KIJIJINI KWA BIBI (14)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA KUMI NA NNE
TULIPOISHIA...
"Hapana" Sajenti Minja alijbu,

"Kwanini?" Yule bwana aliuliza,

"Nimepata tatizo la afya, nikaona ni bora nipumzike" Sajenti alijibu,

"Lete cheti cha daktari kinachothibitisha wewe no mgonjwa"

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Yule bwana alimwambia Sajenti Minja,

"Nimekiacha nyumbani" Sajenti Minja alijibu ila alitoa jibu la uongo kwa maana hakuna cheti wala kitu chochote kinachoweza kuthibitisha yeye ni mgonjwa,

"Ni tatizo gani la kiafya ulilonalo?" Yule bwana aliuliza,

"Pumzi inanibana sana kiasi kwamba nashindwa kupumua" Sajenti Minja alijibu,

"Ooh pole, basi nenda kapumzike, tutaendelea baadae na maswali" Yule bwana aliongea,

"Sawa mkuu" Sajenti Minja alijibu na kuanza kuondoka,

"Unaenda wapi?" Yule bwana alimuuliza kwa mshangao,

"Umeniambia nikapumzike mkuu, naenda nyumbani" Sajenti Minja alijibu huku akisimama,

"Utapumzikia hapa hapa kambini ili nitapohitaji kuongea na wewe, nikuite" Yule bwana aliongea kisha akapiga simu katika namba anayoijua yeye na kumtaka yule anaongea nae aende ofisini, kisha akakata simu.

Baada ya sekunde kadhaa aliingia mwanajeshi na kusimama kikakamavu,

"Mpeleke huyu akapumzike" Yule bwana alimwambia mwanajeshi aliyeingia,

"Upande gani" Yule mwanajeshi aliyeingia akauliza,

"Kwa wenye Matatizo ya kupumua au kwa wagonjwa wa mapafu na kifua" Yule bwana alijibu na kisha akamshuhudia yule mwanajeshi akimuongoza Sajenti Minja kwenda nje ya ofisi.

Yule bwana akatoa tabasamu huku akitingisha kichwa kwa masikitiko.

Huyu mchungaji ambaye Kayoza atamtembelea anaitwa Batoromeo

mathayo wingo, jina maarufu

lililozoeleka na wahumini wake ni

Mchungaji Wingo, tokea ahamie pale

kanisani ana muda wa mwaka mmoja

na nusu, na watu wanaodaiwa kuwa

wachawi, wameshadondoka kwenye

eneo la makazi yake zaidi ya mara

nne, hii ilimjengea imani sana kwa wahumini wake na pia alijikuta waumini wengine kutoka makanisa mengine wakifurika katika kanisa lake kila siku ambayo alifanya maombi kwa ajili ya wagonjwa na walemavu.

Ndani ya muda mfupi Mchungaji Wingo aliweza kupata jina na heshima kubwa mkoani shinyanga.

Kesho yake ilipofika, mama Kayoza na Kayoza

pamoja na Omari wakaongozana

usiku ule mpaka kwa mchungaji

Wingo, Walipofika, mchungaji na

familia yake, wakawakaribisha ndani,

na baada ya maongezi ya muda mrefu, mchungaji aliwaambia kuwa,

mama kayoza na Omari warudi

nyumbani, ila Kayoza abakie, kwa

sababu anataka akeshe nae huku wakimfanyia maombi na familia

yake, mama kayoza na Omari wakajiondokea zao, wakamuacha

kayoza kwa mchungaji…

KAMA MCHUNGAJI ANGEJUA KITAKACHOMTOKEA, ASINGEKUBALI

KUBAKIA NA KAYOZA…

Baada ya mama kayoza kuondoka, Mchungaji alielekea katika chumba kimojawapo ndani ya nyumba yake na kukaa kwa muda wa dakika chache kisha akarejea tena mahali alipomuacha Kayoza,

"we ni mkristo wa dhehebu gani?" Mchungaji wingo alimuuliza Kayoza baada ya kukaa.

"ni mromani, romani catholic" Kayoza

alijibu huku akijaribu kutabasamu.

"ok, je unaamini katika

ulokole?" Mchungaji Wingo akarusha swali

jingine.

"mi naamini katika dini

yeyote na dhehebu lolote ambalo linafuata matakwa na njia za

Mungu" Kayoza akajibu,

"Umeshawahi kukaa peke yako hata siku moja na kufanya maombi?" Mchungaji Wingo alimuuliza Kayoza huku akimuangalia kwa umakini,

"Hapana" Kayoza alijibu,

"Na kanisani uwa unaenda?" Mchungaji Wingo aliendelea kumuuliza Kayoza,

"Hapana" Kayoza akajibu,

"Sasa unaamini vipi katika dini zinafuata matakwa ya Mungu aliye hai ungali wewe hufuati njia za Mungu?" Mchungaji alimuuliza Kayoza,

"Kuna kipindi uwa Nataka sana kwenda kanisani, ila uwa najikuta napata uvivu mkubwa sana" Kayoza alitoa jibu lililomfanya Mchungaji Wingo atabasamu,

"Wewe unafikiri ni kitu kinapelekea upate uvivu siku ya kwenda kanisani?" Mchungaji Wingo aliuliza tena,

"Mwanzo nilikuwa sijui, ila kwa hizi habari alizonieleza mama, nafikiri ni mzimu ndio ulikuwa unaniletea hali hiyo" Kayoza alijibu na kufanya mchungaji atabasamu tena,

"Mbona mama yako alikuwa anaenda kanisani akiwa chini ya huo mzimu?" Mchungaji Wingo aliuliza,

"Hivi mchungaji unadhani nyumba ya jirani yako unaweza kuitawala kama unavyoitawala nyumba yako?" Kayoza alitoa swali lililomfanya Mchungaji Wingo ashtuke kidogo,

"Unamaanisha nini kusema hivyo?" Mchungaji Wingo aliuliza,

"Mzimu kanifanya mimi kuwa nyumba yake, sasa anaweza kunikontroo atakavyo yeye, kwa hiyo mamlaka anayoweka juu yangu ni lazima yawe yana nguvu kuliko anayoweka juu ya mama yangu" Kayoza alimjibu Mchungaji Wingo,

"Jibu lako zuri sana, ila lina kasoro, hakuna kiumbe kitakachoweza kukutawala hapa duniani kama utamuamini Mungu" Mchungaji Wingo aliongea huku anaangalia mazingira ya sebuleni kwake,

"Kwa maana hiyo mimi simuamini Mungu?" Kayoza aliuliza,

"Hiyo ni Imani iliyopo moyoni kwako, kwa hiyo hilo swali jiulize wewe" Mchungaji Wingo aliongea huku akitabasamu,

"Kwani Mchungaji imani ipo kwenye nyumba za ibada tu?" Kayoza aliuliza,

"Hilo swali nitakujibu siku nyingine. Nikuletee maji ya baridi au ya moto?" Mchungaji Wingo alimuuliza Kayoza huku akitabasamu,

"ila mchungaji mimi sijaomba maji na wala sina kiu" Kayoza alijibu huku akionekana kumshangaa Mchungaji Wingo,

"Sijamaanisha una kiu, na sio kila unachopewa, kuna vitu unapewa bila hata kuomba" Mchungaji Wingo aliongea huku akiondoka na kumuacha Kayoza akimuangalia huku akitabasamu kutokana na maneno ya Mchungaji Wingo.

Sajenti Minja alitolewa moja kwa moja kutoka katika ofisi za mkuu wake wa jeshi na kuanza kupelekwa katika nyumba moja nzuri ambayo ilionesha haikuwa inakaliwa na mtu au anaekaa pale atakuwa hayupo au ni watu ambao hawapendi kelele, uzuri mwingine ni kwamba ile kambi ni ngeni machoni kwa Sajenti Minja ila si ngeni masikioni mwake kwa maana alishapata habari za kambi hii kutoka kwa wenzake wachache aliokutana nao mafunzoni.

Waliendelea kuisogelea ile nyumba huku kila mmoja akiwa kimya na uzuri wa ile nyumba kwa nje, tayari Sajenti Minja kichwani kwake alishatengeneza fikra za kule ndani ya nyumba kutakuwaje. Aliwaza kutakuwa na kitanda kikubwa, jakuzi, upepo mzuri wa Air condition na kila aina ya chumba kizuri ambacho mwanajeshi kama yeye anastahili kupumzika.

"Mheshimiwa vua viatu" Mwanajeshi aliyeongozana na Sajenti Minja aliongea na kumfanya Sajenti Minja atoke kwenye dimbwi la mawazo,

"Alaah! Kumbe tumefika?" Sajenti Minja aliuliza huku akitabasamu lakini yule Mwanajeshi hakushughulika kumjibu na badala yake alibonyeza namba zilizopo kwenye mlango na mlango ukafunguka, hapo ndipo alipokuta wanajeshi wengine wawili wakiwa mlangoni wakiwasubiri,

"Huyu wa wapi?" Mwanajeshi mmoja kati ya wale wawili aliuliza,

"Mgonjwa wa kifua" Mwanajeshi aliyeongozana na Sajenti Minja alijibu na kufanya Sajenti Minja ajikohoreshe kidogo,

"Kumbe kweli unaumwa? Twende ukapate matibabu upumzike" Mwanajeshi yule mwenye herufi zilizoandikwa MP aliongea na kumfanya mwenzake atabasamu na wakati huo huo yule Mwanajeshi aliyemleta Sajenti Minja aliishia mlangoni na kurudi alipotoka.

Wale wanajeshi wakiwa na Sajenti Minja walivipita vyumba kadhaa na mwisho waliingia katika chumba kimoja kilichoandikwa "BREATH",

"Ebu ruka ruka kichura chura kidogo ili mwili upate joto" MP mmoja alimwambia Sajenti Minja,

"Ni moja ya matibabu au?" Sajenti Minja aliuliza kwa mshangao,

"Ruka bwana, dawa unazotakiwa kunywa zinahitaji joto kubwa la mwili" Yule MP aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja.

Sajenti Minja akaanza kuruka kichura chura kwa kasi huku akicheka na kubadilisha mitindo mbalimbali ya kuruka kichura chura.

Baada ya dakika mbili jasho lilianza kumtoka, akaamua asimame,

"Nadhani hapa nipo poa, mwili umeshachemka huu" Sajenti Minja aliongea huku akitabasamu, lakini alikuwa amekosea sana, alishtukia akipigwa kofi zito sana la shingo,

"Endelea kuruka, nani kakupa ruhusu ya kusimama?" MP mmoja aliongea kwa ukali huku akiwa amemkunjia uso Sajenti Minja,

"Kwani ni adhabu hii?, sio lazima niruke" Sajenti Minja nae aliongea kwa ukali huku akiwa amepaniki,

"Tutajua kama ni adhabu au sio adhabu" MP mwingine aliongea na kumpiga ngumi Sajenti Minja iliyompata vizuri usoni. Sajenti Minja alivyoona hivyo akaona imeshakuwa hatari, akaanza kupambana na wale MP, alipambana nao vizuri na akawadhibiti, maana alitoa kichapo cha hatari mpaka wale MP wakawa wanaogopa kumsogelea.

Sajenti Minja akiwa bado anajiamini kwa kichapo alichotoa, alianza kuondoka kibabe, ila hata kabla hajapiga hatua mbili alitokea mwanajeshi mwingine akiwa na bastola,

"Ukileta fujo nakufumua miguu, lala chini na uweke mikono juu" Mwanajeshi aliongea huku akiwa hatanii,

"Kwani kuna tatizo gani, mbona siwaelewi?" Sajenti Minja aliuliza,

"Lala chini ndio uhoji" Mwanajeshi aliongea kwa sauti kubwa na kumfanya Sajenti Minja akubaliane nae, akalala chini na wale MP waliokula kichapo wakamwendea na kumfunga pingu kwa nyuma, kisha wakambeba juu juu mpaka katika chumba kingine na kumuweka juu ya kiti cha chuma na kumfunga na kamba, kisha wakaanza kumpiga kwa hasira walimchakaza haswa.

Baada ya kuridhika na kipigo walichokitoa, ndipo alipoingia yule bwana mkuu wa jeshi aloyekuwa anamuhoji mwanzo kule ofisini, MP wakampigia saluti na kumsogezea kiti kwa kukiweka mbele ya kiti alichokalia Sajenti Minja,

"Umelijua kosa lako?" Yule bwana alimuuliza Sajenti Minja huku akimuangalia kwa huruma, lakini Sajenti Minja hakuweza kujibu kitu,

"Ulichofanya wewe ni kudhalilisha jeshi. Huwezi kuacha kazi kwa kuogopa kitu kwa sura wala muonekano. Ni bora ungeomba muda wa kujipanga tungekuelewa. Alafu ulipoamua kuacha kazi ukaamua utumie na kigezo cha kuumwa, hilo ni kosa pia, unadanganya wakati uliahidi kusimamia ukweli" Yule bwana mkuu wa jeshi aliongea kwa sauti ya upole ila iliyosikika vyema masikioni kwa Sajenti Minja.

Kisha yule bwana akasimama huku akimuangalia Sajenti Minja,

"Mpelekeni sehemu tulivu apoze maumivu" Yule bwana aliongea na kuanza kuondoka huku akiwa haonekani kama ni mtu mwenye kupenda kucheka.

Yule bwana alitembea mpaka alipofika mlango wa kutokea nje ya lile jengo, ndipo aliposikia sauti kubwa ya Sajenti Minja ikipiga kelele kutokana na maumivu aliyokuwa anayapata muda huo,

"Siku zote mwanajeshi mpumbavu utulivu anaostahili ni huo unaoambatana na maumivu" Yule bwana mkubwa aliongea huku akitabasamu na wakati huo huo alikuwa anatoka nje ya lile jengo lililokuwa tulivu kwa nje, ila kwa ndani si sehemu salama kwa wanajeshi wenye makosa.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)