Notifications
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…
  • MY DIARY (27)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SABATULIPOISHIA...Alinamba eti hayo ya mimi kuolewa tuyaeke pembeni na kwa nini siku hiyo nisilale Moshi tukumbushie enzi zetu. Mwalimu John aliendelea kusema kuwa amenimiss sana na anomba nisahu yaliyopita na turudie yale maisha yetu ya zamani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijifanya simwelewi lakini ukweli ni kwamba nyota ya mwanaume huyu ilikuwa ni kali sana zaidi yangu na…
  • MY DIARY (26)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SITATULIPOISHIA...Joyce alinambia yeye haendi kujipanga foleni kama makahaba wengine hivyo yeye hufanya biashara hiyo kitaalamu zaidi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alisistiza pia kuwa eti huwa anatumia kinga kuwakinga wengine. Wakati mwingine alinambia acha awaambukize kwa sababu wanaume wangekuwa na akili basi wasingeenda kununua mwanamke. Anasema kuwa laiti biashara hiyo…
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (24)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NNETULIPOISHIA...Kwa kweli siku hiyo niliwaza sana na kutafakri vitu vingi. Wale wanachuo wenzangu wamenambia kuwa Msouth alikuwa kwa kimada mwingine na japo stori haikumalizikia ila ukweli ni kwamba alifumaniwa na kupigwa vibaya na huenda walimtupa mahali na ndio maana chanzo cha kifo chake hakieleweki.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijaribu kuijikontrol ili nisiwaze kitu…
  • MY DIARY (23)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TATUTULIPOISHIA...Alinisihi sana nisitoe niilee na yeye atatoa huduma zote lakini tuendelee kufanya siri ili tusije tukahatarisha ndoa yake na kusababisha familia yake kuyumba. Kwa kweli sikuweza maana ilikuwa ni kujipa tabu mimi na huyo mtoto atakayezaliwa. Bora ataa ingekuwa ni mimba ya ule mwalimu ambaye hajaoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilitamani nimchomekee hiyo mimba…
  • MY DIARY (22)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILITULIPOISHIA...Alitumia vizuri umbo lake la kimiss kutembea kimiss na kuweka mapozi ya maana. Na baada hapo alilala kwenye kile kigodoro na akachojoa vyote isipokuwa kufuli jeupe ambalo nalo alipewa hapo hapo kwa ajili ya kazi hiyo. IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi sikumpa nafasi Joyce niliingilia nafasi yake na kuchukua ule uume wa bandia nikamfuta yule dada.…
  • MY DIARY (21)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJATULIPOISHIA...Nilichomeka simu chaji na kuiweka hewani ili nione kama kutakuwa na sms yeyote iliyoingia.Hofu ilizidi kunitawala na wakati naendela kufikira simu yangu iliita niakzani labda ni Joyce na nilipoiangalia nilimkuta ni Msouth. Sikutaka kuipokea nikaiacha iite mpaka ikate yenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikajiuliza kwani amepatwa na nini usiku huo mpaka…
  • MY DIARY (20)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINITULIPOISHIA...Nikamwambia kuhusu namba zangu za simu amuombe aliyemtuma anisaidie na kuhusu hilo la pili je hatuwezi kufanya kesho kwa sababu kuna mahali nilikuwa nikienda? Alifikiria kwa sekunde kadhaa na kuniambia kuwa hapana anaomba nimsaidie leo kama yeye alivyonisaidia mimi kwa sababu ningekuwa kwenye foleni nisingeweza kuondoka kirahisi hivyo kama ninavyofikiria.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…

KIJIJINI KWA BIBI (40)

Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA AROBAINI
TULIPOISHIA...
"bila kupoteza muda kijana, hali ya ndugu yako umeiona na hakuna jinsi zaidi ya kuondolewa jicho, kwa hiyo tunasubiri azinduke, maana amepoteza fahamu, fahamu zikimrudia itambidi asaini kitabu cha upasuaji ili tumuondoe lile jicho",Daktari alikuwa anampa maelezo Kayoza,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"hakuna shida Dokta",Kayoza alijibu,

"sio unasema hakuna shida tu, je pesa ipo?",Daktari alimuuliza Kayoza,

"kwani inahitajika shilingi ngapi?",Kayoza akauliza,

"laki tatu",Daktari akajibu,

"hakuna tatizo, pesa ipo",Kayoza alimwambia Daktari.

"Wewe unafanya kazi?" Daktari akamtupia swali lingine Kayoza,

"Hapana, mimi ni mwanafunzi" Kayoza alijibu,

"Sasa pesa utazitoa wapi?" Daktari aliuliza,

"pesa ipo kaka" Kayoza alijibu kwa kifupi,

"Basi wewe nenda kalete hela" Daktari alimwambia Kayoza,

"Je naweza kumuona mgonjwa wangu?" Kayoza aliuliza,

"Hapana, utamuona akishafanyiwa upasuaji?" Daktari alijibu,

"Sawa" Kayoza alijibu kwa unyonge.

Kisha Kayoza akatoka katika ofisi ya Daktari, na kuelekea nyumbani, njia nzima alikuwa anawaza mtiririko wa matukio yanayomtokea, ila kwa sasa aliamini adui yake mkubwa ni Mkuu wa Polisi.

Kayoza akaondoka na kwenda katika bar iliyo jirani na pale hospitali, akanywa soda, kisha akaondoka huku akiwa na mawazo mengi sana,

"lazima nimuue yule mzee, ameniharibia tumaini langu la kupona na sijui hatma yangu ya maisha mpaka sasa, Mjomba minja anakuwa mlemavu kwa sababu yangu mimi, Omari rafiki yangu kipenzi nisamehe, umenisaidia sana ila mwisho umekuwa maiti kwa sababu yangu mimi, Denis nilikupenda sana jamaa yangu, ila…",Kayoza akashindwa kuendelea machozi yakawa yanamtoka, akasimama pembeni ya barabara huku machozi yakimtoka.

Akashindwa hadi kutembea, akakodi taxi ya kumfikisha nyumbani.

Kayoza alipofika nyumbani, aliwaambia waanze kutayarisha chakula cha mgonjwa, kisha Kayoza akaenda kuoga, alipotoka akaenda kuvaa, kisha akala chakula, alafu akachukua chakula cha mgonjwa na safari ya kuelekea hospitali ikaanza ingawa hakuwa na uhakika kama Sajenti Minja ataweza kula ila ilibidi abebe tu hivyo hivyo.

alipokuwa anatoka nje, ndipo macho yake yalimshuhudia mtu ambae alikuwa anaelekea katika nyumba aliyokuwepo yeye.

Kayoza machozi yakaanza kumtiririka katika mashavu yake, sababu ya uchungu wa yaliyomtokea, aliamua kulia kwa sauti kubwa huku akimuangalia yule mtu anaekuja, mwisho akaamua kuweka chakula chini na kukimbia kumuelekea yule mtu, yule mtu nae alikua anakimbia kumuelekea Kayoza….

…jinsi walivyozidi kusogeleana ndio machozi katika macho yao yalizidi kuongezeka, walikumbatiana kwa furaha iliyoambatana na uchungu wa kumbukumbu mbaya za nyuma, kwa dakika nzima hakuna aliyemsemesha mwenzake,

"pole mwanangu, hiyo yote ni mitihani ya dunia", ndivyo mama Kayoza alianza kuongea maneno hayo ambayo aliamini yatamfariji mtoto wake,

"kwanini mimi tu mama, kila uchungu unapita katika njia ya moyo wangu, kwanini mimi, nimemkosea nini Mungu?", Kayoza aliongea huku akilia,

"yanapita hayo mwanangu, vumilia na uamini mungu yuko pamoja na wewe", Mama kayoza aliendelea kumfariji mwanae, kisha akaendelea,

"hata mimi mjomba wako aliponipigia simu na kunieleza kifo cha Omary na bibi yako, nilisikitika sana na mbaya zaidi aliniambia kuwa bibi yako alikufa wakati anajiandaa kukutoa hilo dubwana linalokusumbua", Mama Kayoza alipofika hapo akanyamaza baada ya kuona Kayoza analia kwa uchungu sana.

"mjomba wako yuko ndani?", Mama Kayoza aliuliza swali lililozidisha kilio kwa mwanae,

"ina maana mama hujui?", Kayoza akajikuta anamtupia swali mama yake,

"sijui nini?, mbona unanipa wasiwasi tena!", Mama Kayoza aliuliza kwa mshangao,

"habari za mjomba Minja", Kayoza akaendelea kumfafanulia mama yake,

"ehe, kaka yangu kafanyaje tena", Mama Kayoza akaendelea kuuliza huku tayari akiwa amejaa wasiwasi sana, kwa maana kauli za Kayoza zilianza kumtisha,

"Mjomba minja alipigwa risasi, ila hakufa na jana kavamiwa na mtu asiejulikana na akamchoma kisu cha…", Kayoza alishindwa kumalizia baada ya mama yake kuanguka chini na kupoteza fahamu.

Ikambidi Kayoza awaite ndugu zake wamsaidie, dakika tano zikapita bila Mama Kayoza kuzinduka.

"Umemfanyaje mama yako?" Baba ake mdogo Kayoza alimuuliza Kayoza,

"Sijamfanya kitu" Kayoza alijibu,

"Amekuja saa ngapi?" Baba mdogo aliendelea na Maswali,

"Ameingia muda si mrefu" Kayoza alijibu,

"Mbona hajasema kama anakuja, au wewe alikupa taharifa?" Baba mdogo aliuliza,

"Na wewe nawe punguza maswali yako bwana, si umsubiri azinduke ndio umuulize yeye mwenyewe hayo maswali" Kayoza aliongea kwa hasira baada ya kuona maswali yamekuwa mengi kuliko vitendo,

"We unamjibu nani hivyo?" Baba mdogo aliuliza kwa hasira,

"Kwani naongea na nani, au naongea na nyani?" Kayoza nae aliongea kwa hasira, na kufanya baba yake mdogo atake kumvaa ila ndugu wengine waliingilia kati na kumzuia baba yake mdogo apunguze hasira,

"Kwanza tokea mmekuja hapa ndio matatizo nayo yamekuja, mna mikosi tele imewajaa" Baba mdogo aliongea kwa hasira,

"Na bado mkosi mwingine unakuja" Kayoza alijibu huku akimpepea mama yake aliyekuwa bado amepoteza fahamu,

"Tusijibishane Kayoza ujue nitakupiga" Baba mdogo aliongea huku akimnyooshea kidole,

"Kunipiga huwezi, na sitaki tena malumbano na wewe, vinginevyo nitafanya kitu ambacho hutokaa unisahau" Kayoza aliongea huku akimuangalia baba yake mdogo kwa jicho Kali sana,

"Utafanya nini sasa wewe?, we si Mbwa tu" Baba mdogo aliongea kwa hasira na kufanya watu wamtoe eneo lile kwa maana waliona hakukuwa na umuhimu tena watu hao kukaa pamoja muda huo.

Baada ya baba mdogo kutolewa kidogo amani ilirejea katika eneo lile,

"Mimi naona hawezi kuamka, ni bora tumpeleke hospitali" Ndugu mmoja aliongea huku akimuangalia Kayoza,

"Hata mimi nilikuwa na wazo kama hilo" Ndugu mwingine aliongezea,

"Twendeni tu, Hamna jinsi" Kayoza aliongea.

Uhamuzi uliopitishwa ni kumpeleka hospitali, wakakodi gari la abiria, wakampakia mama Kayoza, huku Kayoza na Shangazi yake wakichukua jukumu la kumsindikiza.

Walipokaribia eneo la hospitali, mama Kayoza alirejewa na fahamu zake,

"unajisikiaje wifi?", Shangazi yake Kayoza alimuuliza Mama Kayoza,

"safi, tunaelekea wapi?", mama Kayoza aliuliza,

"hospitali", Kayoza alimjibu mama yake,

Mama kayoza baada ya kusikia neno "hospitali", kumbukumbu zikamrudia, akaanza kuangua kilio ndani ya gari huku akitaja jina la Sajenti Minja.

"Mama na wewe bwana, kwani amekufa?" Kayoza aliuliza kwa jazba,

"Muache alie ili apunguze uchungu" Shangazi yake alijibu,

"Sasa inakuwa ni Makelele tu kama tunamsiba bwana" Kayoza aliongea kwa kulalamika,

"Siku hizi umekuwaje wewe, hivi hata hujioni kuwa upo tofauti?" Shangazi yake aliuliza huku akiwa amemkazia macho Kayoza na kufanya Kayoza akae kimya tu.

Walipofika hospitali, Kayoza akaenda katika chumba cha Daktari. Maana alishakariri kila sehemu ya hospital na karibu madaktari wote wa ile hospitali walikuwa wanamjua Kayoza kutokana na kushinda sana eneo la Hospitali.

"ooh, afadhali dogo umekuja, maana tulikuwa tunakusubiri wewe", Daktari alikua akimwambia Kayoza maneno hayo,

"vipi hali ya mgonjwa wangu?",Kayoza alimtupia swali Daktari,

"mgonjwa wako bwana,…tayari tumeshamfanyia upasuaji, na tumefanikiwa kulitoa jicho lake la kushoto, ila tumemuwekea jicho la kondoo", Daktari alijibu kwa ufasaha swali la Kayoza,

"kwa hiyo gharama zote ni kiasi gani?", Kayoza aliuliza,

"ni milioni mbili na laki tatu, kwa sababu hata hilo jicho la kondoo tumelinunua kwa pesa nyingi kidogo", Daktari alimuelewesha Kayoza,

"Ila dokta si ulisema ni laki tatu tu?" Kayoza alimuuliza daktari huku akimshangaa,

"Ila si nimekwambia hilo jicho la kondoo tumelinunua" Daktari aliongea huku akitabasamu,.

"Sasa hicho la kondoo ndio milioni moja?, si ungeniambia mimi nilete, ningekuja nalo tu kwa maana nyumbani tuna kondoo wengi tu" Kayoza aliongea huku akimshangaa daktari,

"Ninaposema jicho la kondoo simaanishi ni jicho la kondoo mnyama, ninachomaanisha ni jicho la bandia" Daktari aliongea huku akitabasamu,

"Ila milioni mbili na laki tatu ni nyingi sana, siwezi kuzimudu" Kayoza aliongea kwa sauti ya unyonge.

"Wewe una shilingi ngapi?" Daktari alimuuluiza,

"Mimi nilijiandaa na hiyo laki tatu, ila itanibidi niongeze na laki mbili, kwani ndio niliyonayo" Kayoza alizungumza,

"Sawa nipe hiyo, ila mwenzangu yoyote akikuuliza useme umenipa laki tatu" Daktari aliongea huku akimtazama Kayoza,

"Ila hapa sina" Kayoza alijibu,

"Aaaagh dogo, zikwapi sasa?" Daktari aliuliza huku akionekana hajafurahishwa na kauli ya Kayoza,

"Nitakuletea kesho asubuhi" Kayoza alimuelewesha Daktari,

"Zamu yangu inaisha leo ila itanibidi nikusubiri mpaka kesho utakapoleta, na ulete kweli kesho" Daktari aliongea kwa mkazo,

"sawa dokta, nitazileta kesho hasubui", Kayoza alijibu.

Baada ya hapo, Daktari akatoka na Kayoza na kwenda katika wodi aliyolazwa Sajenti Minja, huku wakiambatana na Mama na Shangazi wa Kayoza.

BAADA YA MWEZI

Jumamosi asubuhi ndiyo siku ambayo Sajenti Minja aliruhusiwa kurudi nyumbani huku akiwa na ulemavu wa maisha. Kayoza na Mama yake ndio walikwenda kumchukua hospitali.

Walipofika nyumbani, walipokelewa kwa furaha sana,

"itabidi leo tufanye sherehe ya kumshukuru Mungu kwa maajabu aliyoyaonesha kwa bwana Minja", Baba yake mdogo Kayoza alitoa wazo,

"hapana baba, sherehe iwe kesho",Kayoza aliongea huku akiwa na sura ya furaha,

"kwanini unataka iwe kesho mwanangu?", Baba yake mdogo alimuuliza Kayoza,

"kwa sababu kesho nataka kufanya kitu ambacho kitakua kama historia ya kumbukumbu nzuri ya ushujaa kwangu", kama kawaida yake, Kayoza aliongea huku akiwa na tabasamu,

"mh! kitu gani hicho?", Mama Kayoza alimuuliza mtoto wake,

"hampaswi kuwa na haraka, nyie ngojeni nataka iwe kama tukio la kushtukiza kwenu", Kayoza alimjibu mama yake,

"haya bwana, sisi tunasubiri kwa hamu.

Kesho yake ambayo ilikua jumapili, mida ya saa nne asubuhi, Kayoza akaondoka kwao bila ya kuaga na kuelekea katika ile guest aliyopanga Mkuu wa Polisi, alipofika mapokezi, alimuuliza yule muhudumu kama mtu aliyemfuata yupo, akajibiwa yupo tena amelewa sana, Kayoza akaenda mpaka katika mlango wa chumba cha Mkuu wa Polisi, aliingiza mkono katika mfuko wa suruali na kutoa kitambaa ambacho alifunga puani, kama mtu anayezuia harufu fulani.

kisha akagonga mlango huku akiwa kashika chupa tupu ya soda mkononi, mkuu wa Polisi akauendea mlango, kisha akaufungua, alipofungua tu, alikutana na chupa ya kichwa iliyompeleka moja kwa moja sakafuni, Kayoza akatumia vizuri nafasi ya kumshambulia mfululizo mpaka Mkuu wa Polisi akawa hatamaniki kwa jinsi alivyokuwa anavuja damu kichwani, ghafla Mkuu wa Polisi akampiga teke Kayoza na kusababisha chupa imponyoke Kayoza, Mkuu wa Polisi kwa kasi ya mshale, akakimbilia katika kitanda chake, akaunyanyua mto, kisha akachukua bastola yake na kumuelekezea Kayoza,

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
60 Kijijini kwa Bibi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni