KIJIJINI KWA BIBI (8)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA NANE
TULIPOISHIA...
Baada ya Sajenti Minja kuondoka eneo la tukio,

ilichukua mda kama wa dakika tano

kayoza kupata fahamu.

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
Alishtuka akamkuta Omary yuko pembeni yake,

"mapolisi wameenda wapi?" Kayoza ndio

lilikuwa swali lake la kwanza kumuuliza

Omary,

"umewaua" Omary akajibu na kumfanya Kayoza ashangae,

"Mimi nimewaua?" Kayaza aliuliza kwa mshangao,

"Ndio, si hapo wamelala" Omary alijibu huku akiwaonyeshea kidole Askari waliikuwa wamekufa,

"na Denis nae kaenda wapi?" Kayoza akauliza

tena.

Hapo wote wakashtuka,

wakaenda kuingalia gari waliyokuwa

nayo lakini hawajamkuta, ndipo Omary akakumbuka kuwa aliporejewa na fahamu pembeni yake kulikuwa na mtu, ndipo alipohisi huyo mtu atakuwa Denis.

Wakarudi mpaka eneo la mwanzo, masikini ya mungu, walimkuta

Denis Paul Simiwe, akiwa amelala

huku damu zikiwa zimeganda kwenye

pua na midomo yake.

wote wakajikuta machozi yanawatililika mashavuni.

"Tuondoke, hili eneo sio salama" Omary alimtahadhalisha Kayoza,

Wakachukua kitambulisho cha Denis

kama kumbukumbu ya jamaa yao,

kisha wakabeba mabegi yao, wakawa

wanaelekea barabani.

walipofika barabarani

walikaa kama nusu saa, wakaiona

gari ndogo inakuja na aliyekuwa anaendesha ni mzee mmoja wa makamo.

Omary alisimama katikati ya barabara na kuipungia

mkono ile gari, ikasimama,

"shikamoo mzee"

wakamsalimia kwa pamoja,

"marhaba waheshimiwa" Mzee makamo aliwaitikia.

"mzee tunaomba

Lifti" Omary akasema katika sauti

tulivu,

"mnaelekea wapi?" Mzee wa makamo akawauliza,

"tulikuwa tunaenda

tanga, ila hata ukitufukisha eneo

lenye usafiri tutakushukuru" Omary akajibu,

"vizuri, hata mi naelekea

Tanga, mbona mko katika hali hiyo?"

yule Mzee wa makamo akauliza baada ya kuwaona wana damu katika baadhi ya sehemu mwilini,

"tumepata

ajali"Omary akajibu huku akijifuta damu shavuni,

"poleni sana,

ingieni twendeni" Mzee

akaongea.

Wakaingia, safari ikawa

inaendelea, mwendo kama wa nusu

saa hivi, yule mzee kupitia kioo cha

juu mbele, alishuudia kitu,

kinachoendelea kwenye siti ya

nyuma, ambayo walikaa wakina

kayoza, akapata mshtuko,

akapunguza mwendo wa gari, kisha akageuka ili kuhakikisha kama ni kweli au kioo kinamdanganya?..

"mbona unalia kijana?" yule mzee alimuuliza

kayoza,

"ni maumivu tu, mzee

wangu" Kayoza akadanganya huku akijifuta machozi, ila

kilichokuwa kinamliza, ni mambo ya ajabu ambayo yanayomtokea, na kikubwa

haswa ni kumpoteza rafiki yake,

denis. Mzee akairudisha gari barabarani baada ya kuridhika na majibu ya Kayoza.

Gari ikaenda hadi morogoro

mjini, yule mzee akaipaki gari nje ya

hoteli moja maarufu pale Morogoro.

"twendeni tukale waheshimiwa" Yule mzee

aliwaambia wakina Kayoza huku

akiuchomoa ufunguo wa gari kutoka

mahali pake, wakina kayoza

wakashuka, huku kila mmoja akiwa

kabeba suruali na fulana ili wakazivae mariwatoni, kwa hali

waliyokuwa nayo, watu wengi

waliwashangaa kutokana na nguo zao kuchanika na kuchafuka kutokana na ajali waliyoipata.

Wakaingia hadi ndani, kisha Omary akaomba

kuelekezwa choo kilipo,

alipoonyeshwa, wakaenda kisha

wakabadili nguo, alafu wakarudi

kujumuika na yule mzee pale

mezani.

Baada ya kumaliza kula,

wakajipakia kwenye gari, kisha safari

ikaendelea.

"mnaenda Tanga katika

eneo gani?" Mzee yule aliwauliza wakati

gari ikianza kushika kasi.

"Chumbageni" Omary akajibu huku safari ikiendelea.

Tanga mjini waliingia saa nne usiku. Yule mzee

akawashusha, wakamshukuru sana,

kisha yule mzee akaendelea na safari

zake, hakuna aliyejua yule mzee alikuwa

anaelekea wapi?, ila walichoshukuru

ni kufika salama.

"kwa muda huu

hatuwezi kupata usafiri, itabidi tutafute guest ya kulala, kesho

tutaamka na hiyo safari yachumbageni" Omary alimwambia

Kayoza hayo maneno,

"mi nakusikiliza wewe" Kayoza ndivyo

alivyomjibu. Wakatafuta nyumba ya wageni, wakaipata.

wakaweka mizigo yao,

kisha wakaenda kutafuta chakula, waliporudi wakalala.

Waliamka saa

nne za hasubui, wakaoga, kisha

wakaenda kupata chai, alafu

wakarudi kuchukua mabegi yao,

safari ya kwenda Chumbageni

ikaanza, wakaulizia sehemu

yanapopaki magari ya Chumbageni,

wakaonyeshwa, wakatafuta gari

iliyokuwa karibu kuondoka,

wakajipakia.

Sajenti Minja alifikia moja kwa moja kituo

kikuu cha polisi, akatoa ile taharifa

ya mauaji, ikatayarishwa gari,

ikambeba yeye pamoja na askari

wengine watatu, wakaondoka, huku

nyuma wakifuatiliwa kwa karibu na

gari la wahandishi wa habari,

wakaenda hadi eneo la tukio,

likapigwa picha pamoja na maiti

zote, kisha miili ya marehemu

ikawekwa ndani ya gari, safari ya

kurudishwa Dodoma mjini ikaanza,

walipofika, maiti zote zikaenda

kuifadhiwa katika monchwari ya

hospitali ya mkoa, kisha polisi

wakafanya kikao na waandishi wa

habari, kuhusu ule mlolongo wa

matukio ya kutisha, ila kwa bahati

nzuri, Sajenti Minja alikuwa na

kitambulisho cha Omari Said Mkwiji,

kwa hiyo akawapa nafasi waandishi

wa habari waipige picha, huku

Sajenti Minja akiwaambia ile picha ni

ya mmoja kati ya wale watuhumiwa

watatu wa mauaji na akaongeza

kuwa mtuhumiwa mwingine (Denis)

amekufa katika ajali iliyotokea wakati

wanakimbizana na polisi.

Kesho yake asubuhi, magazeti yote yalitoka na

habari hizo za mauaji, na pembeni

ya hizo habari kulikuwa na picha

kubwa ya Omari, akitajwa kama

mmoja wa wahusika wa mauaji ya unyonyaji damu.

Wakina kayoza walipoingia ndani ya basi, walikaa

siti ya nyuma kabisa, siti ya mbele

yao walikaa wakina mama wawili

ambao walikuwa wanazungumzia juu

ya mauaji ya kutisha yaliyotokea kati

ya Dodoma na Morogoro.

"na tena hadi picha ya muuaji imetolewa"

mama mmoja wapo. ambae alikuwa

kabeba mtoto katika miguu yake

alikuwa akimsimulia mwenzie,

"imetolewa na gazeti gani?" yule

mama mwingine wa makamo

akamuuliza yule mama mwenye

mtoto.

"magazeti yote unayoyajua

wewe wametoa hiyo habari" mama

mwenye mtoto akajibu.

"chumbageni

si hapo tu tunakaribia, nitanunua

gazeti ili na mimi nione" yule mama wa makamo

akajibu.

Kipindi chote wakati

wanaingia, hadi safari ilipoanza,

wakina Omary walikuwa

wanawasikiliza tu, ila habari

iliyowashtua ni kuchapishwa kwa

picha ya Omary kwenye magazeti.

"Bab hii ishu imeshakuwa kubwa kupita kiasi" Kayoza alimwambia mwenzake wakati wale wakina mamá wanaongea,

"Maji tumeshayavulia nguo, kuyaoga haina budi" Omary aliongea kwa sauti ndogo,

"Maisha ya kukimbia kimbia tutaishi mpaka lini sasa?" Kayoza aliuliza kwa masikitiko,

"Kila lenye mwanzo halikosi mwisho" Omary alijibu kifupi.

Walipofika karibu na

chumbageni, ile gari ikasimama kwa

dharura, kulikuwa na mushkeli katika

upande wa injini, wale wakina mama

wakanunua gazeti, wakawa wanasoma

ile habari

"mimi nikimuona, yaani

haraka nawajulisha polisi" yule

mama mwenye mtoto aliongea.

"hata mimi, mwenzangu milioni kumi

nyingi" yule mama wa makamo

akajibu baada ya kusoma habari

kuwa atayemkamata au atakayefanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa atapewa kiasi

hicho cha pesa, kipindi chote hicho wakina Kayoza walikaa tu kwenye siti za nyuma ya gari, hawakuthubutu kushuka.

Gari lilipotengemaa likaendelea na

safari. Kipindi chote Omari alikuwa

kaielekeza sura yake sanjari na

dirisha ili kukwepa sura yake isionekane na abiria wengine kwa maana alishapatwa na wasiwasi.

Gari ikafika mwisho wa safari,

watu wakaanza kutelemka, wale

wakina mama kwa ajili ya kuwa na

mtoto, ikabidi wasubiri ili watu wote watoke na wao watoke wa

mwisho, sasa wakati wakina kayoza

wanawapita, Omary akamkanyaga yule

mama mwenye mtoto kwa bahati

mbaya,

"samahani mama" Omary

akamtaka radhi yule mama huku akimwangalia

usoni, yule mama akapata mshtuko,

"ah!, si ndo

huyu?" Yule mama alisema kwa kupayuka.

"sio mimi" Omary aliongea bila kutarajia huku akijinasua kutoka kwenye mkono wa yule mwanamke, kisha wakatoka haraka ndani

ya ile gari na kukimbilia nje.

Yule mama akachukua

gazeti kutoka kwa mwenzake, kisha

akaiangalia ile picha ya Omary iliyokuwepo katika gazeti

"mh!, haswaa

ndiye yeye" Yule mama akajisemea moyoni, kisha

akatoka kwa lengo la kuwatazama

walipoelekea wakina Omari, ila

alichelewa, akakuta peupe.

akaangaza tena, hakuona mtu,

akaishia kusonya.

Baada ya wakina

kayoza kufanikiwa kushuka kwenye

gari, wakakimbilia nyuma ya ile gari,

wakawa wanamchunguza yule mama,

paka alivyotoka ndani ya gari na kuanza kuangaza

walikuwa wanamuangalia, mpaka ule

msonyo uliotolewa na yule mama pia waliusikia, wakasubiri mpaka yule mama alipoondoka, nao

ndio wakaondoka ila kwa kujificha ficha sana nyuma ya magari mengine yaliyokuwepo pale.

"Yaani tayari habari zimeshasambazwa katika vyombo vya habari?" Omary alimuuliza mwenzake wakiwa tayari wameshatoka katika kituo cha mabasi,

"Tena wamechelewa kweli, ilitakiwa watoe taharifa jana" Kayoza alijibu huku akikagua mandhari ya mji wa Tanga,

"Ebu twende pale tukasome some magazeti" Omary aliongea huku akielekea sehemu ambapo kulikuwa na magazeti yametandazwa juu ya meza,

"Acha ujinga wewe" Kayoza aliongea huku akiwa anamzuia Omary,

"Kwanini?" Omary aliuliza huku akimshangaa Kayoza,

"Unajua kuwa sisi tunatafutwa na mbaya zaidi picha yako ndiyo imeonekana kwenye magazeti, kwa hiyo wewe huoni kwenda eneo kama lile ni rahisi sana kukamatwa?" Kayoza aliuliza baada ya maelezo marefu,

"Ila kweli, basi nenda wewe kaangalie, alafu uje unijulishe" Omary alimwambia Kayoza,

"Mimi naenda, ila sio kuangalia. Naenda kununua gazeti tutaenda kusoma mbele Safari" Kayoza aliongea huku akielekea pale walipotandaza magazeti mezani. Alifika na kununua magazeti mawili ya kisiasa na jamii na kisha akarudi mahali Omary alipo na kumpa gazeti moja, nae akabaki na moja,

"Alafu ujue umenishangaza sana" Omary alimwambia Kayoza,

"Kwanini?" Kayoza aliuliza,

"Kwanini yule Askari mweupe haujamuua?" Kayoza aliuliza huku akimaanisha Sajenti Minja,

"Mimi?" kayoza aliuliza tena,

"Ndio, ni wewe" Omary alikazia swali lake,

"Sasa mimi nitajuaje wakati unajua kabisa mimi nikiwa katika hali ile uwa sijitambui?" Kayoza nae alijibu kwa mtindo wa kuuliza,

"Hicho kitu kimenishangaza sana" Omary aliongea huku akiendelea kushangaa,

"Wewe mwenyewe uwa sikudhuru na Kwanini hushangai?" Kayoza alimuuliza Omary,

"Dah, tuachane na hayo, maana tukiulizana sana hatutapata majibu ila tutaongeza maswali" Omary aliamua kupotezea huo mjadala,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)