Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA NANE
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Baada ya Sajenti Minja kuondoka eneo la tukio,
ilichukua mda kama wa dakika tano
kayoza kupata fahamu.
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
Alishtuka akamkuta Omary yuko pembeni yake,
"mapolisi wameenda wapi?" Kayoza ndio
lilikuwa swali lake la kwanza kumuuliza
Omary,
"umewaua" Omary akajibu na kumfanya Kayoza ashangae,
"Mimi nimewaua?" Kayaza aliuliza kwa mshangao,
"Ndio, si hapo wamelala" Omary alijibu huku akiwaonyeshea kidole Askari waliikuwa wamekufa,
"na Denis nae kaenda wapi?" Kayoza akauliza
tena.
Hapo wote wakashtuka,
wakaenda kuingalia gari waliyokuwa
nayo lakini hawajamkuta, ndipo Omary akakumbuka kuwa aliporejewa na fahamu pembeni yake kulikuwa na mtu, ndipo alipohisi huyo mtu atakuwa Denis.
Wakarudi mpaka eneo la mwanzo, masikini ya mungu, walimkuta
Denis Paul Simiwe, akiwa amelala
huku damu zikiwa zimeganda kwenye
pua na midomo yake.
wote wakajikuta machozi yanawatililika mashavuni.
"Tuondoke, hili eneo sio salama" Omary alimtahadhalisha Kayoza,
Wakachukua kitambulisho cha Denis
kama kumbukumbu ya jamaa yao,
kisha wakabeba mabegi yao, wakawa
wanaelekea barabani.
walipofika barabarani
walikaa kama nusu saa, wakaiona
gari ndogo inakuja na aliyekuwa anaendesha ni mzee mmoja wa makamo.
Omary alisimama katikati ya barabara na kuipungia
mkono ile gari, ikasimama,
"shikamoo mzee"
wakamsalimia kwa pamoja,
"marhaba waheshimiwa" Mzee makamo aliwaitikia.
"mzee tunaomba
Lifti" Omary akasema katika sauti
tulivu,
"mnaelekea wapi?" Mzee wa makamo akawauliza,
"tulikuwa tunaenda
tanga, ila hata ukitufukisha eneo
lenye usafiri tutakushukuru" Omary akajibu,
"vizuri, hata mi naelekea
Tanga, mbona mko katika hali hiyo?"
yule Mzee wa makamo akauliza baada ya kuwaona wana damu katika baadhi ya sehemu mwilini,
"tumepata
ajali"Omary akajibu huku akijifuta damu shavuni,
"poleni sana,
ingieni twendeni" Mzee
akaongea.
Wakaingia, safari ikawa
inaendelea, mwendo kama wa nusu
saa hivi, yule mzee kupitia kioo cha
juu mbele, alishuudia kitu,
kinachoendelea kwenye siti ya
nyuma, ambayo walikaa wakina
kayoza, akapata mshtuko,
akapunguza mwendo wa gari, kisha akageuka ili kuhakikisha kama ni kweli au kioo kinamdanganya?..
"mbona unalia kijana?" yule mzee alimuuliza
kayoza,
"ni maumivu tu, mzee
wangu" Kayoza akadanganya huku akijifuta machozi, ila
kilichokuwa kinamliza, ni mambo ya ajabu ambayo yanayomtokea, na kikubwa
haswa ni kumpoteza rafiki yake,
denis. Mzee akairudisha gari barabarani baada ya kuridhika na majibu ya Kayoza.
Gari ikaenda hadi morogoro
mjini, yule mzee akaipaki gari nje ya
hoteli moja maarufu pale Morogoro.
"twendeni tukale waheshimiwa" Yule mzee
aliwaambia wakina Kayoza huku
akiuchomoa ufunguo wa gari kutoka
mahali pake, wakina kayoza
wakashuka, huku kila mmoja akiwa
kabeba suruali na fulana ili wakazivae mariwatoni, kwa hali
waliyokuwa nayo, watu wengi
waliwashangaa kutokana na nguo zao kuchanika na kuchafuka kutokana na ajali waliyoipata.
Wakaingia hadi ndani, kisha Omary akaomba
kuelekezwa choo kilipo,
alipoonyeshwa, wakaenda kisha
wakabadili nguo, alafu wakarudi
kujumuika na yule mzee pale
mezani.
Baada ya kumaliza kula,
wakajipakia kwenye gari, kisha safari
ikaendelea.
"mnaenda Tanga katika
eneo gani?" Mzee yule aliwauliza wakati
gari ikianza kushika kasi.
"Chumbageni" Omary akajibu huku safari ikiendelea.
Tanga mjini waliingia saa nne usiku. Yule mzee
akawashusha, wakamshukuru sana,
kisha yule mzee akaendelea na safari
zake, hakuna aliyejua yule mzee alikuwa
anaelekea wapi?, ila walichoshukuru
ni kufika salama.
"kwa muda huu
hatuwezi kupata usafiri, itabidi tutafute guest ya kulala, kesho
tutaamka na hiyo safari yachumbageni" Omary alimwambia
Kayoza hayo maneno,
"mi nakusikiliza wewe" Kayoza ndivyo
alivyomjibu. Wakatafuta nyumba ya wageni, wakaipata.
wakaweka mizigo yao,
kisha wakaenda kutafuta chakula, waliporudi wakalala.
Waliamka saa
nne za hasubui, wakaoga, kisha
wakaenda kupata chai, alafu
wakarudi kuchukua mabegi yao,
safari ya kwenda Chumbageni
ikaanza, wakaulizia sehemu
yanapopaki magari ya Chumbageni,
wakaonyeshwa, wakatafuta gari
iliyokuwa karibu kuondoka,
wakajipakia.
Sajenti Minja alifikia moja kwa moja kituo
kikuu cha polisi, akatoa ile taharifa
ya mauaji, ikatayarishwa gari,
ikambeba yeye pamoja na askari
wengine watatu, wakaondoka, huku
nyuma wakifuatiliwa kwa karibu na
gari la wahandishi wa habari,
wakaenda hadi eneo la tukio,
likapigwa picha pamoja na maiti
zote, kisha miili ya marehemu
ikawekwa ndani ya gari, safari ya
kurudishwa Dodoma mjini ikaanza,
walipofika, maiti zote zikaenda
kuifadhiwa katika monchwari ya
hospitali ya mkoa, kisha polisi
wakafanya kikao na waandishi wa
habari, kuhusu ule mlolongo wa
matukio ya kutisha, ila kwa bahati
nzuri, Sajenti Minja alikuwa na
kitambulisho cha Omari Said Mkwiji,
kwa hiyo akawapa nafasi waandishi
wa habari waipige picha, huku
Sajenti Minja akiwaambia ile picha ni
ya mmoja kati ya wale watuhumiwa
watatu wa mauaji na akaongeza
kuwa mtuhumiwa mwingine (Denis)
amekufa katika ajali iliyotokea wakati
wanakimbizana na polisi.
Kesho yake asubuhi, magazeti yote yalitoka na
habari hizo za mauaji, na pembeni
ya hizo habari kulikuwa na picha
kubwa ya Omari, akitajwa kama
mmoja wa wahusika wa mauaji ya unyonyaji damu.
Wakina kayoza walipoingia ndani ya basi, walikaa
siti ya nyuma kabisa, siti ya mbele
yao walikaa wakina mama wawili
ambao walikuwa wanazungumzia juu
ya mauaji ya kutisha yaliyotokea kati
ya Dodoma na Morogoro.
"na tena hadi picha ya muuaji imetolewa"
mama mmoja wapo. ambae alikuwa
kabeba mtoto katika miguu yake
alikuwa akimsimulia mwenzie,
"imetolewa na gazeti gani?" yule
mama mwingine wa makamo
akamuuliza yule mama mwenye
mtoto.
"magazeti yote unayoyajua
wewe wametoa hiyo habari" mama
mwenye mtoto akajibu.
"chumbageni
si hapo tu tunakaribia, nitanunua
gazeti ili na mimi nione" yule mama wa makamo
akajibu.
Kipindi chote wakati
wanaingia, hadi safari ilipoanza,
wakina Omary walikuwa
wanawasikiliza tu, ila habari
iliyowashtua ni kuchapishwa kwa
picha ya Omary kwenye magazeti.
"Bab hii ishu imeshakuwa kubwa kupita kiasi" Kayoza alimwambia mwenzake wakati wale wakina mamá wanaongea,
"Maji tumeshayavulia nguo, kuyaoga haina budi" Omary aliongea kwa sauti ndogo,
"Maisha ya kukimbia kimbia tutaishi mpaka lini sasa?" Kayoza aliuliza kwa masikitiko,
"Kila lenye mwanzo halikosi mwisho" Omary alijibu kifupi.
Walipofika karibu na
chumbageni, ile gari ikasimama kwa
dharura, kulikuwa na mushkeli katika
upande wa injini, wale wakina mama
wakanunua gazeti, wakawa wanasoma
ile habari
"mimi nikimuona, yaani
haraka nawajulisha polisi" yule
mama mwenye mtoto aliongea.
"hata mimi, mwenzangu milioni kumi
nyingi" yule mama wa makamo
akajibu baada ya kusoma habari
kuwa atayemkamata au atakayefanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa atapewa kiasi
hicho cha pesa, kipindi chote hicho wakina Kayoza walikaa tu kwenye siti za nyuma ya gari, hawakuthubutu kushuka.
Gari lilipotengemaa likaendelea na
safari. Kipindi chote Omari alikuwa
kaielekeza sura yake sanjari na
dirisha ili kukwepa sura yake isionekane na abiria wengine kwa maana alishapatwa na wasiwasi.
Gari ikafika mwisho wa safari,
watu wakaanza kutelemka, wale
wakina mama kwa ajili ya kuwa na
mtoto, ikabidi wasubiri ili watu wote watoke na wao watoke wa
mwisho, sasa wakati wakina kayoza
wanawapita, Omary akamkanyaga yule
mama mwenye mtoto kwa bahati
mbaya,
"samahani mama" Omary
akamtaka radhi yule mama huku akimwangalia
usoni, yule mama akapata mshtuko,
"ah!, si ndo
huyu?" Yule mama alisema kwa kupayuka.
"sio mimi" Omary aliongea bila kutarajia huku akijinasua kutoka kwenye mkono wa yule mwanamke, kisha wakatoka haraka ndani
ya ile gari na kukimbilia nje.
Yule mama akachukua
gazeti kutoka kwa mwenzake, kisha
akaiangalia ile picha ya Omary iliyokuwepo katika gazeti
"mh!, haswaa
ndiye yeye" Yule mama akajisemea moyoni, kisha
akatoka kwa lengo la kuwatazama
walipoelekea wakina Omari, ila
alichelewa, akakuta peupe.
akaangaza tena, hakuona mtu,
akaishia kusonya.
Baada ya wakina
kayoza kufanikiwa kushuka kwenye
gari, wakakimbilia nyuma ya ile gari,
wakawa wanamchunguza yule mama,
paka alivyotoka ndani ya gari na kuanza kuangaza
walikuwa wanamuangalia, mpaka ule
msonyo uliotolewa na yule mama pia waliusikia, wakasubiri mpaka yule mama alipoondoka, nao
ndio wakaondoka ila kwa kujificha ficha sana nyuma ya magari mengine yaliyokuwepo pale.
"Yaani tayari habari zimeshasambazwa katika vyombo vya habari?" Omary alimuuliza mwenzake wakiwa tayari wameshatoka katika kituo cha mabasi,
"Tena wamechelewa kweli, ilitakiwa watoe taharifa jana" Kayoza alijibu huku akikagua mandhari ya mji wa Tanga,
"Ebu twende pale tukasome some magazeti" Omary aliongea huku akielekea sehemu ambapo kulikuwa na magazeti yametandazwa juu ya meza,
"Acha ujinga wewe" Kayoza aliongea huku akiwa anamzuia Omary,
"Kwanini?" Omary aliuliza huku akimshangaa Kayoza,
"Unajua kuwa sisi tunatafutwa na mbaya zaidi picha yako ndiyo imeonekana kwenye magazeti, kwa hiyo wewe huoni kwenda eneo kama lile ni rahisi sana kukamatwa?" Kayoza aliuliza baada ya maelezo marefu,
"Ila kweli, basi nenda wewe kaangalie, alafu uje unijulishe" Omary alimwambia Kayoza,
"Mimi naenda, ila sio kuangalia. Naenda kununua gazeti tutaenda kusoma mbele Safari" Kayoza aliongea huku akielekea pale walipotandaza magazeti mezani. Alifika na kununua magazeti mawili ya kisiasa na jamii na kisha akarudi mahali Omary alipo na kumpa gazeti moja, nae akabaki na moja,
"Alafu ujue umenishangaza sana" Omary alimwambia Kayoza,
"Kwanini?" Kayoza aliuliza,
"Kwanini yule Askari mweupe haujamuua?" Kayoza aliuliza huku akimaanisha Sajenti Minja,
"Mimi?" kayoza aliuliza tena,
"Ndio, ni wewe" Omary alikazia swali lake,
"Sasa mimi nitajuaje wakati unajua kabisa mimi nikiwa katika hali ile uwa sijitambui?" Kayoza nae alijibu kwa mtindo wa kuuliza,
"Hicho kitu kimenishangaza sana" Omary aliongea huku akiendelea kushangaa,
"Wewe mwenyewe uwa sikudhuru na Kwanini hushangai?" Kayoza alimuuliza Omary,
"Dah, tuachane na hayo, maana tukiulizana sana hatutapata majibu ila tutaongeza maswali" Omary aliamua kupotezea huo mjadala,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi