MWANAFUNZI MCHAWI (21)
Zephiline F Ezekiel
---
Jina: MWANAFUNZI MCHAWIMtunzi: Enea Faidy
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Lakini kwa bahati mbaya sana simu ilipokelewa na jini Mansoor kwa namna ya ajabu sana. Na jini huyo aliongea sauti ya Mama Dorice na kuwafanya walimu wajiaminishe vizuri kuwa waliongea na mama Dorice lakini kumbe haikuwa hivyo na hakuna aliyejua siri hiyo zaidi ya Mansoor pekee.
IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI
TUENDELEE...
"Mama tena nilipiga simu Mimi.. Na ulikubali mwanao aache shule.." Alijitetea madam Amina lakini hakueleweka.
Wazazi wa Dorice waliondoka kwa hasira sana shuleni pale huku wakiwa hawajui binti yao alienda wapi. Roho iliwauma sana lakini hawakuwa na jinsi. Waliondoka na gari yao waliokuwa wamekodi ikawafikisha kituo cha mabasi Iringa mjini.
Walishuka ili watafute sehemu ya kula chakula kwani hawakula chochote tangu asubuhi kisha wakate tiketi, ghafla kwa mbali sana Mama Dorice alimwona msichana kama Dorice. Alijifuta macho yake na kutazama vizuri akamtazama vizuri binti yule.
"Kaka Dorice yule pale"
"Yuko wapi?" Kaka yake alishtuka sana.
"Pale mbele kwenye watu wengi.. Tumfate haraka.." Alisema Mama Dorice akiwa tayari ameanza kupiga hatua kuelekea kule alipo msichana yule.
********
"Chukua hii" Bi Tatile alimpa hirizi moja Doreen. Doreen aliipokea kwa mkono wake wa kushoto na kusikiliza maelekezo kwa umakini kutoka kwa Bi Tatile.
"Hii umeze sasa hivi.... Haraka sana.." Aliamrisha Bi Tatile na Doreen alifanya hivyo haraka. Akaibugia mdomoni na kuimeza. Alihisi maumivu makali sana ya Tumbo, akapiga kelele kwa kulalama.
"Hapa inabidi urudi haraka nyumbani... Ukajisaidie haja kubwa sebuleni kwenye sahani safi.. Kisha uzunguke sebuleni Mara Saba kutokea kona moja hadi nyingine huku akitamka jina la msichana yule... Umenielewa?"
"Nimekuelewa mtukufu.." Alijibu Doreen kwa woga kiasi.
"Haya ondoka haraka.." Aliamrisha Bi Tatile huku akimalizia na kicheko kikali cha kutisha.
Bila kuchelewa Doreen aliopotea eneo lile na kutokea nyumbani kwa Mama Pamela. Pindi alipokuwa anaingia ndani kilisikika kishindo kizito sana. Doreen aliingia ndani na kupulizia dawa ya kuwalaza usingizi wote waliokuwa ndani kisha akaenda sebuleni. Akachukua sahani nzuri sana Kabatini, akaiweka chini na kujisadia haja kubwa yenye harufu Kali sana kwenye sahani ile. Kisha akaenda kwenye kona ya kwanza na kuanza mzunguko wa kwanza huku akitamka jina la Pamela.
Akamaliza mizunguko saba kama alivyoambiwa punde Pamela alitokea sebuleni pale. Doreen alicheka kicheko kikali sana cha kutisha, huku akimsogelea Pamela aliyekuwa ameinamisha kichwa chino bila kumtamzama Doreen.
Doreen alisigeza mkono wake na kuusogeza kifuani kwa Doreen kwenye titi lake la kushoto. Akalishika titi lile huku akitamka maneno Fulani kisha titi lile likapotea kifuani kwa Pamela akabakiwa na titi moja tu. Pamela alikuwa hajielewi kabisa akiwa pale. Baada ya titi kuchukuliwa akapotea. Na Doreen pia akapotea huku moyoni mwake akifurahia ushindi alioupata kwani tayari kazi iliyomleta ilikuwa imekamilika.
Asubuhi na Mapema, Mama Pamela aliamka usingizini akiwa mchovu sana. Alijikongoja na kwenda chumbani kwa mwanaye alikuta amelala fofofo, akamshtua.
"Mbona umelala sana Leo?"
"Mama naumwa sana." Alisema Pamela kwa sauti ya kichovu.
"Unaumwa? Unaumwa nini? " mama Pamela alishangaa.
"Kifua kinaniuma sana.. Titi linauma balaa.."
"Titi?" Alishtuka mama Pamela.
"Ndio.."
"Pole sana.. Halafu kuna harufu naisikia humu ndani.. Sijui pua zangu.." Alisema mama Pamela na kulipuuza suala la binti yake kwani alihisi ni ugonjwa wa kawaida tu.
"Hata Mimi naisikia..." Alisema Pamela.
"Ngoja niangalie angalie basi huko sebuleni." Alisema Mama Pamela na kwenda sebuleni. Alipoingia tu alikaribishwa na harufu mbaya sana iliyomfanya apige chafya. Na kwa ukali wa harufu ile alitamani atapike. Macho yalitua moja kwa moja mpaka kwenye sahani yake iliyokuwa imejaa kinyesi pale sebuleni kwake.
"Oh My God!" Alishtuka Mama Pamela huku macho yamemtoka kama yai la kisasa.
"Ama kweli dunia ina mambo.. Pamelaaa! Njoo!" Alisikika mama Pamela.
Pamela aliitika na ndani ya sekunde chache alifika sebuleni pale.
"Oh gash! Nani kafanya ivi?" Alishangaa Pamela baada ya kushuhudia tukio lile pale sebuleni.
"Shangaa wewe! Maana mie nimeishiwa nguvu kabisa!" Alisema mama Pamela. Walishangaa kupita kiasi na muda si muda Doreen alifika sebuleni sebuleni pale na kuungana na wenye nyumba kushangaa tukio zima.
"Alaaniwe sana aliyefanya tukio hili.." Alisema Doreen huku akipiga makofi ya mshangao.
"Halafu Dada Pamela hapo kifuani pakoje?" Aliuliza Doreen.
Pamela alishtuka kusikia swali lile. Akajiangalia kifuani kwake na kugundua kifua chake kimetuna upande mmoja lakini upande mwingine hauna kitu. Hofu kuu na mshangao vikamvamia akajifunua shati na kujikagua zaidi.
"Mama Eddy.. Nashukuru sana mdogo wangu kwa ulichonifanyia... Mungu tu ndo anaejua.... Kwaheri." Alisema Dada yake mama Eddy na kutoka sebuleni Pale.
Mr Aloyce alijtahidi kumzuia asiondoke ilishindikana. Mwanamke yule aliondoka kistaarabu na kuwaachia nyumba yao.
"Mke wangu ulichofanya sio ustaarabu.." Alisema Mr Alloyce.
"Ustaarabu haulipwi... Kwahiyo hauna faida.." Alijibu mama Eddy na kukaa kitini.
"Mh! Sawa..."
"Hebu tuachane na yaliyopita kuna jambo nataka nikuambie.
"Mama kwanini umefanya vile? Mbona umebadilika sana?"
"Na wewe sitaki kelele... Hebu ondoka hapa niongee na mume wangu.."
"Sawa lakini mamkubwa alikuwa tatari kunisaidia tatizo langu" alisema Eddy.
"Ulimwambia sio?"
"Ndio..." Alijibu Eddy kwa hasira na kutoka sebuleni pale akiwaacha na mazungumzo yao. Roho ilimuuma sana Eddy kwa kitendo alichofanya mama yake, lakini hakuwa na jinsi.
"Nisikilize mume wangu mpenzi.." Alisema ma Eddy.
"Sema"
"Nataka tumrudishe Eddy shuleni... Maana masomo yanampita sana.."
"Unasemaje? Vipi kuhusu tatizo lake?"
"Hilo lishakuwa la maisha cha msingi arudi shule"
"Hapo sijakuelewa mke wangu.. Si ni bora tumpeleke hata kwenye maombi?" Alisema Baba Eddy na katika vitu alivyovichukia mama Eddy yule wa bandia ni suala la maombi.
"Maombi kitu gani? Unawaamini wachungaji wenyewe waongo tu? Sitaki maombi kwa mwanangu asije akatupiwa majini bure..." Alisema mama Eddy.
"Kuombewa ataombewa tu... Tena nimekumbuka kitu..." Alisema Mr Aloyce na kunyanyuka kitini pale haraka..
.BAADA ya kujikagua kwa muda Pamela aligundua hana titi lake moja la kushoto. Jasho jembamba lilimtiririka kwa kasi ya ajabu. Hakutaka kuamini kile alichokiona, akaanguka chini ghafla na kupoteza fahamu. Mama Pamela alipigwa na butwaa la ajabu, uvumilivu ukamshinda akamwita Pamela Mara kadhaa lakini Pamela hakuitikia. Kwa mshtuko alioupata pia mama Pamela alidondoka chini Puuh! Kama mzigo na kupoteza fahamu palepale.
Doreen alisimama pembeni yao, alicheka kwa kiburi sana kisha akaondoka zake sebuleni na kuingia chumbani kwa mama Pamela moja kwa moja. Aliingia chumbani kinyumenyume kisha akatamka maneno Fulani halafu akageuka na kusogelea kitanda cha Mama Pamela, akatazama chumba kizima kisha akagundua sehemu yenye pesa. Akatikisa kichwa na kuisogelea droo moja ya 'dressing table' na kuchukua pesa zote zilizokuwemo mle. Na droo ile ndio ambayo aliitumia mama Pamela kuhiffadhi pesa zote.
Bila huruma Doreen alichukua pesa zote alizozikuta mle, zilikuwa takribani laki tano kisha akaenda chumbani kwake na kubadili nguo haraka kisha kisha akachukua begi lake dogo akaondoka zake.
Doreen alitembea mwendo wa haraka sana mpaka alipofika barabarani na kupanda daladala inayoelekea stendi kuu ya Nanenane.
Mama Pamela na mwanaye walilala pale chini kwa muda wakiwa hawajitambui. Ndani ya nusu saa nzima ndipo mama Pamela alipopata fahamu na kuwezs kuinuka, alikaa dakika tano nzima ndipo kumbukumbu zikamrejelea. Machozi yalimdondoka huku akiinuka na kwenda kuchukua simu kitu cha kumpepea mwanae ili azinduke. Alichukua khanga laini na kuanza kumpepea Pamela mpaka alipozinduka. Lakini muda wote huo kuna kitu alikifikiria na alihisi kimepungua mle ndani. Akawaza kwa muda ni kitu gani hicho ndipo akakumbuka kuwa hakumwona Doreen.
"Doreen! Doreen!" Aliita mama Pamela lakini hakusikia sauti yoyote iliyoitikia. Akaachana nae akijua labda yupo nje.
"Mama siamini! Sitaki kuamini kilichonitokea!" Alisema Pamela huku akilia.
"Sijui nani amefanya hivi?" Aliuliza mama Pamela.
"Mama! Kuna ndoto niliota... Ila sikudhani kama ni kweli kumbe ilibeba ukweli mzito sana!" Alisema Pamela kwa huzuni huku akilia.
"Ndoto gani hiyo? Na je ulimwona Mtu yeyote?"
"Ndio mama nilimwona!"
"Alikuwa nani?"
Kabla Pamela hajasimulia chochote kuhusu ndoto aliyoota, simu ya Mama Pamela iliita na kumfanya ainuke haraka na kwenda kuifata simu yake. Mpigaji alikuwa ni Baba Pamela, mama Pamela alipokea simu huku huzuni ikimzidia.
"Haloo mume wangu..."
"Halloo... Habari za huko?"
"Mmh.. Za huku si nzuri...!"
"Mh! Kwanini?" Alishtuka baba Pamela. Mama Pamela akamsimulia kila kitu kilichotokea nyumbani kwake tangu alipoondoka. Mkasa ule mzito ulimshangaza sana Baba Pamela, alikuwa haamini kabisa kilichomtokea binti yake.
"Ina maana Pamela hana titi moja sasa?"
"Ndi..ndioo..."
"Unaona sasa mke wangu? Nilikwambiaje Mimi?? Nilikwambia nini kuhusu yule mgeni wako?" Baba Pamela alianza kumlaumu mkewe kwa kutokuwa mwelewa lakini suala lile likazua ubishi kwa mama Pamela kwani hakuamini kabisa suala la Doreen kuhusika ns ushirikina.
"Mume wangu... Unamkosea Mungu kumhusisha yule binti na ushirikina, yule mtoto ni mpole tena mstaarabu.." Alisema mama Pamela.
"Tatizo lako mke wangu ni hilo... Hutaki kuukubali ukweli na ndio maana umesababisha matatizo kwa mwanangu bora yangekukuta we we.." Alisema Baba Pamela.
"Baba Pamela mbona we king'ang'anizi hivyo? Doreen sio mchawi... Waliofanya hivyo watakuwa ni majirani tu..."
"Mh umenishinda we mwanamke." Baba Pamela alikata simu kwa hasira.
Akili ya Mama; amela ilikuwa ngumu sana kuamini maneno ya mumewe. Alijua mumewe anamsingizia tu binti wa watu, mtoto mwenye adabu kupita kiasi, mchapakazi tena mwenye hekima. Hivyo ndivyo mama Pamela alivyomchukulia Doreen bila kujua upande wa pili Doreen alikuwa ni mtu wa aina gani.
"Hebu nisimulie vizuri hiyo ndoto yako Pamela.."
"Mama tuondoe kwanza hicho kinyesi maana harufu yake inanisumbua sana..." Alisema Pamela.
Mama Pamela alienda jikoni na kutafuta mifuko ya plastiki kisha akajivalisha mikononi halafu akaenda kubeba ile sahani yenye uchafu kutoka tumboni mwa MTU mwingine na kuubeba kwa kinyaa sana kisha akaenda nao nje. Alitafuta eneo zuri na kuchimba shimo dogo akafukia uchafu ule pamoja na sahani.
Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni