Notifications
  • MY DIARY (48)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA NANETULIPOISHIA...Familia yangu haikukubali kabisa mimi kuolewa na rangi nyeusi hivyo walinitenga na kusema hawanitambui kuwa mimi ni ndugu yao.Lakini kutokana na mapenzi mazito niliyokuwa nayo kwa baba yake na Leah nilijikuta nipo tayari kwa lolote hivyo nikahama na kwenda kuishi Tanzania.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Katika miaka hiyo tuliyokaa nilibahatika kupata mtoto huyu…
  • MY DIARY (47)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA SABATULIPOISHIA...Lakini ilifikia mahali ndoto hiyo inanijia hata mchana nikiwa nimekaa mahali tulivu.Ilikuwa inanipa taswira nzuri ya sehemu ambayo madini yalikuwepo.Basi nilianza mikakati ya kulitafuta eneo hilo na hiyo ni mara baada ya ushauri wa mpenzi wangu Candy hapo akimaaanisha yule dada aliyekuwa naye pale jukwaaani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Candy alinisihii sana…
  • MY DIARY (46)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA SITATULIPOISHIA...Nilikuwa kama niliyepigwa butwaa nisiamini nilichokuwa nakiona mbele yangu. Oooooh my God hold me on yalikuwa ni maneno yaliyonitoka kutoka kwenye uvungu wa moyo wangu mara baada ya kumuona James kwa uzuri zaidi na kuamini kuwa yule kweli alikuwa ni kaka yangu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilishindwa kuelewa nini kimetokea mpaka yeye kurudi katika hali yake ya…
  • MY DIARY (45)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA TANOTULIPOISHIA...Ndio niliona hipo haja ya kuokoka na kuishi maisha ya utakatifu kwa maana nishaishi maisha yote ya kuwa mbali na mungu. Nakumbuka nilipokuwa mdogo kipindi hicho naujua mlango wa kanisani tuisahawahi kufundishwa kuwa mtetezi wa kweli wa maisha ya mwanadamu ni Mungu.Na siku zote alaaniwe mtu yule amtegemeaye mwanadamu.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Sio kazi ya…
  • MY DIARY (44)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA NNETULIPOISHIA...Yani alianza kutaka uhusiano na mimi tena uhusinao wa mapenzi.Mda wote alikuwa akiniganda kama luba.Na mimi nilikuwa mjanja sana maana nilijifanya sinywi pombe wala kuvuta sigara.Pia baada ya kugundua kuwa wahusika wengine walikuwa wanajiachia niliamua kujifanya mshauri wa mapenzi na mahusiano.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilikuwa nawasshauri sana mshiriki wa…
  • MY DIARY (43)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA TATUTULIPOISHIA...Wakati nabadilisha staili kwa kukichua kile kifaa na kukiweka vizuri huku nikibinya ile switch hili iongeze spidi Mark aliingia. Ni kweli nilimuona ila sasa sikuwa na jinsi ilibidi nimalizie furaha hiyo ya uwongo uwongo. Yaani wazungu jamani sijui walifikiria nini maana kile kifaa ukikiminya kwa juu kinakuwa kinajizungusha chenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (42)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA MBILITULIPOISHIA...Uzalendo ulinishinda ikabidi nimuulize ni kwanini bado wanatumia njia hiyo ya kizamani kutunza kumbukumbu wakati siku hizi kuna kitu kinachoitwa Human Resource Informaion system ambapo kumbukumbu zote za wafanyakazi kama waliochishwa kazi, wagonjwa, walioenda likizo ,waliopandishwa vyeo na taarifa nyingine muhimu uhifadhiwa kwa kutumia komputa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (41)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINI NA MOJATULIPOISHIA...Mark anashangaazwa sana na mwanamke huyo lakini kwa kuwa shida yake ilikuwa ni hela anaamua kuachana nae na kuanza maisha mapya hapo jijiini Dar es salaamMaisha yanaendela lakini Mark amekuwa tajiri na mtu mwenye mafanikio sana kiuchumi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Pamoja na mafanikio hayo ni mtu ambaye mapenzi bado yalikuwa yakimuumiza siku hadi siku.Filamu…
  • MY DIARY (40)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA AROBAINITULIPOISHIA...Alikuwa akinyata kwa kweli. Kweli hata mimi nilimkubali tu siku ya kwanza ingawa bado nilikuwa sijajua ufanisi wake wa kazi.Nilikaa nae hapo kwangu kwa mda wa siki tatu huku asubuhi tukiamka na kuendelea na kazi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Ndani ya mda huo nikagundua kuwa alikuwa na uzorfu mkubwasana hivyo kazi hiyo alikuwa akiimudu kabisa.Hapo sasa nilimkubali sana…
  • MY DIARY (39)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA THELATHINI NA TISATULIPOISHIA...Nilikuwa na furaha sana huku nikiamini kuwa ndoto zangu za kuja kuwa mtu maarufu zinaweza kufanikiwa hata kabla ya kuyapata yale madini. Sikutaka mbwembwe niliamua kuikopi na kuipesti hiyo stori kama ilivyo na kuifowadi kwa Mark.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Baada ya kama lisaa hivi Mark alipiga na kuniuliza kama kweli ilikuwa nai mimi nimetunga hiyo…

KIJIJINI KWA BIBI (23)

Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU
TULIPOISHIA...
"hii kesi ya huyu mzee mbona mnaiendesha pole pole sana". Mkuu wa

polisi aliwauliza wale askari.

"ushaidi ndio unatuchelesha mkuu" Askari mmoja alijibu

"niambieni katika uchunguzi wenu mmefikia wapi" Mkuu wa Polisi

akawatupia swali jingine,

"hakuna mwanga wowote tuliopata" yule askari akamjibu tena mkuu wa polisi.

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"nyie wazembe kweli, ile maiti iliyoibiwa si iliokotwa pamoja na

zile maiti zilizonyonywa damu?" Mkuu wa polisi akauliza kwa jazba,

"ndio mkuu" wale askari wakajibu kwa pamoja,

"mlienda kumuhoji yule mtu aliekutwa hai?" Mkuu wa Polisi akawapa

swali jingine.

"hapana mkuu" akajibu yule Askari ambae siku zote uso wake

utawaliwa na hasira.

"kwanini" mkuu wa polisi akaendelea kuwabana na maswali.

"yule anahusika na kesi ya sajenti Minja" yule askari akajitetea

kipumbavu.,

"ok, sasa hii kesi ya huyu babu nampa sajenti Minja kwa sababu

mmesema zinaingiliana, basi atazishughulikia zote" Mkuu wa polisi

alimaliza kisha akawaamuru watoke ofisini kwake, wamuache babu wa

monchwari peke yake, wakamtii kisha wale askari wakaondoka.

Kisha mkuu wa polisi akachukua simu yake ya mkononi alafu akapiga,

"hallow Minja uko wapi?"mkuu wa polisi aliuliza. Baada ya kujibiwa

akaendelea,

"Nipo ofisini kwangu" Sajenti Minja alijibu huku akishangaa ile

simu ya ghafla kutoka kwa mkubwa wake,

"ok, njoo ofisini kwangu" Mkuu wa Polisi aliongea kisha akakata

simu.

"nakukabidhi kwa mtu anaejua kazi" Mkuu wa polis alimwambia babu wa

mochwari,

"Nashukuru sana kwa kunijali mwanangu" Babu wa monchwari aliongea

huku akiangalia chini.

"Sio nakujali, huo ndio utaratibu wa kazi" Mkuu wa Polisi aliongea.

Sajenti Minja baada ya simu aliyopigiwa na mkuu wake kukatwa,

akatoka ofisini kwake huku akiwa na maswali kibao juu ya kuitwa

kwake na Mkuu wa Kituo.

Akawa anaelekea ofisi ya mkuu wa polìsi, alipofika mlangoni

akagonga hodi,

"yes, come in" sauti ya mkuu wake kutoka ndani ilimjibu,

Sajent Minja akashika kitasa cha mlango akanyonga kwa nia ya

kufungua mlango…..

…sajenti Minja akanyonga kitasa, haikuonekana dalili ya mlango

kufunguka, mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani, mara akasikia mlango

unafunguliwa, akatoka mkuu wa polisi,

"minja nisubiri ndani mara moja, naenda msalani dakika moja", mkuu

wa polisi alipofungua mlango aliongea maneno hayo huku akiwa

anatembea kumuacha sajenti Minja, mlango ulikuwa bado uko wazi,

Sajenti Minja akanyanyua mguu wa kulia ili kuingia ndani,

"jesus christ" alijikuta anasema kwa sauti ya chini baada ya

kugundua kuwa aliekuwa ndani ni babu wa mochwari, ila bahati nzuri

ni kwamba yule babu alikuwa ameinamia chini, kwa hiyo hakuweza

kumgundua Sajenti Minja.

Sajenti Minja alirudi nje kwa kasi, kisha akaurudishia mlango huku

anahema kwa fujo kama katoka kukimbia mbio ndefu,

"vipi Minja, mbona unaonekana hauko kawaida", sauti ya mkuu wa

polisi ilimshtua Sajenti Minja,

"nimepigiwa simu, nyumbani kuna matatizo" Sajenti Minja alitumia

uongo,

"ila kulikuwa na kazi nataka kukupa, tuingie ndani kuna kesi nataka

kukupa, alafu utaendelea na ratiba zako", Mkuu wa Polisi alimwambia

Sajenti Minja,

"samahani mkuu, niko chini ya miguu yako, naomba hiyo kesi unipe

baadae, uko nyumbani sio kwema kabisa", Sajenti Minja aliongea uku

akiwa ameweka sura ya huzuni,

"mmmh, ok, sawa, ukimaliza ya nyumbani, unijulishe, maana nataka

nikupe kesi ya mzee mmoja hivi", Mkuu wa polisi alimkubalia,

"Nikimaliza nitakujulisha na asante mkuu kwa kunikubalia niende

nyumbani, nikirudi nitakufahamisha" , Sajenti Minja alijibu huku

akiwa anaanza kuondoka,

"Minja" Mkuu wa Polisi aliita tena wakati Sajenti Minja anaanza

kuondoka,

"naam mkuu" Sajenti Minja aliitikia baada ya kuitwa,

"unaondoka tu, ila hujaniambia nyumbani kuna tatizo gani", Mkuu wa

Polisi alihoji,

"kuna kajomba kangu, ambacho ni katoto ka dada yangu ambae

nilikuambia anaishi hapa, nimeambiwa amegongwa na gari na hali yake

sio nzuri", Sajenti Minja aliendelea kutunga uongo mbele ya bosi

wake,

"ooh, poleni sana, haya bwana wahi,"Mkuu wa Polisi alimruhusu

sajenti Minja kwa mtindo huo.

Sajenti Minja aliondoka kwa mwendo wa haraka haraka mpaka gari yake

ilipokuwepo,

"mhm, nimesevu so hadi raha, leo nilikua nahaibika mbele ya bosi",

Sajenti Minja aliongea wakati anajipakia kwenye gari yake.

"duh, mama ujue mi nashindwa kuelewa, naona kama ndio mmeniacha

niendelee kuwa katika hali hii", Kayoza alimwambia mama yake wakiwa

wanapata chakula cha mchana,

"ebu, acha uwendawazimu uko, mzazi gani anaependa mwanae awe katika

matatizo?, we msubiri mjomba ako arudi labda atakuwa na mpya", Mama

kayoza alimjibu mwanae huku akiwa anasafisha mikono yake kwa maji,

"lakini mama", Kayoza kabla hajamaliza kuongea, ilisikika sauti ya

mtu ikigonga mlango,

"sukuma, mlango uko wazi", Mama Kayoza aliongea kwa sauti ya juu

kidogo, ili mgongaji amsikie,

"hodi mpaka ndani, eeh, nina mguu mzuri kweli, yaani nimefika

wakati wa mahakuli", Sajenti Minja aliongea huku akiurudishia

mlango

,"karibu anko, ingawa ndo kinaisha", Omari alimwambia sajenti

Minja, kisha wote wakacheka,

"ebu tuachane na hayo, leo kidogo nipate aibu ya mwaka mbele ya

bosi wangu", Sajenti Minja alibadilisha stori,

"ehe, nini tena?", Mama Kayoza aliuliza kwa shauku.Sajenti Minja

aliwaeleza mwanzo mpaka mwisho,

"kwa hiyo inavyoonekana anataka na kesi ya yule babu wa mochwari

iwe chini yako?" Mama Kayoza aliuliza,

"ndio hivyo" Sajenti Minja alijibu kinyonge,

"sasa utafanyaje" Mama Kayoza aliuliza,

"nitamkimbia kimbia hivyo hivyo mpaka achoke", Sajenti Minja

alialiongea,

"Mimi naona bora uichukue na hiyo kesi hili uweze kuwadhibiti

vizuri wahusika" Omary alichangia

"Hapana, mimi nitajitahidi niikwepe tu" Sajenti Minja aliongea,

"Ichukue hiyo kesi kwa maana huwezi jua mipango ya Mungu" Mama

Kayoza aliongea,

"Tutajua uko mbele ya safari. jamani kuna kaugali kalichobaki?"

Sajenti Minja aliuliza,

"ugali upo, ila mboga ndo imeisha, ngoja wajomba zako wakakununulie

maziwa kwa mchungaji", Mama kayoza alimjibu Sajenti Minja huku

akimpa kayoza hela ya maziwa,

"Kwani hatuwezi kununua mboga nyingine zaidi ya maziwa" Sajenti

Minja aliuliza,

"Mbona tunaweza kununua hata maharage au nyama, tatizo tukiinjika

mpaka viive si utakuwa umeshakufa na njaa yako?" Mama Kayoza

aliongea,

"Kweli Dada, basi nyie wahini, maana njaa niliyonayo ni ya

hatari…

baada ya wakina kayoza kutoka, Sajenti Minja na dada yake

waliendelea na maongezi yao.

"afadhali umekuja mwenzangu, maana mjomba ako kanichachamalia

hapa", Mama Kayoza alimwambia Sajenti Minja

"kachachamaa na nini tena?"Sajenti Minja akauliza,

"eti anadai tuko kimya katika kufuatilia matatizo yake", Mama

Kayoza akajibu,

"kuna askari niliongea nae jana, akaniambia kuna mtaalam wa jadi

ana uwezo mkubwa wa kusaidia watu", Sajenti Minja alimwambia dada

yake

,"kwa hiyo ulimwambia una ndugu yako ananyonya damu?", mama Kayoza

aliuliza kwa mshtuko,

"kwani mi sina hakili mpaka nimwambie hivyo?, nilimdanganya

natokewa na mauzauza kila nikitaka kulala", Sajenti Minja akamjibu

dada yake,

"ataweza kweli kumtibia kayoza?", Mama kayoza akamtupia mdogo wake

swali jingine,

"dada nawe kwa maswali!, tutajua uko uko kama ataweza au lah",

Sajenti Minja alimjibu dada yake,

"lini mtaenda uko", mama Kayoza akauliza tena

"nafikiri kesho, kama nitapata nafasi", Sajenti Minja alijibu

"haya bwana, wacha nikakutayarishie chakula jikoni", mama kayoza

aliongea huku akinyanyuka kwenye kochi,

"hayo ndo mambo sasa, kama kuna pilipili niwekee", Sajenti Minja

alisema na kumfanya mama kayoza ahangue kicheko.

"Sasa hiyo pilipili utaiweka katika maziwa?" Mama Kayoza aliuliza

huku akicheka,

"Nitaitafunia tu na ugali" Sajenti Minja alijibu,

"Ngoja nikutafutie kama ntaipata" Mama Kayoza aliongea huku

akiingia jikoni.

"Sema siku hizi umekuwa mswahili kweli Dada yangu" Sajenti Minja

aliongea huku akitabasamu,

"Kwanini unasema hivyo?" Mama Kayoza aliuliza huku akisimama,

"Naona nawe unakubali tu tumpeleke mwanao kwa waganga sio kama

zamani ulivyoshikilia msimamo wako wa kanisani" Sajenti Minja

alimwambia Dada yake,

"Ujue Mungu hana njia moja ya kukupa mafanikio, unatakiwa upitie

njia nyingi lakini ukimuamini yeye tu na sio vitu vingine" Mama

Kayoza alimwambia Sajenti Minja,

"Sawa mama mchungaji, inabidi na wewe ujenge kanisa lako sasa"

Sajenti Minja alimwambia Mama Kayoza,

"Ebu kwenda zako uko, kwanza ulivyosema mchungaji umenikumbusha awa

wendawazimu waliofuata maziwa, mbona wamechelewa hivyo?" Mama

Kayoza aliuliza,

"Wana mambo mengi wale vijana, usikute wanamnyatia yule binti wa

mchungaji" Sajenti Minja aliongea kwa utani huku akicheka,

"Acha uwendawazimu wako, watoto wa mchungaji wana maadili wewe"

Mama Kayoza aliongea,

"Sio wote, kama yule binti mcharuko niliekutana nae juzi ni bure

kabisa, bora angeishi uswahilini tu" Sajenti Minja aliongea huku

akicheka,

"Kwani ana kosa gani? Si alikuwa anaenda polisi kusema habari za

ukweli" Mama Kayoza aliongea huku akitabasamu,

"We si ni mlokole? Nenda na wewe polisi kaseme hizo hizo habari

kuwa mwanao muuaji" Sajenti Minja alimwambia Mama Kayoza,

"Mtoto anauma bwana, mtoto mwenyewe ndio huyo huyo mmoja kama roho"

Mama Kayoza aliongea huku akicheka,

"Nenda jikoni bwana, maana story zimezidi mpaka unasahau kuwa mimi

njaa inaniuma" Sajenti Minja alimwambia Dada yake,

"Hata baba, usije ukanifia bure kwa njaa" Mama Kayoza aliongea huku

akielekea jikoni.

Baada ya mkuu wa polisi kurudi ndani, alimpgia simu askari mwingine

na kumwambia amrudishe rumande Babu wa mochwari,

"jamani nitakaa huku mpaka lini, nina mke na watoto mimi",Babu wa

mochwari aliongea huku machozi yakimtoka,

"usijali mzee wangu, upepelezi utakamilika hivi karibuni", Mkuu wa

polisi alimjibu Babu wa mochwari kwa huruma.

"Mwanzo askari wako waliniambia nikiri kosa ili niachiwe, nikakiri

kosa kuwa ni kweli mwili umeibwa, lakini hawajaniachia, naambulia

kipigo tu mpaka viungo vinateguka" Babu wa monchwari alilalamika,

"Mzee ujue upelelezi sio kitu cha kukurupuka tu, inahitajika muda

mrefu wa kuchunguza na kujiridhisha na jibu la kile

kilichopelelezwa, na hapo sasa ndipo sisi tutaachana na wewe na

kesi yako itakuwa mahakamani" Mkuu wa polisi alimuelewesha Babu wa

monchwari,

"Mahakamani tena?, si nitafungwa jamani mie?" Babu wa monchwari

aliuliza huku akilalamika,

"Sasa sisi hatutaki ufungwe, na ndio maana tunaendelea kukuhifadhi

ili utusaidie kumpata huyo aliyeichukua hiyo maiti" Polisi

alimwambia Babu wa monchwari,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
60 Kijijini kwa Bibi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo (2)
Maoni 2
  1. 3 Julai 2024, 16:40
    Profile
    Bila jina
    Said: Simulizi zako kali sana asante kwa kutuburudisha
    Simulizi zako kali sana asante kwa kutuburudisha