KIJIJINI KWA BIBI (11)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA KUMI NA MOJA
TULIPOISHIA...
"Naomba moja tu, tena iliyoandikwa na mfanyakazi aliyeacha kazi muda mfupi baada ya kuanza" Sajenti Minja aliongea huku akiangalia chini,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"Mh…wewe unaitaka ya nini?" Dada alimuuliza huku akitilia shaka hali aliyokuwa nayo Sajenti Minja,

"Kuliko kuendelea na hii kesi, nimeona bora niache kazi" Sajenti Minja alitoa kauli iliyomshangaza yule Dada,

"Kwanini usingeandika barua ya kuomba hiyo kesi apewe mtu mwingine?" Dada aliuliza,

"Nikiulizwa sababu nitajibu nini?" Sajenti Minja aliuliza,

"Dah, kweli mtihani" Dada alijibu baada ya kufikiria kwa muda mfupi,

"Sasa kama wewe uliye mzoefu na kazi hii unaona huo ni mtihani, je mimi ambaye sina uzoefu wa kutosha?" Sajenti Minja aliuliza huku akiamini hawezi kujibiwa,

"Ila hiyo sio sababu ya kuacha kazi, wewe si umeanza kazi juzi tu? Ungeizungusha hii kesi muda mrefu bila mafanikio yoyote ni lazima angepewa mtu mwingine" Dada alijaribu kumshawishi Sajenti Minja,

"Mafunzo niliyopitia mimi sio uliyopitia wewe, mafunzo niliyopitia mimi yananifundisha kusimamia Ukweli" Sajenti Minja aliongea,

"Hakuna mafunzo ya uaskari yanayofundisha kusema uongo, ila mimi nimeona bora utumie hiyo njia kuliko kuacha kazi" Dada aliongea kwa huruma ili kumshawishi Sajenti Minja akubaliane nae,

"Naomba nipatie hiyo nakala ya barua, nitaenda kufikiria mbele ya safari" Sajenti Minja aliongea kuonesha amedhamiria kutekeleza hadhma yake,

"Sawa bwana" Dada aliongea kisha akamtafutia hiyo nakala na kumpatia, Sajenti Minja akapokea na kuondoka.

Mama kayoza

ni jina lake la ukubwani tu, jina

alilozaliwa nalo ni Aika John Minja,

ni mtoto wa tatu kutoka familia ya

watoto wanne, na ni mtoto wa kike

pekee katika familia yao, kaka zake

wawili ni wafanya biashara wakubwa

kiasi katika jiji la Arusha, na mdogo

wake ni afisa wa polisi, anaitwa Joel

John Minja.

Mama Kayoza alipokuwa na umri wa

miaka kumi na saba, alijiingiza katika masuala ya mahusiano ya

mapenzi, ila aliambulia kupata ujauzito na kukataliwa na mwanaume

aliempa huo ujauzito na mbaya zaidi hata nyumbani kwao alifukuzwa.

Baada ya kuangaika na mimba yake mtaani na Maisha kumuendea vibaya, aliamua arudi nyumbani na kuwaomba msamaha wazazi, wazazi wake wakamkubalia kwa hali aliyonayo ila

kwa kuwa alikuwa bado mwanafunzi,

wazazi wake wakamshauri akaitoe ile

mimba, nae akakubali.

Ila katika

utoaji wa hiyo mimba ilipelekea au kile kitendo cha Kutoa mimba kilitaka

kumgharimu maisha yake, kwani alivuja damu nyingi kiasi kwamba

ilimbidi alazwe hospitali takribani mwezi

mmoja na nusu kutokana na damu kumpungukia mwilini.

Alipotoka hospitali

akahapa kutopenda tena

mwanaume na akaahidi kutilia mkazo katika masomo yake.

Baada ya kupona kabisa,

aliendelea na shule na Mungu akamjaalia kumaliza

kidato cha nne salama, ila alama aliyopata haikua salama kwani haikumruhusu kujiunga au kuendelea na madarasa yanayofuata.

Baada ya miaka miwili ya kukaa nyumbani, kwa bahati nzuri akatokea mwanaume, mwenyeji

wa Bukoba, alieitwa Ezekiel Kayoza

Lutashobi na kutoa posa kwa wazazi

wa Aika, wakamkubalia bila kipingamizi kwa sababu ya fedha

alizokuwa nazo na pia waliona binti yao tayari amefikia umri wa kuishi na mume.

Baada ya miezi kadhaa ya kufuata utaratibu wa dini na mila, bwana Ezekiel na bi Aika wakaoana kwa ndoa ya kikristo iliyokuwa na kila aina ya furaha kutoka kwa ndugu wa pande zote mbili, yaani upande wa mwanaune na upande wa mwanamke.

Walikaa miaka miwili bila kupata mtoto, hapo ndipo chokochoko zikaanza kutoka kwa upande wa mwanaume wakidai wifi yao ni mgumba.

Baada ya uvumilivu wa maneno na kashfa nyingi kutoka kwa mawifi, Aika alifanikiwa kupata ujauzito na kujifungua mtoto mmoja wa kiume aliyefuatiwa na wengine wawili wote wakiwa wa kiume na jumla ni kwamba alibahatika kupata watoto watatu.

Wa kwanza aliitwa

Zakaria, wa pili, Buguzo na wa tatu ndiyo huyu bwana mdogo alisebabisha niandike huu mkasa, anaitwa Kayoza.

Mama Kayoza akatayarisha

chakula, akawatengea wanae mezani,

kisha akajumuika nao kula. Wakati wakiwa wanakula hakuna aliyemkumbusha mama Kayoza kuwa awasimulie ule mkasa, wote walikuwa kimya.

Baada ya kula na kuoga, wote walikaa sebuleni

wakawa wanaangalia filamu za

Tanzania, kayoza akavunja ukimya,

"mama, baadae yenyewe si ndio sasa

hivi?, tuadithie basi" Kayoza alimkumbusha mama yake,

"khaa!, nawe

nae usahau?" Mama kayoza

akamwambia mwanae kwa utani

huku anacheka.

"matatizo

yanasahaulika nini?", kayoza akamjibu mama yake.

"haya basi,

nianzie wapi?" Mama kayoza akauliza huku akimuangalia mwanae.

"anzia mwanzo" kayoza

akajibu huku akitega masikio ili kusikiliza kisa kilichopelekea yeye kuwa mtu wa kubadilika na kuwa kama mnyama.

Mama kayoza akaanza

kuwaelezea…

Alianza namna hii, "mimi

nilipoolewa na baba yako, nilimkuta

ana fedha zake za kutosha, alikuwa

ana magari makubwa ya kubebea

mizigo, alikuwa na daladala pale

Bukoba mjini, alikuwa na gari ndogo

tatu za kutembelea, na nyumba tatu

pia.

Kwa hiyo yeye alitoka Bukoba

mpaka Kilimanjaro kuja kunioa mimi,

kwa madai ya kuwa alinipenda toka

zamani na alikuwa ananifuatilia chini

chini.

Baada ya ndoa nilitoka nyumbani na kuhamia kwenye nyumba ya baba yako ambayo aliijengea Bukoba.

Ila baada ya kuhamia Bukoba,

nilikaa pale nyumbani kwangu wiki

mbili ndani, hakuna hata jirani

mmoja aliyekuja kuniona, mule

ndani nilikaa na wafanyakazi tu, na

baadhi ya ndugu wa baba yako

ambao walikuwa ndio

wananichangamsha changasha, ila

kingine kilichokuwa kinanishangaza ni

kwamba kila ilipofika mwisho wa

mwezi, baba yako alinunua, mbuzi

wawili weusi na kondoo mmoja, alafu

wanaukoo wote walikuja pale

nyumbani, walikuwa wanaingia katika

chumba kimoja kilichopo uwani na kujifungia uko, mimi sikuruhusiwa kuingia.

Na nilipomuuliza, yeye

aliniambia kile chumba ni kitakatifu,

mimi sikuwa mtu wa kuhoji hoji sana,

kwa hiyo sikutaka kudadisi zaidi kwa maana nilipojaribu kufanya hivyo uso wake ulionesha kutofurahishwa na maswali yangu.

Ila niliendelea kujiuliza mwenyewe ni nini utakatifu

wa hicho chumba?.

Wanandugu wa baba yako na baba yako mwenyewe waliendelea kuingiaingia katika

chumba iko ambacho ni kikubwa,

kilikuwa na uwezo wa kubeba watu

mia na zaidi.

Kingine cha kushangaza ni kwamba, wote walikuwa wanavaa

mavazi meusi, iwe shuka au nguo ya

kawaida, ili mradi mwanamke avae

nguo ndefu hadi katika vidole vya

miguu yake.

Na kila siku wanayoingia katika hicho chumba ikifika usiku mkubwa,

walichukua magari makubwa ya

mizigo na kuenda wanapopajua

wenyewe, pamoja na wale mbuzi na

kondoo.

Ila baadae baba yako alikuja

kuniambia kuwa uwa wanaenda

kutoa sadaka katika mzimu wa mababu

zao walikufa miaka iliyopita, na kwa sasa yeye ndio

kaachiwa mamlaka ili autunze mzimu mmoja ambao ni mkuu kuliko mizimu yote wanayoiabudu.

Sikufurahishwa

na hali hiyo, ila sikutaka kumuudhi

mume wangu, baada ya miaka miwili

ya ndoa, nikajifungua mtoto wangu

wa kwanza ambae ni kaka yako", Mama Kayoza aliongea kisha akamimina maji katika kikombe na kunywa,

"mama mbona

huyo kaka yangu simfahamu, au yupo mbali na nchi hii?" kayoza

akahoji.

"Subiri sasa mbona una

haraka hivyo?" mama Kayoza

akauliza huku akimshangaa mwanae,

"Maswali ni lazima, sasa nisipouliza utajuaje kama nimekuelewa?" Kayoza alihoji

"Sikiliza kwanza, maswali utauliza nikimaliza kusimulia" Mama kayoza alijibu kisha akaendelea,

"baada ya kumzaa

kaka yako wa kwanza, furaha

iliongezeka katika familia yetu, ila kitu ambacho

kilikuwa kinanitatiza ni kuwa,

majirani hawakutaka kabisa

kunizoea na wala hawakutaka hata kuja kutujulia hali kipindi nimejifungua, sikujua sababu, ila siku

moja kuna jirani mmoja ndio

akanipasulia sababu, eti kuwa mume

wangu na ukoo wake ni wachawi wa

kutupwa, na kila mke aliyemuoa

hakukaa hata mwaka, alikufa,

wananishangaa mimi nimemaliza

miaka mitatu, na ninae mtoto

mkubwa tu wa mwaka mmoja.

Kiukweli ile habari ya wanawake kufa

iliniogopesha, ikabidi jioni ilipofika

nimuulize mume wangu, kwa kuwa

alinipenda alinieleza ukweli…

SEHEMU YA KUMI NA SABA.

Aliniambia kuwa, kila mwanamke

ambaye alimuoa, alimshauri aachane

na mambo ya mizimu, ilo suala

lilimuudhi na kuwaua kwa njia ya

kuwadhoofisha kiafya, ila mwisho wa

siku, mzimu wenyewe ukamshauri

asioe mwanamke ambae anatokea

Bukoba, ndo akaja kunioa mimi.

Akaendelea kuniambia

"tangu nimekuoa, sijaona hata siku

moja ukifatilia mambo yangu, na leo

ndio umeniuliza kwa mara ya kwanza

kuhusu mambo yangu yaliyopita

kipindi cha nyuma".

Baada ya baba

yenu kuniambia maneno haya,

niliridhika nayo kabisa na wala sikutaka kuuliza tena ingawa nilianza kuishi kwa hofu.

Baada ya miaka miwili nilifanikiwa

kuzaa mtoto wa pili, na hapo tukapanga

tusizae tena, na baba yako kwa mara

ya kwanza akaniambia kuwa

anaachana na mambo ya mizimu, mimi

nilipingana nae, ila hakunielewa.

Mimi niliendelea kupingana nae kwa sababu

nilihisi kuwa ndugu zake wanaweza

kuona mimi nilimshawishi baba yenu kuachana na mambo ya mizimu.

Baada ya

miezi sita tangu aitoe kauli ya

kuachana na mizimu, ni kweli aliacha kununua kondoo wa kuchinjwa kila mwisho wa mwezi, na pia aliwaambia ndugu zake warafute sehemu ya kufanyia ibada zao kwa kuwa yeye hakuwa tayari kuendelea na hizo ibada.

Mwanzo walikuwa wagumu kumuelewa, ila baadae walikubaliana nae ila kwa shingo upande.

Baada ya mwaka mmoja, tulianza kufilisika, gari zilipata ajali

kiutatanishi zikafa, nyingine

alidhulumiwa na ndugu zake ambao

walikuwa wanazisimamia, na hatua

ya mwisho kabisa na ambayo sikuwa

naifikiria kabisa, ni kwamba baba

yako aliamua kuuza nyumba zake

zote, hadi ile tuliyokuwa tunakaa,

kisha akatuchukua mimi na kaka

zako akatupeleka kijijini kwa mama

yake, ambaye ni bibi yako.

Huko sasa ndipo mauza uza yakaanza, Siku moja

wakati natoka kisimani kuchota maji,

nikamkuta kaka yako mkubwa,

amekufa kifo cha ajabu sana,

shingoni alikuwa na alama za meno,

kile kifo hata baba yako

kilimshangaza, tuliomboleza tukalia tukazika, mwishowe tukasahau.

Siku ya harobaini baada ya kile kifo, usiku wakati tumelala

na baba yako, tulishtushwa na

upepo mkali ulioezua paa la nyumba

tuliyokuwa tunakaa, wote tukakurupuka kitandani na kuanza kushangaa hiyo hali, wakati

tunautafakari ule upepo, 

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)