Mwandishi: Alex Kileo
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Baadae wakina Kayoza walipofika, Sajenti Minja alimsimulia Kayoza kila kitu, Kayoza alishtuka, na kuahidi hatoondoka katika eneo la hospitalini mpaka Sajenti Minja apone.
"Sasa wewe ukikaa hapa muda wote ni Mani ataniletea chakula?" Sajenti Minja alimuuliza Kayoza,
KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO
SASA TUENDELEE...
"Sasa unadhani ni nini kifanyike kukulinda kipindi hiki ambacho una bandeji machoni?" Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,
"Mi nadhani tumtafute mtu awe analeta chakula, alafu wewe ushinde hapa mpaka usiku alafu unaondoka" Sajenti Minja alimwambia Kayoza,
"Sio kushinda tu, itanibidi nilale kabisa" Kayoza aliongea,.
"Kulala na mgonjwa hawaruhusu" Sajenti Minja alimwambia Kayoza,
"Itabidi waruhusu tu, kwa maana hawajaweka ulinzi wa kutosha" Kayoza aliongea huku hasira zikianza kumtawala,
"Muda mwingine kuvunja sheria za mahali penye uongozi wake, unaweza kujitafutia matatizo, ni bora ufanye kama nilivyokuagiza" Sajenti Minja alimwambia Kayoza ambaye hakutaka kuendelea na mabishano badala yake alikitoa kwenye kikapu chakula walichomletea Sajenti Minja,
"Hicho chakula mbona kinanukia vizuri, inaelekea kitakuwa kitamu sana" Sajenti Minja aliongea baada ya kusikia harufu ya chakula.
"We ongea yote, ila usiku wa leo itanibidi niwe eneo hili" Kayoza aliongea kisha akatoka nje kwenda kununua maji na kumuacha Sajenti Minja akiongea mwenyewe
Mkuu wa Polisi baada ya kushindwa kufanikisha azma yake, alirejea katika Guest aliyofikia na kujipanga upya, baada ya kupita pita katika kichaka cha fikra zake, akaamua kuwa usiku lazima arudi kule hospitalini.
Nae alishajua inawezekana asubuhi ile alishtukiwa baada ya kuondoka, na yeye sasa akaongeza akili za ziada ili usiku aweze kufanikisha lengo lake, na ilimbidi siku hiyo asiguse hata pombe kabisa. Chakula alichokula Sikh hiyo ni matunda tu, ndio alliamini kufanya hivyo kutaifanya akili yake ifanye kazi vizuri.
Baada ya kula alipumzika nusu saa kisha akaenda kuoga, alipotoka kuoga alipanda kitandani na kulala ili kujiandaa na misheni aliliyopo mbele yake. Kumbuka hapo ilikuwa ni saa name mchana.
Aliamka saa mbili usiku na kwenda kuoga tena, kisha akavaa nguo zake za mazoezi na raba nyeusi, kisha akaichukua bastola yake na kuifanyia ukaguzi kidogo na kisha aliipachika kibindoni, alafu akachukua kisu kidogo kiasi na kukitia mfukoni kisha akanywa maji mengi sana na kushusha pumzi ndefu,
"Mwenyezi Mungu naomba unilinde kwa kila hatua ninayopiga" Mkuu wa polisi aliongea na kutoka chumbani kwake na kuelekea nje.
Safari ya hospitali ilikuwa inaanza sasa.
Usiku wa saa tano na dakika zake, mkuu wa Polisi alikuwa katika maeneo ya hospitali, akajipenyeza mpaka mahali ilipo wodi aliyolazwa Sajenti Minja, kipindi hicho chote Kayoza alikuwa anamuona, Kayoza nae akawa anafuata kila hatua iliyokuwa inafanywa na Mkuu wa Polisi.
Mkuu wa polisi alifanikiwa kupenya penya na mpaka kuingia katika wodi aliyolazwa Sajenti Minja.
Mkuu wa Polisi baada ya kuingia katika wodi aliyolazwa Sajenti Minja, aliingia kisha akafunga mlango kwa ndani, akachomoa kisu kilichokuwa katika mfuko wake. Aliamua kutumia kisu kwa maana aliona akitumia bastola inaweza kutoa sauti kubwa na kusababisha watu kujaa eneo lile, kwa hiyo kufanya hivyo ni kujiweka hatarini.
Kwa hiyo maamuzi aliyofikia ni kutumia kisu tu ili kutimiza dhamira yake.
"Nani wewe?" Sajenti Minja aliuliza baada ya kusikia vishindo vya mtu vikimsogelea,
"Mimi ni mtu mbaya" Mkuu wa polisi alijibu kwa sauti kavu iliyojaa utulivu,
"Usiku huu unataka nini kwangu?"Sajenti Minja aliuliza huku akijitahidi kupapasa engo za kitanda,
"Minja nimekuja kukuua, nimekuja kukuua Minja",Mkuu wa Polisi aliongea kwa hasira, wakati Sajenti Minja anataka kunyanyuka ili ajiokoe ilihali haoni, Mkuu wa Polisi alikishusha kishu katika jicho la kushoto la Sajenti Minja, na kujikuta Sajenti Minja akipiga kelele ambazo ziliwashtua wagonjwa wa wodi za jirani ambao wenye ahueni walienda katika mlango wa wodi ambako walimkuta Kayoza anaangaika kufungua, huku akilia kwa maana alihisi tayari mjomba wake yupo katika hatua za kupigania uhai wake kutokana na kelele alizozitoa.
Wakashirikiana na kufanikisha kuuvunja mlangp, walipofika ndani kila mtu mwenye moyo mwepesi aliishia kulia au kuzimia, Sajenti Minja alikuwa amelala kitandani huku akiwa amejaa damu mwili wote, na kisu kikubwa kiasi kikiwa kimeshindiliwa katika jicho lake la kushoto, ila ndani hawakumkuta mtu mwingine zaidi ya Sajenti Minja peke yake na hakukuwa na dalili ya dirisha kuvunjwa wala njia nyingine iliyoonesha kuna mtu alitumia kutokea mule ndani.
Watu wakawa wanashangaa lile tukio, wengine walidai ni mambo ya kishikirina, wengine wakasema alitaka kujiua, ila Kayoza yeye aliamini mule ndani kuna mtu, kwa hiyo akawa anaangaika kuangaza angaza kila mahali huku akiendelea na kilio kilichoambatana na chuki zilizojaa hasira.
Mkuu wa Polisi baada ya kumchoma visu visivyo na idadi Sajenti Minja, alisikia watu wakijaa mlangoni, alichoamua ni kupanda juu na kuingia kwenye singboard, lengo lake lilikuwa ni kutembea juu mpaka katika eneo ambalo atakuwa salama, ili atoke.
Alitembea juu ya Dari mpaka alipofika usawa wa choo, akashuka na kuanza kuelekea nje, alitoka salama kabisa na alifanikiwa kwenda katika guest aliyofikia salama salmini, akiwa na imani kuwa kazi yake imekamilika, na sasa anadili na Kayoza pekee.
Alipofika chumbani kwake aliingia bafuni na kunawa mikono, kisha akarudi ndani na kujitupa juu ya kochi, akajijiminia konyagi katika glass yake na kuigida yote kwa fujo…
Mkuu wa polisi akainuka katika kiti na kuelekea tena bafuni, akaoga na kutoka kisha akavaa suruali ya kitambaa na shati, kichwani akavaa kofia ya uviringo maarufu kama parma au watu was miaka ya themanini na tisini uwa wanaziita Marlboro kutokana na nembo moja maarufu ya sigara ambayo ilikuwa na picha ya mtu akiwa juu ya farasi huku akiwa amevaa kofia ya namna hiyo, pia baadae hiyo picha iliweza kuweka kwenye picha za mifuko ya Tanzania na hiyo mifuko ikapewa jina hilo, yaani mifuko ya Marlboro.
Mkuu wa polisi akatoka na kuelekea mitaa ya nyumba ya bibi yake Kayoza ili aone kama atakutana na habari za msiba wa Sajenti Minja.
Aliweza kufika kwenye mtaa huo ila hakubahatika kusikia habari yoyote, ikaendelea kuzunguka zunguka pale bila mafanikio yoyote na mwisho akaamua arudi zake katika ile nyumba ya wageni huku akiamini kuwa tayari Sajenti Minja ameshakufa, aliamua kuamini hivyo tu ingawa hakusikia habari yoyote, aliamua tu kuamini kutokana na ule unyama alioutenda kule hospitali.
Aliingia ndani ya chumba chake na kuvua shati lake na kofia, kisha akajitupa kitandani na kuwasha runinga na kuangalia vipindi vilivyokuwa vinaoneshwa kipindi hicho.
Ndani hospitali kulikuwa na patashika, madaktari walimuweka Sajenti Minja katika kitanda cha magurudumu na kuanza kusukuma kile kitanda kitanda mpaka chumba cha upasuaji, walipofika ndani ya chumba kile, walimuondoa nguo zote mwilini na kuanza kumfuta damu iloyokuwa imemtapakaa mwili mzima, walipomaliza kumfuta damu walikuta mwili wake una majeraha matatu tu, walikuta amechomwa kisu mbavuni, kifuani na katika jicho lake la kushoto.
Walichofanya ni kuangalia kama hivo visu alivyochomwa kama vina madhara makubwa, mwisho waligundua kisu cha mbavuni na kifuani havina madhara sana, walichofanya ni kusafisha vidonda hivyo na kuvipaka dawa kisha wakavifunga na bandeji laini, ila tatizo kubwa lilikuwa katika kisu alichochokwa katika jicho lake la kushoto, ilionekana ndio kina madhara makubwa sana.
"Ni nani mwenye ujasiri huu was kuingia hapa na kufanya unyama wa namna hii?" Daktari mmoja aliuliza,
"Hapa kwetu usalama hakuna, huo ndio ukweli, na kama hii habari itafika ngazi za juu, basi tutakuwa mashakani" Daktari mwingine alijibu,
"Ila mtu aliyefanya hivi inaelekea ana kiasi na huyu bwana, haiwezekani atoke uko na kuja moja kwa moja katika wodi aliyolazwa huyu bwana" Daktari mwingine alijibu,
"Hilo sio jukumu letu, tunachotakiwa ni kumtibu tu mgonjwa, hayo mengine ni ya walinzi" Daktari wa tatu aliongea,
"sasa itakuaje?", Daktari mmoja aliuliza huku akitegemea jibu kutoka kwa wenzake, lakini ilikua tofauti, kwa sababu hakuna hata mmoja alienyanyua mdomo wake kujibu,
"ina maana hamjanisikia au?", yule Daktari aliuliza tena baada ya kuona kimya,
"hapo mkuu hamna jinsi, itabidi aondolewe tu!",Daktari mmoja aliyevaa suruali ya jeans alijibu hivyo,
"kwa hiyo inabidi afanyiwe uperation, si ndio?", yule Daktari ambae ndio alionekana mkuu aliuliza tena.
"Hamna jinsi, itabidi iwe hivyo" Daktari mwingine aliongezea,
Na makubaliano waliyofikia ilikua ni kumuondoa Sajenti Minja jicho lake.
Na ndipo jicho lake la kushoto likaondolewa, na kupata kilema cha milele kilichotokana na shambulio lililofanywa na mkuu wa polisi.
Kipindi chote, Kayoza alikuwa amekaa nje ya wodi huku machozi yakimtoka, mara ghafla Kayoza akashuhudia mlango wa wodi ukifunguliwa na wakatoka wauguzi wawili ambao walikuwa wanakisuma kitanda chenye magurudumu manne, huku wakifuatiwa na Madaktari wawili, Kayoza nae akaamka, kisha akaongozana nao mpaka katika mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi, Madaktari wakaingia ndani, Kayoza alibaki nje, muda wote Kayoza alikua hatulii, mara akanyanyuka kwenda katika mlango wodi aliyolazwa Sajenti Minja, akawa anatafuta upenyo ili aweze kuona kinachoendelea ndani, lakini bado hakufanikiwa, mwisho akaamua kusimama tu! kama mtu aliyekosa matumaini.
Baada ya dakika kadhaa za kusubiri pale nje, Daktari mmoja akatoka ndani huku akiwa anaelekea maeneo zilipo ofisi za hospitali, ila alipofika usawa wa viti vya watu wanavyokaa watu wanaosubili wagonjwa wapo, Kayoza akasimama na kumkimbilia daktari,
"Samahani Daktari, mgonjwa wangu ana hali gani?" Kayoza aliuliza huku akimuangalia Daktari aliyekuwa anatembea,
"Mgonjwa wako yupi?" Daktari aliuliza huku akiendelea kutembea,
"Yule aliyevamiwa na kuchomwa visu" Kayoza alijibu,
"Ooooh. kijana, mgonjwa ni ndugu yako?",Daktari alimuuliza Kayoza,
"ndio dokta",Kayoza alijibu,
"mbona uko peke yako, hakuna watu wakubwa ulioongozana nao?",Daktari akauliza swali lingine,
"hakuna, kwani vipi?",Kayoza akauliza huku akiwa na wasiwasi,
"ok, nifuate ofisini",Daktari aliongea huku akiwa anaondoka.
Kayoza akaongozana na Daktari mpaka katika ofisi ya huyo Daktari, akakaribishwa kiti, akakaa,
"bila kupoteza muda kijana, hali ya ndugu yako umeiona na hakuna jinsi zaidi ya kuondolewa jicho, kwa hiyo tunasubiri azinduke, maana amepoteza fahamu, fahamu zikimrudia itambidi asaini kitabu cha upasuaji ili tumuondoe lile jicho",Daktari alikuwa anampa maelezo Kayoza,
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi