Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"Naomba moja tu, tena iliyoandikwa na mfanyakazi aliyeacha kazi muda mfupi baada ya kuanza" Sajenti Minja aliongea huku akiangalia chini,
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
"Mh…wewe unaitaka ya nini?" Dada alimuuliza huku akitilia shaka hali aliyokuwa nayo Sajenti Minja,
"Kuliko kuendelea na hii kesi, nimeona bora niache kazi" Sajenti Minja alitoa kauli iliyomshangaza yule Dada,
"Kwanini usingeandika barua ya kuomba hiyo kesi apewe mtu mwingine?" Dada aliuliza,
"Nikiulizwa sababu nitajibu nini?" Sajenti Minja aliuliza,
"Dah, kweli mtihani" Dada alijibu baada ya kufikiria kwa muda mfupi,
"Sasa kama wewe uliye mzoefu na kazi hii unaona huo ni mtihani, je mimi ambaye sina uzoefu wa kutosha?" Sajenti Minja aliuliza huku akiamini hawezi kujibiwa,
"Ila hiyo sio sababu ya kuacha kazi, wewe si umeanza kazi juzi tu? Ungeizungusha hii kesi muda mrefu bila mafanikio yoyote ni lazima angepewa mtu mwingine" Dada alijaribu kumshawishi Sajenti Minja,
"Mafunzo niliyopitia mimi sio uliyopitia wewe, mafunzo niliyopitia mimi yananifundisha kusimamia Ukweli" Sajenti Minja aliongea,
"Hakuna mafunzo ya uaskari yanayofundisha kusema uongo, ila mimi nimeona bora utumie hiyo njia kuliko kuacha kazi" Dada aliongea kwa huruma ili kumshawishi Sajenti Minja akubaliane nae,
"Naomba nipatie hiyo nakala ya barua, nitaenda kufikiria mbele ya safari" Sajenti Minja aliongea kuonesha amedhamiria kutekeleza hadhma yake,
"Sawa bwana" Dada aliongea kisha akamtafutia hiyo nakala na kumpatia, Sajenti Minja akapokea na kuondoka.
Mama kayoza
ni jina lake la ukubwani tu, jina
alilozaliwa nalo ni Aika John Minja,
ni mtoto wa tatu kutoka familia ya
watoto wanne, na ni mtoto wa kike
pekee katika familia yao, kaka zake
wawili ni wafanya biashara wakubwa
kiasi katika jiji la Arusha, na mdogo
wake ni afisa wa polisi, anaitwa Joel
John Minja.
Mama Kayoza alipokuwa na umri wa
miaka kumi na saba, alijiingiza katika masuala ya mahusiano ya
mapenzi, ila aliambulia kupata ujauzito na kukataliwa na mwanaume
aliempa huo ujauzito na mbaya zaidi hata nyumbani kwao alifukuzwa.
Baada ya kuangaika na mimba yake mtaani na Maisha kumuendea vibaya, aliamua arudi nyumbani na kuwaomba msamaha wazazi, wazazi wake wakamkubalia kwa hali aliyonayo ila
kwa kuwa alikuwa bado mwanafunzi,
wazazi wake wakamshauri akaitoe ile
mimba, nae akakubali.
Ila katika
utoaji wa hiyo mimba ilipelekea au kile kitendo cha Kutoa mimba kilitaka
kumgharimu maisha yake, kwani alivuja damu nyingi kiasi kwamba
ilimbidi alazwe hospitali takribani mwezi
mmoja na nusu kutokana na damu kumpungukia mwilini.
Alipotoka hospitali
akahapa kutopenda tena
mwanaume na akaahidi kutilia mkazo katika masomo yake.
Baada ya kupona kabisa,
aliendelea na shule na Mungu akamjaalia kumaliza
kidato cha nne salama, ila alama aliyopata haikua salama kwani haikumruhusu kujiunga au kuendelea na madarasa yanayofuata.
Baada ya miaka miwili ya kukaa nyumbani, kwa bahati nzuri akatokea mwanaume, mwenyeji
wa Bukoba, alieitwa Ezekiel Kayoza
Lutashobi na kutoa posa kwa wazazi
wa Aika, wakamkubalia bila kipingamizi kwa sababu ya fedha
alizokuwa nazo na pia waliona binti yao tayari amefikia umri wa kuishi na mume.
Baada ya miezi kadhaa ya kufuata utaratibu wa dini na mila, bwana Ezekiel na bi Aika wakaoana kwa ndoa ya kikristo iliyokuwa na kila aina ya furaha kutoka kwa ndugu wa pande zote mbili, yaani upande wa mwanaune na upande wa mwanamke.
Walikaa miaka miwili bila kupata mtoto, hapo ndipo chokochoko zikaanza kutoka kwa upande wa mwanaume wakidai wifi yao ni mgumba.
Baada ya uvumilivu wa maneno na kashfa nyingi kutoka kwa mawifi, Aika alifanikiwa kupata ujauzito na kujifungua mtoto mmoja wa kiume aliyefuatiwa na wengine wawili wote wakiwa wa kiume na jumla ni kwamba alibahatika kupata watoto watatu.
Wa kwanza aliitwa
Zakaria, wa pili, Buguzo na wa tatu ndiyo huyu bwana mdogo alisebabisha niandike huu mkasa, anaitwa Kayoza.
Mama Kayoza akatayarisha
chakula, akawatengea wanae mezani,
kisha akajumuika nao kula. Wakati wakiwa wanakula hakuna aliyemkumbusha mama Kayoza kuwa awasimulie ule mkasa, wote walikuwa kimya.
Baada ya kula na kuoga, wote walikaa sebuleni
wakawa wanaangalia filamu za
Tanzania, kayoza akavunja ukimya,
"mama, baadae yenyewe si ndio sasa
hivi?, tuadithie basi" Kayoza alimkumbusha mama yake,
"khaa!, nawe
nae usahau?" Mama kayoza
akamwambia mwanae kwa utani
huku anacheka.
"matatizo
yanasahaulika nini?", kayoza akamjibu mama yake.
"haya basi,
nianzie wapi?" Mama kayoza akauliza huku akimuangalia mwanae.
"anzia mwanzo" kayoza
akajibu huku akitega masikio ili kusikiliza kisa kilichopelekea yeye kuwa mtu wa kubadilika na kuwa kama mnyama.
Mama kayoza akaanza
kuwaelezea…
Alianza namna hii, "mimi
nilipoolewa na baba yako, nilimkuta
ana fedha zake za kutosha, alikuwa
ana magari makubwa ya kubebea
mizigo, alikuwa na daladala pale
Bukoba mjini, alikuwa na gari ndogo
tatu za kutembelea, na nyumba tatu
pia.
Kwa hiyo yeye alitoka Bukoba
mpaka Kilimanjaro kuja kunioa mimi,
kwa madai ya kuwa alinipenda toka
zamani na alikuwa ananifuatilia chini
chini.
Baada ya ndoa nilitoka nyumbani na kuhamia kwenye nyumba ya baba yako ambayo aliijengea Bukoba.
Ila baada ya kuhamia Bukoba,
nilikaa pale nyumbani kwangu wiki
mbili ndani, hakuna hata jirani
mmoja aliyekuja kuniona, mule
ndani nilikaa na wafanyakazi tu, na
baadhi ya ndugu wa baba yako
ambao walikuwa ndio
wananichangamsha changasha, ila
kingine kilichokuwa kinanishangaza ni
kwamba kila ilipofika mwisho wa
mwezi, baba yako alinunua, mbuzi
wawili weusi na kondoo mmoja, alafu
wanaukoo wote walikuja pale
nyumbani, walikuwa wanaingia katika
chumba kimoja kilichopo uwani na kujifungia uko, mimi sikuruhusiwa kuingia.
Na nilipomuuliza, yeye
aliniambia kile chumba ni kitakatifu,
mimi sikuwa mtu wa kuhoji hoji sana,
kwa hiyo sikutaka kudadisi zaidi kwa maana nilipojaribu kufanya hivyo uso wake ulionesha kutofurahishwa na maswali yangu.
Ila niliendelea kujiuliza mwenyewe ni nini utakatifu
wa hicho chumba?.
Wanandugu wa baba yako na baba yako mwenyewe waliendelea kuingiaingia katika
chumba iko ambacho ni kikubwa,
kilikuwa na uwezo wa kubeba watu
mia na zaidi.
Kingine cha kushangaza ni kwamba, wote walikuwa wanavaa
mavazi meusi, iwe shuka au nguo ya
kawaida, ili mradi mwanamke avae
nguo ndefu hadi katika vidole vya
miguu yake.
Na kila siku wanayoingia katika hicho chumba ikifika usiku mkubwa,
walichukua magari makubwa ya
mizigo na kuenda wanapopajua
wenyewe, pamoja na wale mbuzi na
kondoo.
Ila baadae baba yako alikuja
kuniambia kuwa uwa wanaenda
kutoa sadaka katika mzimu wa mababu
zao walikufa miaka iliyopita, na kwa sasa yeye ndio
kaachiwa mamlaka ili autunze mzimu mmoja ambao ni mkuu kuliko mizimu yote wanayoiabudu.
Sikufurahishwa
na hali hiyo, ila sikutaka kumuudhi
mume wangu, baada ya miaka miwili
ya ndoa, nikajifungua mtoto wangu
wa kwanza ambae ni kaka yako", Mama Kayoza aliongea kisha akamimina maji katika kikombe na kunywa,
"mama mbona
huyo kaka yangu simfahamu, au yupo mbali na nchi hii?" kayoza
akahoji.
"Subiri sasa mbona una
haraka hivyo?" mama Kayoza
akauliza huku akimshangaa mwanae,
"Maswali ni lazima, sasa nisipouliza utajuaje kama nimekuelewa?" Kayoza alihoji
"Sikiliza kwanza, maswali utauliza nikimaliza kusimulia" Mama kayoza alijibu kisha akaendelea,
"baada ya kumzaa
kaka yako wa kwanza, furaha
iliongezeka katika familia yetu, ila kitu ambacho
kilikuwa kinanitatiza ni kuwa,
majirani hawakutaka kabisa
kunizoea na wala hawakutaka hata kuja kutujulia hali kipindi nimejifungua, sikujua sababu, ila siku
moja kuna jirani mmoja ndio
akanipasulia sababu, eti kuwa mume
wangu na ukoo wake ni wachawi wa
kutupwa, na kila mke aliyemuoa
hakukaa hata mwaka, alikufa,
wananishangaa mimi nimemaliza
miaka mitatu, na ninae mtoto
mkubwa tu wa mwaka mmoja.
Kiukweli ile habari ya wanawake kufa
iliniogopesha, ikabidi jioni ilipofika
nimuulize mume wangu, kwa kuwa
alinipenda alinieleza ukweli…
SEHEMU YA KUMI NA SABA.
Aliniambia kuwa, kila mwanamke
ambaye alimuoa, alimshauri aachane
na mambo ya mizimu, ilo suala
lilimuudhi na kuwaua kwa njia ya
kuwadhoofisha kiafya, ila mwisho wa
siku, mzimu wenyewe ukamshauri
asioe mwanamke ambae anatokea
Bukoba, ndo akaja kunioa mimi.
Akaendelea kuniambia
"tangu nimekuoa, sijaona hata siku
moja ukifatilia mambo yangu, na leo
ndio umeniuliza kwa mara ya kwanza
kuhusu mambo yangu yaliyopita
kipindi cha nyuma".
Baada ya baba
yenu kuniambia maneno haya,
niliridhika nayo kabisa na wala sikutaka kuuliza tena ingawa nilianza kuishi kwa hofu.
Baada ya miaka miwili nilifanikiwa
kuzaa mtoto wa pili, na hapo tukapanga
tusizae tena, na baba yako kwa mara
ya kwanza akaniambia kuwa
anaachana na mambo ya mizimu, mimi
nilipingana nae, ila hakunielewa.
Mimi niliendelea kupingana nae kwa sababu
nilihisi kuwa ndugu zake wanaweza
kuona mimi nilimshawishi baba yenu kuachana na mambo ya mizimu.
Baada ya
miezi sita tangu aitoe kauli ya
kuachana na mizimu, ni kweli aliacha kununua kondoo wa kuchinjwa kila mwisho wa mwezi, na pia aliwaambia ndugu zake warafute sehemu ya kufanyia ibada zao kwa kuwa yeye hakuwa tayari kuendelea na hizo ibada.
Mwanzo walikuwa wagumu kumuelewa, ila baadae walikubaliana nae ila kwa shingo upande.
Baada ya mwaka mmoja, tulianza kufilisika, gari zilipata ajali
kiutatanishi zikafa, nyingine
alidhulumiwa na ndugu zake ambao
walikuwa wanazisimamia, na hatua
ya mwisho kabisa na ambayo sikuwa
naifikiria kabisa, ni kwamba baba
yako aliamua kuuza nyumba zake
zote, hadi ile tuliyokuwa tunakaa,
kisha akatuchukua mimi na kaka
zako akatupeleka kijijini kwa mama
yake, ambaye ni bibi yako.
Huko sasa ndipo mauza uza yakaanza, Siku moja
wakati natoka kisimani kuchota maji,
nikamkuta kaka yako mkubwa,
amekufa kifo cha ajabu sana,
shingoni alikuwa na alama za meno,
kile kifo hata baba yako
kilimshangaza, tuliomboleza tukalia tukazika, mwishowe tukasahau.
Siku ya harobaini baada ya kile kifo, usiku wakati tumelala
na baba yako, tulishtushwa na
upepo mkali ulioezua paa la nyumba
tuliyokuwa tunakaa, wote tukakurupuka kitandani na kuanza kushangaa hiyo hali, wakati
tunautafakari ule upepo,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi