Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA THELATHINI NA SABA
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
"Mk….juu …wa…pol…isi" Omary aliongea kauli ambayo watu wengine hawakuielewa isipokuwa Sajenti Minja pekee.
Omary baada ya kutamka maneno hayo, shingo yake ililegea na kuanguka, huo ndio ukawa mwisho wa maisha ya Omary, roho yake ikatengana na mwili akiwa ugenini, kauli ya babu yake ikatimia…..
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
..maneno aliyoyatamka Omari, watu wote ambao walikuwa jirani nae akuna hata alielewa alichokimaanisha, Sajenti Minja peke yake ndiye aliyekuwa anaelewa kinachoendelea,
Sajenti Minja alipogundua Omari amekufa, alilia sana. Na Kayoza ndio alichanganyikiwa zaidi, kwa maana alipata mapigo mawili kwa Mara moja, la kwanza ni kifo cha rafiki yake aliyetoka nae mbali toka mwanzo wa matatizo mpaka walipofikia, na pigo la pili ni kifo cha bibi yake ambaye ndio alikuwa msaada pekee wa kumsaidia mzimu umuachie.
Sasa ikawa misiba miwili ndani ya nyumba moja.
Misiba iliyoletwa na mkuu wa polisi, mmoja aliudhamilia ila mwingine hakuhudhamilia ila umetokea tu pasipo kutegemea na aliyesababisha hiyo misiba hana habari kama kitendo chake kimemuondoa mtu ambaye hausiki kabisa katika mipango yake.
Na jambo vzuri ni kwamba hakuna aliyemuona mkuu wa polisi wakati akifanya tukio hilo isipokuwa Omary pekee ambaye nae ameshamtaja aliyemuua.
Wanandugu walikaa na Sajenti Minja, na mwisho wakakubaliana kuwa Omari azikwe pale pale ili kuepusha gharama. Lakini Sajenti Minja alipinga na kusema yeye atagharamia kila kitu kuhusu mwili wa Omary, na alichofanya ni kuwasiliana na wazazi wa Omary na kisha ndugu wa Omary walifika Bukoba na wakauona mwili wa ndugu na wenye kulia wakalia.
Baada ya hapo ndugu hao waliondoka na mwili wa ndugu yako na kwenda nao Tanga kwa ajili ya maziko.
Huku kwa Bibi Kayozs Wakafanya maziko ya Bibi yake Kayoza.
Walifanya maziko ya heshima kwa bibi Kayoza kwa maana yeye nae alikuwa make wa chief ambaye ndiye Babu yake Kayoza ambaye ndiye inaesemekana ndio huo mzimu aliokuwa nao Kayoza.
Msiba ulipoisha, Sajenti Minja alimuita Kayoza na kumuweka kitako,
"yaliyotokea nafikiri umeyaona, ni kama ajali kazini na hakuna jinsi zaidi ya kujipanga upya, maana bibi yako tuliekuwa tunamtegemea kuwa msaada kwako, amekufa, na Omari nae amekufa",Sajenti Minja alimwambia Kayoza ambae muda wote alikuwa amekaa kimya,
"kwani huyo aliyempiga risasi Omari ulimuona?",Kayoza akamuuliza Sajenti Minja,
"sikumuona na wala sikubahatika kuongea na Omari, ila neno la mwisho aliloniambia ni MKUU WA POLISI",Sajenti Minja alimfahamisha Kayoza,
"ina maana Mkuu wa Polisi ndiye aliempiga risasi?",Kayoza akahoji,
"mimi ndio nimeelewa hivyo, na niliwaambia kuwa nilimuona Mkuu wa Polisi, nyie mkabisha, haya ndio matokeo yake sasa",Sajenti Minja aliongea kwa uchungu,
"nafikiri atakuwa bado hajaondoka pale Guest, na naimani ataondoka maiti",Kayoza aliongea huku akiwa anaondoka, hiyo kauli ikamshtua Sajenti Minja,
"njoo, unakwenda wapi?",Sajenti Minja alimzuia Kayoza,
"nipo hapa hapa",Kayoza alijibu huku akiwa amesimama mlangoni,
"sasa mbona unaondoka huku tukiwa bado hatujafikia muafaka?",Sajenti Minja alimuuliza Kayoza,
"muafaka gani tena?",Kayoza aliuliza kwa jazba,
"ya yaliyotokea na hatua za kuchukua",Sajenti Minja aliongea kwa kubembeleza,
"wewe uliniambia imetokea kama ajali na muafaka ulioniambia ni kujipanga upya, ila kwa kuwa huyu Mkuu wa Polisi amefanya ujinga kama kulipa kisasi kwa binti yake, ila akamuua Omari ambae hausiki na kifo cha binti yake, pia amesabisha zoezi la kutolewa mdudu mwilini kwangu lishindikane, basi adhabu anayostahili ni kifo, tena nitamuua nikiwa mzima kabisa, tena kwa mikono yangu miwili",Kayoza aliongea huku machozi yakimtoka, moja kwa moja akaamua kuenda nje kwa kuwa aliona kuendelea kuogelea hilo jambo ni kujiongezea hasira tu,
"hapa nisipokuwa makini, naweza kumpoteza na huyu Kayoza",Sajenti Minja aliongea huku akijilaza katika kajitanda cha pale chumbani.
"Mkuu wa polisi anachofanya ni kisasi, kama amemuua Omary, basi na Kayoza nae anahitajika kuuwawa, sio Kayoza peke yake, hata Mimi ni mmoja kati ya watu wanaowindwa na mkuu wa polisi, sasa sijui yupo peke yake au amekuja na watu wengine wa kumsaidia? Hii ni vita, tena vita ambayo tunapigana na adui aliye na silaha, cha muhimu ni kuwa makini, au tuondoke tu huku kwa maana hatuna cha kufanya tena, kilichotuleta kimeshindikana" Sajenti Minja alikuwa anawaza
**"*
Mkuu wa Polisi aliamini kwa asilimia zote kuwa, pale alipofikia, hakuna aliegundua kati ya wakina Sajenti Minja.
"nimeanza na yule kibaraka, alafu anafata yule mshenzi Minja, Yuda Eskarioti, anaisaliti serikali?",Mkuu wa Polisi alijiuliza mwenyewe huku akijimiminia mzinga wa konyagi katika glass ndogo iliyokuwepo juu ya meza katika chumba chake.
"Hivi kwanini nilivyogonga mlango asingekuja Minja kufungua? angeanza yeye kufa kazi ingekuwa rahisi sana. Ila hata hivyo sawa tu, kwa maana wanapambana na adui wasiyemtambua, hata atumie mbinu zake za kijeshi sijui, hawezi kunijua" Mkuu wa polisi aliongea kisha akatoa cheko kubwa sana alilolishushia na tusi la nguoni kumuelekea Sajenti Minja kisha akagida tena ile konyagi iliyokuwa katika glass yake ndogo iliyopo juu ya meza.
"Alafu hii kazi imekuwa rahisi sana, kumbe naweza kuimaliza mapema kuliko hata nilivyodhani?, inawezekana, inawezekana kabisa, nataka Sikh ninayorudi shinyanga, nirudi nikiwa sina kisasi na mtu, nirudi nikaanze upya katika maisha yangu. Hivi utajisikiaje unapobahatika kupata mtoto mmoja, tena kwa tabu sana na miaka Mingi sana sana ya kusubiri huku ukivumilia maneno mengi sana kutoka katika jamii iliyokuzunguka?, alafu anatokea mpumbavu mmoja na kumuua huyo mtoto, ni lazima uchanganyikiwe, ni lazima uone dunia inakuelemea, dah jamani Martha wangu, my martha, baba yako nipo kwa ajili ya kukulipia kisasi, damu yako haijapotea bure mwanangu" Mkuu wa polisi aliongea huku akiwa anaiangalia picha ya Martha iliyokuwa katika simu yake ya mkononi.
Siku hiyo aliifanya kama sherehe kwake, maana alikuwa anakunywa tu, huku alitaja sana jina la Sajenti Joel Minja.
Saa moja baadae akawa hajitambui wala hajielewi, alizima huku akiwa amekaa katika kochi la chumba cha Guest.
"Hivi si naweza tu kummaliza huyu mtu, mbona hanishindi kabisa, au nitakuwa namuonea? Lakini mbona na yeye amemuonea Omary, Omary hana hatia, Omary alipaswa kufa kwa mipango ya Mungu na wala hakupaswa kufa kinyama namna hii tena ugenini. Ni vipi wazazi wake watajisikia? Haiwezekani kwa kweli, hii kitu kuivumilia ni sawa na kuacha matatizo yaendelee ingali una ufumbuzi wa kufumbua kinachokukabili" Sajenti Minja alikuwa akifikiri huku macho yake yakiangalia juu ambapo kulikuwa na paa ya nyumba ambayo ilijaa uchakavu kiasi.
Sajenti Minja baada ya kufikiria sana, akaamua kwenda katika Guest aliyofikia Mkuu wa Polisi, akupata tabu kuingia ndani, akaenda mpaka ulipo mlango wa chumba alichofikia Mkuu wa Polisi, kwa taratibu na tahadhali kubwa, huku akiwa ameweka chupa ya soda katika mfuko wake wa suruali, kwa ajili ya kummaliza Mkuu wa Polisi.
Tayari roho ya kinyama ilikuwa imefunika damu ya Sajenti Minja, roho iliyokuwa na imani ya kuwa njia nzuri ya kujilinda ni kumuua adui unayepambana nae.
Sajenti Minja ameamua kuua na hakutaka kwenda na bastola bali ameona silaha inayomtosha ni chupa ya soda tu.
Akashika kitasa cha mlango, kisha akaminya kwa chini…
..mlango haukufunguka,
"amejifungia kwa ndani huyu",Sajenti Minja aliongea peke yake.
Kisha akainamisha jicho lake mpaka kwenye tundu la ufunguo, pia hakuweza kumuona kwa ajili ya ufunguo uliokuwepo pale.
Sajenti akaamua kuahirisha hazma yake, akatoka nje na kuelekea nyumbani.
Kayoza muda wote alikuwa na mawazo tu, alikuwa hataki kuongea na yeyote zaidi ya Sajenti Minja. Nyele alikuwa hachani, mafuta hapaki, nguo moja aliweza kuvaa hata wiki, hakuwa mtanashati tena kama zamani, wageni wa eneo lile walikuwa wanamuona kama mvuta bangi.
"vipi anko?",Kayoza alishtuliwa na sauti ya Sajenti Minja,
"safi, ulikuwa wapi?, maana sijakuona muda mrefu kidogo",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,
"nilienda pale hotelini kumchunguza huyo bwana mkubwa",Sajenti Minja aliongea huku akikaa chini,
"umefanikiwa?",Kayoza akauliza kwa ufupi,
"nilifika pale hotelini, ila yeye alikuwa ndani na mlango alikuwa ameufunga kwa ndani",Sajenti Minja alimjibu Kayoza,
"kumbe ulitaka kuingia mpaka ndani!?",Kayoza akauliza kwa mshtuko,
"ndio",Sajenti Minja akajibu kwa kifupi,
"sasa ungefanikiwa kuingia ndani ungemfanya nini?",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,
"unaona hii chupa, ndio ingekuja kutoa ushaidi wa chochote ambacho ningemfanyia",Sajenti Minja alijibu huku akimuonyesha Kayoza chupa ya soda,
"na afadhali hukufanikiwa",Kayoza akaongea huku akikwepesha macho yake yasigongane na Sajenti Minja,
"alah!, kwanini!?"Sajenti Minja akahoji,
"nilishakuambia kuwa yule nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe",Kayoza alijibu akiwa anaelekea ndani,
"mh, hii kasheshe",Sajenti Minja alijisemea peke yake.
Jioni ya siku hiyo, pale kwa bibi yake Kayoza kulikuwa na shughuli ya kutoa ng'ombe ambao ni wagonjwa, ili kesho alfajili wapelekwe mnadani, hiyo kazi ilifanywa na vijana wa pale, wakiwemo Kayoza na Sajenti Minja.
Mkuu wa Polisi baada ya kuzinduka, akaenda kuoga kisha akaenda kuagiza chakula, baada ya kula akaingia chumbani kwake, kisha akaibeba bastola yake na kuelekea walipofikia wakina Sajenti Minja, giza lilikuwa limeshachukuwa nafasi yake,
"afadhali wako nje",Mkuu wa Polisi alisema, baada ya kuona watu ndani ya zizi la ng'ombe.
Akaenda sehemu ambayo imejificha na pia karibu na zizi waliokuwemo wakina Kayoza, akatoa bastola yake na kumuweka Sajenti Minja katika shabaha yake, aliweza kumtambua kutokana na taa ya chemri ambayo Sajenti Minja alikuwa kainyanyua juu usawa wa kichwa chake kwa ajili ya kuwamulikia wenzake.
Mkuu wa Polisi akaikamata vizuri bastola yake,
"ukalale mahali pabaya motoni Minja, usaliti ndio umekuponza, moja..mbili…tatu",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti ndogo, kisha akahesabu na kufyatua risasi kumuelekea Sajenti Minja
…ukafuata mlio mkali ulioambatana na risasi, kisha kwa macho yake, Mkuu wa Polisi akashuhudia giza limetanda ndani ya zizi la ng'ombe alilokuwamo Sajenti Minja, huku kukifatiwa na kelele za watu, na wengi wao walikuwa wakionekana wanakimbia huku wakitoka ndani ya zizi la ng'ombe na tena wakiomba msaada.
Kuona hivyo, Mkuu wa Polisi akaondoka katika lile eneo taratibu bila kuonekana na mtu, hata kama ungekutana nae njiani usingedhani kuwa ule mlio wa bastola uliosikika muda muchache uliopita ni yeye ndiye aliyefyatua, kwa maana nae alikuwa anakimbia hivyo kama watu wengine wa eneo lile walioshtuliwa na mlio wa risasi.
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi