Mwandishi: Hassan O Mambosasa
SEHEMU YA PILI
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"Siyo uzawa wa ukoo wa mfalme huyu ndiyo maana taji limemkataa na wala siye mtoto halisi wa Zaif, taji hili linahitaji abadilishwe kiongozi kwani kizazi cha ukoo wa mfalme alibaki Mfalme Zulain tu ambaye amefariki tayari.
KUNA MATANGAZO YANATOKEA YAGUSE ILI KUNIPA NGUVU YA KUENDELEA
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA CnZ Media APP INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
Ufalme unatakiwa uhamishwe katika koo nyingi.." Mnajimu alishindwa kumalizia kauli yake na akajikuta amepigwa kofi zito hadi akaanguka chini, akiwa hajajua nani aliyempiga akahisi anakabwa shingoni huku akinyanyuliwa juu. Walinzi walipoona hali hiyo walitaka kusogea ili wamdhibiti kiumbe anayemkaba Mnajimu mkuu lakini walisita baadaya kiumbe mwenyewe kujitokeza hadharini, Salmin ambaye anajulikana na wanajamii hiyo kama jini mwenye nguvu kuliko wote ndiye aliyeonekana akimkaba Mnajimu huyo shingo.
"Kwanini unasema uongo ilihali wewe ni Mnajimu unayeheshimiwa na kuaminiwa katika himaya hii" Salmin alimuuliza Mnajimu huku akizidi kumkaba, Mnajimu aliomba aachiwe ili aongee na alipoachiwa ndipo akamwaga uhalisia wa jambo lenyewe.
"Wanahimaya na wakuu wote naomba mnisamehe sana kwa kusema uongo juu ya mjukuu wa mfalme, tamaa ya madaraka ndiyo imesababisha niseme uongo. Niliahidiwa kupewa nafasi ya mkuu wa baraza la sheria ikiwa tu nitafanya hila ufalme uhamishiwe katika ukoo wa waziri mkuu ili waziri mkuu awe mfalme wa Himaya hii, narudia tena viongozi wangu na wanahimaya wenzangu naomba mnisamehe kwani mimi nina nafsi na tamaa ni kitu cha kawaida kwa mwenye nafsi" Mnajimu alitoa maelezo hayo akiwa na aibu usoni kutokana na jambo alilolifanya, kuomba kwake msamaha hakukusaidia kitu kwani alikamatwa yeye na Waziri mkuu baada ya mkuu wa baraza la sheria kutoa amri hiyo. Baada ya kukamatwa kwa Waziri mkuu na Mnajimu mkuu Salmin alilitazama taji la kifalme kisha akamtazama Zalabain kwa umakini, macho yake yalianza kutoa nuru mithili ya almasi iliyomulikwa na mwanga mkali.
"Zalabain.......Zalabain mrithi wa kiti cha mfalme aliyestahiki kuvishwa taji la ufalme wa himaya hii lakini taji limemkataa kutokana na jambo moja tu ambalo mrithi wa kiti hiki hatakiwi kuwa nalo kabisa ambalo wewe unalo, udhaifu.....udhaifu wako ndiyo chanzo cha taji hili kukukataa. Ikiwa unatakiwa kuwa mrithi wa taji hil na kuna ubaya ambao umetendewa unatakiwa ulipe kisasi kwanza na si kusamehe ili upate taji hili, baba yako Zaif ameangamizwa na wanadamu akiwa na miaka 1500 na wanadamu hao ndiyo chanzo cha taji hili kukukataa na pia kuwa zito kuinuka kwa yoyote mwenye wazo la kuliweka kichwani mwako. Kisasi cha ubaya uliofanyiwa ndiyo kinahitajika ili hili taji likae kichwani mwako na hakuna mwingine atakayelivaa isipokuwa wewe, unapaswa utambue kwamba himaya hii yote inahitaji kiongozi na haiwezi kuendelea bila kiongozi na pia kiongozi ni wewe unatakiwa ulipe kisasi ili watu wako uwaongoze na si usamehe wapotee. Je upo tayari kuongoza himaya hii?" Salmin alifafanua chanzo cha kutokea jambo lililotokea kisha akamuuliza Zalabain.
"Nipo tayari kuongoza, nipo tayari kisasi cha kuuawa kwa baba yangu na nipo tayari kulipa kisasi cha ubaya uliotendwa kwangu" Zalabain aliongea huku macho yakibadilika na kuwa mekundu kabisa na yenye kung'aa, Salmin alimsogelea akamshika mkono kwa sekunde kadhaa kisha akamuachia halafu akamuambua "kazi njema". Salmin aliliokota taji la kifalme akamkabidhi Mkuu wa baraza la sheria kisha akaondoka, sherehe hizo ilivunjwa hapohapo na Zalabain akahitajika atimize kile alichoahidi mbele ya majini wote wa himaya hiyo.
****
Asubuhi ya siku iliyofuata tangu litokee tukio la kutoveshwa Zalabain taji, wafanyakazi wa kampuni ya upangishaji nyumba iitwayo Extoplus walikuwa wanasafiri kuelekea katika kijiji cha Duga Maforoni kwenda kuhudhuria sherehe ya uzinduzi wa nyumba mpya za kupangishwa za ksmpuni hiyo. Siku hiyo wafanyakazi wote waliotakiwa kwenda kwenye sherehe hiyo walijawa na hofu, karibu kila mfanyakazi alikuwa anasita kwenda anasita kwenda kwenye sherehe lakini hawakuwa na uwezo wa kukataa kwani ni idara nzima imeteuliwa kuhudhuria sherehe hiyo. Saa mbili kamili wote walikuwa kwenye basi wakielekea Duga kuhudhuria sherehe hizo, ndani ya basi kimya kilitawala kuanzia mwanzo wa safari na kilikuja kuvunjwa baada ya gari aina ya toyota coaster waliyokuwa wanaitumua kuvuka daraja la Utomfu. Mwanamke mmoja wa makamo alivunja ukimya uliopo ndani ya gari kwa kusema, " jamani mimi jana usiku nimeota ndoto ya ajabu sana".
"mmh! Hebu tueleze ni ndoto gani hiyo" Mwenzake aliyekuwa pembeni naye alidakia.
"nimeota nashuka kwenye gari natoka kazini nikakutana na mtoto wa miaka sita hizi akaniamkia kwa uchangamfu na mimi nikaitikia, yule mtoto kaniuliza unaujua mtego wa panya mimi nikamjibu ndiyo. Akaniuliza je kiumbe chochote kikiugusa unamnasa au unanasa panya tu, nikamjibu yoyote akiugusa ananaswa haijalishi kama Panya au siyo panya. Nilipomjibu akatabasamu nikamuuliza mbona umeniambia hivyo, akanijibu safari yako ya kesho Duga ni mtego wa panya ukienda utanasa ingawa wewe sio panya. Nimeshtuka usingizini hapohapo nikawa najiuliza kuhusu ndoto hiyo jamani ina maana gani" Yule mwanamke alieleza ndoto yake na alipomaliza wafanyakazi wote walikuwa wameingiwa na woga hapohapo.
"jamani hata mimi hii ndoto nimeiota" Mwanamke mwingine akadakia huku akionesha kuogopa.
"hata mimi" Mwanaume wa makamo ambaye ni mmoja wa wafanyakazi hao naye akadakia na mwishowe wote kwa pamoja wakatamka kwamba wameiota ndoto hiyo na hofu ikawa imetawala nafasi zao huku wengine wakimsihi dereva ageuze gari wasiende. Walikuwa wameshafika Amboni na sasa wapo kwenye daraja la kulia la mto Sigi hivyo dereva alikuwa yupo makini kulimaliza daraja hilo na hakuwasikiliza kabisa, baada ya kulipita daraja ndipo dereva akasema "jamani hata mimi nimeota ndoto ya namna hiyo lakini nimeipuuzia kwani si kila ndoto ni ya kweli".
"unasemaje wewe hebu simamisha nishuke nipande mabasi yanayotoka Horohoro nirudi mjini" Mwanamke yule aliyeeleza kuhusu ndoto alikuja juu.
"sawa ngoja tufike Mpirani kwenye kituo ili upate hilo gari" Dereva akimwambia yule mwanamke lakini hakutaka kumuelewa.
"simamishe gari nakuambia!" Yule mwanamke alizidi kufoka, dereva hakuwa na jinsi ilimbidi akanyage breki lakini gari ilikataa na ndiyo mwendo ulikuwa unazidi na usukani ikawa unajiongoza wenyewe.
"we mwanaharamu wewe simamisha gari nishuke sio kuongeza mwendo" Yule mwanamke alizidi kufoka baada ya kuona mwendo wa gari unazidi kuwa mkali, dereva hakumjibu yule yeye alitoka kwenye usukani akasimama kisha akawaangalia wafanyakazi wa idara nzima akiwa na hofu.
"si mimi ninayeendesha jamani gari linaenda lenyewe hili hebu oneni" Dereva aliongea huku akiwaonesha wafanyakazi wote jinsi usukani ulivyokuwa unajiongoza wenyewe, wafanyakazi wote walipoona hicho kioja walijikuta wakijaribu kutoka nje lakini walishindwa kwani milango haikufunguka na vioo vyote vilijifunga ghafla hata vile vilivyokuwa wazi vyote vilijifunga. Wafanyakazi wote walijaribu kupiga vioo ili wavunje lakini walishindwa kwani vioo vilikuwa vigumu sana, gari nayo ilizidi kuongezeka mwendo hadi ikawa kama ipo kwenye mashindano.
****
Makelele ya woga ndiyo yalitawala kwa watu wote kasoro kijana mmoja ambaye ni mmoja kati ya wafanyakazi wa idara hiyo ya kampuni ya Extoplus, yeye alikuwa kauchapa usingizi na wala hakunekana kama anatambua kuna tatizo, mwendo wa gari ulivyozidi kuwa mkali ilibidi wamuamshe huku wakimpigia kelele hadi akaamka. Kijana huyo alipoamka alionekana kukerwa na sauti za watu waliokuwa wanampigia kelele, kisha akalala tena akionekana kazidiwa na usingizi.
"We Saleh hebu amka si tupo kwenye hatari we unalala,.amka tusaidiane kutoka ndani ya gari hili tutakufa wote" Yule mwanamke aliyekuwa aking'ang'ania kushushwa alipaza sauti kumuambia yule kijana aamke aache kulala wapo hatarini, yule kijana aliinua kichwa mara ya pili akiwa anaonekana kama mtu ambaye alikuwa hajalala na hana dalili ya kusinzia. Saleh alikuwa amejawa na tabasamu alipoinua uso wake hadi wenzake wote wakawa wanamshangaa sana, wenzake walipozidi kumtazama kwa hofu yeye aliangua kicheko kabisa akionekana kufurahishwa na hofu ambayo imevamia nyuso za wenzake. Alipoona wamezidi kumshangaa aliamua kuwaambia, "mtakufa nyinyi ila sio nitakufa mimi". Kauli hiyo ilizidi kuwashangaza sana wenzake waliokuwa wana hofu na kifo, wote walimuona kama mtu aliyechanganyikiwa kwani si jambo la kawaida kwa mtu mwenye akili timamu kutamka maneno hayo katika eneo la kuelekea kwenye mlango wa kifo.
"We Saleh ni wewe kweli tunaokujua ni muoga au umechanganyikiwa tayari?" Mwanamke mwingine aliyekaa pembeni yake alimuuliza akionekana kuchanganywa na kauli ya Saleh.
"ushasema Saleh ni muoga sasa, utaulizaje ni Saleh au siyo wakati unaona kabisa mimi siyo muoga, labda jibu la kukusaidia ni kwamba Saleh yupo nyumbani kwake Mikanjuni amepumzika baada ya kuota ndoto iliyokuwa na onyo juu ya safari hii aliyoizingatia lakini nyinyi mnaojifsnya wapuuzaji wa mambo kisa elimu zenu leo utakuwa mwisho wenu" Yule kijana aliyesadikika kuwa ni Saleh alianza maneno yaliyozidi kuwashangaza wafanyakazi wote pamoja na dereva wa gari. Mwanamke mmoja aliyekaa pembeni yake yule kijana akiwa upande wa dirishani aliamua kumtandika makofi mawili mazito ya mashavu huku akisema, " hebu amke Saleh nahisi umelala bado".
"Nishaamka tayari ngoja nikulaze wewe sasa ulale milele" Yule kijana aliongea kisha akampiga yule mwanamke ngumi moja ya kichwani juu kidogo ya sikio, ngumi hiyo ilitoboa kichwa cha huyo Mwanamke na ubongo wake uliochanganyika na damu ukaruka hadi kioo cha dirishani na kuibadilisha taswira ya eneo la karibu na hapo kuwa damu na madonge ya ubongo yakiwa yameruka hadi kwa wengine waliopo jirani na endo hilo. Mayowe ya uoga yalizidi ndani ya gari hilo huku watu karibia wote wakitamka majina ya mama zao kutokana na tukio waliloliona, Yule kijana alipoona makelele yamezidi aliamua kunyanyuka akawatazama wafanyakazi huku macho yake yaking'aa kama macho ya paka. Mikono yake ilianza kutoa kucha ndefu kama za Simba na sura yake ikabadilika ikawa ya kutisha, mabegsni alitoa mabawa kama ya popo na kinywaji akawa anatoa cheche za moti pamoja na mngurumo unaoashirua hasira.
"Kwa jina la yesu pepo mchafu usiyehitajika tokaaaaa!" Mwanaume mmoja ambaye alikaa kiti cha nyuma kabisa alipaza sauti huku akimnyooshea mkono yule kijana ambaye muda huo alikuwa amegeuka kiumbe wa ajabu, Yule kiumbe aliangua kicheko huku akimtazama yule Mwanaume kwa jinsi anavyobabaika kukemea kama Mlokole.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi