MZIMU WA WAUFU (9)

0

SEHEMU YA TISA
TULIPOISHIA...
“Noooooo” Masu alipiga kelele huko akmsonta sheikh Mwinyigoha, watu wote walitahayari, viti vikawa vichungu wakasimama juu, lakini Sheikh jabu alikua ni jasiri sana aliendelea kumshika tu masu huku akimuhoji

KAMA UNASOMA SIMULIZI HII NJE YA APPLICATION YA CnZ Media INSTALL ILI USIPITWE NA MIENDELEZO

SASA TUENDELEE...
“We una tatizo gani?”

“Huyu mzee hafai, si shekh huyu, ni mfuasi wa Waufi”

BAADA ya Masu kumtuhumu sheikh Mwinyigoha kua nae ni mmoja wa wafuasi wa Dini ya Waufi kila mmoja akapigwa na butwaa, lakini kabla hawajamjibu chochote Masu akendelea kusema

“Hiyo Pete aliyoivaa ni kama hii yangu, zote ni za Waufi” Mzee Kikoko akashtuka, akamuangalia usoni Sheikh Jabu, kasha kwa pamoja wakamuangalia kidoleni Sheikh Mwinyigoha lakini cha ajabu hawakuiona hiyo Pete

“Pete gani tena Masu? Mbona hana Pete yoyote” Sheikh Jabu aliongea kwa utulivu kiasi,

“Jamani pete si hii hapo tena ni kubwa tu inaonekana vizuri” Masu alipomuangalia Mwinyigoha akaiona pete ile kidoleni, sasa ikawa ni kama muujiza yaani Masu anaiona ile pete lakini wazee wake hawaioni, Mzee Kikoko akawa anatikisa kichwa kwa unyonge kabisa akiamini kua sasa mwanae amaeanza kuchanganyikiwa, wakati wote wakiwa wamepatwa na mfadhaiko Masu akawaponyoka na kutoka nje

“Sasa unaenda wapi wewe Masu” alihoji Mzee Kikoko lakini masu hakujibu kitu akaondoka kwa kasi.. Hali ya simanzi ikazidi kutamalaki pale nyumbani kila mtu sasa aliamini kua Masu amechanganyikiwa

“Itakua Masu amechanganyikiwa tu” alisema Sheikh Mwinyigoha

“Hapana, Masu ni mzima kabisa ila hapa kuna jambo tu, tena kubwa sana” alidakia Sheikh Jabu

“Ni jambo gani sasa lisilojulikana?”

“Cha kujiuliza ilikuaje Masu akapotelea Bafuni, kisha akarudi ghafla akiwa amevaa nguo zingine?”

Kabla Mwinyigoha hajajibu ghafla akadakia Yule Askari polisi huku akimuangalia usono Judith mke wa Masu “Tena akiwa na Pete kubwa, au hua anayo siku zote?”

“No, sijawahi kumuona nayo hata sikumoja” alijibu Judith huku akitokwa na Machozi

“No ndio nini sasa? Ongea Kiswahili ueleweke, unataka kuleta nyodo za kizungu hapa wakati mmeshamroga mwanangu, na wewe ndo chanzo” Kikoko alimkaripia Juddy mpaka kila mtu akashangaa maana hapakua na haja ya kuleta mada mpya

*****

‘Ngo! Ngo! Ngo’

Mlango wa mbele uligongwa kwa nguvu sana, ni maeneo ya Tabata Matumbi, nyumbani kwa mzee Kishindo, wakati huo Mzee Kishindo alikua chumbani akimalizia kuswali hivyo hakuweza kujibu hodi ile, akaendelea tu kuswali lakini kelele za kugongwa kwa mlango zilimshtua sana maana mlango ulikua ukigongwa kwa nguvu bila shaka palikua na mtu aliekua na shida ya haraka sana au mtu aliekuja kiushari vilivyo,

“Mzee Kishindo! Mzee Kishindo!”

Japo Mzee Kishindo hakumjibu kitu kwa kuhofia kuharibu swala yake kwani kwa mujibu wa dini yake hakupaswa kuacha kusali na kumjibu mtu lakini tayari alikua ameishaing’amua sauti inayomuita, Naam ilikua ni sauti ilyojaa mchoko na hofu, ni sauti ya MASUMBUKO. Baada ya kumaliza kuswali Mzee Kishindo akaenda mpaka kwenye mlango wake akaufungua taratibu ili achungulie nje ndipo ghafla Masu akaingia kwa kasi ndani huku akitweta, Mzee Kishindo alijikaza japo alikua nae ameshtuka kwa hali aliyokua nayo Masu ikabidi tu aurudishe mlango akihofia kujifungia nae ndani, alipomgeukia Masu alikua akilia sana kwa uchungu

“Unalia nini Masu?” alianza Mzee Kishindo kwa kumtupia swali Masu

“Mzee Kishindo, ninateseka sana, napitia kila aina ya taabu, Waufi wataniua” Baada ya Masu kujibu vile Mzee kishindo alikua amesimama wima, akamsogelea mpaka pale alipokua ameketi nae akaketi pamoja nae

“Pole sana mwanangu”

“Sijapoa hata kidogo”

“Nadhani unakumbuka nilishakudokeza kua tatizo lako ni kubwa sana..”

“Ndio nakumbuka, na ndio maana nimekimbilia kwako unisaidie”

“Natamani sana kukusaidia ila baba yako mzee Kikoko anasumbua sana, ananitusi mbele za watu na kusema kua mimi ndie ninaekuroga na ananipa kila aina ya vitisho kwa ajili yako, unakumbuka nilikuuliza kua una kifua? Ukasema ndio, sasa ikawaje tena hata kabla sijakuelezea ukaanza kuvujisha habari mpaka zikamfikia baba yako na sasa unanileyea tabu mie?”

“Mzee Kishindo huu sio muda wa kulaumiana kabisa, kwa sasa nahitaji tu msaada wako, pia mimi sijamueleza chochote baba ila nadhani ni mke wangu tu huyo kwakua walimbana sana baada ya mimi kuanguka” Baada ya maelezo hayo ya Masu Mzee Kishindo akainuka na kutoka uani kwake akamuacha Masu peke yake pale Sebuleni, Kisha baada ya muda mfupi Mzee Kishindo akarudi akiwa amebeba sahani mbili ya chakula, moja akampa Masu alionekana kua na njaa sana na nyigine akawa nayo yeye mwenyewe mkononi..

“Kula kwanza upate nguvu mpya” aliongea Mzee kishindo

“Ahsante lakini mie nimeshiba”

“Hujashiba chochote zaidi ya kuvimbiwa na hofu tu, kula ukimaliza tufanye mazungumzo” Basi Masu japo alijisikia kushiba ikabidi tu aanze kula hivyo hivyo ili kumridhisha Mzee Kishindo aweze kumpa msaada maana Mzee hyu ndie anaeonekana kujua kila kitu kuhusiana na tatizo la Masu kulazimishwa kujiunga na Dini ya Waufi, Iliwachukua takribani dakika karibi ishirini wakawa wamemaliza kula na tayari mke wa Mzee Kishindo alikua ameshawasogezea maji ya kunywa na kunawa. Baada ya kumaliza kunywa maji na kunawa ndipo mazungumzo yakaanza tena

“Hebu nihabarishe kwa mukhtasari mambo yako yakoje” alianza mzee Kishindo

“Mkasa wangu ulianzia kwenye ndoto, kuna siku nilikua nimelala…”

“Hapana huko unaanzia mbali ulishanihadithia tukiwa kule dukani, sasa anzia tangu baada ya pale” Kishindo alimkatisha Masu, maana Masu alikua ameshamsimulia jinsi tatizo lake lilivyomuanza, ikabidi sasa Masu aanzie pale alipokutana na Hunudu kwa mara ya kwanza ikiwa ni nje ya Ndito, ilikua ni stori ndefu nay a kuogofya sana, Masu alikua akiihadithia kwa uchungu mpaka anadondosha machozi, Mzee Kishindo alikua akimbembeleza huku akimfuta machozi mpaka akamalizia tukio la mwisho kule bafuni

“We ni motto wa kiume hivyo achana na mambo ya kulia hovyo, jikaze hii sasa ni vita umeivaa”

“Sawa Mzee”

“Pili nakupongeza kwa ushujaa wako na ujasiri wa kua kila jambo unalisema wazi japo huyo Hunudu anakutishia kua usitoe siri maana ungemtii tu masharti yake ndio ingekua mwanzo wa kukutawala” Masu sasa akawa anamsikiliza kwa makini Mzee Kishindo akiamini kua huenda akapata ukombozi

“Ulishajiuliza kwa nini uliitwa Masumbuko wakati kwenu hakuna hata mmoja katika babu zako aliewahi kuitwa jina hilo?”

“Hapana”

*****

TABORA

Mwaka 19970 ndipo bwana Rashid Kikoko alipohamia rasmi mkoani Tabora akitokea kwao Kigoma, na alipofika tabora alikua akijishughulisha na biashara ya kuuza samaki na dagaa aliokua akiwatoa Kigoma na kuwaleta Tabora, biashara yake ilikua nzuri mno, ilimpa faida nzuri na kubwa, ndani ya muda mfupi tu maisha yake yakawa mazuri nay a kuridhisha, akiwa Tabora alikutana na wazee na vijana wenzie kutoka kigoma ambao wanaishi hapo Tabora huku wakijishughulisha na masuala ya kiutafutaji… Kikoko nae alifanya Biashara zake kwa takribani miaka minne mpaka mwaka 1974 alipokwenda kwao Kigoma kufuatia wito alioitwa na Baba yake mzazi..

Baada ya Kikoko kurudi Kigoma kuitika wito wa baba yake alikutana na baba yake huyo Mzee Hassan Kikoko, kikubwa alichoitiwa alitakiwa sasa Aoe maana umri wake ulikua ni mkubwa na pia uwezo wa kifedha alikua nao, japo alijaribu kutaka kuleta vipingamizi lakini alizidiwa na hoja za baba yake mzazi hivyo ikabidi tu akubali kuoa, Bw Kikoko alirudi mjini Tabora kujipanga kwa ajili ya kutafuta mchumba ndipo akakutana na Bi Kapemba Masanja kutokea Shinyanga nae alikua ni mfanyabiashara akiendea vitenge vya wax huko Bujumbura na kuja kuviuza Kigoma, Tabora, na Shinyanga kwao, Kikoko hakua na pingamizi kua amezama katika huba kwa dada huyo.

Mwaka 1975 Bw Kikoko na Bi Kapemba wakafunga ndoa huko Shinyanga na kisha harusi ikaenda kumaliziwa Kigoma kwa baba yake na Kikoko, ilikua ni sherehe kubwa na ya kifahari, kila mtu aliburudika na kufurahikia harusi hiyo, baada ya sherehe za harusi Kikoko akarudi tabora alikokua ameweka makazi yake ili kuendelea sasa na utafutaji wa Riziki, Maisha ya ndoa yalikua mazuri kwao na miaka alikatika wakiwa na furaha. Tatizo Kubwa lilianza kuchomoza kama uyoga kwenye Kichuguu kutokana na Bi Kapemba kutopata ujauzito. Naam mpaka mwaka 1977 takribani mitatu baada ya ndoa bi mkubwa huyo hakupata ujauzito. Hivyo sasa ndugu zake na Mzee Kikoko wakaanza kuleta ghasia za chini kwa chini na hatimae ghasia zikaota mbawa na kutanda katika anga la huba kati ya Mzee Kikoko na Bi Kapemba. Wenyewe walijitahidi kuyapuuza malalamiko ya ndugu huku wakipambana kutafuta tiba kwa kila mganga mashuhuri waliesikia habari zake, lakini jitihada hazikuzaa matunda, ndipo sasa baba yake na Kikoko

akamuamuru Kikoko aoe mke mwingine ili ampatie watoto kwa kua Bi Kapemba ni Mgumba

Mwaka 1979 kwenye mwezi wa kumi na moja hivi, nakumbuka ilikua ni karibu na mfungo wa Mwezi wa Ramadhani hivi Bw Kikoko ilibidi tu sasa Aoe mke mwingine baada ya mikwara ya haja kutoka kwa familia yake, Alimuoa msichana fulani ambae huyu alikua ni mzawa na mwenyeji wa mkoani Tabora, aliitwa Bi Mwajabu Fundikira, ukoo wa Bi mdogo huyu ni ukoo wa kitemi hivyo ulikua ni ukoo ulioheshimika sana pale mkoani Tabora, akatekeleza suala hilo la kuoa lakini hakumuacha mkewe mkubwa Bi Kapemba Masanja, akawa sasa ana wake wawili, wote akiishi nao tabora. Maisha yakasonga mbele bila ajizi, Kikoko alijitahidi sana kuwaunganisha wakeze hao ili waishi kwa kupendana na kufurahiana, alijitahidi kwa kiasi Fulani kukawa na amani japo matatizo ya chichini hayaepukiki ila yalipojitokeza alijitahidi kuyatatua kwa ustadi wa hali ya juu

Naam mwaka 1980 ndoa ikajibu, Bi Mwajabu alipata ujauzito ilikua ni kwenye mwezi wa kwanza hivi yaani miezi mitatu hivi baada ya kuolewa kwake, kila mmoja alifurahia suala hilo, habari zikafika mpaka Kigoma nyumbani kwao na Kikoko nao wakafurahi sana, Lakini hali ikawa tofauti kwa Bi Kapemba kwa kua yeye hakujaaliwa kupata ujauzito hivyo alijiona kama mzigo, lakini Mzee Kikoko aliendelea kumfariji mkewe huyo bila ya kumtenga, ilipofika kwenye mwezi wa tano na ujauzio wa Bi Mwajabu ukiwa nao na miezi mitano, ghafla Bi Kapemba akaomba ruhusa kwa mumewe ambae ni Mzee Kikoko ili akapumzishe akili kidogo nyumbani kwao Shinyanga ikiwa ni pamoja na kwenda kuwasalimu wazazi wake, Mzee Kikoko alimkubalia, akamuandalia safari na kasha wiki moja baadae akaondoka na kwenda Shinyanga..

CHA AJABU, Ilipofika kwenye mwezi wa sita ghafla hali ya Bi Mwajabu ikaanza kubadilika, kila siku lile tumbolake la ujauzito likaanza kuyeyuka mithili ya pulizo lililotoboka na hatimae ujauzito ukatoweka kabisa

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendeleza Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)