MZIMU WA WAUFU (8)

0

SEHEMU YA NANE
TULIPOISHIA...
“Nyie ni askari gani msiojua hata kujitambulisha kisheria? Taja jina lako, namba yako ya kazi, kitabulisho chako, nk” Yule afande akamuangalia sana mzee Kikoko kisha ikabidi Yule askari atoe Kitambulisho chake cha kazi akamuonesha Mzee Kikoko

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
“Umeridhika eeh?”

“Sio nimeridhika lazima utambue majukumu yako na ufuate taratibu za kazi yako, sasa usipojitambulisha nitakujuaje kama wewe ni askari? Kama ni hizo bunduki na sare hata majambazi wanazo, mie sio wa kijijini, mimi ni mtoto wa mjini”

“Sawa mzee utaenda kutuonesha na hao majambazi wanaomiliki bunduki na sare zetu” Askari Yule alikua amekasirika sana,

Wakati Mzee Kikoko anaendelea kujibizanana maafande hawa Sheikh Jabu nae akawa tayari ameshawasili na pikipiki yake akiwa amembeba Sheikh Mwinyigoha, Kikoko alipomuona Sheikh Jabu ndo akazidikupata kiburi lakini hakupata furaha kumuona Sheikh Mwinyigoha kutokana na malalamiko ya mwanae kua Mwinyigoha nae alikua ni mmoja wa wafuasi wa Dini ya Waufi

“Habari zenu..” alisalimia Sheikh Jabu baada ya kuingia uani

“Nzuri..” waliitikia kwa pamoja, wengine wakamuamkia

“Poleni na matatizo jamani”

“Matatizo ya kujitakia tu haya, huyu mwanamke anajua Masu alipo ila anataka kutuchezea tu vichwa” Mzee kikoko alijibu kwa hamaki ya hali yajuu

“Hebu Bw Kikoko njoo faragha kidogo” Wakasogea pembeni Sheikh Jabu, Mwinyigoha, na Kikoko

“Imekuaje tena mzee mwenzangu naona kuna polisi huku namuona mkweo analia, kuna nini hasa?”

Kikoko akaanza kusimulia kila kitu kuanzia alipofikapale mpaka Masu alivyotoweka katika mazingira ya kutatanisha

“Umefanya makosa makubwa Bw Kikoko” alijibu Sheikh Jabu baada ya kusikiliza maelezo ya Kikoko

“Kivipi?”

“Kwanza haukupaswa kuanza kuongea na Masu masuala ya kumuacha huyu mwanamke wake kwakua akili ya Masu bado haijatulia kabisa, Pili umefanya makosa kumpiga makofi huyo binti hiyo ni kesi kubwa ikifikishwa mahakamani inaweza kukuletea dhahama kubwa sana” Maneno yale yalimuingia sana Kikoko sasa akawa anaanza kujuta lakinitayari ameshatenda kosa na waswahili wanasema majuto ni mjukuu..

“Mzee tunaomba tuelekee kituoni tafadhali..” Afande mmoja alimuita Kikoko ili waondoke nae

*****

Baada ya Masu(Shamsa) kuongea na Hunudu kwa muda mrefu Hunudu akatoka na kuaga kisha akaondoka zake, Shamsa alizidi kuumia sana kwa ndani. Alitamani wale kina mama wajue kua yeye ni mwanamke na wala haitwi Shamsa kama wanavyomuita, yeye ni Mwanaume na anaitwa Masu lakini hakuweza kufanya hivyo, alitamani hata ikiwezekana Baba yake na mkewe wangejua mahala alipo ili wamsaidie kumuokoa lakini haikuwezekana, alitamani angepata walau dakika moja tu kuonana na Mzee Kishindo ambae ndie alionekana kua mkombozi wake lakini haikua rahisi tena, Kikubwa zaidi kila akivuta picha kua sasa anatakiwa kuolewa wiki inayofuata ndio alitamani kupasuka lakini kila alipojaribu kujiangalia vizuri alikubali kua sio Mwanaume tena lakini aliendelea kupingana na ukweli huo!

Alikaa mule ndani kwa takribani wiki mbili mpaka akayazoea Mazingira na kuwaelewa wenyeji wake, Yule Somo yake alikua ni Shangazi yake anaitwa Bi Habiba, pia alimjua Bi mkubwa mwingine kua ndie anaejulikana kama mama yake Mzazi anaitwa Bi Shammy. Maisha yaliendelea kusonga mbele kila siku alikua akifundishwa namna ya kwenda kuishi kwa mume, namna ya kumlea na kumtunza mumewe, nk.

Siku moja zikiwa zimebaki siku mbili tu kufika siku ya harusi Masu(Shamsa) akiwa chumbani kwake waliingia watu watatu, Somo yake Bi Habiba na wadada wengine wawili ambao ukiwaangalia tu utajua kua ni magwiji wa unyago na ni watoto wa mjini haswa, mmoja anaitwa Nunuu alikua aemevaa kikuku mguu wa kushoto ile kiMombasa, na huyu mwingine anaitwa Shumbana, kama kawaida yao huja kumfunda mwali wao ambae ni Shamsa(Masu),

Wakiwa wanaendelea na mafunzo yao yaliyojaa mambo ya ajabu ajabu kama muwajuavyo tena Makungwi walikua wakimpa somo Masu(Shamsa) huku wakifanya vitendo kabisa, Masu aliumia sana na mambo yale ghafla

“Jamani lakini mnanifanyia hivi mjue kua mimi si mwanamke, mimi ni Mwanaume kabisa”

“Unasemaje wewe?” aliuliza kwa ukali Bi Habiba huku wake madada wengine wakionesha mshangao mkubwa kutokana na maneno aliyoyatoa mwali wao

“Ndi hivyo, mie Siwezi kuolewa, mimi ni mwanaume” Basi kwa hasira Bi Habiba akainuka kwa jazba mpaka pale alipokua amesimama Masu kasha akamvua kwa nguvu ile kanga aliyokua amejifunga, Masu akabaki kama alivyozaliwa kasha Bi Habiba akamuuliza

“Haya jiangalie una uanamume gani?” baada ya Bi Habiba kusema hivyo wale wapambe wakacheka kwa sauti za kishangingi, kasha Nunuu akadakia

“Dada Habiba kua makini, makungwi wenzio watakua wameshafanya yao hapo haiwezekani ghafla mtoto wakike aseme ahataki kuolewa eti ni mwanaume…”

“Hakuna cha kuchezewa wala nini ni huyu huyu mpuuzi tu anataka kutuharibia shughuli, na hii si mara yake ya kwanza alishakataa kuolewa zaidi ya mara mbili huyu, ngoja tu nimuite Mama yake Bi shammy aje amalizane nae mie nimeshachoka na vioja hivi” Bi Habiba akatoka nje kumuendea Bi Shammy, hawa wadada nao wakatoka nje wakamuacha Masu(Shamsa) akiwa amesimama chumbani kama alivyozaliwa, walipotoka tu nae akainama akachukua kanga yake na kujifunga upya akijua sasa kua mambo yameshavurugika,

Baada ya muda mfupi mlango ukafunguliwa, Masu akajua sasa balaa tayari limeshamfika, lakini aliponyanyua macho yake akakutanisha na macho yako na HUNUDU, Akataka kutaharuki Ila Hunudu akamsogelea na kumuuliza Masu

“Ndo umefanya nini sasa?”

“Kivipi?”

“Kwanini umewaambia kua wewe ni mwanaume?”

“Kwakua kweli mimi ni mwanaume, siwezi kuolewa”

“Sasa hiyo ni hatari kwako, huyu Mama atakufanyia kitu kibaya sana”

“Basi kama mmeamua kunimaliza nyie nimalizeni mmenitesa vya kutosha”

“Khaa, yaani na wewe unajiona umeteswa? Tutakapoanza kukutesa si hautoamini”

“Lakini Hunudu kwanini mnanifanyia hivi?”

“Kwa sababu ya dharau na kiburi chako, na utateswa zaidi muda ukifika, taka usitake utaolewa tu na utazaa tu na kisha ndo mateso yataanza rasmi” Masu alijaribu kumuomba Hunudu amsaidie, Hunudu hakua na shida hata ya kumuangalia Masu usoni lakini baada ya Masu kulalamika sana Hunudu alimuahidi kumsaidia asipate tabu endapo tu kama atakubali kuolewa au Laa sivyo akubali kumtoa mwanae mmoja ndipo atarejeshewa maumbile yake ya kiume na kua huru huku akiwa ni mwanachama wa dini yao ya WAUFI, Kutokana na matatizo kumfika shingoni Masu akakubali kutekeleza matakwa ya Hunudu

“Hii ni nafasi ya mwisho kwako, ukitoa siri na kuvuruga utaratibu sitakuvumilia tena, sawa Masu?”

“Sawa mkuu”

“Ninakurejesha katika maumbile yako ya kiume na kisha nitakuchukua mpaka kwa Mkuu wetu ili ukaungame uovu wako.. halafu nitakurejesha duniani” Baada ya makubaliano hayo, Hunudu akatoa Pete katika mfuko wa suruali yake na kumvisha Masu katika kidole chake cha kati

Baada tu ya kumvisha ile Pete Masu akajishanga ghafla anaanza kubadilika na kurudi katika maumbile yake ya awali, lakini ghafla akaanza kujisikia vibaya mwili mzima, mara kichefuchefu, mara kizunguzungu, yaani akawa taabani kama mtu anaekaribia kukata roho, Masu akajikua anaishiwa nguvu mwishowe akaanguka chini kama mzigo, wakati huo Hunudu alikua akiendelea kumtazama tu bila ya kumsaidia chochote bila shaka alikua akijua alichokifanya ndani ya Pete ile, Masu aljaribu kutaka kumuomba msaada Hunudu lakini mdomo ulikua mzito kutamka maneno huku akitokwa na udenda, ikabidi amuoneshe kwa Ishara kua anamuomba msaada Lakini Hunudu alionekana kutabasamu kwa dharau tu, Masu aliendelea kutapatapa bila msaada wowote mpaka akaanza kuhisi kupoteza fahamu, na kweli baada ya kama dakika mbili Masu akapoteza fahamu..

Akawa kama alietoka usingizini bila ya kujua yuko wapi, Masu alijikuta akiwa Juu ya maji, katika kati ya bahari akiwa peke yake, Hofu ilimuingi sana mwilini, alijaribu kuangaza huku na kule lakini hakuona mtu yoyote, alikua amevaa nguo nyeupe tupu, nguo zake zilikua ni nyepesi mno kiasi cha kumfanya ahisi baridi kali lililotokana na upepo mkali wa baharini, Hakika Masu alikua kama chizi vile maana hakuna alichokielewa, ghafla kwa mbali aliwaona watu kama watano hivi nao wakiwa wamevaa nguo nyeupe, dalili zao zilionyesha wanakwenda usawa ule aliokuwepo yeye, Masu akachanganyikiwa akaamua kuondoka eneo lile huku akikimbia ghafla alipogeuka aliwaona vijana wale nao wakimkimbiza kwa kasi ya ajabu, alijitahidi kuongeza kasi ya kukimbia lakini vijanawale nao walizidi kumkaribia, alipoangalia mbelea aliona mnyama mkubwa mithili ya Kiboko lakini hakua kiboko, nae mnyama huyo alikua akikutana sasa uso kwa uso na Masu, Mnyama huyo alikua akiunguruma kwa sauti kali

kama Radi vile, Masu alipomuona mnyama Yule akajikuta anapiga kelele hovyo kama mwendawazimu

“Uwiiiiiiiiiiiiiiii, Nakufaaaaaaaaa”

Ghafla akajikuta ametokea tena kule Bafuni kwake alikokua anaoga mara ya kwanza, Masu hakuamini kama amerudi huku tena, alikua anahema kwa nguvu sana,

*****

Mzee Kikoko na Sheikh Jabu walikua wakijadiliana nini cha kufanya ili ile kesi isifikishwe Polisi ndipo ghafla wakasikiahiyo Sauti kali ya Masukutoka Bafuni, wote wakashtuka, hawakutegemea kusikia sauti ile, haraka wakakimbilia kule bafuni wakiwa pamoja na wale maaskari, na kweli wakamkuta Masu akiwa amesimama, kila mtu aliogopa kumsogelea, maana ilikua ni kama mazingaombwe vile, hata maafande wale walioonekana kua ni majasiri nao walipigwa na butwaa, hakuelewa kabisa kinachoendelea,

Safari hii Masu alikua amevaa nguo nyeupe alizotoka nazo kule baharini, kidoleni alikua na ile Pete aliyovishwa na Hunudu, Sheikh Jabu alijikaza na kumshika mkono kisha akamtoa nje ya bafu, Masu bado alikua hajielewielewi wala haelewi amefikaje tena huku ghafla kiasi kile

“We Uliku wapi?” aliuliza Mzee Kikoko lakini swali lake lilikatizwa na Sheikh Jabu

“Bwana Kikoko huu sio muda wa kuongea mambo hayo” Jabu akamshika mkono Msu mpaka ndani huku nyuma akifuatwa na Mzee Kikoko na sheikh Mwinyigoha, baada ya kufika ndani na kuketi ndipo Sheikh Jabu akamuuliza Masu

“Vipi umeshakula?” Masu alijibu tu kwa kutikisa kichwa kua ameshakula

“Ehnhee imekuaje tena?” Jabu alikua akimuuliza Masu maswali kwa mitego ya hali ya juu, lakinikabla Masu hajajibu kitu macho yake yakapiga kwenye kidole cha sheikh Mwinyigoha, Naam akaona Pete kubwa nyekundu, alipojiangalia kwenye kidole chake akagundua ni pete kama aliyoivaa yeye, ni PETE ya waufi

“Noooooo” Masu alipiga kelele huko akmsonta sheikh Mwinyigoha, watu wote walitahayari, viti vikawa vichungu wakasimama juu, lakini Sheikh jabu alikua ni jasiri sana aliendelea kumshika tu masu huku akimuhoji

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)