Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"Shauri yao bwana kama walichezea masomo, ngoja nikajimwagie maji" Sajenti Minja alijibu huku akinyanyuka na kuondoka ili kuyakwepa maswali ya Mkuu wa polisi, maana yalimpa mashaka na akahisi inawezekana babu wa monchwari alimchoma.
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
Kuanzia hapo akaanza kuishi kwa wasiwasi akihisi kuwa inawezekana kabisa Mkuu wa polisi anawapeleleza wakina Kayoza pasipo wao kujua.
Baada ya Martha kumuhudumia Sajenti Minja, Martha alirudi chumbani kwake, usiku ulikuwa umeshaingia,
"sasa mimi nitatokaje humu?",Martha alipokelewa na swali la Kayoza ambae alikuwa yuko ndani ya kabati,
"subiri bwana, sasa hivi wanaenda kulala, sebule itakuwa haina mtu",Martha alimjibu Kayoza kwa kujiamini,
"Alafu mbona unajiamini sana, we huogopi kuniingiza mwanaume chumbani kwako?" Kayoza aliuliza huku akiwa ana hasira,
"Lazima nijiamini, sasa nimuogope nani wakati nipo kwetu?" Martha alijibu kwa nyodo huku akitandika vizuri kitanda chake,
"Usiwe unajiamini kwa kila kitu, vingine vitakutokea puani, shauri yako" Kayoza aliongea kwa hasira huku akichungulia dirishani,
"Nikuletee chakula?" Martha alimuuliza Kayoza,
"Hapana, sihitaji" Kayoza alijibu huku akionekana amesusa,
"Ukisusa sisi twala" Martha aliongea kwa madaha huku akielekea sebuleni.
Martha alibeba chakula kingi na kwenda kulia chumbani kwake kwa lengo la kula pamoja na Kayoza.
"Njoo rule bwana K, usiwe unasusa Susa kama mtoto wa kike" Martha alimwambia Kayoza huku akimpa kijiko, lakini Kayoza hakutaka hata kujisumbua kupokea, badala yake alikaa tu kitandani huku mkono ukiwa shavuni.
Baada ya masaa mawili, kila mtu aliyekuwa sebuleni alienda kulala, sebule ikabaki tupu.
Ilikuwa ni mishale ya saa nne usiku, katika chumba cha Martha kulikuwa na sauti za mabishano ambazo zilikuwa zinasikika kwa chini chini sana,
"Martha niachie niende, mama atakua na wasiwasi nyumbani",Kayoza alimlalamikia Martha,
"ni vigumu kutoka Kayoza, lazima mlinzi kesho atamwambia baba alafu iwe msala kwako",Martha alijibu akiwa na lengo la kumzuia Kayoza asiondoke ili atimize azma yake ya kufanya nae mapenzi,
"kulala na wewe ni kitu ambacho akiwezekani Martha, kwanza tulikubaliana kuwa watu wakienda kulala ndio unanitoa, ona sasa unaleta sababu nyingine",Kayoza aliongea kwa kulalamika,
"isiwe tabu mwenzangu, wewe lala kitandani mimi nitalala chini",Martha aliongea huku akikunjua godoro jingine alilolitoa juu ya kabati.
"Nani kakwambia anataka kulala hapa?" Kayoza aliuliza kwa jazba,
"Alafu usiongee kwa sauti kubwa, Baba akisikia itakuwa tabu kwako, shauri yako" Martha alimtisha Kayoza,
"Basi nitoe nje niende kwetu" Kayoza aliongea kwa sauti ndogo,
"We lala, ikifika saa saba au saa sita nitakutoa, mlinzi atakuwa amesinzia" Martha alimlaghai Kayoza, ikambidi alale, ila kwa sharti moja, wasilale pamoja, ambapo Martha alikubali na kutandika godoro chini na kitandani alilala Kayoza.
Ilimchukua saa moja tu Kayoza kupata usingizi, akalala fofofo huku akikoroma, saa sita ikafika, ikapita na saa saba ikafika na kupita na sasa ilikuwa saa Tisa usiku,
Martha akakurupuka kutoka katika godoro la chini, taratibu akavua nguo zake zote, kisha akapanda kitandani kwa hadhari ya kutomshtua Kayoza, akaingia ndani ya blanketi, kisha akaanza kufungua zipu ya suruali ya Kayoza,
"mmmh, mbona yuko hivi?",Martha aliguna baada ya kumuona Kayoza kalegea kama mtu aliepoteza fahamu, ila hiyo haikumzuia kuendelea na anachokifanya, akafanikiwa kuishusha suruali ya Kayoza hadi miguuni, sasa akawa anajiweka sawa ili atimize lengo lake, Kayoza aliinuka kama mshale, kwa kasi ya mwanga na meno yake yakapenya sawia katika shingo ya Martha,
"mamaaaaaaaa nakufaaaaaaaaa",sauti ya Martha ilisikika kwa nguvu na kuwaamsha watu wote waliolala mpaka majirani…………..
…Ni kitendo cha dakika tano tu, familia nzima ilikuwa imeuzunguka mlango wa chumba cha Martha,
"we Martha fungua mlango, kuna nini?",Mkuu wa polisi aliita kwa sauti kubwa, lakini hakujibiwa na mtu, na kipindi hicho wale majirani wa karibu na nyumba ya Mkuu wa polisi walikuwa wameshafika kutoa msaada kwa tukio lolote haya ambalo lingetokea.
Aliendelea kuita kwa muda wa dakika tano, lakini hali ilikuwa ile ile.
Ndipo wakashauriana na baadhi ya majirani ambao walikuwa tayari wamefika kutoa msaada, kwa sauti moja wakakubaliana kuvunja mlango.
"Tunaweza kupata kisu au bisibisi?" Jirani mmoja aliuliza baada ya kugundua ule mlango wa kitasa ni mgumu sana, yule bwana aliuliza huku akimuangalia Mkuu wa polisi aliyekuwa ameganda tu,
"We Dada ebu tuletee kisu" Sajenti Minja alimwambia Dada wa kazi ambayo alikuwa jirani nae, kisha yule Dada akakimbilia jikoni haraka na kurudi visu viwili na kumpatia yule bwana jirani aliyeagiza hicho kifaa.
Kisha kwa kushirikiana watu wengine waliopo ple wakafanikisha zoezi lao la kutegua kitasa cha mlango na mlango ukafunguka.
Sasa walichokiona mbele yao ndicho kilikuwa kitu cha ajabu sana kilichopelekea mke wa Mkuu wa Polisi kupoteza fahamu pale pale.
Mkuu wa polisi yeye aliangalia mara moja tu, kisha akatoka nje huku macho yake yakiwa yametawaliwa na machozi, baadhi ya majirani wakaenda kumfariji na wengine wenye roho ngumu walichukua shuka lililokuwepo juu ya kitanda na kuusitiri mwili.
Ulikuwa mwili wa Martha ukiwa na chupi tu mwilini, ulikuwa umelala juu ya kitanda, na damu zikiwa zimemuenea shingoni zikiwa zimechirizika kwenda sakafuni, alikuwa tayari ni mfu, tayari mwili umetengana na roho kutokana na tamaa zake za mwili.
"Ni nini kimemkuta?" Jirani mmoja alimuuliza Sajenti Minja,
"Sasa Mimi nitajuaje ndugu yangu wakati mlango tumevunja wote na kuukuta mwili umelala?" Sajenti Minja alijibu huku moyoni mwake akiwa na mawazo ya kuwa inawezekana Kayoza ndiyo aliyefanya hill tukio.
Sajenti Minja aliamini hivyo baada ya kuona sehemu ya dirishani kulikuwepo na vioo vilivyopasuka, pamoja na nondo kadhaa kuondolewa, akakumbuka Kayoza alishawahi kuondoka kwa mtindo huo kipindi cha nyuma alipojaribu kumtegea askari ndani ya lodge kipindi anaanza kuipeleleza hii kesi ya Kayoza mjini Dodoma.
"Sasa kama ametoka akiwa kama mzimu si ataenda kupoteza fahamu maeneo ya jirani tu? Nitoke nikamuangalie nini? Nikitoka pia watu wa hapa si watanishangaa?, bora nibaki tu hapa hapa huku nikiomba Mungu amfikishe salama nyumbani" Sajenti Minja aliongea peke yake huku akielekea sebuleni alipokaa Mkuu wa polisi na majirani wengine waliokuwa wanamfariji.
Ila hakuridhika kukaa tu pale, kuna fikra zilimjia. Akanyanyuka taratibu na kuelekea nje ya nyumba lakini ndani ya geti. Akamtafuta mlinzi na kumkuta akiwa amekaa kimajonzi sana,
"Ni kitu kimefanya tukio hili?" Sajenti Minja alimuuliza mlinzi kwa ajili ya kutaka kujua kama ni kweli Kayoza alikuja hapo,
"Nashindwa hata kueleza, ila nimekiona kiumbe cha ajabu sana kikitokea chumbani kwa Martha, sijui ni nini lile" Mlinzi aliongea huku akiwa anasimumuka mwili,
"Kuna nani aliingia leo kipindi tumetoka?" Sajenti Minja alimuuliza tena huku akitaka kujua kama mlinzi atamtaja Kayoza ingawa tayari Sajenti Minja alishagundua kuwa yale mauaji yamefanywa na Kayoza, sasa hapo alitaka kujua kama Mlinzi anaweza kumtaja Kayoza ndio pekee aliyeingia kipindi hawapo au kuna wengine,
"Aliingia yule mjomba wako mpole mpole" Mlinzi alijibu na kumfanya Sajenti Minja aone hatari iliyopo mbele yao, maana kama Mkuu wa polisi akimbana mlinzi kuhusu watu waliokuja siku hiyo, basi lazima atajwe Kayoza,
"Huyo tupo nae ndani mbona, hakuna mwingine aliyekuja zaidi ya huyo?" Sajenti Minja alizuga ili kumfanya mlinzi asimuhisi vibaya Kayoza,
"Leo hakuna zaidi ya huyo" Mlinzi alijibu na kumfanya Sajenti Minja ahisi hatari kubwa iliyopo mbele yao,
"Sasa ndugu yangu, kwa usalama wako, ni bora tu ukimbie, kwa maana hii kesi unaangushiwa wewe, nimemsikia boss wako ndani akisema hivyo" Sajenti Minja aliongea baada ya kufikiria kwa muda, alifanya hivyo ili kumtisha mlinzi akimbie ili ushahidi wa Kayoza kuingia ndani kwa Mkuu wa polisi ufutike,
"Lakini Mimi sijaua, kwanini nikamatwe?" Mlinzi aliuliza huku akitetemeka,
"Haukamatwi kwa kuua, utakamatwa kwa uzembe wa kumuachia huyo muuaji apite" Sajenti Minja alizidi kumtisha mlinzi,
"Lakini utakuwa uonevu huo" Mlinzi alilalamika huku akitaka kulia,
"Acha ujinga, ni bora tu ukimbie kabla hujatiwa mikononi mpwa polisi, mpaka wake kujua wewe hujaua, itakuwa umeshakuwa mlemavu tayari kwa ajili ya mateso utakayopata" Sajenti Minja alizidi kumtisha mlinzi,
"Dah, sasa utanisaidiaje?" Mlinzi aliuliza baada ya kufikiria kwa muda,
"We mpumbavu nini, nikupe msaada gani zaidi ya huu niliokupa sasa hivi?" Sajenti Minja aliuliza huku akijifanya ana hasira,
"Takimbilia Wapi na sina hata pesa ya nauli?" Mlinzi aliuliza,
"Wewe mwanaume mwenzangu, nakusaidia huku nikiamini hata Mimi naweza kupata tatizo na wewe ndio unaweza kuna kuwa msaada" Sajenti Minja aliongea huku akiingiza mkono mfukoni na kutoa noti nyingi nyingi zilizokaa bila mpangilio na kumpatia mlinzi,
"Dah, asante sana" Mlinzi alipokea na kuzitia mfukoni,
"Sasa usikimbie hivyo kama Mbwa, hapa unatakiwa utoke kama unaenda kujisaidia nyuma ya nyumba, ukifika tu nje ya geti ndio uanze riadha" Sajenti Minja alimwambia mlinzi ambayo aliishia kujibu kwa kichwa tu, kisha akafanya kama alivyoelekezwa na Sajenti Minja na kutokomea nje ya geti na kumuacha Sajenti Minja akisikitika kwa mengi, kwanza kumpotezea hajira huyo mlinzi, pili kumpoteza Martha, msichana mdogo aliyekuwa mchangafu na waliyezoena kwa Siku chache tu, na tatu ni Kayoza.
Majirani wengine wa mkuu wa polisi wakatoa taharifa polisi na hospitali,
gari ya wagonjwa ikaenda usiku ule ule kuuchukua mwili wa Martha.
Ambulance haikuchukua muda sana barabarani ilifika haraka sana nyumbani kwa Mkuu wa polisi, nadhani na cheo alichonacho kilichangia gari hiyo kuwahi kufika na sababu ya pili ni kutokana na kutokuwepo na magari mengi barabarani usiku ule.
Gari ya hospitali ilipofika, mwili wa Martha ulibebwa juu juu na kuingizwa ndani ya gari, kisha gari ikaondoshwa kwa kasi sana, utasema ndani amelazwa mgonjwa ambayo anahitaji matibabu ya haraka, kumbe amelazwa maiti ambayo hata useme ukimbize gari mpaka iruke hewani kama ndege lakini bado hutoweza kuurudisha uhai wake.
Ambulance ilikuwa inasindikizwa na gari mbili za polisi, moja walikaa askari wa kawaida wapatao sita, na nyingine alikuwepo Sajenti Minja na askari wawili, ila Sajenti Minja hapa alisimama kama mwanafamilia na wala hakuwa polisi.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi