USALITI WA KIAPO (5)

0
Mwandishi: Nea Makala

SEHEMU YA TANO
ILIPOISHIA...
“Hahahahahaha! Kwanini umeuliza?”

“Nimeuliza tuu maana inaitaji moyo”

“Kwani wewe mkeo akiwa bize hivi utafanyaje?”

“Binafsi siwezi kusema kitu kwasababu sijawahi kuwa nae”

KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE KILA UNAPOFUNGUA SIMULIZI ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
INSTALL CnZ Media ILI USIPITWE NA MIENDELEZO KILA INAPOKUWA TAYARI

SASA ENDELEA...
Ooh! Real? (Kweli?)”

“Ndio”

“What are you waiting for? (Unasubili nini?)

“Namsubiri yule atakayeufanya moyo wangu kusimama walau kwa dakika na kuacha kufikiria yote na kumuwaza yeye tuu”

“Keep on praying u will find her soon, (endelea kuomba utampata hivi karibuni)”

“Thanks for your advice (akhsante kwa ushauri wako)”

“Your welcome, (karibu)”

“Lakini bado hujanibu swali langu”

“Ooh! Ukweli kwamba sina muda na mapenzi kwa sasa, moyo wangu upo kwenye kazi yangu, hivyo tuu Jose”

“Mhmhmh! Haya”

Jose alijikuta akikatishwa tamaa na jibu alilopewa na Martha aliwaza Zaidi afanye nini walau mrembo yule arudishe hisia za mapenzi japo hakuwa anajua historia yake ya nyuma iko vipi, akajiuliza Zaidi je mrembo yule alishawahi kuwa kwenye mapenzi nini kilimtokea hadi leo kusema kuwa hana muda na mapenzi, kama hakuwai kuwa kwanini aogope kuingia katika ulimwengu huo wa huba.

Baada ya mipango yote kukamilika, wafanyakazi wote wakiongozwa na Martha wakaanza safari ya kuelekea mkoani Tanga kwa ajili ya kuandaa Makala itakayoonesha utamaduni wa mkoa huo ambao kwa hakika unasifika kwa mahaba.

“Sasa jamani nani ataongoza upigwaji wa picha maana Tony simuoni!” aliuliza Jose.

“Mimi nitaongoza,” Martha akajibu.

“Hiyo si sawa,” akasema Jose.

“Kwanini?”

“Umekuwa ukifanya kazi nyingi zinazomuhusu Tony, kwa nini azembee kiasi hiki hata kama yeye ni mkurugenzi lazima hawajibike sehemu yake,” aliongea Jose.

“Lakini alichosema Jose ni kweli, yeye ni muongozaji na anajua kila kitu kuhusiana na hii safari sasa kwanini hasiwepo,” alisema mfanyakazi mwengine.

“Jamani tuachane na hayo kila mtu achukulie hii safari kama sehemu ya kutuliza akili mbali na kazi inayotupeleka, tujitahidi kufanya vizuri bila kujali mtu flani hayupo”

Ikabidi wote wakubaliane na Martha japo kishingo upande, maswali mengi yakazuka vichwani, inakuaje mkurugenzi amtete Tony kwenye maswala ya uwajibikaji au kuna mambo yanayoendelea nyuma ya pazia ambayo wao hawayajui.

Safari ya kuelekea jijini Tanga ikaanza huku wote wakiamini kuwa Tony anaingiza maswala ya kibinafsi kwenye kazi, sababu mara nyingi walishuhudia wakurugenzi hao wawili wakitofautiana kimitazamo na utendaji pia, japo wote walikuwa na nia moja ya kufanya kampuni kukua na kuingiza faida maradufu.

Safari ilikua nzuri na yenye kuburudisha sana, wengi wao ilikuwa mara ya kwanza kwenda mkoa huo hivyo kwao ilikuwa kama kufanya utalii wa ndani,

“Samahani bosi sijajua tunafikia wapi?” aliuliza Jose.

“Tanga beach resort,” alijibu Martha.

“Aah! Sasa kwani uliwapa taarifa mapema?”

“Hilo ni jukumu la Tony”

“Sasa Tony mwenyewe hakuja tutafanyaje!”

“Usijali! Tutajua tukifika”

Wakati msafara wa wafanyakazi ukikaribia kabisa kuingia jijini Tanga, Tony alifika mapema sana na akawa ashafanya mipango yote ya hotelini. Tony toka amefika hotelini hapo hakutulia sehemu moja, uwepo wa warembo wengi eneo hilo ulimfanya ajihisi yupo paradiso ndogo,

“Braza eenh! Naona huku mambo sio mabaya,” alisema Tony baada ya kusogea katika kibanda cha mlinzi wa getini ambaye alikuwa zamu kwa wakati huo.

“Kwanini?”

“Braza! Huku kuna warembo kama wameshushwa hivi”

“Hahahahaha! Hii ndio Tanga sasa”

“Daah! Braza wee acha tuu nahisi mtaji wangu wa kuuza matunda nitaufirisi huku”

“Hahahahaha! Angalia utakosa hata nauli ya kurudi Dar”

“Ila broo kwani sehemu nyingine zipi ambazo kuna watoto wakali kama hawa na kumechangamka sana tofauti na hapa?” aliuliza Tony.

“Mhmhmh! Sehemu zilizochangamka ni nyingi kama utaenda Usagara, Chumbageni au kule Raskazone ndio balaa maeneo ya ufukwe nini unaweza kusahau kabisa kurudi kwenu, alafu watoto wakule wanajua mahaba kweli,” alijibu Mlinzi.

“Duuh! Broo uko vizuri kona zote unazijua”

“Hahahahaha! Kawaida tuu”

“Hivi broo umeoa kweli maana daah si mchezo”

“Hahahahahaha! Unafurahisha sana dogo na maswali yako, ukweli mimi nina mke na mtoto mmoja wa kiume, lakini si unajua tena kila siku uwezi kula mboga moja lazima ubadirishe kesho nyama, kesho kutwa maharage japo vyote ni protini” alisema Mlinzi.

Tony alijikuta akijenga Urafiki na Mlinzi yule ndani ya muda mfupi sana, sababu walionekana wote kupenda vitu vinavyofanana. Walizungumza vitu vingi sana, hii ikamsaidia Tony kujua picha nzima ya mkoa huo japo kwa uchache.

Tony akarudi sehemu ya beach na kupunga upepo wa eneo lile, hakuacha kusifia uumbaji wa Mungu kwa hakika alishuhudia warembo walioumbwa wakaumbika, alijisikia furaha sana moyoni mwake.

“Sasa huu si mtihani hata sijui nimsemeshe yupi kati ya hawa, kila mtu ni mzuri na ana kitu cha utofauti ambacho mwenzake hana,” alisema Tony kwa sauti ya chini ambayo haikusikika na yeyote yule.

Baada ya muda mfupi wafanya kazi wenzake wakawa wamefika hotelini Pale, Tony alipigiwa simu baada ya wao kuambiwa kuwa tayari kuna mtu aliyewaandalia sehemu ya kufikia. Tony akawafata na kuwakaribisha kwa tabasamu zito, tabasamu lile likakata hasa baada ya macho yake kukutana na ya Martha. Wawili hao wanasiri nzito sana ambayo kila mtu hataki kuikumbuka na ndio maana mara zote wanazokuwa karibu mmoja wao anajikuta akishindwa kuuficha ule mfukuto wa moyo.

“Daah! Sisi tulijua ndio umetuacha kwenye mataa,” alisema Jose.

“Nadhani unanifahamu vizuri linapokuja swala la kazi masihara uwa naweka pembeni”

“Maana kila tukikutazamia hukutokea kumbe mwenzetu umetuwahi huku au ndio vile nini!”

“Hahahah! Kama kawaida si unajua jiji la mahaba hili,” alisema Tony.

“Kwa hiyo ushachukua namba za wangapi?” Jose aliendelea kuuliza,

“Wengi tuu!”

“Jamani mtaongea mambo yenu mkiwa wenyewe tupo kwa ajili ya kazi, tuambie umechukua vyumba vingapi?” alisema Martha.

“Vyumba 6 tuu”

“Nini! Tunawezaje kulala kwenye vyumba 6 wakati sisi tupo 12?”

“Tutalala wawili wawili”

“No thanks! Siwezi kulala na mtu naomba uongeze vyumba”

Kauli ile ilimfanya Tony ajisikie vibaya mno kwani hakupenda pesa nyingi itumike kwa ajili ya malazi wakati pesa ile inaweza ikagaiwa kwa wafanyakazi kwa ajili ya kuwaongezea pesa za kujikimu kwa kipindi ambacho watakuwepo katika jiji hilo. Akawaangalia wafanyakazi wengine na kuwauliza,

“Na ninyi mnasemaje?”

Wote wakaunga mkono kauli ya Martha, hivyo Tony akapiga simu mapokezi na baada ya muda mfupi mhudumu akafika akiwa na funguo nyingine 6. Martha na Tony wakakosa vyumba upande ule ikabidi waende ghorofa moja Zaidi na huko wakapata vyumba ambavyo milango yao ikawa inatazamana.

“Samahani mhudumu! Siwezi kupata chumba tofauti na hiki?” alisema Tony.

“Hapana kaka yangu vyumba vya hadhi yenu ni hivi tuu na vingine vyote vinawatu si unajua tena msimu wa sikukuu huu,” alisema Mhudumu.

“Sawa akhsante”

“Mkiwa na shida yeyote mtapiga simu mapokezi”

Mhudumu akaondoka na kuwaacha Tony na Martha wakiingia vyumbani mwao kila mmoja. Katika ulimwengu huu wakidigitali mambo mengi hufanyika kwa njia ya mtandao, hii ikampa fursa Martha ya kutoa taarifa ya kikao kitakachofanyika jioni ya siku hiyo. Wafanya kazi wote wakaipata taarifa hiyo sababu kampuni hiyo ilihakikisha wafanyakazi wake wote wanakua na simu zenye uwezo wa internet hii imerahisisha kwa kiasi kikubwa ufikiwaji wa taarifa za dharula kwa wafanya kazi wote.

Tony alipohakikisha kuwa kila mmoja yupo katika chumba chake, hakuwa na kazi tena kwa wakati huo kama kawaida yake ikabidi ashuke kwa swahiba wake wa Muda mfupi ambaye ni mfanyakazi katika hoteli hiyo kama mlinzi.

“Braza nimerudi tena!”

“Aah! Karibu asee tupo tunavuta masaa tuu hapa”

“Sasa broo mi shida yangu unielekeze huko Raskazone maana vya kuadithiwa sitaki nataka nikathibitishe kwa macho yangu”

“Hahaha! Kumbe unamaanisha kweli, ila mbona msafara wenu unawarembo tuu tena kama yule sijui ni meneja sijui nani asee acha tuu”

“Aaah! Wale kila siku nawaona nataka sura mpya”

“Poa basi kuna tax apo nje pia kuna bajaji mbele kidogo, hivyo uamuzi wako juu ya usafiri wa kuutumia ukiwatajia jina la Raskazone hamna hasiyepafahamu”

“Poa broo shukrani”

“Karibu tena!”

Tony akatoka tayari kwa safari ya huko Raskazone, akasogea zilipo Tax na kuanza kumpa dereva maelekezo,

“Huko napafahamu vizuri, usiwe na shaka,” alisema dereva wa tax.

“Sasa inakuwa shilingi ngapi?”

Kabla dereva hajajibu simu ya Tony ikaita, kuangalia akakuta ni namba ngeni ikabidi haipokee,

“Uko wapi kuna vitu tunahitaji kuviweka sawa kabla ya kikao cha jioni,” ilisema sauti ya upande wa pili.

Tony akaisikiliza vizuri na kugundua kuwa ni Sauti ya Martha mwanamke ambaye kiukweli hakupenda kuwa karibu naye hata kidogo.

“Samahani siwezi kuja nimetoka sipo Hotelini,” alijibu Tony.

“Ulisema linapokuja swala la kazi, masihara unaweka pembeni, sasa nini hiki ambacho unaniambia. Mimi nawe tu wakurugenzi na kabla ya kukaa na wenzetu jioni lazima tukutane tuwe na mipango inayoshabihiana,” alisema Martha.

Tony akamsikiliza mrembo yule kwa makini kisha akaamua kuvunja safari yake na kurejea hotelini ambapo akapanga akutane na Martha katika fukwe iliyopo hotelini hapo. Haikuchukua muda wawili hao kukutana tayari wakaka na kuanza kujadili mpango kazi.

“Makala yetu lazima ioneshe utamaduni, vivutio vya asili na sehemu za kihistoria katika mkoa huu, hivyo nafikilia tufanye maojiano na hawa waongozaji wanaokuwa katika sehemu hizi za kihistoria awe anasimulia na sisi tunamrekodi,” alisema Martha.

“Wazo zuri lakini mimi ninafikiri tofauti kidogo” alisema Tony baada ya kumsikiliza Martha kwa makini mno.

“Wewe unataka iweje?”

“Mimi naona tusimrekodi huyo muongozaji badala yako tuchukue clip za sehemu tunazozitaka alafu wengine wafanye kazi ya kuchukua historia ya hizo sehemu kisha, tutaingia studio na kutengeneza audio zenye kuelezea hayo maeneo tutakuja kuzichanganya na hizo picha”.

Martha hakuwa na la kupinga juu ya wazo lile, akamuunga mkono Tony kwa asilimia zote,

“Sawa nadhani tumemaliza tutaonana jioni,” alisema Tony.

Wakati wawili hao wakiongea kwa mbali Jose akawa anaangalia, akaanza kuhisi wivu na kwa kuwa alimjua vyema Tony kuwa huwa afanyi makosa akiachwa karibu na msichana sio yeyote ila mrembo ndio kigezo kikubwa. Jose akahisi kuwa endapo ukaribu huo utazidi basi ni wazi hatoweza kumpata Martha mwanamke ambaye alitokea kumpenda kwa muda mrefu toka alipotua nchini ila akakosa tuu ujasiri wa kuelezea hisia zake.

“Nina nini Mimi? Mbona moyo wangu unaenda kasi kuliko kawaida, je nina hisia zozote juu ya mrembo huyu, ooh! Tony kwa wengine wote sawa ila kwa huyu hapana,” alisema Tony moyoni huku bado akimtazama Martha.

USIKOSE SEHEMU IYOFUATA

Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)