Notifications
  • MY DIARY (29)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TISATULIPOISHIA...Hapo sasa nikazidi kuchanganyikiwa ikabidi nimuulize mama huyo alikuwa akifanyia shughuli zake za kujipatia kipato sehemu gani.? Yule dada akanambia kuwa anafanyia soko la ndizi huko Korongoni. Sikuwa na jinsi nilimuomba anipeleke lakini na yeye alisita sita kwa madai kuwa alikuwa na kazi nyingi za kufanya na bado anatakiwa ampeleke mtoto shule.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (28)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NANETULIPOISHIA...Sisi tumesomea mambo haya bhana waliendela kuzungumza wale walinzi huku wakishuka ngazi kwa polepole. Hapo na mimi nikawa nimejifunza kitu kuwa kumbe unaweza kuingia na mtu guest akakuzuru kisha akaondoka zake.Sasa sijui kwenye zile guest zetu za uswahilini kama wanalijua hili.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi nilala japo usingizi ulikuwa hautaki kuja kwa…
  • MY DIARY (27)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SABATULIPOISHIA...Alinamba eti hayo ya mimi kuolewa tuyaeke pembeni na kwa nini siku hiyo nisilale Moshi tukumbushie enzi zetu. Mwalimu John aliendelea kusema kuwa amenimiss sana na anomba nisahu yaliyopita na turudie yale maisha yetu ya zamani.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijifanya simwelewi lakini ukweli ni kwamba nyota ya mwanaume huyu ilikuwa ni kali sana zaidi yangu na…
  • MY DIARY (26)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA SITATULIPOISHIA...Joyce alinambia yeye haendi kujipanga foleni kama makahaba wengine hivyo yeye hufanya biashara hiyo kitaalamu zaidi.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Alisistiza pia kuwa eti huwa anatumia kinga kuwakinga wengine. Wakati mwingine alinambia acha awaambukize kwa sababu wanaume wangekuwa na akili basi wasingeenda kununua mwanamke. Anasema kuwa laiti biashara hiyo…
  • MY DIARY (25)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TANOTULIPOISHIA...Sikuisha hapo pia nilimpongeza kwa kunijali na kunipenda na kuhakisha kuwa siingii kwenye majanga kama yake mara baada ya kutoka jela. Siku hiyo nilimuelewa sana Joyce na nilikuwa tayari kumsapoti kwa lolote ili mradi tu atimize athma yake hiyo ya kuzaa. Tuliongea mengi sana na baadaye alinionesha picha ya mtu ambaye alitaka kuzaa naye.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…
  • MY DIARY (24)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA NNETULIPOISHIA...Kwa kweli siku hiyo niliwaza sana na kutafakri vitu vingi. Wale wanachuo wenzangu wamenambia kuwa Msouth alikuwa kwa kimada mwingine na japo stori haikumalizikia ila ukweli ni kwamba alifumaniwa na kupigwa vibaya na huenda walimtupa mahali na ndio maana chanzo cha kifo chake hakieleweki.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilijaribu kuijikontrol ili nisiwaze kitu…
  • MY DIARY (23)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA TATUTULIPOISHIA...Alinisihi sana nisitoe niilee na yeye atatoa huduma zote lakini tuendelee kufanya siri ili tusije tukahatarisha ndoa yake na kusababisha familia yake kuyumba. Kwa kweli sikuweza maana ilikuwa ni kujipa tabu mimi na huyo mtoto atakayezaliwa. Bora ataa ingekuwa ni mimba ya ule mwalimu ambaye hajaoa.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nilitamani nimchomekee hiyo mimba…
  • MY DIARY (22)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILITULIPOISHIA...Alitumia vizuri umbo lake la kimiss kutembea kimiss na kuweka mapozi ya maana. Na baada hapo alilala kwenye kile kigodoro na akachojoa vyote isipokuwa kufuli jeupe ambalo nalo alipewa hapo hapo kwa ajili ya kazi hiyo. IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Basi sikumpa nafasi Joyce niliingilia nafasi yake na kuchukua ule uume wa bandia nikamfuta yule dada.…
  • MY DIARY (21)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJATULIPOISHIA...Nilichomeka simu chaji na kuiweka hewani ili nione kama kutakuwa na sms yeyote iliyoingia.Hofu ilizidi kunitawala na wakati naendela kufikira simu yangu iliita niakzani labda ni Joyce na nilipoiangalia nilimkuta ni Msouth. Sikutaka kuipokea nikaiacha iite mpaka ikate yenyewe.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI👉INSTALL👈TUENDELEE...Nikajiuliza kwani amepatwa na nini usiku huo mpaka…
  • MY DIARY (20)
    Jina: MY DIARYMtunzi: __SEHEMU YA ISHIRINITULIPOISHIA...Nikamwambia kuhusu namba zangu za simu amuombe aliyemtuma anisaidie na kuhusu hilo la pili je hatuwezi kufanya kesho kwa sababu kuna mahali nilikuwa nikienda? Alifikiria kwa sekunde kadhaa na kuniambia kuwa hapana anaomba nimsaidie leo kama yeye alivyonisaidia mimi kwa sababu ningekuwa kwenye foleni nisingeweza kuondoka kirahisi hivyo kama ninavyofikiria.IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA…

KIJIJINI KWA BIBI (41)

Mwandishi: Alex Kileo

SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
TULIPOISHIA...
Kayoza akatumia vizuri nafasi ya kumshambulia mfululizo mpaka Mkuu wa Polisi akawa hatamaniki kwa jinsi alivyokuwa anavuja damu kichwani, ghafla Mkuu wa Polisi akampiga teke Kayoza na kusababisha chupa imponyoke Kayoza, Mkuu wa Polisi kwa kasi ya mshale, akakimbilia katika kitanda chake, akaunyanyua mto, kisha akachukua bastola yake na kumuelekezea Kayoza,

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
"mwanaharamu mkubwa wewe, kwa kitendo ulichonifanyia, sio rahisi nikikuacha hai", Mkuu wa Polisi aliongea huku akikoti risasi katika bastola yake, Kayoza alitawaliwa na hofu na kukata tamaa. Aliamini hapo ndipo mbio za kupambana na Mkuu wa polisi zake zilipoishia.

Mkuu wa polisi akaweka target katika paji la uso wa Kayoza, Kayoza akafumba macho kuashiria kukata tamaa, Kisha Mkuu wa Polisi akafyatua risasi..

…lakini risasi haikutoka, Mkuu wa polisi akajaribu tena, lakini hali ikawa ile ile, bastola ilikua haina risasi, Mkuu wa Polisi akaruka mpaka kwenye kabati, akachukua mfuko wa risasi, Kayoza kuona hivyo, akaikimbilia chupa ya soda aliyokuja nayo, ambayo ilikuwa karibu na mlango, ile kuikota ili amuwai akakuta tayari Mkuu wa Polisi anaikoki bastola, Kayoza akamuwai, akarusha ile chupa ambayo iliupiga mkono wa Mkuu wa Polisi ambao ulikua umeshika ile bastola na kufanya ile bastola iende chini, Kayoza akaruka juu na kumpiga teke Mkuu wa Polisi, Mkuu wa Polisi akadondoka chini, Kayoza akaiokota ile bastola na kumfyatulia Mkuu wa Polisi risasi zisizo na idadi mpaka akafa. Kisha hapo ndipo akakiri kuwa ana kosa sasa la mauaji, kwa maana ameua kwa kukusudia tofauti na anavyoua kipindi mzimu unapompanda.

Kayoza akaenda katika kabati na kuvunja kioo, akachukua kipande cha kioo, kisha akachukua ndoo iliyo mule ndani na kwenda sehemu ulipo mwili wa Mkuu wa Polisi, akaanza kuuchinja huku akikinga damu kwa kutumia ile ndoo, mpaka aliporidhika. Na kumbuka kipindi chote hicho alikuwa na kitambaa puani ambacho alikipulizia pafyumu kwa ajili ya kuzuia harufu ya damu ya aina yoyote ile.

Baada ya kufanya ukatili huo ambayo hakutaka kabisa kuujutia, Kayoza alicheka mwenyewe ndani ya chumba ambacho alifanyia mauaji na kisha Kazi kubwa ambayo ilimkabiri kwa wakati huo ikawa ni kutoka nje, maana watu walishajaa nje.

Akachukua kichwa cha Mkuu wa Polisi akakiweka ndani ya ndoo, kisha akaifunika ndoo, safari ya kwenda nje ikaanza, alipofungua mlango watu wote wakatawanyika, kwa maana waliamini Kayoza sio mtu wa kawaida kabisa, na ili kuwatisha zaidi, Kayoza akapiga risasi hewani, watu wakakaa nae mbali kabisa, nguo zote alizozivaa zilikuwa zimetapakaa damu, ila yeye hakuweza kuisikia harufu ya damu kutokana na kitambaa alichojifunga puani kwa ajili ya kuhofia mzimu kumpanda endapo harufu ya damu itapenya puani mwake.

Akatoka na ndoo yake mpaka kwao, huku akifuatwa na kundi la watu na waandishi wa habari walikuwepo, tena wengi walikuwa na furaha kwa sababu ya kupata habari itakayouza magazeti yao.

Njia nzima alikuwa akitembea huku kundi kubwa sana la watu likimfuata na kila mmoja akisema lake kutokana na ukatili ule waliokuwa wanaushuhudia mubashara, kwa maana vitu kama vile walishazoea kuviona katika filamu za watu wa mashariki mpwa dunia au kukutana navyo katika simulizi za wakina ALEX KILEO.

Alipofika kwao, akatoa onyo kuwa, mtu yeyote asimsogelee, na mtu ataekaidi amri, atampiga risasi. na kweli walimuogopa kwa maana Kayoza wa siku hiyo hakuwa na chembe za ubinadamu kabisa, hata sura yake ilidhihirisha hiyo kwa maana zile damu zilizomtapakaa mwili mzima na macho yake yalivyokuwa mekundu yalionesha hakuna hatari anayoiona mbele yake. Tayari alishaamua kuwa mnyama na aliona hiyo ndiyo bora ya kufanya kwa wakati huo.

Baada ya kufika kwao, Kayoza akaingia katika chumba chake akajifungia mlango kwa ndani, hapo ndipo alipodhamilia kufanya kama Maelezo ya mganga wa mwisho kumtembelea yalivyosema, akakumbuka kuwa mganga alisema kuwa njia ya kuundoa huo mzimu inaweza kugharimu na maisha yake, yaani maisha ya Kayoza, hata Sajenti Minja alipouliza ni njia gani hiyo? Mganga alijibu kuwa itabidi achinjwe kondoo alafu Kayoza awekwe katika kitanzi ili harufu ya damu itakapoingia puani kwa Kayoza ni lazima mzimu umpande, na hapo ndipo ile kamba ya kitanzi ivutwe na imnyonge kayoza, ni lazima kayoza ni lazima afe na mzimu ufe kwa maana mzimu hutegemea pumzi katika kutoka na kuingia katika mwili wa Kayoza.

Baada ya Kayoza kuyakumbuka maneno hayo, alijikuta akitabasamu, tabasamu la umauti lililokuwa linatoka pasipokuwa na furaha ila hasira zilizotokana na kukata tamaa ya kupata suluhisho la matatizo yake.

kisha akachukua kamba akaitundika juu na kuweka kitanzi, kisha akaweka stuli na kupanda juu, alafu akaifunua ile ndoo ambayo aliiwekea damu ya Mkuu wa Polisi, akakitoa kile kichwa na kukitupia chini ya kitanda, kisha akajifungua kile kitambaa puani, harufu ya damu ikampenya sawa sawa katika matundu ya pua yake, alivyoanza kuhisi dalili ya kupandwa na mzimu akaitupa ile ndoo, na kuitegua stuli, mzimu ukawa tayari umeshampanda, na kitanzi kikambana sawa sawa, Kayoza na mzimu wake, akaanza kupiga kelele kwa sauti ya ajabu, hali iliyofanya watu waliokuwa nje ya nyumba watawanyike.

Nje, kwanza ilipiga radi kubwa sana, huku ikifuatiwa na upepo mkali sana, mpaka nyumba zenye udhaifu zilianguka, alafu ikanyesha mvua kubwa sana ikiambatana na jua kali sana.

Kayoza ilimchukua kama dakika thelathini kuangaika juu ya kitanzi, mwishowe alitulia kimya kabisa, na ukawa ndio mwisho wa maisha yake na mzimu wake.

Polisi ndio walikuja kuvunja mlango na kuukuta mwili wa Kayoza unatoa moshi na ulikuwa mweusi sana kuashiria alikuwa anaungua, macho na masikio yalikuwa yametoboka, hakika kilikuwa kifo kilichosikitisha sana, kifo ambacho kilihitimisha urithi wa kimizimu katika ukoo.

Sajenti Minja alilia kama mtoto kutokana na yote aliyofanya katika kumlinda Kayoza na uhai wake, lakini ilikuwa kama bure, na mbaya zaidi aliyakumbuka maneno ya Kayoza ya jana yake, ambayo Kayoza alidai anataka sherehe ifanyike leo kwa sababu anataka kufanya jambo la kukumbukwa daima.

"kumbe jambo lenyewe ndio hili, umelifanya mapema sana mjomba, ungesubiri mjomba, kama ungesubiri nina uhakika uhai wako usingetoweka", Sajenti Minja aliongea mbele ya jeneza la Kayoza ambalo liliwekwa mbele ya watu kwa ajili ya kuuaga mwili wa marehemu Kayoza.

Mama Kayoza alianguka na kuzimia mara nne, kitendo ambacho kilisababisha apelekwe hospitali na ikagundulika mshtuko wa moyo.

Mambo ya maziko yalienda kama kawaida na kumalizika salama.

Kwa upande wa Mkuu wa Polisi, mwili wake ulizikwa na manispaa ya mkoa wa Kigoma kutokana na kutopatikana kwa kichwa chake ambacho Sajenti Minja alikificha makusudi ili kupoteza ushahidi na baada ya Siku alienda kukizika.

Uko kwao Shinyanga hawakupata taharifa yoyote, habari zilizotangazwa kwa wafanyakazi wenzake yaani polisi wenzie ni kuwa amepotea na hajulikani halipo.

BAADA YA MIAKA 3

Anaonekana Sajenti Joel Minja akiwa na familia yake, wakiweka shahada la maua katika kaburi la Mama Kayoza ambae alikufa mwaka mmoja uliopita kutokana na ugonjwa wa mshtuko wa moyo alioupata kutokana na mshtuko wa kifo cha mwanaye kipenzi (Kayoza).

Sajenti Minja aliacha kazi kutokana na ulemavu alioupata, sasa hivi ni mjasiliamali ambae ana kampuni yake binafsi ya usafirishaji wa abiria, ambayo inamiliki mabasi, maroli, daladala na taxi. Mabasi yake ni maarufu sana katika mikoa ya Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya na Tanga, Yanaitwa GHOST MEMORY.

Ana mke na watoto wawili, wa kwanza anaitwa Kayoza, na wapili anaitwa Omari, ikiwa kumbukumbu kwa watu wake wa karibu.

MWISHO

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi
60 Kijijini kwa Bibi Simulizi
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni