KIJIJINI KWA BIBI (5)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA TANO
TULIPOISHIA...
"mimi ni kaka yake" Denis alijibu,

"Sawa, mdogo wako anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kuua wasichana wawili akishirikiana na wenzake ambao nao bado wanatafutwa"

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"Sawa, nipe dakika kumi nitakuja hapo" Denis

akamalizia kisha akakata simu na kuanza kupumua kwa nguvu,

"kaka kumeshaharibika, beba mabegi tuondoke" Denis alimwambia kayoza,

"Sikuelewi, ebu nyoosha maelezo" Kayoza aliongea huku akimuangalia kwa makini Denis,

"Omary amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za mauaji ya pale guest" Denis alimjibu Kayoza,

"Mimi si niliwaambia hapa sio pa kukaa tena?" Kayoza aliuliza huku hiyo habari ikionekana kumgusa,

"Hakuna muda wa kubishana hapa" Denis aliongea kwa ukali kisha wakabeba mabegi yao haraka, safari ya

kwenda mjini ikaanza.

Omari baada ya kuchukuliwa na

polisi, alifkishwa kituoni kwa ajili ya mahojiano hawali.

"unaitwa Omary Said

Mkwiju, si ndio hivyo?" Sajenti Minja alikuwa anamuuliza Omary huku

kashuka kitambulisho cha Omary,

"ndio" Omary akajibu.

"sisi hatuna ubaya na wewe, ila ukweli wako ndiyo

utaokusaidia" Sajenti Minja alianza kwa mtindo huo, kisha akaendelea,

"mlikua watatu,

wenzako wako wapi mlioshirikiana

nao katika mauaji?"

"jaman mimi sijaua,

huyu dada kanifananisha" Omary alijitetea huku macho yakiwa makavu,

"mchukueni mmuweke

ndani, naona hayuko tayari kutoa ushirikiano" Sajenti Minja alitoa amri.

Omary akabebwa juu juu akapelekwa

Selo ingawa aliendelea kulalamika anaonewa kwani yeye hajui chochote kuhusu vifo vya hao wasichana.

"Kwanini asipelekwe magereza kabisa" Askari mmoja aliuliza,

"Muacheni huku kwanza, nitamrudia usiku" Sajenti Minja alijibu huku akichukua koti lake la suti alilokuwa amelitundika ukutani, na kisha aliondoka.

Usiku Sajenti Minja alirudi

tena, akaongea na askari wa zamu, kisha Omary akatolewa nje, akavuliwa

nguo zote, kisha akaanza kuhojiwa tena, ila bado alikua mbishi,

wakaitwa watu wanne waliokuwa wameshiba

haswa, ni mijibaba ya miraba minne,

wakaamrishwa wamchape.

walimchapa haswa. Hadi akalainika, akawataja wenzake. Mda huo huo wa usiku Sajenti Minja akamfundisha

Omari jinsi ya kuongea na simu, kisha akawapgia wakina wakina

kayoza.

"oya mko wapi wana?" Omary alianza kuongea

hivyo,

"vipi, wewe si uko polisi?" Kayoza

aliuliza huku akishangaa mwenyewe,

"ni habari ndefu ila

wameniachia, wamedai

wamenifananisha, wamenipa hela

kwa ajili usumbufu" Omary alijibu huku akishusha pumzi ndefu,

"ehe siku hizi polisi wanatoa hela!?, aya

upo wapi?" Kayoza aliuliza,

"Mi niko guest moja hivi karibu na Railway,

nimeona giza limeshaingia nikaona bora nipumzike tu kwa maana polisi wamenisumbua sana. Nyie mko

wapi?" Omari aliuliza,

"tupe ramani tukufuate hapo ulipo kwa maana hata mabegi yako ya nguo tumekubebea" Kayoza alimwambia Omary,

"Chukuenu bajaji, mwambieni awapeleke kilimani lodge, mtanikuta hapo" Omary aliongea huku Sajenti Minja akiwa pembeni akimfundisha maneno ya kuongea na kisha akakata simu.

Baada ya mtego wa Sajenti Minja kukamilika na kufanikiwa kwa

asilimia nyingi, akachukua taxi, kwa maana aliogopa kwenda na gari ya polisi kwa kuwa endapo wakina kayoza wataiona kipindi wamawasili, basi wanaweza kukimbia.

Sajenti Minja alichukua taxi na askari watatu wenye bunduki, wakafunga safari hadi eneo walilopanga kukutana na wakina Kayoza, akachukua chumba,

kisha wakamuingza omari na askari wote watatu wakaingia chumbani kwa ajili ya kuwakamata wakina Kayoza pindi watakapofika, kisha Sajenti Minja yeye alirudi

nje kakaa ndani ya ile taxi na Dereva, huku akifuatilia kila kinachoendelea nje.

Wakina kayoza walipofika Kilimani lodge, wakampigia simu Omary,

"Tumefika, tupo nje hapa" Denis aliongea baada ya Omary kupokea simu,

"njoon chumba namba

7" Omary akawaambia wenzake ambao walimlipa dereva wa bajaji pesa waliyokubaliana nae, kisha wakabeba mabegi yao na kuelekea ndani.

Sajenti Minja hakuwa na wasiwasi na vijana wake,

aliona jinsi wakina Kayoza wanavyopiga simu na aliwasikia pia wanachoongea na Omary,

ila hakua na pupa, aliamini wakina Kayoza wanaenda kukamatwa na vijana wake aliowaweka chumbani pamoja na Omary, kwa hiyo akaacha vijana wake wafanye kazi.

Denis na Kayoza

walipofika mlango namba 7, wakagonga mlango, na Omary akafungua,

"Karibuni ndani, ingieni" Omary aliongea huku akiwa amechangamka na wakina Kayoza wakaingia ndani bila kujua katika hicho chumba walichoingia,wapo Askari watatu wenye bunduki wakiwasubiri wao…..

wakakaribishwa na mdomo wa

bunduki,

"mko chini ya ulinzi" Polisi

mwenye bunduki aliwaambia. Ghafla

bin vuu, kayoza alimrukia yule askari

mwenye bunduki, akatua shingoni

mwake, ila hakumnyonya damu, badala yake yule Askari alipokea kofi zito na kuanguka chini huku bunduki yake ikidondokea chini ya kitanda.

Yaani hapo Kayoza alikuwa tayari kishabadilika,

macho yamekua meupe, meno yamechomoza.

Askari wa pili kuona

vile, nae akaokota bunduki,

akamfyatulia Kayoza risasi, Kayoza

akamuacha Askari wa kwanza, akamrukia wa

pili nae akamtandika kofi lilimfanya apoteze fahamu, yule

askari wa tatu kuona vile akakimbilia

mlangoni, Omari akachukua bunduki,

akampiga risasi ya mgongoni na akadondoka

pale pale.

Kayoza akiwa katika hali ile ile, akaenda dirishani akavunja nondo za madirisha, alikuwa na nguvu kama mnyama na alikuwa akiunguruma kama Simba.

Alipomaliza kuvunja zile nondo za madirisha, akawarudia wale Askari ambao wawili walikuwa hawana fahamu na mmoja alikuwa anaugulia maumivu baada ya kupigwa risasi ya mgongoni.

Akasukumia wale majeruhi chini ya

kitanda kisha akawaangalia wenzake ambao walikuwa wamekaa kwenye kona moja Pale chumbani huku wakiwa na hofu kutokana na muonekano wa Kayoza, kwa maana hawajawahi kumuona hivyo kabla.

Kayoza akarudisha macho dirishani na kisha akatokea dirishani, wenzake wakabaki wanaangalia,

"Bab umeiona hiyo?" Omary alimuuliza Denis,

"Ebu tutoke kwanza hapa, hayo tutayajadili baadae" Denis alijibu kwa upole,

"Poa twende basi" Omary aliongea huku akianza kuondoka kuelekea mlangoni,

"Usipitie uko wewe" Denis alimwambia mwenzie,

"Sasa na sisi tupitie dirishani?" Omary aliuliza,

"Hiyo ndio njia sahihi kwetu, maana nahisi Polisi wengine watakuwa nje" Denis aliongea,

"Sio unahisi, ni kweli kuna Polisi nje" Omary aliongea baada ya kukumbuka kuwa Sajenti Minja alibaki nje. Wakatoka nje wote kwa kupitia dirishani huku wakibeba mabegi yao na begi la Kayoza.

Nje, Sajenti Minja baada ya kusubiri muda mrefu

bila majibu, akapata wasiwasi, mara

akasikia mlio wa bunduki,

akakurupuka kwa kasi hadi mlango mkuu wa kuingilia ile guest, alipata

shida kuingia, kutokana na wingi wa

wapangaji ambao walikua wanatoka

huku wanakimbia baada ya wao kusikia pia mlio wa bunduki. Mara mlio

mwingne wa bunduki ukasikika.

Sajenti Minja akafanya juhudi binafsi, mpaka

akafanikiwa kuingia, alipofika mlangoni, akausukuma mlango lakini

haukufunguka, kipindi iko

wahudumu walikuwa wanamuangalia

tu,

"nipeni ufunguo wa hapa" Sajenti Minja akawaambia wale wahudumu waliokuwa wanamtolea macho,

"mwenye funguo

kakimbilia nje" wahudumu wakamjibu,

"Sawa, mimi navunja sasa" Sajenti Minja aliongea huku akionekana ana hasira,

"huwez kuvunja bila meneja wetu

kuwepo" Wahudumu wakamjibu.

Mara kwenye mlango mkubwa wa kuingilia ile Guest wakaingia askari wanne, wote

wamebeba bunduki, nyuma yao

anaonekana askari mwingine mrefu,

mweupe ana mwili wa mazoezi, huyu

anaitwa Afande Juma Ally Mbago.

"Sajenti Minja, umefika saa ngapi huku" Afande Mbago alimuuliza

Minja aliyemkuta eneo hilo na kisha Sajenti Minja akampa mkasa

mzima hadi yeye kuwepo pale.

"kama wamesema ufunguo hawana vunjeni

mlango" Afande Mbago aliwaamuru vijana wake.

Vijana wakavunja

mlango, walipoingia tu, wakakuta

dirishani hakuna nondo,

"bwana Minja si umesema, vijana wako

walikuwepo humu pia?" Afande Mbago aliuliza,

"ndio," Sajenti Minja

akajibu,

"sasa mbona hamna mtu

humu?" Afande Mbago akauliza tena,

"hata mimi nashangaa" Minja akajibu huku akishangaa.

Askari mmoja akapanda kitandani ili aende

karibu ya dirisha, alipofika mwisho

wa kitanda, akaangalia chini

akashtuka, tena alishtuka haswa,

"kuna mtu chini ya

kitanda" Askari akalopoka huku macho yakiangalia chini ilipokuwepo miili ya wale Askari waliopoteza fahamu. Wakavuta

kitanda, wakakuta miili ya askari

watatu ambao alikuja nao Sajenti

Minja,

"Wazima kweli hawa?" Sajenti Minja aliuliza huku hali ya hofu ikimuingia kuhusu watu anawafuatilia,

"Wote wazima" Afande Mbago alijibu baada ya kuwakagua kisha wakawachukua na wakawapakia kwenye gari la

Polisi, safari ya kuwapeleka hospitali

ikaanza.

kayoza akiwa katika hali yake ya kutisha,

aliendelea kukimbia,

mbele kidogo akadondoka chini, akawa

anajigeuza geuza kama mtu anayekata roho, mara akatulia kama mtu aliyekufa.

Wenzake ambao ni Denis na Omary walikuwa pia wanakimbia huku wakiwa hawana uhakika wa kumpata mwenzao, ila wakiwa katika marathon hizo, ndipo walipomkuta Kayoza akiwa amelala chini.

"Kafa au?" Omary alimuuliza mwenzake huku kila mmoja akiwa na uoga wa kumsogelea Kayoza kutokana na hali waliyoiona Pale lodge,

"Sijui" Denis alijibu. Baada ya muda wa mrefu wa sintofahamu kati yao, mwisho walijitoa mhanga na kuusogelea mwili wa Kayoza na kugundua kuwa amepoteza fahamu, ila baada ya muda kidogo fahamu zilimrudia na akarudi kwenye

hali yake ya kawaida, ila mwili wake haukuwa na nguvu.

Wenzake wakambeba, ila bahati nzuri wakaona taxi inakuja, wakaisimamisha, kisha wote wakaingia ndani ya ile taxi.

"tupeleke hospitali yoyote

Iliyo karibu na hapa" Omary akamwambia dereva

taxi,

"hospital kufanya nini?, we mjinga nini" Denis akaongea kwa ukali,

"polisi wamenitandika sana mgongoni, kwa hiyo nina vidonda vikubwa sana mgongoni" Omari

alimwambia Denis huku

akimuonesha hivyo vidonda,

"poa, suka twende hospital" Denis

akakubali baada ya kuviona hivyo vidonda.

Walipofika hospitali, gari

ikawa inaelekea sehemu ya maegesho, ilipofika ikasimama pembeni ya gari la polisi, wakati wanataka kushuka, Mara ghafla Sajenti Minja

akawa anatoka ndani ya hospitali na

kuelekea sehemu ya maegesho ya magari.

Akaenda mpaka ilipopaki gari ya polisi,

akawa anaongea na mwenzake

kuhusu ishu iliyopelekea wale askari

wenzake kuwa vile, na kibaya zaidi ni kwamba alimwambia mwenzake kuwa wale Askari wote wameshakufa, tena aliongea kwa hasira mpaka machozi yakawa yanamtoka.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)