Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA TISA
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"Wewe mwenyewe uwa sikudhuru na Kwanini hushangai?" Kayoza alimuuliza Omary,
"Dah, tuachane na hayo, maana tukiulizana sana hatutapata majibu ila tutaongeza maswali" Omary aliamua kupotezea huo mjadala,
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
"Na mbona hawajaandika habari za Denis katika haya magazeti?" Kayoza alimuuliza Omary,
"Hata mimi sijaelewa, au labda kuna sababu waliyofanya wafiche kifo chake?" Omary aliongea ila wote walilijadili jambo hilo huku wakiwa na huzuni,
"Muda bado upo, Ngoja tusubiri habari za kesho, labda wanaweza kuja na habari zake" Kayoza aliongea na baada ya hapo ukimya ukafuata.
Sajenti Minja hakuwa na raha kabisa siku hiyo, maana ndani ya siku chache alishuhudia vifo vya ajabu sana na pia na yeye aliponea chupuchupu kufa na akaachwa na alama ya meno kwenye shingo,
"Kiongozi bora uende hospitali ukaangaliwe kama ayo meno yanaweza kukuletea madhara" Askari mmoja alimshauri Sajenti Minja,
"Nina mpango huo, ila mkuu amesema anataka kuongea na mimi muda huu, so nasubiri nimalize nae maongezi ndio niende hospitali" Sajenti Minja alimjibu yule Askari na muda huo huo kuna Askari mwingine akaja kumwambia Sajenti Minja kuwa anahitajika na mkuu.
Sajenti Minja akanyanyuka na kwenda moja kwa moja ofisini kwa mkuu wake.
"Poleni kwanza kwa matukio mabaya" Mkuu wa polisi aliongea baada ya salamu,
"Tumeshapoa" Sajenti Minja alijibu kwa unyonge,
"Nini maoni yako kuhusu hii kesi?" Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja,
"Naomba mnitoe kwenye hii kesi, naona kama nimeishindwa" Sajenti Minja aliongea kwa heshima mbele ya mkuu wake,
"Kwanini?" Mkuu aliuliza,
"Nafikiri hiyo ndio njia pekee ya kuweka maisha yangu salama, maana wale tunaowafuatilia sio watu wa kawaida" Sajenti Minja alimueleza mkuu wake,
"Wewe unadhani kufanya hivyo ni sahihi?" Mkuu aliuliza,
"Nadhani inaweza kuwa sahihi" Sajenti Minja alijibu,
"Sawa, nakupa muda wa kwenda kujiuliza tena kuhusu hili, alafu kesho uje tena kuzungumza kuhusu jambo hili hili" Mkuu aliongea na kumruhusu Sajenti Minja aondoke.
Sajenti Minja akatoka na akili yake yote akaielekeza hospitali kwa nia ya kwenda kuangalia kama jeraha aliloachiwa na Kayoza lina madhara gani.
?
Kayoza na Omary baada ya mwendo mrefu kutoka kituo cha mabasi, Wakatafuta
baiskeli za kuwafikisha kijijini, bahati
nzuri wakaipata. Walitumia muda wa
dakika ishirini kufika kijiji husika,
wakawalipa madereva ujira wao,
kisha wakaanza kutembea kwa
miguu, walitembea hadi wakafika
sehemu moja, ambayo kulikuwa na
kajumba kadogo kamejitenga kidogo
na nyumba nyingine,
"sijui ndio hapa, ebu ngoja tujaribu" Omari
aliongea bila ya uhakika,
wakiisogelea ile nyumba, kisha wakagonga mlango,
"karibu" sauti
ikajibu kutoka ndani, wakasubiri
mwenyeji hatoke, lakini hakuna
aliyetoka, wakarudia tena kugonga
"shabashi, pita ndani" ile sauti ikajibu kwa ghadhabu kidogo, Omari
akausukuma mlango kisha akaingia,
akamkuta mzee mmoja mfupi mweupe, kavaa baraghashia,
"shikamoo babu" 0mari akamsalimia
kwa furaha.
"marhaba, karibu" yule
mzee aliitikia huku sura yake
ikionesha anajaribu kuvuta
kumbukumbu fulani.
"asante" 0mari
akajibu huku akitambua alichokuwa
anakifikiria babu yake,
"Karibuni mkae" Yule mzee aliongea huku akiendelea kuvuta kumbukumbu,
"babu mimi
mjukuu wako 0mari" Omari akasema huku akitabasamu,
"omari, omari, Omary wa wapi? " Babu aliuliza akiwa bado
anafikiria huku akijaribu kuvuta
kumbukumbu.
"omari mkwiji mtoto wa mwanao wa Dodoma" Omari akamsaidia babu yake kumuelewesha.
"ooh, karibu babu, vipi
mbona umekuja bila taharifa" Babu
akauliza huku akimpa mkono Omary na Kayoza.
"ni matatizo babu,
nitakusimulia tu babu" 0mari akamwambia babu yake huku akifurahi babu yake kumtambua,
"Naona umekuja na mwenzako?" Babu akamuuliza Omary,
"ndio babu" 0mari akajibu,
"karibu kijana" Babu akamwambia Kayoza huku
akimpa mkono, ila kitu cha ajabu,
babu aliung'ang'ania mkono wa
kayoza kwa dakika mbili nzima huku akiwa amemkazia macho,
"kijana una mzigo mzito sana wa matatizo" Babu alimwambia Kayoza huku machozi yakimtoka….
"ooh, karibu babu, vipi
mbona umekuja bila taharifa" Babu
akauliza huku akimpa mkono Omary
na Kayoza.
"ni matatizo babu,
nitakusimulia tu babu" 0mari akamwambia babu yake huku
akifurahi babu yake kumtambua,
"Naona umekuja na mwenzako?"
Babu akamuuliza Omary,
"ndio babu" 0mari akajibu,
"karibu kijana" Babu akamwambia
Kayoza huku
akimpa mkono, ila kitu cha ajabu,
babu aliung'ang'ania mkono wa
kayoza kwa dakika mbili nzima huku
akiwa amemkazia macho,
"kijana una mzigo mzito sana wa matatizo" Babu alimwambia Kayoza
huku machozi yakimtoka..
ENDELEA….
kayoza akashtuka,
"hapana babu, mimi
niko sawa tu" Kayoza akamjibu babu
huku akijilazimisha kutabasamu,
"kijana jaribu kuwa mkweli,
vinginevyo utapata matatizo zaidi ya hayo
yaliyokukuta" Babu akamsisitiza
Kayoza,
"babu tutakusimulia baadae" Omary akaingilia kati baada ya kuona Kayoza hawezi kukubali.
Babu yake na Omary
anaitwa Mzee Salum Said Omari
Shekindile Mkwiji, ila jina maarufu
lililozoeleka kwa watu wa pale
kijijini, wanamuita Mzee Mkwiji,
huyu mzee katika maisha yake ya
ujana alioa wanawake saba na
kuwazalisha watoto zaidi ya hamsini,
na ana wajukuu wasio na idadi, ila
kitu ambacho kilichokuwa
kinawachanganya watoto wake, ni
kuwa huyu mzee hakuitaji kabisa
msaada wao, wakimpelekea pesa,
anawarudishia.
Kuna kipindi watoto wake walijipanga
wamjengee nyumba nzuri, akakataa,
ila watoto wake hawakujua sababu
ya yote hayo, ila sababu aliijua
mwenyewe mzee Mkwiji, na sababu
yenyewe ni kuwa na mizimu ya
kiganga aliyorithishwa na baba yake,
ambayo yenyewe inataka anayeimiliki
awe anatoa tu misaada, na asiwe
anapokea, anaishi peke yake, wake
zake watano walishafariki, na wawili
aliwapa talaka.
Ni mganga
anayependwa sana katika eneo
analoishi.
Baada ya kupata chai na
mihogo, Omary na Kayoza walimsaidia
kazi ndogo ndogo babu yao, baada
ya shughuli za hapa na pale kuisha,
wakatindika mkeka nyuma ya
nyumba, wakaanza kumsimulia Mzee
Mkwiji, kuanzia mwanzo hadi
mwisho, Mzee Mkwiji aliwasikiliza
kwa makini, kisha akaingia ndani
kwake akatoka na kibuyu kidogo,
alafu akamwambia Kayoza ateme
mate chini, Kayoza akatema, Mzee
Mkwiji akamimina dawa kidogo
kutoka kwenye kibuyu alafu
akaichanganya na mate ya kayoza,
ukatokea moshi mweusi, ukawa
unapanda juu kuelekea mashariki,
"mh, kazi ipo" Mzee Mkwiji
akajisemea huku akitingisha kichwa kwa masikitiko, kisha akarudia tena
kufanya kama mwanzo, sasa hivi ule
moshi ulipotoka, ukaingia puani kwa
mzee Mkwiji, kisha akapiga chafya,
akawa kama kasinzia, alikuwa katika
hali hiyo kwa muda ya dakika tatu, kisha
akafungua macho na kusema,
"pole
sana kijana, ningekusaidia ila
mizimu yangu imeingiwa na uoga
kupambana na mzimu ulionao" Mzee Mkwiji aliongea huku akimuangalia Kayoza kwa jicho la huruma,
Kayoza akapoteza matumaini, ila
babu akaendelea kumwambia,
"mama yako ndio anaweza kuwa
msaada mkubwa kwako" Mzee Mkwiji alitoa kauli ilijenga swali kwa Kayoza,
"Samahani babu, umesema nina mzimu?" Kayoza aliuliza kanakwamba hakumsikia Mzee Mkwiji,
"Tena wa hatari sana" Mzee Mkwiji alijibu,
"Sasa unaposema mama yangu ndio anaeweza kuwa msaada kwangu hapo unanivuruga kidogo, kwa maana mama yangu sio mganga, kwa hiyo ni vipi atakuwa msaada kwangu?" Kayoza alimuuliza Mzee Mkwiji,
"Kwa kweli hilo swali nitashindwa kukujibu, ila mizimu yangu ndio imeniambia hivyo" Mzee Mkwiji alijibu huku akimwaga yale maji yake aliyofanyia uganga,
"Ila naweza kupona, si ndio?" Kayoza alimuuliza tena Mzee Mkwiji,
"Kama mizimu imesema msaada upo, basi unaweza kupona" Mzee Mkwiji alitoa jibu lililompa matumaini Kayoza,
"Sasa inabidi kesho tu nisafiri, niende kwa mama" Kayoza aliongea huku akimuangalia Omary,
"Ungepumzika kwanza mjukuu wangu, yaani jana umekuja alafu uondoke kesho? Shinyanga ni mbali kutoka hapa" Mzee Mkwiji aliongea na kumfanya Kayoza ashtuke,
"Umejuaje Nataka niende shinyanga?" Kayoza aliuliza huku akishangaa,
"Si ndio mama yako yupo uko?" Mzee Mkwiji nae aliuliza badala ya kujibu,
"Ndio, sasa umejuaje yupo uko?" Kayoza aliuliza tena huku akistahajabu maono ya Mzee Mkwiji,
"Sina uganga wa kubahatisha, mizimu yangu uwa inaniambia ukweli" Mzee Mkwiji alijibu huku akitabasamu,
"Aisee wewe mzee ni kiboko" Omary aliongea huku akicheka,
"Kama nilivyosema hawali, kesho naondoka" Kayoza alirudia Kutoa taharifa,
"Itabidi twende wote" Omary aliongea,
"Wewe baki tu ndugu yangu, msaada ulionipa ni mkubwa sana. Nakushukuru sana" Kayoza alimwambia Omary,
"Hapana siwezi kubaki, kama kutafutwa ni mimi ninayetafutwa kwa maana picha yangu ndio ipo katika vyombo vya habari, kwa hiyo ni bora niwe na wewe popote niendapo kwa maana wewe pekee ndiye unaweza kuniokoa mikononi kwa polisi" Omary aliongea kwa huzuni,
"Omary unafuata kifo uko" Mzee Mkwiji alimwambia mjukuu wake,
"Kivipi babu?" Omary aliuliza,
"Mnapoenda mtapata utatuzi wa tatizo lenu, ila kurudi salama ni kazi sana" Mzee Mkwiji aliwaambia na kufanya vijana waogope,
"Kwa hiyo tukienda uko shinyanga tunakufa?" Omary aliuliza kwa taharuki,
"Shinyanga hamtokufa, ila kazi isipofanikiwa shinyanga, basi mtakuwa na safari nyingine itakayoambatana na kifo" Mzee Mkwiji alizidi Kutoa taharifa mbaya kwa vijana,
"Kwa hiyo tusiende au?" Kayoza aliuliza,
"Usipoenda itakuwa umeridhika na Maisha ya kuua, cha muhimu ni uende, ila kuweni makini na maamuzi yenu uko muendako" Mzee Mkwiji aliongea huku akijinyanyua mkekani,
"Mbona umakini tunao tu babu" Kayoza alijibu wakati babu akiingia ndani,
"Pamoja na umakini wako, kifo chako kitakuwa cha kujiua mwenyewe" Babu aliongea kwa utani huku akipotelea ndani,
"Babu mzinguaji kweli, kaongea vya maana wee, ameona amalizie na utani" Kayoza aliongea huku akicheka,
"Ndivyo alivyo huyo, akiona maswali yanakuwa mengi uwa anayapotezea kwa utani" Omary aliongea huku wakikunja mkeka kwa lengo la kuingia ndani.
Sajenti Minja alienda hospitali na kufanyiwa vipimo katika jeraha lake na hakukutwa na tatizo lolote,
"Daktari rudia kunipima, haiwezekani nikutwe sina kitu" Sajenti Minja aliongea na pia akishangaa majibu ya vipimo,
"Ridhika na majibu, au kama hutuamini nenda kajaribu kucheki kwenye hospitali nyingine, labda jibu linaweza kuwa tofauti" Daktari alimjibu kistaharabu Sajenti Minja,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi