Notification
Tidak ada notifikasi baru.

MWANAFUNZI MCHAWI (16)

Mtunzi: Enea Faidy

SEHEMU YA KUMI NA SITA
TULIPOISHIA...
Furaha take aliyoitafuta kwa muda mrefu sasa ilitawala moyoni mwa Mansoor kwani tayari alishampata ampendae. Dorice hakuwa na furaha sana na ndoa yake kwani mawazo yake yote yalikuwa juu ya uhai wa mpenzi wake wa Moyo Eddy Alloyce. Kila mara alimfikiria Eddy,

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
na aliona amefanya kosa kubwa sana kufunga ndoa na jini.

Wakiwa wametulia tuli katika pozi la mahaba, Dorice na Mansoor. Dorice alifungua kinywa na kuyasema Yale yanayomsibu, masuala yanayousumbua moyo wake kwa kipindi kirefu.

"Mansoor..!"

"Niite Mume wangu.." Alisema Mansoor, Dorice akacheka kidogo.

"Mume wangu!"

"Naam! Hapo sawa mke wangu.!"

"Nataka nikukumbushe kitu."

"Sema tu mpenzi wa roho yangu!"

"Vipi kuhusu ahadi yako ya kunipeleka duniani na kumwokoa Eddy?"

Maneno hayo yaliupasua moyo wa Mansoor na kuiyeyusha ghafla furaha yake. Hakutamani wala hakuwa tayari kuwa mbali na mkewe, alimpenda sana na alitamani awe wake daima milele. Kwake, Doreen alikuwa kama chanda ambayo bila hiyo Pete haina uthamanu wowote, machozi yalimlenga machoni mwake.

"Unataka kuondoka?"

"Ikumbuke ahadi yako..."

"Mke wangu unataka kunitenga? Unadhani ukienda duniani utakuwa wangu tena????"alisema Mansoor. Dorice akamtazama kwa mshangao.

..DORICE alimshangaa Mumewe Mansoor kwa maneno yake. Machozi yalimlengalenga machoni mwake kisha akajiondoa kifuani kwa Mansoor na kujitenga kando.

"Vipi mke wangu?"

"Najuta Mansoor.. Najuta sana kukukubalia, sikujua kama hautakuwa mwaminifu kwa ahadi zako!" Alisema Dorice kwa hasira.

"Sina maana mbaya mke wangu mpenzi.. Usinielewe vibaya tafadhali...Nakupenda sana!"

"Unanipenda? Unanipenda nini uongo mtupu..!" Alisema Dorice kwa hasira huku machozi yakimshuka mashavuni mwake. Alijikuta anamchukia Mansoor kupita kiasi. Hakutaka hata kumsogelea karibu.

"Baby! Nimekuelewa basi naomba uwe na amani moyoni mwako" alisema Mansoor huku akimsogelea Dorice na kutaka kumkumbatia lakini Dorice alimsukumia kando Mansoor na kuongeza kilio chake.

"Sitaki uniguse mpaka utakaponiambia ni lini utatimiza ahadi yako"

"Baada ya wiki moja nitaitimiza ahadi yako..!" Alisema Mansoor kwa huzuni kwani alijua ni kiasi gani Dorice alimpenda Eddy na alijua kwamba endapo angemrudisha Dorice duniani basi angemsahau Yeye na kuponda raha na Eddy. Kila alipofikiria hilo Mansoor aliumia sana moyoni mwake. Hakutamani kumkosa Dorice lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kutunza uaminifu wa kutimiza ahadi yake.

"Una uhakika utanipeleka baada ya wiki moja?" Aliuliza Dorice akimtazama Mansoor.

"Ndio.. Usijali!" Mansoor alijibu kwa unyonge sana.

"Hapo umenifurahisha!" Alisema Dorice na kumkumbatia Mansoor.

"Lakini kabla haujaenda huko kuna kitu muhimu unatakiwa ufanye!" Alisema Mansoor akiwa bado amemkumbatia Doreen.

"Kitu gani?" Aliuliza Dorice.

Mansoor alimuachia Dorice kisha akanyoosha mkono wake na kumuonesha Dorice kiganja cha mkono wake. Kwa mshangao kidogo, Dorice akatazama kiganja cha Mansoor.

"Unaona nini hapa?"

"Sioni kitu.."

"Huoni kitu? Hebu tazama vizuri"

"Naona Pete" alijibu Dorice kwa mshangao.

*********

Eddy alimtazama kwa mshangao mlinzi wao. Alimkazia macho huku akimwomba msamaha kwa kumjibu vibaya hapo mwanzo.

"Usijali.. Najua matatizo yako yanakufanya uwe hivyo" alisema mlinzi.

"Sasa utanisaidiaje? Maana nateseka sana!"

"Nitakusaidia tu wala usiwe na haraka... "

"Lazima niwe na haraka Anko maana mpaka sasa hivi sijawahi hata kukojoa!"

"Mmh! Haraka zilimponza chura zikafanya awe na mabaka. Vuta subira tu maana umefanyiwa mchezo mbaya sana." Alisema mlinzi yule huku akijifunika vyema shuka lake na kujigesha ukutani ili amalizie usingizi wake. Lakini ghafla akapigwa Kofi zito shavuni, aliruka kama kuku aliyeona hatari. Kabla hajakaa sawa Kofi lingine zito lilitua shavuni kwake, akajishika shavu na kutazama kama alikuwa amechanika lakini haikuwa hivyo kwani hakukuwa na damu yoyote ile.

Mlinzi yule akatazama huku na kule lakini hakuona Mtu aliyempiga makofi Yale mazito yaliyotua shavuni kama radi wakati wa mvya Kali.

"Vipi Anko?"

"Ah.. Hanna kitu.. Niko sawa tu.."

"Mbona umeruka sana?"

"Usijali Eddy.. Mimi nimeaga kwetu Musoma.. Niliwaaga wajita wenzangu..!" Alisema Mlinzi huku akisikilizia maumivu makali ya vibao alivyopigwa.

"Sikuelewi Anko ."

"Nimeaga.. Hakuna wa kunichezea!" Alizidi kuropoka mlinzi yule kisha akatulia kimya. Mawazo tele yakamjaa kuhusu vibao vile alivyopigwa kiuchawi. Aliwaza sana kwani alikuwa ana zindiko kubwa sana, sasa kwanini apigwe vile wakati ana kings anayoiamini? Alijiuliza sana bila kupata jibu.

Kulipambazuka kabisa, kimwanga kidogo cha jua kilianza kuchomoza kwa mbali. Wakati huo Mr Alloyce alikuwa kwenye gari take kuelekea msituni alikopotelea Mama Eddy.

Kichwani mwake alifikiria sana jinsi ya kutatua matatizo yanayoikumba familia yake. Hakupata njia kamili ya kuweza kutatua matatizo yake.

Aliendesha gari kwa mwendo wa SAA moja na nusu hatimaye akawasili kwenye eneo alilotakiwa kufika, akashuka kwenye gari na kuangaza macho yake huku na kule kuona kama atamwona mkewe.

******

"Amka mama Pamela kuna jambo nataka nikuambie"

"Bwana utaniambia asubuhi"

"Huu ndo muda mzuri wa kukuambia lakini kama hutaki basi.. " Alisema baba Pamela kwa sauti ya utulivu sana . Licha ya ubishi aliokuwa nao mama Pamela katika suala la kuamka lakini ilimbidi tu aamke ili amsikilize mume wake. Kwani alijua huenda ana jambo muhimu anataka kumueleza wakati ule.

"Niambie basi mume wangu!" Alisema mama Pamela huku akipiga miayo ya uchovu wa usingizi.

"Asubuhi ya Leo nina safari kikazi.."

"Unaenda wapi?" Aliuliza mama Pamela.

"Naenda Arusha mke wangu... Nilitemea nikuambie Jana ila uliniudhi mpaka nikashindwa kukuambia"

"Mmh! Utakaa muda gani?"

"Mwezi mmoja!"

"Mwezi mzima? Mbona mrefu hivyo?"

"Ndio hivyo mke wangu ni masuala ya kazi tu, sina jinsi"

"Imekuwa ghafla!"

"Ndio nimepewa taarifa juzi jioni, lakini...."

"Lakini nini?" Alishtuka mama Pamela

"Nikiondoka tu, na huyo mgeni wako atoke hapa nyumbani kwangu"

Alisema Baba Pamela kwa sauti ya msisitizo sana akidhihirisha kuwa alimaanisha kile alichokisema.

"Baba Pamela utaniudhi.. Sitaki maudhi yako na hiyo roho mbaya yako"

"IPO siku utafahamu kwanini nasema hivo.. Kaa vizuri na Mungu utafahamu mengi!" Alisema Baba Pamela kisha akajifunika vizuri na kulala ili aamke baada ya nusu saa.

Mama Pamela alibaki na mawazo mengi sana ila katu hakuwa tayari kumwacha Doreen aende zake. Alimwonea huruma binti yule kwani alishamwambia historian nzima ya maisha yake.' Mime wangu sijui yukoje siku hizi.. Ana roho mbaya.. Simfukuzi ng'oo Doreen. Mtoto ana adabu tena mstaarabu' aliwaza Bi Carolina.

Asubuhi na Mapema Baba Pamela alijiandaa na kuwahi uwanja wa ndege, Bi Carolina alimsindikiza mumewe hadi uwanja wa Songwe Airport Kisha akamuaga.

"Ila tekeleza nilichokuambia"

"Sawa !" Alijibu Bi Carolina kisha akaingia kwenye gari na kuondoa gari kuelekea nyumbani kwake.

Haukupita muda mrefu Bi Carolina alitia timu nyimbani kwake, akapaki gari na kuingia ndani. Lakini alipoingia ndani alikutana na hali ya utofauti.

.BI CAROLINA alipiga hatua za taratibu kuelekea sebuleni lakini hali iliyokuwemo ndani mle ilizidi kumshangaza kwani alisikia harufu Kali na mbaya ya kitu kuungulia. Alifika sebuleni lakini hakukuta Mtu yeyote, akaamua kwenda jikoni.

Alipoingia jikoni tu, alipiga chafya tatu mfululizo kutokana na moshi mzito ulioambatana na harufu Kali sana uliotawala jikoni mle. Aliisogelea mpaka sehemu ya kupikia akagundua moto uliwashwa na kuna kitu kilichomwa. Akaangalia sufuria zote lakini hakukuta kitu chochote, akabaki na mshangao.

"Doreen!" Aliita Bi Carolina akiwa ameshika mkono kiunoni.

"Abee mama!" Sauti ya Doreen ilisikika kutoka chumbani.

"Njoo huku jikoni"

Bila ya kuchelewa Doreen alifika jikoni kule na kumkuta Bi Carolina akiwa ameshika kiuno akimsubiri kwa hamu amuulize kilichotokea.

"Abee mama" aliitikia Doreen kwa adabu sana.

"Nini kimetokea huku jikoni?"

"Nisamehe mama... Nilitaka kupika.. Ila kwa bahati mbaya nikaunguza kwani sijui kutumia jiko la gesi." Alijitetea Doreen huku akitia huruma sana.

"Ulitaka upike nini asubuhi yote hii?"

"Nili...nilikuta maziwa.. Nyama kwenye friji nikataka nipike.."

"Mara maziwa mara nyama.. Mbona sikuelewi? Haya ulipikia sufuria gani?" Bi Carolina alishindwa kumuelewa Doreen ila kutokana na ugeni aliokuwa nao hakuweza kumfokea sana kwa kuhofu kuwa atajisikia vibaya.

"Nilichukua nyama... Sufuria ilipoungua sana nikaamua kuiosha.." Alisema Doreen akidai kutetemeka kwa woga.

"Sawa ila usirudie tena.. Nitakufundisha jinsi ya kupikia jiko la gesi.."

"Sawa mama" alisema Doreen kwa sauti ya upole iliyojaa hekima ya viwango vya juu.

"Sawa mwanangu nenda kaendelee na kazi zako"

Doreen alitoka jikoni mle na kuelekea chumbani kwake. Alichukua kimfuko cheusi kidogodogo kisha akafungua na kuutoa ungaunga mweusi. Kisha akaweka kiganjani na kusogelea kila kona ya chumba kile na kuupuliza kwa midomo yake. Alifanya hivyo mpaka unga ule ilipoisha, akasogelea kitanda chake na kukaa.

"Hapa sasa nimemaliza kazi... Mpaka huo moshi uishe nitakuwa nimefanikiwa kabisa." Alisema Doreen akitabasamu kwani ule moshi uliotapakaa ndani mle ulisababishwa na Doreen. Alikuwa amechoma dawa ambayo ingewafanya wakaaji wa nyumba ile kumpenda Doreen kupita kiasi, na wasingeweza kumfukuza hata iweje mpaka pale atakapoamua kuondoka yeye mwenyewe.

Aliangalia SAA yake ya mkononi ilikuwa tayari ni saa nne na nusu asubuhi. Doreen alisikia sauti ya Bi Carolina ikimwita. Akatii wito na kumfuata Bi Carolina.

"Abee mama" aliitikia kwa heshima.

"Umeoga?"

"Bado"

"Kaoge unywe chai."

"Sawa mama"

Doreen alitoka sebuleni pale na kwenda bafuni kuoga. Alipomaliza alipaka mafuta na kuvaa tena nguo alizokuwa amevaa kabla ya kuoga kisha akaenda sebuleni. Akamkuta Bi Carolina akiwa amekaa huku akitazama televisheni.

"Mbona umevaa nguo chafu?"

"Sina zingine"

"OK.. Baadae tutaenda Mwanjelwa ukatafute nguo za kuvaa.. Sasa hivi nenda ukanywe chai.." Alisema Bi Carolina.

"Sawa mama.. Vipi kuhusu Dada Pamela?" Aliuliza Doreen.

"Atakuja si muda mrefu.. Ameniambia yupo njiani. Baada ya kumwambia hivyo ghafla mlango ukagongwa. Akaingia msichana mmoja mrefu kiasi, mweupe, matiti yenye ukubwa kiasi, kiuno chembamba kama sindano na makalio makubwa kama milima miwili iliyopangana vyema. Wote walishtuka kidogo.

"Ah Pamela kumbr ulikuwa jirani tu.. Tumekuongelea sasa hivi hapa.."

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)
Mwanafunzi Mchawi Simulizi Z77
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni