Mtunzi: ___
SEHEMU YA TANO
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
“Nalijua hilo”, Joram alisema. “Siendi kwa sababu ya sura wala sauti yake kama nilivyosema. Kilichonivutia ni maelezo yake. Anasema yeye ni yule msichana ambaye alipigwa pale baa ya Forest of Flowers.
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
TUENDELEE...
Anadai kuwa nia yake ni kunishukru pamoja na kunipa habari fulani ambayo inasisimua”.
“Malaya kama yule! Hana habari yoyote. Anachotaka ni kukupata wewe tu”.
“Hapana”, Joram alimkatisha. Sauti yake ndiyo iliyonifanya nivutiwe hata kumwahidi kuwa nitakwenda. Inavyoonyesha kuna kitu zaidi ya anachosema. Nahitaji kujua ni nini. Zaidi ya sauti, nadhani utakumbuka kuwa jana binti huyo alilia sana akilitaja jina langu. Sijui alivyonijua”.
“Ni mimi niliyekutaja kwanza”.
“Ni kweli, lakini hiyo siyo sababu ya kumfanya aniite jina langu mara nyigi tena kwa ufasaha kiasi kile. Ni kama mtu aliyekuwa akinifahamu kitambo”.
“Wewe si mtu unayefafamika Joram?”.
“Pamoja na hilo”, Joram aliongeza. “Ni wapi alikopata namba yangu ya simu? Tuseme kwenye vitabu vya simu. Kwa nini ahangaike kiasi hicho? Na kwa nini iwe mapema hivyo? Neema, huoni ni mwujiza huu? Jana tu alikuwa hoi. Leo anazungumza kwa uchangamfu kabisa na yuko logi badala ya hospitali! Huoni kama kuna jambo hapo? Yaonyesha kuwa ananitafuta. Yawezekana hata jana alikuwa akinihitaji mimi tu hakuwa majeruhi wala mgonjwa!” Akasita kidogo kabla hajaongeza kwa sauti ya chini akisema: Na atanipata. Kwa muda mrefu nimekuwa sina kazi ya kufanya”.
Wakati huo Joram alikuwa wima akivuta droo hii na ile, akiweka hiki mifukoni na hiki kiunoni. Mara akaanza hatua za haraka kuelekea mlangoni.
“Yaani unakwenda Joram, mara hii!”, Neema aliuliza kwa mshangao.
“Naam”.
“Mapema namna hiyo? Si umemwambia baada ya saa moja?”.
“Niliamua kumdanganya. Siamini kama yeye ananieleza ukweli mtupu, hivyo nami sioni ubaya wa kumweleza uongo kidogo. Nataka kufika mapema kidogo nione anachofanya”.
“Lakini ujihadhari”, Neema alimwambia wakati akivuka kizingiti cha mlango.
“Usijali Neema”, Joram akamjibu bila kugeuka nyuma.
“Anakuja! Na atakufa!” Proper alimwambia Waridi.
“Ondoa hiyo mikunjo ya hofu usoni uvae suruali yako nzuri kama ilivyo. Akifika mpe tabasamu, mpe mapenzi, kisha mkaribibishe pombe. Usisahau chupa hilo hapo ni kwa ajii yake, akionja tu yamekwisha, asipoinywa mpake hii kwa hila”.
Walikuwa katika chumba fulani, ghorofa fulani, katika jumba hili la light ambalo liko katika mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam. Proper alikodi chumba hiki kwa ajili ya kazi hii tangu jana alipomtoa Waridi kule hospitali. Usiku mzima aliutmia kumtisha Waridi kwa kila namna pale alipojaribu kuleta ubishi. Kisha alikuwa amemlazimisha kufanya naye mapenzi kwa njia zake za kinyama. Ilipofika alfajiri ndipo wakaanza kupanga mikakati ya mauaji.
Waridi alivishwa vazi jeupe la hariri, vazi hili lilifichua kila kitu kilichofaa kifichwa katika mwili wake. Kila jicho liliweza kuona mwili mzuri wa msichana huyo, ulikuwa ukimelelemeta kwa wekundu ndani ya mavazi hayo. Uso wake pia ulikuwa “kioo” kwa uzuri wake wa asili ulioshinikizwa kwa vipodozi murua vilivyotumiwa kistaarabu. Nywele zake zilitengenezwa kwa ile mitindo ya kisasa. Kwa kila hali, msichana huyu alionekana mtu tofauti kabisa na yule binti ambaye usiku wa jana tu alilala chini pale baa akiwa nusu uchi, akilia. Huyu alikuwa katika hali ambayo ilikusudiwa na ilitosha kuushinda ukaidi wa Joram Kiango dhidi ya wasichana warembo.
“Uwe msichana hodari. Ni kazi ndogo tu. Baada ya hapo utakuwa huru. Nitakulipa pesa za kutosha ukanisubiri Nairobi. Kutoka hapo tutakwenda zetu London au New York, tukatumie. Unasemaje?”.
Waridi hakujibu.
“Mbona husemi neno?” Proper alimwuliza Waridi. “Hofu ya nini? Hii ni kazi ndogo mno kuliko ile uliyoifanya kwa Bomba. Na bado itakulipa pesa nyingi zaidi ya ule uchafu uliochukua. Jitie furaha na ucheke kidogo”.
Kikcheko kilikuwa mbali na Waridi. Aliendelea kuduaa kama mzoga akisubiri lolote aliloelekezwa kulifanya. Hilo likamchukiza sana Proper.
Akasema. “Sikia wewe, endapo utavuruga tena mpango huu, sitasita kukuua papa hapa. Sasa hivi bado dakika ishirini Joram ataingia hapa. Nitakuwa chumba cha pili nikiangalia kila kitu. Ukishindwa au kuvuruga mpango huu nitakuua wewe na huyo Joram papa hapa. Nitakuua wewe kwanza na kisha Joram kwa hili hapa”, akatoa bastola ndogo kutoka kwenye mfuko wa koti lake.
“Sipendi kukuua”, Proper aliongeza. “Lakini ukinilazimisha nitaitumia kuwaua”. Akaitazama tena saa yake. “JOram anaweza kuwa anakuja sasa. Natoka. Kumbuka kuwa niko karibu na tayari kukuua endapo utavuruga mpango huu. Sawa? Proper alitoka na kumwacha Waridi ameduwaa kama alivyokuwa.
Baada ya dakika kadhaa mlango wa chumba hiki uligogwa, kisha ukafunguliwa. Joram Kiango alichungulia ndani na kisha kuingia polepole macho yake yakiwa yamepumbazwa na uzuri wa Waridi. Hakutegemea.
“Sisiter… mimi ni mgeni wako nadhani. Naitwa Joram Kiango”, alieleza Joram huku akiandaa tabasamu ambalo alijua linamfaa binti mzuri kama huyu.
Ndipo Waridi alipogeuka kumtazama.
Kama kuna wanawake ambao husimbua mioyo ya wanaume mara tu watokeapo mbele yao hata wanaume hao wakajisahau na kuzisahau shughuli zao, basi ni dhahiri pia wapo wanaume ambao huisumbua mioyo ya wanawake kwa kiwango kile kile. Na kama kweli wapo, miongoni mwao yumo Joram Kiango. Hayo yalijidhihirisha baada ya Waridi kumtia machoni Joram alipoingia chumbani.
Moyo wake ulipoteza mapigo kwa sekunde kadhaa. Roho yake ilihisi kupaa nje ya mwili wake. Kadhalika, damu ilimsisimka kiasi cha kumfanya ahisi ganzi mwili mzima. Hivyo, hakuweza kuyaondoa macho yake juu ya umbo la Joram ambaye alimsogelea polepole. Nusura wazimu umpande Waridi alipoona uso na tabasamu la Joram, lililotosha kuwa tiba kwa maradhi yake. Maradhi aliyoamini kuwa hayangeweza kutibika.
Kwa bahati mbaya, Waridi hakuwahi kupenda mwanaume katika maisha yake. Hivyo hakujua mapenzi ni nini. Hakuwahi kuyaonja. Kama angejua, angefahamu nini kitatokea. Badala yake alihisi maumivu moyoni na huzuni kubwa akilini mwake. Akanusurika kutokwa na machozi. Hakujua nini kinamtokea. Isipokuwa kitu kimoja tu alikifahamu, Joram hakuwa mtu wa kufa, Hakuona sababu ya kumwua, Asingeweza…
Tazama alivyosimama mbele yake kwa upendo na utulivu kama malaika asiye na hatia. Tazama anavyochekelea kwa furaha kama nuru, Mtazame. La, huyu kijana si mtu wa kufa. Waridi akawa ameamua hivyo.
“Nadhani mimi ni mgeni wako, mpenzi, Joram alisema tena, akinyoosha mkono wake kumgusa Waridi kwenye bega lake la kuume.
Joram alikuwa ameshangazwa na uzuri wa msicha huyu. Vipi wengine waumbwe kwa upendeleo kiasi hiki wakati wengine wasitofautiane sana na vinyago? alijiuliza. Mavazi mazuri ya msichana huyu pia yalimchanganya Joram; yalikuwa mavazi mapya ya thamani kubwa, kisha ya kihuni kama yalivyondaliwa mahususi kwa ajili ya kumtongoza! Hicho hakikumshangaza Joram, Lakini alishangazwa na uso mzuri wa msichana huyu ukiwa katika dimbwi la majonzi, mashaka, hofu na msiba. Hilo halikumshangaza hata kidogo.
“Ndio…ka… karibu kaka”, waridi alianza kusema huku akibabaika,
Joram alimvuta mkono na kumwongoza hadi kitandani, ambako alimketisha kisha naye akaketi kando yake huku akiendelea kuushika mkono wa Waridi.
“Nilikwambia kuwa sauti yako ni tamu kama ilivyo sura yako? Naamini sikukosea. Ama kweli umeumbika bibie. Ulimhonga nini muumba hata akakupendelea?”
Sauti ya Joram, tabasamu lake likasindikiza kila neno, hali hiyo ikamfanya Waridi aanze kuchangamka. Akasahau yote yaliyokuwa mbele yake na kujikuta kazama katika maongezi na Joram. Katika kipindi hicho kifupi bila kujifahamu Waridi alijikuta tayari akiwa ameufunua moyo wake wote kwa Joram, akimsimulia matatizo yake yote. Alipotanabahi alikuwa akisema: “Najisikia kutoweka nje ya nchi hii”.
“Kwanini?”.
Swahili hilo lilimzindia Waridi. Hakujua yapi alikuwa tayari kuyatamka ambayo hayakustahili kuiacha milki ya kinywa chake, Hofu ikamrejea. Akalikumbua jukumu lililokuwa mbele yake: kumfanya kijana huyu kuwa marehemu. Ama ni yeye atajayefanywa marehemu.
Hofu hiyo, ilizidi baada ya Joram kuinuka na kuiendea meza iliyokuwa na chupa mbili za pombe huku akisema: “Bia hii? Unaonaje nikianza kuimimina tumboni mwangu ili kupoza joto la Dar es Salaam kabla hujanieleza sababu za kuniita hapa? Siamini kwama kweli umeniita kwa ajili ya kunishukuru tu, yaani hilo likusukume kunitafuta…”
“Usinywe hiyo pombe”, Waridi alifoka.
“Kwanini mpenzi? Nilidhani umeiandaa kwa ajili yangu”, Joram alifuatwa na tabasamu la kukata na shoka.
Waridi alikuwa akitetemeka. Lakini asingeweza kusahau maneno ya yule mtu katili Proper alipomwambia: “Nitakuwa chumba cha pili… Ukishindwa tena nitakuua papa hapa…” Waridi hakupenda kufa, lakini pia hakuwa tayari kumuona kijana huyu asiye na hatia, afe. Afanye nini? Kwa kutojua la kufanya akaanza kulia. Mikono ya Joram ilitua tena mabegani kwa Waridi akimfariji na kumkumbatia huku akisema.
“Kama hutaki ninywe hii bia ni wazi kwamba kuna zawadi kubwa na tamu zaidi ya bia uliyoiandaa kwa ajili yangu. Kwa bahati mbaya nina mazoea ya kunywa pombe kabla ya yote. Kwa maana hiyo niruhusu ninywe bia moja tafadhali”.
“Usi…” Waridi alijaribu kufoka tena. Joram alimzuia kwa kuuziba mdomo wake kwa kiganja cha mkono wake huku akiweka kinywa chakr karibu na sikio la Waridi, akamnong’oneza.
“Najua kitakachotokea. Sinywi pombe hiyo. Acha nijifanye kama nakunywa ili nimpumbaze huyu anayetaka kuniua. Nitakuomba wewe uwe msiri wangu. Mwache aamini kuwa ameniua. Mwache kila mtu aamini kuwa nimekufa. Nataka kufahamu hawa waliokusudia kuniua jambo gani wanakusudia kutenda”.
waridi aliduaa. “Ume… umewezaje kujua? aliuliza kwa kunong’ona.
“Niliwahi kufika eneo hili mapema na kumsikia alivyokuwa akikuamru. Nawe pia lazima ufahamu kuwa uko hatarini. Huyu ni mtu hatari. Mara tuu utakapotoka hapa, toroka uende kokote asikoweza kukufikia. Sasa acha nijifanye nainywa pombe yake”. Joram akaongeza sauti kusema. “Glasi? Acha ninywe kihuni”.
Joram aliifungua chumpa moja na kuingia nayo msalani ambako aliimimina nusu kwenye tundu la choo, Akarudi na kuitua mezani huku akiendelea kuongea na Warid, mazungumzo yao yalifanyika taratibu kwa sauti ya chini. Mara kadhaa Joram alimshika waridi na kumtomasa hapa na pale kwa ajili ya kumtoa hofu.
“sasa mpenzi sikia”, aliongeza. “Ninaye mgeni ambaye atakuja ofisini kwangu baada ya nusu saa kuanzia sasa.
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)