KIJIJINI KWA BIBI (4)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA NNE
TULIPOISHIA...
Walipofika eneo la chuo wakaingia kwenye chumba chao, Denis na Omari wakaingia kuoga,

Kayoza akajitupa kitandani ila sio kwamba alitaka kulala, hapana, mawazo ndio yaliutawala ubongo wake muda wote.

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Ilipofika mida ya saa 10 jioni, habari zikaenea

chuo chote kuwa kuna wanafunzi

wawili wa kike wamekutwa wamekufa

Katika nyumba ya kulala wageni, kwa denis na Omari hiyo habari kwao

haikuwa ngeni ila hofu waliyokuwa nayo mwanzo sasa iliwazidia kupita kiasi.

Usiku wa siku hiyo, Kayoza hakulala kabisa kila dakika

alikua anazunguka chumbani tu huku tukio la kumuua Tausi likimrudia kichwani mara kwa mara pamoja na sura ya Stellah, wakina Omary pia hawakulala ni

kutokana na uoga, walikua

wanaogopa kulala wakijua kuwa

kayoza anaweza kuwaua pia.

Kesho yake asubuhi wanafunzi

wakatangaziwa waende wakaage miili

ya wenzao, na utaratibu mzima

utakuwa katika hospitali kuu ya mkoa

wa dodoma inayoitwa jenero hospital(general).

"Jamani mimi nitaenda kuaga pia, maana ni watu ninaowafahamu" Omary aliwaambia wenzake baada ya kupata ratiba kamili ya kuiaga miili ya Tausi na Stellah,

"Kayoza na sisi itabidi tuende, haina haja ya kuogopa kitu ambacho hatujahisiwa nacho" Denis alimshawishi Kayoza,

"Hapana, nyie nendeni tu, mimi siendi" Kayoza aliwaambia wenzake,

"Ilo futa kichwani kwako, watu wote wanajua ulishawahi kuwa na uhusiano na Stellah, sasa usipoenda watu watakuchuliaje?" Denis alimwambia Kayoza,

"Hivi nyie hamuoni hatari iliyo mbele yetu?" Kayoza aliuliza huku akisikitika,

" hakuna hatari yoyote kwa sababu hakuna atayejua ni nani amewaua wakina Stellah" Denis alizidi kumueleza Kayoza,

"Na pia usipoenda haitakuwa picha nzuri kwa watu wanakufahamu" Omary alichangia na mwisho Kayoza alikubali kuambatana na wenzie ifikapo saa kumi jioni.

SAA KUMI JIONI

_______.

Wanafunzi wengi walijitokeza eneo la hospitali, pia Kayoza na

wenzake walifika kuaga miili ya wenzao. Eneo lote lilitawaliwa na vilio vya wasichana wa chuo pamoja na walimu wao wachache walioguswa na vile vifo.

Baada ya wahudumu kukaa mda mrefu bila

kuona wakina stellah wakitoka, walipata wasiwasi kidogo na waliitana wenyewe kwa wenyewe na kuulizana bila kupata jibu la uhakika, na mwisho walipanga kwenda kuwaogongea, ila

walitaka kutumia njia ya kutaka kufanya usafi ndio iwe kigezo, wakanteua mwenzao mmoja akawagongee mlango.

Mhudumu alipofika mlangoni akagonga,

hakusikia jibu, akagonga tena kwa nguvu kidogo pia hakusikia jibu,

akarudi nyuma kidogo alafu akachungulia korido, hakuona mtu,

akaenda upande wa vyoo na bafu pia

hakuna mtu, akakata shauri ya kurudi kufungua mlango ambao ndani alikuwepo Stellah na Tausi, akanyonga

kitasa akazama ndani, akakuta hamna mtu,

"khaa! wametutapeli!" Mhudumu akashangaa moyoni mwake huku akiwa amejishika kiuno, wakati akiendelea kuwaza na kuwazua, mbele akaona suruali ya

kike iko chini pamoja na pochi, ndio akapata faraja kidogo,

"Hodi wadada" Mhudumu aligonga hodi ilihali ameshaingia ndani, lengo lake alitaka kujua wakina Stellah wapo upande gani, alijaribu kuita tena na tena bila mafanikio,

"Ebu Ngoja niwaokotee pochi yao" Mhudumu aliongea huku akiinama chini kuokota pochi, wakati anaokota ndio

akaona mkono wa mtu chini ya

kitanda, akashtuka, akasimama

akalinyanyua godoro kidogo, alichokiona kilipekea kupiga kelele

hadi akapoteza fahamu.

Alipopata fahamu alijikuta yupo hospital huku pembeni yake yuko polisi,

"habari

yako dada, unajisikiaje?" Polisi alimsalimia yule

mhudumu,

"nzuri" Mhudumu akajibu huku akishangaa mazingira yaliyomzunguka,

"unajisikiaje sasa, una nguvu

kidogo?" Polisi aliendelea kuuliza.

"najiskia vizuri" Mhudumu alijibu,

Polisi akatoa simu akapiga, baada ya

dakika mbili, akaja daktari na askari

mwingne, daktari akamuuliza

maswali mawili matatu mhudumu

kuhusu hali yake, kisha akampima

pima, alafu akamruhusu.

Akapelekwa kituoni kwa ajili ya mahojiano. Pale kituoni walimkuta askari mmoja kijana mdogo mdogo, mweupe ila alikuwa amevaa nguo za kiraia, kilichomtambulisa kuwa ni Askari ni saluti kadhaa alizokuwa anapewa na askari wengine. huyu polisi kijana jina lake ni Joel Minja, ila jina ambalo hutumiwa na wengi kumuita ni Sajenti Minja.

"Mkuu, binti mwenyewe ni huyu hapa" Askari aliyeongozana na Mhudumu wa bar alimuongelesha Sajenti Minja,

"Oooh vizuri, mpeleke kule katika chumba cha mahojiano, mimi nakuja" Sajenti Minja aliongea huku akimuangalia yule Mhudumu, kisha akaelekea nje ambapo alienda mpaka katika moja iliyokuwa imeegeshwa hapo nje na kuchukua simu, kisha akaelekea katika chumba cha mahojiano na kumkuta yule dada Mhudumu akiwa amekaa anamsubili.

"unaitwa nani mrembo?" sajenti joel Minja alimuuliza mhudumu.

"Sania" Mhudumu ndivyo alivyojibu,

"huna baba au ubini?

Jitambulishe majina yako yote matatu" Sajenti Minja akatia msisitizo,

"Sania Juma Baruti" Mhudumu akajibu,

"unakumbuka tukio lililosababisha

ukapelekwa hospitali?" Sajent Minja

akauliza tena.

Mhudumu akaelezea

mwanzo hadi mwisho.

"je unawakumbuka vijana waliongia

na hao mabinti?" Sajenti Minja akauliza,

"nikiwaona nitawajua" Mhudumu

akajibu kwa ufasaha kabisa. Baada ya mahojiano yule Mhudumu alipelekwa selo kwa ajili ya usalama wake.

Kesho yake mishale ya saa kumi jioni, Sajenti Minja akiwa na Askari wengine, wakamchukua Mhudumu na kwenda nae hospitali ili

akahakishe kama wale maiti ni wateja aliowapokea au sio wao

Baada ya wakina Kayoza kutoka kuaga

maiti, Omari akaaga anaenda msalani

kukojoa na kuwaacha kayoza na Denis wakitangulia kutoka na kwenda nje ya eneo la hospitali.

Omari alipotoka msalani akawa anaelekea nje kuwafuata wenzake, ndipo mbele yake akawaona Askari wapatao watano wakiwa wanaelekea upande aliopo huku wameongozana na msichana ambae hakuweza kumtambua kutokana na umbali ulikuwa kati yao, ila kadri walivyozidi kusogeleana ndipo sura ya yule msichana ilivyozidi kumjia, zilipofika hatua mbili kabla hawajapishana ndipo Omary alipopata mshtuko baada ya kugundua kuwa yule msichana ni Mhudumu wa ile bar ambayo Kayoza alifanya mauaji.

Omary aliuficha mshtuko wake ila sasa yule Mhudumu akawa anamuangalia sana Omary, Omary akatamani hata apotee ghafla kama upepo ila ilishindikana na akaamua aendelee tú kwenda mbele kiume.

Wale Askari na mhudumu walipomfikia Omary wakampita na kufanya Omary ashukuru Mungu baada ya kupishana nao.

Yule Mhudumu alipompita Omary, alihisi hiyo sura siyo ngeni kwake, alitembea hatua mbili kisha akasimama, ikabidi Askari wote nao wasimame, kisha Mhudumu akageuka na kumtupia jicho Omary ambaye nae aliwageukia na sura yake ikaonekana vizuri na Mhudumu na kumfanya Mhudumu atoe mguno wa mshtuko..

Omari akaona akijifanya kukimbia atakuwa amejikamatisha, akajifanya hana habari nao na kuendelea kutembea kuelekea nje, tena ukizingatia wale polisi walivaa kiraia basi hata wasiwasi kwa Omary haukuwa mkubwa.

Mhudumu akiwa na

hakika asilimia 95 kwa kile anachokiamini, aliendelea kumuangalia Omary aliyekuwa anatembea na kuzidi kuwaacha,

"Wewe dada vipi?" Sajenti Minja aliuliza huku akimuangalia Mhudumu,

"yule ni mmoja kati ya

watu waliongia guest kwetu na wale wasichana waliokufa" Mhudumu alijibu huku akimuelekezea kidole Omary, Polisi bila

kupoteza muda wakamuita Omary aliyekuwa tayari yuko mbali nao, ila sijui ni kutokana na uoga au kujiamini, Omary alijikuta akirudi mpaka Pale alipo yule Dada Mhudumu na Askari,

"mambo vipi kaka", sajenti minja

akamsalimia omari,

"poa", omari

akajibu huku wasiwasi ukianza kuchukua nafasi,

"sisi ni askari, je unamjua huyu

binti?" Sajenti Minja alijitambulisha na kisha akauliza swali huku akinyooshea kidole

mhudumu.

kiukweli Omary alishtuka

ila hakutaka kuunyesha mshtuko wake, ila tayari askari walishaligundua hilo kitambo.

"simjui, kwani vipi?" Omary akajibu kwa pupa,

"Dada unamjua huyu?" Sajenti Minja alimuuliza Dada Mhudumu huku akimuangalia Omary,

"Ndiyo namjua" Dada Mhudumu alijibu na kumfanya Omary ahisi tumbo likimvuruga,

"Unamjua kama nani?" Sajenti Minja alimuuliza tena,

"Huyu ni mmoja kati ya wale vijana waliokodi chumba na wale wasichana wa chuo waliouwawa" Dada Mhudumu alijibu,

"Wewe dada utakuwa sio mzima wewe" Omary alijikuta anaongea huku amemtolea macho yule dada Mhudumu,

"mkamateni mumfunge pingu, atajieleza zaidi

kituoni" Sajenti Minja akatoa amri.

Omari ujanja mfukoni, akachukuliwa

mpaka kwenye land cruiser ya polisi iliyokuwa imeegeshwa nje.

Ile gari ya polisi ikatoka

eneo la hospital kwa spidi ya ajabu utasema imempakia jambazi sugu.

Baada ya shughuli ya kuaga miili kuisha, uongozi wa chuo

ukatoa risala fupi kuhusu marehemu

na shukrani kwa wanafunzi waliofika

kuaga wenzao, pia uongozi wa chuo

ukachukua mda huo kuwatangazia

wanafunzi likizo ya mwisho wa

semister.

Kayoza na Denis baada ya

kutawanyika eneo lile, wakaenda moja kwa moja nje

ya hospitali.

"mchizi kaenda kukojoa

kamba nini? Mkojo gani nusu saa?" Denis aliuliza huku akiangalia saa yake ya mkononi,

"simu yangu haina

kitu, kama una salio muendee

hewani" kayoza alimueleza mwenzake.

Denis akachukua simu yake akapiga namba ya Omary, lakini

simu iliita muda mrefu bila kupokelewa, akarudia tena na tena lakini hali ilikua ile ile.

"mpotezee, si unajua leo siku ya kufunga shule,

labda yuko na demu" Kayoza akasema.

"poa, nini kinafuata sasa?" Denis akauliza,

"twende chuo tukachukue mabegi, leo tulale mjini" Kayoza akatoa

maoni yake,

"haina mbaya, ni wazo zuri" Denis

alijibu kwa kumuunga mkono mwenzake na kisha wakaenda kutafuta usafiri uliowafikisha chuo.

Walipofika chuo baada ya

kuoga na kujitayarisha kuondoka, Denis akarudia tena kupiga simu ya

Omari, safari hii alipiga mara moja tu na simu ikapokolewa

"wewe dogo vipi

napiga simu muda mrefu haupokei, uko

wapi?" Denis akaongea kwa pupa,

"samahani mwenye simu yuko Polisi, hapa ni kituo kikuu cha Polisi dodoma

mjini" upande wa pili ukajibu,

"Polisi?, amefanya nini tena?" Denis

akauliza,

"wewe ni nani yake kwani?" ule upande wa pili badala ya kujibu, wakaongeza swali.

Denis kichwa kikafanya kazi haraka, akahisi akijibu hovyo hovyo bila kufikiria, anaweza akajiingiza matatizoni,

"mimi ni kaka yake" Denis alijibu,

"Sawa, mdogo wako anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kuua wasichana wawili akishirikiana na wenzake ambao nao bado wanatafutwa"

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)