Notification
Tidak ada notifikasi baru.

MWANAFUNZI MCHAWI (17)

Mtunzi: Enea Faidy

SEHEMU YA KUMI NA SABA
TULIPOISHIA...
Akaingia msichana mmoja mrefu kiasi, mweupe, matiti yenye ukubwa kiasi, kiuno chembamba kama sindano na makalio makubwa kama milima miwili iliyopangana vyema. Wote walishtuka kidogo.

"Ah Pamela kumbr ulikuwa jirani tu.. Tumekuongelea sasa hivi hapa.."

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
"Sikuwa mbali"

"Karibu sana" alisema Bi Carolina wakati huo Pamela alikuwa akiketi sofani na kuweka pembeni mkoba wake. Kwa muda wote huo Doreen alikuwa akimtazama Pamela katika maeneo ya kifuani.

"Shkamoo Dada Pamela" alisalimia Doreen

"Marhaba hujambo? Wewe ndo Doreen?"

"Ndio.." Aliitikia Doreen huku akimgeukia mama Pamela "kumbe una mtoto mzuri namna hii?" Alisema.

Bi Carolina na Pamela walicheka tu.

"Huyu ndo mwanangu mpenzi... Yuko peke yake kama Tanzanite..." Alisema Mama Pamela huku akicheka.

Doreen aliwaacha wakiendelea na mazungumzo kisha yeye akaenda chumba cha kulia chakula (dinning). Moyoni mwake alifurahi sana kwani kwa uzuri aliokuwa nao Pamela titi lake lilifaa sana kwa kazi ya Doreen.

********

Dorice aliitazama Pete ya Mansoor kwa mshangao kwani hakujua lengo kamili la Mansoor kutaka kuitazama Pete ile.

"Umeitazama vizuri Pete hiyo?"

"Ndio"

"Hii Pete, si kama Pete za kawaida, ina nguvu nyingi sana ambayo inazidi nguvu za kaeaida." Alisema Mansoor kisha akakohoa kidogo ili kusafisha koo lake kisha akaendelea.

"Pete hii nilipewa na babu yangu ambaye anaishi mbali sana katika sayari nyingine kabisa, alinipa kwaajili ya ulinzi wangu binafsi kwasababu alikuwa ananipenda. Na Mimi nitakupa wewe pete hii kwasababu nakupenda sana, ili ikusaidie katika kumuokoa mtu umpendae sana." Alisema Mansoor huku akimtazama Dorice. Dorice aliendelelea kumsikiliza kwa umakini sana Mansoor.

"Pete hii ni ya ufalme wangu pale nitakapopewa ufalme na mama yangu... Wewe kwasababu ni mke wangu utakuwa malkia..."

"Nini?"

"Unashangaa nini? Sina njia nyingine ya kukusaidia mbali na hii.. Kama upon tayari nitakupa pete hii na utakuwa na uwezo mkubwa sana wa kijini... Utarudi duniani na utafanya kila unalotaka..." Alisema Mansoor. Maneno yake yalikuwa mazuri masikoni mwa Dorice ingawa yalimpa utata wa kiwango cha juu alijiuliza maswali mengi kichwani mwake juu ya suala la umalkia. Lakini akayapotezea maswali yake kwani alitamani sana kurudi duniani kumuokoa mpenzi wake Eddy na kwenda kwa wazazi wake ambao hakuwaona kwa muda mrefu.

"Sawa... Nipe tu..!" Alisema Dorice akionesha kukubali masharti ya Mansoor.

"Nitakupa Mke wangu lakini kuna jambo muhimu unalotakiwa kuzingatia pindi utakapokuwa na hii pete"

"Jambo Gani?" Dorice alishtuka.

"Hii ni pete ys heshma sana, ambayo haihitaju uchafu wa aina yoyote.. Kwahiyo ukiivaa na kwenda Nayo duniani hutakiwi kufanya mapenzi na mwanaume mwingine zaidi yangu Mimi!" Alisema Mansoor huku akimtazama mkewe kwa macho yaliyoonesha msisitizo kwa kile alichokizungumza.

"Mmh!" Aliguna Dorice kwani alikuwa na wazo la kumsaliti Mansoor pindi atakaporudi duniani. Na alikuwa na lengo la kutorudi tena katika himaya ile ya majini. Hivyo basi masharti ya pete ile yalikuwa magumu sana kwake na kumuweka katika wakati mgumu sana.

"Mbona unaguna?"

"Kwani hakuna msaada mwingine mbali na hiyo pete" aliuliza Doreen

"Upo!"

"UPI.. Nipe msaada mwingine Mansoor tafadhali"

"Unataka njia nyingine?"

"Ndio.." Alijibu Dorice haraka.

**********

Mr Aloyce alitembeatembea katika eneo lile akimsubiri mkewe atokeze lakini muda ukazidi kwenda Vila kuona dalili yoyote. Mr Aloyce alianza kukata tamaa ya kumpata mkewe akahisi huenda alikuwa anadanganywa tu. Akataka kuondoka lakini moyo wake ulisita sana baada ya kuumbuka msemo usemao "atafutaye hachoki, akichoka keshapata" akaamua kuwa mvumilivu kwani siku zote mvumilivu hula mbivu.

Ajasogelea eneo tulivu lenye nyasi fupi kisha akaketi pale. Mawazo mengi yalifurika kichwani mwake, "nimekuwa mtumwa... Mtumwa wa nguvu za giza hii hali mpaka lini? Kila siku yanaibuka mapya... Mmh! Yote hii ni kwasababu ya Eddy.. Ila sipaswi kumlaumu" alijiwazia Mr Alloyce huku machozi yakimtiririka.

Ghafla upepo mkali ulianza kupuliza eneo lile na kumwondoa mawazoni Mr Aloyce. Alinyanyuka pale chini na kutazama juu lakini hakuona chochote.

Upepo ukazidi kupuliza kwa kasi sana mpaka miti ikaanza kuyumbayumba. Miti iliyumba kwa kasi sana na ile isiyo na nguvu ikaanguka. Mr Aloyce aliogopa sana.

Baada ya upepo ule radi Kali zikapiga mfululizo, zikazidi kumtisha Mr Aloyce. Alipiga hatua kuelekea kwenye gari yake ili akajifiche mle maana hali ilitishs lakini ghafla akasikia sauti ya kilio kikali.

"Nisaidie mume wangu.. Nisaidiee!" Mr Aloyce alishtuka sana kwani sauti ile aliijua fika. Ilikuwa ni sauti ya mkewe mpenzi. Akabaki amesimama wima kama mlingoti ili asubiri kitakachoendelea.

Akiwa bado amesimama alishtushwa na kitu kikipita miguuni mwake, akatulia kimya huku akipiga jicho kutazama kilikuwa kitu gani.

"Mamaaa" mr Aloyce alipiga ukunga kwa woga na hofu baada ya kuonana uso kwa uso na chatu aliyekuwa akijiviringa kwa kasi mwilini mwake.

...... MR ALOYCE alibaki kimya akiwa ametulia kimya kama vile amegandishwa na gundi ngumu. Haja ndogo ilipita taratibu katikati ya mapaja yake na kushuka chini ardhini. Alitamani ardhi ipasuke ili walau akajifiche chini ya ardhi kuliko kuendelea kushuhudia tukio lililokuwa linaendelea kwa wakati ule. Akili ilisimama, mwili ulinyong'onyea kwani hakuwa na lolote la kuweza kufikikiria kwa wakati ule. "Nimekamatika kwenye mtego" ndilo wazo pekee lililomjia akilini mwake.

Chatu yule aliendelea kujiviringisha kwa madaha na mbwembwe nyingi mwilini mwa Mr Aloyce na kumfanya mwanaume yule ajihisi mfu aliyebakisha roho yake tu kabla ya mazishi. "Nisaidie Mungu wangu" Mr Aloyce alisali kimoyo moyo akiamini kwamba huenda Mungu atasikia maombi yake na kumkumkumbuka katika Mateso yake. Machozi hayakumtoka hata chembe kwani hofu ilimzidia mpaka chozi lilimkauka.

Akiwa katika hali hiyo ngumu isiyoelezeka Mr Alloyce hakuona mtu yeyote wala dalili ya kiumbe chochote katika eneo lile. Ghafla upepo mkali ukapuliza eneo lile, ulikuwa kama kimbunga kinachoweza kuleta maafa kwa makazi ya watu. Mr Aloyce alijishangaa sana kuona mwili wake ukiwa mwepesi sana tena umejiachia kupita kiasi. Moyo wake ukafurahi na akatumia nafasi hiyo kujitazama mwilini mwake, akagundua yule chatu hayupo tena mwilini mwake Bali amesogea pembeni kidogo na kujituliza kama gogo.

Macho yalimtoka kama njugu akimtazama yule Chatu, ghafla akapigwa na mshangao wa ajabu baada yule chatu kubadilika umbile na kuwa na umbo la mtu. Mr Alloyce akamkazia macho MTU yule aliyetokana na chatu. Hakuamini macho yake pale alipogundua mtu yule alikuwa mkewe, Aloyce alitetemeka sana. Ndipo mwanamke yule alipoachia kicheko kikali sana huku akimsogelea Mr Aloyce. "Nilikukumbuka sana mume wangu.. Ila nasikitika unaniogopa" alisema mwanamke yule mwenye sura na umbile la mama Eddy. Mr Aloyce alitetemeka sana, akapiga hatua za kinyumenyume kumkwepa mwanamke yule.

"Mume wangu! Mbona unaniogopa?" Alisema mwanamke yule.

****

Dorice alimtazama Mansoor na kumsikiliza kwa umakini huku akiwa na hamu kubwa ya kutaka kujua njia nyingine ya kuweza kuondoka katika himaya ile ya kijini na kurudi duniani ili kumkomboa Eddy mpenzi wake wa dhati.

Mansoor alimtazama Dorice kwa unyonge sana, sura yake ilidhihirisha huzuni aliyokuwa nayo moyoni mwake. Akasogeza mkono wake na kuushika mkono wa Dorice kisha akausogeza karibu kabisa na midomo yake mizuri. Akaachia mabusu mazito mfululizo huku chozi likimdondoka. Kisha akainua macho yake na kumtazama Dorice.

"Dorice kwanini hunipendi?" Aliuliza Mansoor. Dorice alimtazama Mansoor bila kujibu chochote.

"Kwanini hunipendi?" Aliuliza tena Mansoor huku macho yake yakizidi kuwa mekundu kama pilipili. Kisha taratibu machozi yake yalianza kubadilika rangi na kuwa kama damu.

"Dorice! Naumia sana moyoni mwangu kumpenda mtu asiyenipenda! Najilaumu sana ingawa sio kosa language ila ni kosa la moyo wangu ambao haukumchagua yeyote ila wewe.. Natamani ungejua thamani ya upendo wangu kabla haujaenda duniani ili unikumbuke moyoni mwako" alisema Mansoor huku machozi mekundu yakizidi kudondokea kwenye mikono mizuri na laini ya Dorice. Maneno Yale yaliugusa moyo wa Dorice, akahisi ni mkosaji sana kwa kuutesa moyo wa Mansoor. Machozi yalimlengalenga machoni mwake akajikuta anamkumbatia Mansoor na kumtakia maneno ambayo hakuwahi kumtamkia hata Mara moja.

"NAKUPENDA SANA MANSOOR" alisema Dorice huku midomo yake ikibusu shingo ya Mansoor kwa huba, na mikono yake ilitembea taratibu mgongoni kwa Mansoor na macho yake yalikuwa yamefumba na kumpa nafasi zaidi ya kuzitafakari kwa kina hisia za mapenzi zilizokuwa kichwani mwake.

"Asante sana mpenzi wangu... Nakupenda na nitazidi kukupenda milele.." Ilisikika sauti iliyojaa huba na mahaba mazito ya Mansoor.

"Asante mpenzi... Lakini naomba unisaidie kwa lile suala langu.. Na umesema kwamba kuna njia nyingine.." Alisema Dorice akiwa bado amemkumbatia Mansoor.

Swali lile lilikuwa kero kwa Mabsoor kwani alijua Dorice hatozungumzia tens suala lile baada ya kumpa maneno matamu zaidi ya asali.

"Mh! Nitakusaidia... " alisema Mansoor.

"Lini?"

"Kuwa na subira... Wala usijali... " Mansoor alimwondoa shaka Dorice. Baada ya muda mfupi Mansoor alimuaga Dorice kisha akatoweka machoni pake huku akimuahidi kuwa atarudi baada ya muda mfupi tu.

Hazikupita dakika nyingi Mansoor alijitokeza tena kwa Doreen lakini alikuwa na kitu kilichomshtua Doreen na kumfanya aogope sana.

******

Siku ya kwanza ndani ya nyumba ya mama Pamela iliisha vizuri sana wakiwa na Doreen. Usiku majira ya SAA NNE baada ya kula na kutazama televisheni huku wakipiga soga za hapa na pale wakaagana na kila mmoja alienda kulala kwenye chumba chake.

Usiku ule Mama Pamela alihisi kuna utofauti ambao hakuuzoea kabisa.

Paka walilia Mfululizo na kumfanya Mama Pamela ahamaki kidogo, sauti ya paka kutoka batini ilisikika ikilia kama mtoto mchanga jambo ambalo lilimtisha mama Pamela. Na haikuwa hivyo kwa mama Pamela tu bali pia hata kwa Pamela kwani alikuwa anaogopa kupita kiasi.

Ghafla usingizi wa ajabu ukampitia Mama Pamela, macho yalikuwa mazito kiasi kwamba alishindwa hata kuyafumbua ingawa akili yake bado ilikuwa inaendelea kuwaza. akajishangaa na kujiuliza usingizi ule ulikuwa wa aina gani kwani kwa kawaida mtu akilala hata akili pia inalala. Ghafla kitu kizito militia juu yake, akashindwa kupumua vizuri na kila alipojaribu kujiinua alishindwa.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)
Mwanafunzi Mchawi Simulizi Z77
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni