Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Kuona hivyo, Mkuu wa Polisi akaondoka katika lile eneo taratibu bila kuonekana na mtu, hata kama ungekutana nae njiani usingedhani kuwa ule mlio wa bastola uliosikika muda muchache uliopita ni yeye ndiye aliyefyatua, kwa maana nae alikuwa anakimbia hivyo kama watu wengine wa eneo lile walioshtuliwa na mlio wa risasi.
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
Alijitahidi kukimbia kwa dakika mbili kisha akaanza kutembea mwendo wa kawaida, ni baada ya kuiacha kwa mbali nyumba aliyoifanyia tukio muda mchache uliopita.
"asante Mungu, sasa nimebakiza kazi ndogo tu, kumuua yule anaejifanya shetani",Mkuu wa Polisi aliongea huku akiwasha sigara yake na kuvuta funda moja kisha apuliza taratibu na kuuangalia moshi uliokuwa unaelekea juu,
"Kama sinema vile au hadithi ya kisasi kwa jinsi ninavyofanya matukio yangu, au kama Rambo anavyowamaliza wavietnam" Mkuu wa polisi aliongea peke yake na kisha akatoa tabasamu moja haya sana.
Alikuwa kama hajitambui ni mtu wa aina gani? mtu anayeua na kufurahi hii inaonesha sio mzika, ila yeye hakujali wala hakufikiria hilo, baada ya kufanya tukio hilo la kinyama, alichokuwa akikiwaza muda huu ni pombe tu, tena alizidisha hatua zake za kutembea ili awahi kufika hotelini akanywe pombe, koo lilikuwa limemkauka.
Baada ya Mkuu wa Polisi kufyatua risasi, ile risasi ilichomoka moja kwa moja na kulenga taa ambayo ilikuwa imeshikiliwa na Sajenti Minja usawa wa uso wake, risasi ikapasua kioo cha chemri na kusababisha baadhi ya vipande vya chupa kuingia kwenye macho ya Sajenti Minja hali ambayo ilisababisha maumivu makubwa sana machoni kwa Sajenti Minja, ila hakutaka kupiga kelele kwa kuhofia adui akimsikia amepiga kelele anaweza kusogea na kummalizia kabisa.
Sajenti Minja aliamua kutulia chini kimya kama amekufa huku maumivu akiyavumilia.
Baada ya muda mchache eneo lile lililokuwa na vurugu zilizotokana na mlio wa risasi lilitulia, ndipo wajomba zake Kayoza walipokuja sehemu aliyolala Sajenti Minja.
"Mjomba upo salama?" Kayoza alimuuliza baada ya kumuona akijigeuza,
"Nahisi nipo salama, ila macho yanauma sana, sijui kama yamesalimika" Sajenti Minja aliongea huku mikono yake ikiwa imeziba macho yake,
"Ebu toa mikono nikuangalie" Kayoza alimwambia mjomba wake,
"Hapana, bora nikishika hivi nasikia nafuu kidogo. Nipelekeni hospitali" Sajenti Minja aliongea,
Wakina Kayoza wakambeba Sajenti Minja ambae alikuwa anaugulia maumivu na kumkimbiza ndani,
"mjomba uko salama?",Kayoza alirudia tena kumuuliza Sajenti Minja,
"macho, macho yangu jamani, naomba mniwaishe hospitali",Sajenti Minja alijibu katika sauti iliyoashiria anataka kulia,
Bila kupoteza muda, wanaume wawili wakambeba juu juu na kumpeleka nje ambapo walienda barabarani na kukodi gari iliyompeleka hospitali.
Walipofika hospitali, wakapokelewa na wauguzi na kupelekwa katika chumba cha Daktari, ambae alimuangalia kwa dakika kumi, na kuwaambia wauguzi wampeleke theatre.
Baada ya Sajenti Minja kuingizwa katika chumba hicho, waliingia madaktari wapatao watano kwa ajili ya kumfanyia upasuaji mdogo wa macho Sajenti Minja,
"Vipi mgonjwa, ilikuwaje kuwaje mpaka ikawa hivyo?" Daktari mmoja alimuuliza Sajenti Minja aliyekuwa amelazwa kitandani,
"Hata sijui, sisi tulikuwa tunatoa mifugo zizini ndio tukasikia mlio wa risasi ghafla na inaelekea ilipiga taa niliyoibeba na vipande vyake vilinirukia machoni" Sajenti Minja alizungumza,
"Mlipitia polisi kuchukua PF3?" Daktari aliuliza,
"Uko ni kupoteza muda, kwa hiyo ningeendelea kupata maumivu kiss PF3?" Sajenti Minja aliuliza,
"Lakini ndio utaratibu huo, bila PF3 hakuna matibabu" Daktari aliendelea kutoa maneno yaliyomchukiza Sajenti Minja,
"Hata mimi ni polisi, kama hamtaki kunitibu niambieni" Sajenti aliongea kwa hasira huku akiingiza mkono mfukoni na kutoa kitambulisho chake,
"Tufanye kazi jamani, tuache malumbano" Daktari mwingine wa kike alizungumza huku akivaa mipira (gloves) mikononi,
"Mwenzako sio muelewa" Sajenti Minja aliongea,
"Mgonjwa nawe mtata sana, haya jiandae nakuchoma nusu kaputi" Daktari wa kike aliongea kisha akamchoma sindano Sajenti Minja na kisha Sajenti Minja akapoteza fahamu, matibabu yakaanza sasa usiku huo huo.
Mkuu wa Polisi alirudi katika guest aliyofikia, kisha akaoga vizuri, akaagiza konyagi, alafu akajifungia ndani kujipongeza kwa kazi aliyofanya.
Kama kawaida yake alikuwa anakunywa huku akitukana matusi kumuelekea Sajenti Minja, na safari hii kabla hajaweka jina Sajenti Minja, alikuwa anaanza na neno marehemu Sajenti Minja, kwa maana alikuwa anaamini amemuua kwa ile risasi moja aliyomlenga, hakujua kama imemkosa.
Baada ya kunywa pombe nyingi, Mkuu wa polisi alilala pale pale kwenye kochi kama kawaida yake, hii ni siku ya tatu hakijui kitanda.
Siku iliyofuatia, majira ya saa nne za asubuhi, Mkuu wa Polisi aliamua apitie katika maeneo ya karibu na nyumba waliyofikia wakina Kayoza kwa ajili ya kuangalia hali ilivyo, lakini alichotarajia kukiona hakukikuta, alitegemea kukuta msiba pale lakini akakuta hali ya kawaida ila kulikuwa na watu ambao walikuwa wamejitenga mafungu mafungu kuzungumzia tukio la siku iliyopita.
"kuna nini kijana, mbona mko kimafungu mafungu hivyo?",Mkuu wa Polisi alimuuliza kinafiki kijana ambae alikuwa jirani na yeye,
"ina maana hujui kilichotokea, au wewe mgeni hapa?",yule Kijana alihoji badala ya kujibu,
"sasa ningejua ningeuliza?, vijana wa Sikh hizi sijui mkoje?",Mkuu wa Polisi akarudishia swali,
"ni hivi mzee wangu, jana kuna mtu kapigwa risasi hapa ila kwa bahati nzuri hajafa, na wiki kadhaa zilizopita kuna mtu katika nyumba ile ile alipigwa risasi na kufa papo hapo",yule Kijana alimueleza Mkuu wa Polisi,
"umesema aliyepigwa risasi hajafa!?",Mkuu wa Polisi aliuliza kwa mshangao,
"ndio, kwani vipi mzee?",yule Kijana aliushangaa mshangao wa Mkuu wa Polisi,
"Hiyo risasi alipigwa wapi mpaka asife?, maana risasi sio kitu cha mchezo" Mkuu wa polisi alihoji huku akiwa ahamini kama ile risasi aliyopiga imemkosa Sajenti Minja,
"Nasikia haijampata, ila ilipiga taa ambayo alikuwa ameibeba" Kijana alijibu na kumfanya Mkuu wa polisi akunje Sura kwa kusikia kuwa ile risasi ilimkosa Sajenti Minja,
"Huu ujinga huu" Mkuu wa polisi aliongea kwa hasira na kujisahau kama na mtu mwingine,
"Kwani vipi mzee?" Kijana aliuliza huku akishangaa hali aliyokuwa nayo Mkuu wa polisi,
"hakuna kitu kijana, kwa hiyo kapelekwa hospitali?",Mkuu wa Polisi alihoji,
"ndio, kapelekwa hospitali ya mkoa",yule Kijana alijibu.
Mkuu wa Polisi akutaka hata kuaga, akageuka na kurudi guest,
"mh!, yule mbwa ana bahati gani?, hapana, lazima nikammalizie pale pale hospitalini",Mkuu wa Polisi aliongea kimoyo moyo, kisha akachukua bastola yake na safari ya kuelekea hospitali ikaanza.
Alipofika hospitalini, hakujua Sajenti Minja amelazwa wodi namba ngapi, ila baada ya kuuliza uliza kwa madaktari alifanikiwa kufika katika wodi aliyokuwepo Sajenti Minja, akaingia ndani ambapo alimkuta Sajenti Minja peke yake huku katika macho yake kukiwa na bandeji zilizomzuia kuona, alifungwa bandeji kubwa machoni make kutoka na upasuaji mdogo aliofanyiwa.
Mkuu wa Polisi aliingia ndani ya wodi na kisha akaanza kumsogelea taratibu Sajenti Minja, alipomfikia, akaichomoa bastola yake, kisha akawa anajitayarisha kummaliza Sajenti Minja, tena alidhamiria kabisa, hata sura na macho yalionesha hivyo…..
..mara mlango wa wodi ukafunguliwa, alikuwa ni Daktari, Daktari alishtuka sana baada ya kumkuta Mkuu wa Polisi kashika bastola, Mkuu wa Polisi aliliona hilo, akawai kutoa kitambulisho,
"alah, kumbe ni polisi, nimekuja kumpa huduma mara moja kwa hiyo nakuomba ukae nje kidogo",Daktari aliongea huku akitabasamu,
Mkuu wa Polisi akatoka nje bila hata kuongea neno huku akishukuru kwa daktari kutokujua kitu chochote na pia alilaani kwa daktari kuingia ghafla kwa maana alimuaribia mpango wake.
"polisi yuko wapi?",Sajenti Minja alihoji baada ya kusikia daktari akiongea na mtu aliyejitambulisha kuwa ni polisi,
"si mlikuwa nae hapa ndani",Daktari akajibu huku akimshangaa Sajenti Minja,
"hapana, hakuna aliengia na kuniambia yeye ni polisi",Sajenti Minja aliongea kwa mkazo huku akimbishia Daktari,
"Unachoongea ni kweli au unatania, kwa hiyo wewe unasema hujamuona!?",Daktari aliuliza kwa mshangao,
"amini nilichokuambia, huyo polisi yukoje, na umejuaje kuwa ni polisi?",Sajenti Minja aliendelea kuhoji,
"umri wake kati ya miaka 45 mpaka 50, alikuwa kashika bastola, aliponiona alinionesha kitambulisho ambacho kinaonesha ni polisi wa shinyanga",Daktari alieleza kwa urefu,
"umesema wa shinyanga!?",Sajenti Minja alihoji kwa mshangao,
"ndio, vipi unamjua?",Daktari aliuliza,
"mhm, hapana",Sajenti Minja alijibu lakini mawazo yake yote akayahamishia kwa Mkuu wa Polisi,
"ina maana amejua niko hospitali na amenifuata na bastola ili animalize?",Sajenti Minja aliongea kwa fikra.
"Au ana mpango gani na mimi? Nani amemwambia nipo hapa? Huyu mzee ni hatari aisee" Sajenti Minja aliendelea kuwaza,
"Mheshimiwa mimi natoka, nilikuja kukubadilishia drip tu" Daktari aliongea na kumfanya Sajenti Minja Stoke mawazoni,
"Jamani kuweni makini na watu wanaoingia humu, sasa kama huyo uliyesema amekuja na bastola hata simjui, angalieni wasije wakanidhuru" Sajenti Minja aliongea kwa kulalamika kwa maana yoga ulimuingia tayari,
"Sasa sisi hatuwezi kuzuia mtu, tunajua wote ni ndugu zako" Daktari alijibu Sajenti Minja,
"Nyie ndugu zangu si mnawajua, kwanza msimruhusu mtu yoyote kuingia humu mpaka awepo yule kijana mwenye nywele nyingi zisizochanwa" Sajenti Minja aliongea huku akimaanisha ni Kayoza,
"Lakini hata wewe si ni polisi?, hata huyu aliyeingia nae ni polisi mwenzako" Daktari alimwambia Sajenti Minja,
"Atakuwa sio polisi, usikute amegushi tu kitambulisho, msimruhusu tena" Sajenti Minja aliongea,
"Inaelekea una maadui wengi sana bosi" Daktari aliongea,
"Fuata nilichokuambia, sitaki maneno mengi" Sajenti Minja aliongea huku zile bandeji zikiwa bado katika macho yake,
"Sawa bosi, lakini kumbuka huwezi kuna alafu unaniletea ubabe" Daktari aliongea kwa utani huku akiondoka,
"Kwa kuwa sioni ndio mumuingize kila mtu humu ndani?" Sajenti Minja aliuliza lakini hakuna aliyemjibu, Daktari alikuwa ameshatoka ndani kitambooo.
Baadae wakina Kayoza walipofika, Sajenti Minja alimsimulia Kayoza kila kitu, Kayoza alishtuka, na kuahidi hatoondoka katika eneo la hospitalini mpaka Sajenti Minja apone.
"Sasa wewe ukikaa hapa muda wote ni Mani ataniletea chakula?" Sajenti Minja alimuuliza Kayoza,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi