Notification
Tidak ada notifikasi baru.

MWANAFUNZI MCHAWI (18)

Mtunzi: Enea Faidy

SEHEMU YA KUMI NA NANE
TULIPOISHIA...
akajishangaa na kujiuliza usingizi ule ulikuwa wa aina gani kwani kwa kawaida mtu akilala hata akili pia inalala. Ghafla kitu kizito militia juu yake, akashindwa kupumua vizuri na kila alipojaribu kujiinua alishindwa.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
Akahisi anakabwa sana shingoni na kila alipojaribu kuinua mkono wake ili ajiokoe alishindwa. Akazidi kuhema kwa nguvu.

Nusu SAA nzima hali ile ilizidi kumsumbua mpaka aliposhtuka na kukaa kitandani huku jasho likimtoka kwa kasi kana vile yupo jijini Dar kumbe yupo Mbeya kwenye baridi Kali. Alikaa kitandani huku akihema sana ghafla akasikia kishindo kikali sana kilichomshtua na kumfanya atahamaki.

"Mamaaaa! Mamaa " sauti ya Pamela ilimshtua sana Bi Carolina. Akatamani ainuke kitandani pale ili akamtazame mwanaye, Mara taa ikazimwa. Akajua umeme umekatika lakini kilichomshangaza .........

.... Leyla alikuwa amechanganyikiwa sana baada ya mumewe kuwa katika Hali ile. Alishindwa kuelewa atafanyaje ili kujimudu katika familia yake kwani Mwalimu John ambaye ni mumewe asingeweza kurudi tena kazini. Kilichomfanya anyong'onyee zaidi ni hali ya Judith kwani hakuweza kuongea wala kusikia. Leyla alikosa raha sana, akakaa kitini akiwa na mawazo mengi sana. Alijiuliza afanye nini ili aweze kuwaokoa wahanga wa tatizo asilojua limetona na nini.

Akiwa katika kutafakari hayo yote ghafla wazo muhimu lilimjia kichwani mwake. Leyla alichukua simu yake na kutafutw namba fulani kisha akapiga. Simu iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa kisha ikakakata. Leyla hakukata tamaa akapiga tena lakini majibu yakabaki Yale Yale, simu haikupokelewa akajaribu tena na tens simu ikapokelewa.

"Bwana asifiwe mchungaji.." Alizungumza Leyla kwa sauti ya unyenyekevu sana kwani aliyempigia alikuwa ni mchungaji wake.

"Amen.. Unasemaje?" Alijibu mchungaji yule kama vile hataki kuzungumza.

"Samahani mchungaji nina shida... Naomba msaada wako!" Alisema Leyla.

"Shida gani"

"Kuhusu familia yangu!".

"Kama ni mumeo mama... Chukua imani hapo ulipoanza maombi Mimi sina muda... Nina mambo mengi ya kufanya.." Alisema mchungaji yule kwa ukali kiasi jambo lililomtisha sana Leyla kwani hakutegemea kama mchungaji wake angemjibu vile.

"Pastor! Tafadhali nisaidie.." Leyla alimbembeleza mchungaji lakini hakumuelewa. Na mchungaji huyu ndiye aliyefanya mazishi ya mwalimu John.

"Kwasasa sipo nyumbani.. Nipo mbali kikazi..." Alisema Mchungaji yule. Kiukweli ilikuwa vigumu kwa Leyla kuamini maneno ya mchungaji wake kwani Siku zote aliamini mchungaji wake angekuwa ndiye mfariji lakini haikuwa hivyo.

"Cha kukusaidia labda nitawaita wanamaombi waje kukusaidia" alisema mchungaji na kukata simu.

Leyla alishindwa afanye nini kwani hata ndugu zake walimtenga. Ilipita nusu SAA nzima , mlango wake ukagongwa. Alifurahi sana kwani alijua tayari mchungaji amewasiliana na wanamaombi ili waje kuombea familia yake. Alinyanyuka kitini na kwenda moja kwa moja kufungua mlango.

*****

Mama Pamela alizidi kutetemeka kwa woga sana, alijikunyata kama mgonjwa kitandani kwake. Lakini alizidi kuisikia sauti ya mwanae ikiendelea kumwita. Mama Pamela akazidi kupata hofu, japo aliogopa sana lakini aliamua kuinuka kitandani na kunyata taratibu kuelekea chumbani kwa Pamela. Na hii ni kwa sababu damu nzito kuliko maji .

Nyumba ilitawaliwa na kiza kizito sana, hivyo ilimpa shida sana Mama Pamela kuelekea chumbani kwa mwanae. Aliingia chumbani kwa Pamela na kuita taratibu "Pamela! Pamela!" Lakini Pamela hakuitikia. Mama Pamela alisogelea kitanda cha Pamela na kuanza kupapasa papasa lakini cha ajabu hakuona dalili zozote za uwepo wa mtu kitandani pale. Mama Pamela alizidi kuchanganyikiwa sana.

Akaita tena "Pamela! Pamela!" Lakini bado hakukuwa na sauti yoyote iliyoitikia. Mama Pamela alihisi akili yake inavurugika. Akauvua woga wake na kumuita Pamela kwa sauti kubwa lakini bado hakuitikia.

Mama Pamela alirudi chumbanu kwake na kupapada sehemu ilipokuwepo simu yake na baada ya kuipata alimshukuru Mungu. Kisha akawasha tochi na kuanza kumulika kila chumba.

Aliingia chumba cha kwanza akamulika lakini hakuona MTU, akamulika, cha pili, cha tatu na kisha akaingia jikoni lakini bado hakumuona Pamela. Roho ya Mama Pamela iliingiwa simanzi, akajua mwanaye amepotea kwa mazingira ya kutatanisha . akaingia bafuni na kumulika lakini Hakumkuta Pamela. Mama Pamela alizidi kuchanganyikiwa zaidi.

"We Mungu bora wangenichukua Mimi sio mwanangu Pamela," alisema Mama Pamela akiingia chooni.

Mama Pamela alistaajabu sana alichokutana nacho. Alimkuta Pamela akiwa amelala chooni huku kajifunika blanketi lake vizuri."

"Pamelaa!" Aliita mama Pamela kwa mshangao na mpaka wakati huo mama Pamela hakujua Doreen anaendeleaje.

****

Mr Alloyce alibaki njia panda, alikuwa haelewi cha kufanya juu ya mwanamke yule. Alijiuliza amkubalie kama mkewe au asimwamini? Mawazo yake hayo mawili yalimezwa na ukarimu wa mwanamke yule kwa jinsi alivyoonesha kumjali Mr Aloyce.

"Mime wangu... Mbona hunichangamkii? Baba Eddy jamani" alisema mwanamke yule na kumsogelea Mr Aloyce "hivi kweli we ni Mke wangu? Mama Eddy?" Aliuliza Mr Alloyce kwa wasiwasi.

"Kha! Kumbe huniamini mume wangu?" Alisema

"Mbona ulitokea kama Chatu?"

"Hahahah unatakiwa kuniamini mume wangu!" Alisema mwanake yule na kumsogelea Baba Eddy kisha akamkumbatia.

Mr Aloyce alitamani kumwamini mwanamke yule kama ndo mkewe lakini moyo wake ulisita. Alimsogelea na kumkumbatia lakini moyoni make alikuwa na mashaka sana.

"Nakupenda mume wangu.. Naomba tuwahi nyumbani ili nikamwone mwanangu" alisema mama Eddy.

"Sawa" alisema Baba Eddy huku akifungua mlango wa gari.

"Lakini unanishangaza mume wangu?"

"Nakushangaza na nini?"

"Huna amani moyoni mwako.. Kwanini?"

"Usijali Niko sawa..."

Wallingia kwenye gari kisha Mr Aloyce aliwasha gari na kuanza kuendesha. Aligeuka kumtazama mkewe yule aliyekuwa ameketi pembeni yake, lakini kuna kitu kilimshangaza.....

.MR Aloyce alizidi kumkazia macho mkewe akahisi ni mrembo zaidi ya Mama Eddy yule anayemfahamu yeye. Halafu alikuwa na madaha sana kuzidi vile alivyomzoea. Wasiwasi ukamtanda akilini make na kumfanya asimwamini sana mwanamke yule kuwa ndiye mkewe halisi.

"Mbona unaniangalia sana? Umemisi busu langu nini?" Aliuliza Mama Eddy.

"Hapana wala usijali"

"Ok kama wewe hukumiss basi Mimi nilimisi sana kiss lako mpenzi".

Alisema Mama Eddy huku akimsogelea Mr Aloyce kwa ukaribu zaidi na kumshikashika kidevu kwa mahaba. Mr Aloyce alionesha kutojali mguso ule aliopapaswa na mikono laini ya mkewe. Hakuelewa ni sababu zipi zilizomfanya asimjali mwanamke yule kwa kiasi kile ila moyo wake ulikuwa mzito sana.

"Baby mbona hivyo...? Embu usiwashe gari kwanza mpaka unibusu" alisema Mama Eddy kwa sauti iliyojaa mdeko wa kimahaba. Mr Aloyce hakutaka kukiri udhaifu, akaachia usukani na kusogeza mdomo wake karibu na mdomo wa mkewe kisha akambusu.

Busu lile lilimpa nafasi nzuri sana Mama Eddy ya kupenyezapenyeza mpaka kuingiza ulimi wake mdomoni kwa Mr Aloyce. Kisha wakabadilishana mate yao kwa mahaba. Lakini wakati tendon hilo likiendelea, Mwanamke yule alimwachia vitu Fulani Mr Aloyce bila yeye mwenyewe kujua. Na ilikuwa ni dawa Kali ya kumfanya Mr Aloyce amwamini mwanamke yule kuwa ndiye mkewe halisi wakati hakuwa yeye. Alikuwa ni mwanamke kutoka himaya ya akina Doreen na alitumwa nyumbani kwa Mr Aloyce ili afanye kazi muhimu sana aliyotumwa.

Kwa vile alivyomfanyia Mr Aloyce, alifanikiwa kuziteka akili za Mwanaume yule. Baada tu ya busu lile la huba, Mr Aloyce alijkuta akimpenda sana mwanamke yule akijua ndie Mkewe halisi na kumbe haikuwa hivyo. Wasiwasi wake ulifutika kichwani mwake, pendo la dhati likatawala moyoni mwake.

"Tuondoke mume wangu" alisema mama Eddy kwa sauti ya upole iliyojaa huba huku akiwa ameachia tabasamu pana usoni mwake.

"Usijali mke wangu.. Nilikukumbuka sana... Nina imani hata mwanetu anakusubiri kwa hamu sana." Alisema Mr Aloyce huku akishikilia vizuri usukanu na kuondoa gari kwa kasi sana.

Mr Aloyce aliendesha gari kwa kasi ya ajabu na baada ya masaa machache tu waliwasili eneo la Ipogoro Iringa kisha wakaelekea nyumbani kwao.

Walifika getini wakapiga honi geti lilifunguliwa. Mr Aloyce aliegesha gari pembeni kisha akashuka kwa furaha kubwa, na baada ya hapo akaelekea upande wa pili wa gari yake na kumfungulia mkewe huku tabasamu mwanana likiwa limechanua mdomoni mwake.

"Shuka malkia wangu... Tumeshafika kwetu.." Alisema Mr Aloyce huku mwanamke yule anayefanana kwa kila kitu na Mama Eddy akishuka kwa madaha kisha akamkumbatia Mr Aloyce na kumbusu. Wakati yote hayo yakiendelea Mlinzi alikuwa pembeni yao akishuhudia penzi la zamani lililochipua upya tena kwa kasi ya ajabu.

"Mh bosi naona mama Amerejea.." Alisema mlinzi kimzaha.

"Ndio.."alijibu Mr Aloyce kwa furaha.

"Baby nataka kuongea jambo na mlinzi wetu naomba utuache kidogo.." Alisema Mama Eddy.

"Ok ila kuwa makini tu nisije kupinduliwa na houseboy.." Alisema Mr Aloyce na kuondoka zake huku akimsisitiza mkewe asichelewe.

Baada ya Mr Aloyce kuondoka pale, Mwanamke yule alimsogelea mlinzi na kumtazama kwa ghadhabu Kali. Hali hiyo ilimtisha sana mlinzi na kumfanya ajiulize maswali mengi ambayo alishindwa kujijibu mwenyewe.

****

Mama Pamela aliishiwa nguvu kabisa. Alijiuliza sana ni kwanini mwanaye amelala chooni kule ilhali ana kitanda kizuri cha kumfaa? Maswali yake hayakuwa na majibu akajikuta anaishia kupiga makofi kwa mshangao.

"Pamela!" Alimwamsha mwanae ambaye bado alionekana ana usingizi mzito sana. Alimtikisa tikisa mpaka alipofanikiwa kumwamsha kabisa. Pamela aliinuka, lakini alibaki mdomo wazi baada kuona mazingira aliyopo si ya kitandani kwake.

"Mama nipo wapi hapa? Mbona kama chooni?" Aliuliza Pamela kwa mshangao.

"Nikuulize wewe mwanangu.. Umefikafikafikaje mpaka ukalala chooni?" Aliuliza Mama Pamela.

"Mbona sielewi mama" alisema Pamela.

"Haya chukua hilo shuka lako twende chumbani.. Hayo mengine tutajua huko huko.."

Walitoka chooni mle na kuelekea chumbani kwa mama Pamela. Pamela alitoa nguo aliyokuwa amevaa kwaajili ya kulalia kisha akavaa nyingine kwani ile tayari ilishapata unyevunyevu wa chooni.

"Lakini mama mbona Doreen hatujaenda kumwangalia si atahisi tunamtenga.." Alisema Pamela.

"Ila kweli"

"Tumfate basi.." Alisema Pamela kisha wakainuka na kwenda chumbani kwa Doreen. Kulikuwa na Giza totoro ambalo bila msaada wa tochi basi wasingeona chochote.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)
Mwanafunzi Mchawi Simulizi Z77
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni