuni na baada ya kumaliza kuoga akavaa nguo zake na kuondoka lakini kabla hajatoka akageuka na kumtazama Tony kisha akamwambia,
“Usihisahau hii siku ipo siku utailipia, nitayafanya maisha yako kuwa ya shida Zaidi”
Tony alicheka sana aliposikia kauli ile, akamsogelea na kumshika kiuno, Jamilah akasogea nyuma na kumsukuma Tony, lakini jamaa alionekana kuwa imara kwani hakuweza kutikisika. Akamtazama Jamilah machoni na kumwambia,
“Usiwe mjinga wa kusahau ubaya unaoufanya kwa mtu, ile siku uliyonidhalilisha kwa ajali ndogo ya gari lako, niliumia sana na niliapa nitafanya lolote kukupata sasa uko mikononi mwangu huna la kufanya. Nilikwambia kamwe usisahau ile siku ila kwakuwa siku zote wanawake mnaongozwa na hisia kwanza bila kufikiria Zaidi, nikakutega ukategeka kwa hiyo bila bila nenda tu na usifikirie kunitafuta tena”.
Baada ya maneno hayo mazito akamuachia Jamilah ambaye kwa kiasi kikubwa aliduwaa huku machozi tuu yakimtoka, kiburi chake kimemuingiza pabaya.
Baada ya kuwa na mafanikio makubwa kama balozi wa kampuni ya Kikorea Martha akawa ni miongoni mwa wasichana ambao habari zao kila siku zinatangazwa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Wanaume wengi walitamani kuwa na mwanamke mwenye sifa kama alizonazo Martha, achilia mbali uzuri na urembo wake linapokuja swala la kazi Martha ni mtu anayependa kuwajibika kwa wakati na kuhakikisha kila kitu kimeenda kama kilivyopangwa. Wanaume wachache waliopata bahati ya kuwa karibu na mrembo huyo walishindwa kuzuia hisia zao na kila mmoja akijaribu kutupa karata yake kwa wakati wake. Kati ya wote hao hakuna hata mmoja aliyebahatika kuusimamisha moyo wa msichana yule.
Joseph huyu ni mmoja kati ya vijana wachache waliojaliwa stara na wenye mafanikio makubwa, hakuwahi kuwa katika mausihano ya kimapenzi na alijenga Imani kuwa hamna mapenzi ya kweli duniani, lakini toka amefahamiana na Martha taratibu mawazo yale yakaanza kufutika na akajikuta akivutiwa sana na msichana yule. Kutokana na kufanya kazi katika kitengo kimoja wakajikuta wakiwa karibu Zaidi hasa baada ya kupewa kazi ya kuandaa Makala itakayoonesha utamaduni wa watu wa pwani hasa wale waishio Tanga.
Iliwalazimu kufanya kazi mchana na usiku kuandaa mpango kazi, jinsi ya kuanza hadi utakapoishia, Jospeh alijisikia furaha sana kuwa na mwanadada yule ambaye muda wote aliwaza kazi tuu,
“Martha naweza kukuliza jambo?” alisema Jose.
“Uliza tuu!”
“Umekuwa bize sana na kazi! Nawaza huyo shemeji yangu anapata muda gani nawe?”
“Hahahahahaha! Kwanini umeuliza?”
“Nimeuliza tuu maana inaitaji moyo”
“Kwani wewe mkeo akiwa bize hivi utafanyaje?”
“Binafsi siwezi kusema kitu kwasababu sijawahi kuwa nae”
USIKOSE SEHEMU IYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi