KIJIJINI KWA BIBI (9)

0
Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA TISA
TULIPOISHIA...
"Wewe mwenyewe uwa sikudhuru na Kwanini hushangai?" Kayoza alimuuliza Omary,

"Dah, tuachane na hayo, maana tukiulizana sana hatutapata majibu ila tutaongeza maswali" Omary aliamua kupotezea huo mjadala,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"Na mbona hawajaandika habari za Denis katika haya magazeti?" Kayoza alimuuliza Omary,

"Hata mimi sijaelewa, au labda kuna sababu waliyofanya wafiche kifo chake?" Omary aliongea ila wote walilijadili jambo hilo huku wakiwa na huzuni,

"Muda bado upo, Ngoja tusubiri habari za kesho, labda wanaweza kuja na habari zake" Kayoza aliongea na baada ya hapo ukimya ukafuata.

Sajenti Minja hakuwa na raha kabisa siku hiyo, maana ndani ya siku chache alishuhudia vifo vya ajabu sana na pia na yeye aliponea chupuchupu kufa na akaachwa na alama ya meno kwenye shingo,

"Kiongozi bora uende hospitali ukaangaliwe kama ayo meno yanaweza kukuletea madhara" Askari mmoja alimshauri Sajenti Minja,

"Nina mpango huo, ila mkuu amesema anataka kuongea na mimi muda huu, so nasubiri nimalize nae maongezi ndio niende hospitali" Sajenti Minja alimjibu yule Askari na muda huo huo kuna Askari mwingine akaja kumwambia Sajenti Minja kuwa anahitajika na mkuu.

Sajenti Minja akanyanyuka na kwenda moja kwa moja ofisini kwa mkuu wake.

"Poleni kwanza kwa matukio mabaya" Mkuu wa polisi aliongea baada ya salamu,

"Tumeshapoa" Sajenti Minja alijibu kwa unyonge,

"Nini maoni yako kuhusu hii kesi?" Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja,

"Naomba mnitoe kwenye hii kesi, naona kama nimeishindwa" Sajenti Minja aliongea kwa heshima mbele ya mkuu wake,

"Kwanini?" Mkuu aliuliza,

"Nafikiri hiyo ndio njia pekee ya kuweka maisha yangu salama, maana wale tunaowafuatilia sio watu wa kawaida" Sajenti Minja alimueleza mkuu wake,

"Wewe unadhani kufanya hivyo ni sahihi?" Mkuu aliuliza,

"Nadhani inaweza kuwa sahihi" Sajenti Minja alijibu,

"Sawa, nakupa muda wa kwenda kujiuliza tena kuhusu hili, alafu kesho uje tena kuzungumza kuhusu jambo hili hili" Mkuu aliongea na kumruhusu Sajenti Minja aondoke.

Sajenti Minja akatoka na akili yake yote akaielekeza hospitali kwa nia ya kwenda kuangalia kama jeraha aliloachiwa na Kayoza lina madhara gani.

?

Kayoza na Omary baada ya mwendo mrefu kutoka kituo cha mabasi, Wakatafuta

baiskeli za kuwafikisha kijijini, bahati

nzuri wakaipata. Walitumia muda wa

dakika ishirini kufika kijiji husika,

wakawalipa madereva ujira wao,

kisha wakaanza kutembea kwa

miguu, walitembea hadi wakafika

sehemu moja, ambayo kulikuwa na

kajumba kadogo kamejitenga kidogo

na nyumba nyingine,

"sijui ndio hapa, ebu ngoja tujaribu" Omari

aliongea bila ya uhakika,

wakiisogelea ile nyumba, kisha wakagonga mlango,

"karibu" sauti

ikajibu kutoka ndani, wakasubiri

mwenyeji hatoke, lakini hakuna

aliyetoka, wakarudia tena kugonga

"shabashi, pita ndani" ile sauti ikajibu kwa ghadhabu kidogo, Omari

akausukuma mlango kisha akaingia,

akamkuta mzee mmoja mfupi mweupe, kavaa baraghashia,

"shikamoo babu" 0mari akamsalimia

kwa furaha.

"marhaba, karibu" yule

mzee aliitikia huku sura yake

ikionesha anajaribu kuvuta

kumbukumbu fulani.

"asante" 0mari

akajibu huku akitambua alichokuwa

anakifikiria babu yake,

"Karibuni mkae" Yule mzee aliongea huku akiendelea kuvuta kumbukumbu,

"babu mimi

mjukuu wako 0mari" Omari akasema huku akitabasamu,

"omari, omari, Omary wa wapi? " Babu aliuliza akiwa bado

anafikiria huku akijaribu kuvuta

kumbukumbu.

"omari mkwiji mtoto wa mwanao wa Dodoma" Omari akamsaidia babu yake kumuelewesha.

"ooh, karibu babu, vipi

mbona umekuja bila taharifa" Babu

akauliza huku akimpa mkono Omary na Kayoza.

"ni matatizo babu,

nitakusimulia tu babu" 0mari akamwambia babu yake huku akifurahi babu yake kumtambua,

"Naona umekuja na mwenzako?" Babu akamuuliza Omary,

"ndio babu" 0mari akajibu,

"karibu kijana" Babu akamwambia Kayoza huku

akimpa mkono, ila kitu cha ajabu,

babu aliung'ang'ania mkono wa

kayoza kwa dakika mbili nzima huku akiwa amemkazia macho,

"kijana una mzigo mzito sana wa matatizo" Babu alimwambia Kayoza huku machozi yakimtoka….

"ooh, karibu babu, vipi

mbona umekuja bila taharifa" Babu

akauliza huku akimpa mkono Omary

na Kayoza.

"ni matatizo babu,

nitakusimulia tu babu" 0mari akamwambia babu yake huku

akifurahi babu yake kumtambua,

"Naona umekuja na mwenzako?"

Babu akamuuliza Omary,

"ndio babu" 0mari akajibu,

"karibu kijana" Babu akamwambia

Kayoza huku

akimpa mkono, ila kitu cha ajabu,

babu aliung'ang'ania mkono wa

kayoza kwa dakika mbili nzima huku

akiwa amemkazia macho,

"kijana una mzigo mzito sana wa matatizo" Babu alimwambia Kayoza

huku machozi yakimtoka..

ENDELEA….

kayoza akashtuka,

"hapana babu, mimi

niko sawa tu" Kayoza akamjibu babu

huku akijilazimisha kutabasamu,

"kijana jaribu kuwa mkweli,

vinginevyo utapata matatizo zaidi ya hayo

yaliyokukuta" Babu akamsisitiza

Kayoza,

"babu tutakusimulia baadae" Omary akaingilia kati baada ya kuona Kayoza hawezi kukubali.

Babu yake na Omary

anaitwa Mzee Salum Said Omari

Shekindile Mkwiji, ila jina maarufu

lililozoeleka kwa watu wa pale

kijijini, wanamuita Mzee Mkwiji,

huyu mzee katika maisha yake ya

ujana alioa wanawake saba na

kuwazalisha watoto zaidi ya hamsini,

na ana wajukuu wasio na idadi, ila

kitu ambacho kilichokuwa

kinawachanganya watoto wake, ni

kuwa huyu mzee hakuitaji kabisa

msaada wao, wakimpelekea pesa,

anawarudishia.

Kuna kipindi watoto wake walijipanga

wamjengee nyumba nzuri, akakataa,

ila watoto wake hawakujua sababu

ya yote hayo, ila sababu aliijua

mwenyewe mzee Mkwiji, na sababu

yenyewe ni kuwa na mizimu ya

kiganga aliyorithishwa na baba yake,

ambayo yenyewe inataka anayeimiliki

awe anatoa tu misaada, na asiwe

anapokea, anaishi peke yake, wake

zake watano walishafariki, na wawili

aliwapa talaka.

Ni mganga

anayependwa sana katika eneo

analoishi.

Baada ya kupata chai na

mihogo, Omary na Kayoza walimsaidia

kazi ndogo ndogo babu yao, baada

ya shughuli za hapa na pale kuisha,

wakatindika mkeka nyuma ya

nyumba, wakaanza kumsimulia Mzee

Mkwiji, kuanzia mwanzo hadi

mwisho, Mzee Mkwiji aliwasikiliza

kwa makini, kisha akaingia ndani

kwake akatoka na kibuyu kidogo,

alafu akamwambia Kayoza ateme

mate chini, Kayoza akatema, Mzee

Mkwiji akamimina dawa kidogo

kutoka kwenye kibuyu alafu

akaichanganya na mate ya kayoza,

ukatokea moshi mweusi, ukawa

unapanda juu kuelekea mashariki,

"mh, kazi ipo" Mzee Mkwiji

akajisemea huku akitingisha kichwa kwa masikitiko, kisha akarudia tena

kufanya kama mwanzo, sasa hivi ule

moshi ulipotoka, ukaingia puani kwa

mzee Mkwiji, kisha akapiga chafya,

akawa kama kasinzia, alikuwa katika

hali hiyo kwa muda ya dakika tatu, kisha

akafungua macho na kusema,

"pole

sana kijana, ningekusaidia ila

mizimu yangu imeingiwa na uoga

kupambana na mzimu ulionao" Mzee Mkwiji aliongea huku akimuangalia Kayoza kwa jicho la huruma,

Kayoza akapoteza matumaini, ila

babu akaendelea kumwambia,

"mama yako ndio anaweza kuwa

msaada mkubwa kwako" Mzee Mkwiji alitoa kauli ilijenga swali kwa Kayoza,

"Samahani babu, umesema nina mzimu?" Kayoza aliuliza kanakwamba hakumsikia Mzee Mkwiji,

"Tena wa hatari sana" Mzee Mkwiji alijibu,

"Sasa unaposema mama yangu ndio anaeweza kuwa msaada kwangu hapo unanivuruga kidogo, kwa maana mama yangu sio mganga, kwa hiyo ni vipi atakuwa msaada kwangu?" Kayoza alimuuliza Mzee Mkwiji,

"Kwa kweli hilo swali nitashindwa kukujibu, ila mizimu yangu ndio imeniambia hivyo" Mzee Mkwiji alijibu huku akimwaga yale maji yake aliyofanyia uganga,

"Ila naweza kupona, si ndio?" Kayoza alimuuliza tena Mzee Mkwiji,

"Kama mizimu imesema msaada upo, basi unaweza kupona" Mzee Mkwiji alitoa jibu lililompa matumaini Kayoza,

"Sasa inabidi kesho tu nisafiri, niende kwa mama" Kayoza aliongea huku akimuangalia Omary,

"Ungepumzika kwanza mjukuu wangu, yaani jana umekuja alafu uondoke kesho? Shinyanga ni mbali kutoka hapa" Mzee Mkwiji aliongea na kumfanya Kayoza ashtuke,

"Umejuaje Nataka niende shinyanga?" Kayoza aliuliza huku akishangaa,

"Si ndio mama yako yupo uko?" Mzee Mkwiji nae aliuliza badala ya kujibu,

"Ndio, sasa umejuaje yupo uko?" Kayoza aliuliza tena huku akistahajabu maono ya Mzee Mkwiji,

"Sina uganga wa kubahatisha, mizimu yangu uwa inaniambia ukweli" Mzee Mkwiji alijibu huku akitabasamu,

"Aisee wewe mzee ni kiboko" Omary aliongea huku akicheka,

"Kama nilivyosema hawali, kesho naondoka" Kayoza alirudia Kutoa taharifa,

"Itabidi twende wote" Omary aliongea,

"Wewe baki tu ndugu yangu, msaada ulionipa ni mkubwa sana. Nakushukuru sana" Kayoza alimwambia Omary,

"Hapana siwezi kubaki, kama kutafutwa ni mimi ninayetafutwa kwa maana picha yangu ndio ipo katika vyombo vya habari, kwa hiyo ni bora niwe na wewe popote niendapo kwa maana wewe pekee ndiye unaweza kuniokoa mikononi kwa polisi" Omary aliongea kwa huzuni,

"Omary unafuata kifo uko" Mzee Mkwiji alimwambia mjukuu wake,

"Kivipi babu?" Omary aliuliza,

"Mnapoenda mtapata utatuzi wa tatizo lenu, ila kurudi salama ni kazi sana" Mzee Mkwiji aliwaambia na kufanya vijana waogope,

"Kwa hiyo tukienda uko shinyanga tunakufa?" Omary aliuliza kwa taharuki,

"Shinyanga hamtokufa, ila kazi isipofanikiwa shinyanga, basi mtakuwa na safari nyingine itakayoambatana na kifo" Mzee Mkwiji alizidi Kutoa taharifa mbaya kwa vijana,

"Kwa hiyo tusiende au?" Kayoza aliuliza,

"Usipoenda itakuwa umeridhika na Maisha ya kuua, cha muhimu ni uende, ila kuweni makini na maamuzi yenu uko muendako" Mzee Mkwiji aliongea huku akijinyanyua mkekani,

"Mbona umakini tunao tu babu" Kayoza alijibu wakati babu akiingia ndani,

"Pamoja na umakini wako, kifo chako kitakuwa cha kujiua mwenyewe" Babu aliongea kwa utani huku akipotelea ndani,

"Babu mzinguaji kweli, kaongea vya maana wee, ameona amalizie na utani" Kayoza aliongea huku akicheka,

"Ndivyo alivyo huyo, akiona maswali yanakuwa mengi uwa anayapotezea kwa utani" Omary aliongea huku wakikunja mkeka kwa lengo la kuingia ndani.

Sajenti Minja alienda hospitali na kufanyiwa vipimo katika jeraha lake na hakukutwa na tatizo lolote,

"Daktari rudia kunipima, haiwezekani nikutwe sina kitu" Sajenti Minja aliongea na pia akishangaa majibu ya vipimo,

"Ridhika na majibu, au kama hutuamini nenda kajaribu kucheki kwenye hospitali nyingine, labda jibu linaweza kuwa tofauti" Daktari alimjibu kistaharabu Sajenti Minja,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)