Notification
Tidak ada notifikasi baru.

MWANAFUNZI MCHAWI (22)

Mtunzi: Enea Faidy

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
TULIPOISHIA...
Mama Pamela alienda jikoni na kutafuta mifuko ya plastiki kisha akajivalisha mikononi halafu akaenda kubeba ile sahani yenye uchafu kutoka tumboni mwa MTU mwingine na kuubeba kwa kinyaa sana kisha akaenda nao nje. Alitafuta eneo zuri na kuchimba shimo dogo akafukia uchafu ule pamoja na sahani.

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
Alinawa mikono kisha akarudi tena sebuleni ambapo bado palikuwa na harufu Kali. Akawasha kiyoyozi na kufungua madirisha yote kisha harufu ile ikaanza kuaga Nyumba taratibu sana na kwa maringo yaliyokithiri.

Baada ya kuhakikisha usalama wa nyumba yake mama Pamela akaketi kitini na kumsikiliza mwanaye.

****

Baba Eddy alisogelea droo yake ya kuhifadhia vitu na kuchukua kijidaftari kimoja kidogo amabacho Mara nyingi alikitumia kuhifadhia namba za simu za watu wake muhimu. Baada kukipata alienda nacho sebuleni na kuketi kitini huku akikipekuapekua kwa uangalifu.

"Nimefanya uzembe kwa muda mrefu lakini sasa nimegundua njia sahihi ya kumtibu mwanangu..." Alisema Mr Aloyce.

"Kwani njia gani umeigundua? Kuna daktari unamfahamu?" Aliuliza mama Eddy.

"Kwahili suala halihitaji daktari..."

"Mh kivipi... Basi mganga...!"

"Mganga wa nini? Umesahau kilikutokea tulipotaka kwenda kwa mganga?" Alisema Baba Eddy huku akizinakiri namba Fulani kutoka kwenye kile kijidaftari na kuweka kwenye simu yake.

"Mbali na hao... Unafikiri nani atatusaidia mume wangu? Hakuna mwingine... Tusipoenda kwa daktari basi ni kwa mganga tu.." Alisema mama Eddy kwa sauti ya ushawishi sana lakini haikumwingia akilini hata kidogo baba Eddy.

"Hao uliowasema watashindwa... Cha msingi ni kumtegemea Mungu tu..."

"Unampigia Mchungaji?" Alishtuka mama Eddy.

"Ndio.." Aliitikia Baba Eddy na tayari muda huo huo alipiga simu na ikaanza kuita.

"Wewe mbona upo ivo? Mchungaji wa nini sasa? Hatokusaidia kitu zaidi ya kupoteza muda.. Hebu kata simu.." Alisema mama Eddy huku akimnyang'anya simu mumewe na kukata. Baba Eddy alimshangaa sana mkewe. Alijikuta anamtandika Kofi zito sana la usoni bila kutarajia.

"We mwanamke ni mchawi nini? Kwanini ukatae maombi ya watu wa Mungu?" .

Mwanamke yule alipiga ukunga kwa maumivu. Akajishika shavu lake kwa kuugulia kipigo kile.

"Unanipiga Mimi?" Alisema mama Eddy. Mr Aloyce alibaki kimya tu bila kusema neno kwani alikuwa na hasira sana. Alichukua simu yake na kuondoka sebuleni pale, akaingia chumbani. Haukupita muda kabla hata hajapiga simu tena mama Eddy aliingia chumbani.

"Si umenipiga? Sawa! Wewe ni mbabe! Ila nitakuonesha!" Alisema Mama Eddy na kuzidi kumtia hasira zaidi Mr Aloyce.

"Sitaki masikhara kwenye vitu vya msingi ondoka huku chumbani!" Alisema Mr Aloyyce huku akijaribu kupiga tena simu.

"Mume wangu... Nisamehe basi... Tuyamalize basi baby!" Alisema mwanamke yule kwa sauti ya mahaba utadhani sio yule aliyekuwa na hasira hapo mwanzo. Alimsogelea mumewe kimahaba na kumyang'anya simu mumewe kisha akamteremshia mvua ya mabusu mdomoni mwake.

"Nakupenda mume wangu..." Alisema mwanamke yule akiwa amekata simu na kuiweka pembeni. Mr Aloyce alibaki kimya akimtazama tu mkewe kwa mambo anayoyafanya. Mwanamke yule aliendelea kumpapasa mumewe akiwa na lengo la kumfanya Mr Aloyce apoteze wazo la kumpigia simu mchungaji. Kwani alifahamu vizuri nguvu ya maombi ya watu wa Mungu na jinsi ambavyo angeshindwa kufanya kazi yake.

Licha ya kutumia mtego ule kwa Mr Aloyce lakini bado ilishindikana kumfunga akili yake ya kumpigia simu mchungaji. Mr Aloyce alisukuma kwa nguv na kuchukua simu yake kisha akaenda chumba cha wageni na kujifungia mlango, akampigia simu mchungaji. Alipopokea tu simu ile, ghafla mlango wa chumba ukafunguliwa. Mr Aloyce alishtuka sana, kwani alikuwa amefunga mlango na funguo. Mkewe aliingia.

"Mchungaji.. Naitwa Mr Aloyce... Nina matatizo makubwa sana kwenye familia yangu nahitaji maombi mchungaji tafadhali..."

Alijieleza mr Aloyce kabla hata ya salamu. Lakini muda huo alisikia sonyo Kali sana kutoka kwa mkewe, na hakuelewa ni kwanini mkewe alisonya kidharau kiasi kile kisha akatoka chumbani mle.

*****

Mama Dorice alitembea mwendo wa haraka sana na kumkaribia msichana yule aliyedhani kuwa ni mwanaye. Alimkaribia msichana yule na kumwita "Dorice!" Msichana yule akageuka na kumtazama aliyemwita ndipo mama Dorice aliposhtika sana baada ya kugundua binti yule hakuwa Dorice.

"Samahani binti nimekufananisha.." Alisema mama Dorice na kumgeukia kaka yake ambaye alikuwa anamfata kama Bendera inayofuata upepo.

"Dada mbona sikuelewi..?" Aliuliza mjomba wake Dorice.

"Kaka acha tu...."

"Kwani vipi?"

"Nilimwona Dorice kabisa lakini nilipofika hapa kumbe sio...."

"Umemfananisha?"

"Nadhani..."

"Haya twende basi tukate tiketi... Turudi nyumbani tuangalie ni jinsi gani ya kumpata mwanetu.... Maana hatuwezi sema alifariki bila uchunguzi labda aliacha shule akaolewa?"

"Ila sidhani kama inawezekana Dorice aolewe kizembe ivo... "

"Usikatae dada yote Yanawezekana..." Alisema mjomba.

Waliondoka eneo lile na kwenda moja kwa moja kwenye mgahawa mmoja ambapo walipata chakula kisha wakaenda kukata tiketi ya basi. Walipokuwa pale , mama Dorice alimwona tena MTU kama Dorice akiwa amevaa mavazi Yale yale kama ya yule aliyemwona mwanzo.

Mama Dorice alishtuka. Akamtazama kwa makini binti yule akagungua ni yeye kabisa tena cha ajabu binti yule alimpungia mkono huku akitabasamu. Na alikuwa amependeza kupita kiasi gauni refu jekundu alilovaa, pamoja na viatu virefu vya bluu alivyovaa vilivyoenda sambamba na mkufu na hereni zake. Huku nywele zake ndefu zilizojimwaga zikimfanya aonekane maridadi zaidi.

Mama Dorice hakulaza damu akaamua kumfuata haraka binti yule lakini cha ajabu

...Lakini cha ajabu kila alipomsogelea binti yule naye alikaza mwendo zaidi. Mama Dorice alishuhudia jinsi ambavyo mwanaye alitembea kwa madaha sana.

"Doriiiice!" Aliita kwa sauti lakini yule msichana alipogeuka hakuwa Dorice tena ilikuwa ni sura ya msichana mwingine kabisa. Mama Dorice alichanganyikiwa sana, ni kwanini hali inakuwa vile? Lakini hakupata jibu. Kaka yake alimfata haraka na kumshika mkono.

"Dada utagongwa na magari... Kwani unamfata nani?" Aliuliza kwa mshangao kwani yeye hakumwona MTU yeyote.

"Namfuata Dorice..."

"Huyo Dorice yuko wapi maana tangu tupo kule unamfuata tu?"

"Sio yeye.. Nimemfananisha...."

"Dada bwana usiwaze sana.... Ona sasa mpaka watu wanakushangaa ujue.. Unaita kila mtu Dorice..."

"Lakini Mimi nilimwona kabisa kaka...."

"Haya tuondoke"

Mama Dorice alikuwa bado anaifikiria ile hali, akajua lazima kuna kitu kinaebdelea kuhusu Dorice, kwanini amfananishe kiasi kile lakini bado hakuwa na jibu sahihi.

Wakati wa safari ulipowadia, waliingia kwenye basi na kukaa kwenye siti zao.Walisafiri kwa mwendo kidogo, ndipo macho ya mams Dorice yalipotua kwenye sura ya yule binti aliyemwona toka wakiwa kituo cha mabasi Jana yake. Na alikuwa amevaa nguo zile zile, alikaa Pembeni yake. Moyo ulimpasuka kwa mshtuko akafikinya macho yake na kumtazama tena binti yule aliyeachia tabasamu mwanana. Akamsalimu mama Dorice. Mama Dorice alishangaa, kilichomshangaza zaidi ni kwamba alipoingia kwenye gari hakumwona MTU yule na hata alipokaa hakukaa na binti yule. Sasa imekuaje yupo nae?

"Mama nilikuona sehemu!"

"Mh hata Mimi nilikuona!" Alisema mama Dorice.

"Kwanini ulikuwa unanifata?" Aliuliza binti yule ambaye kila wakati alipenda kutabasamu.

"Nilikuwa na kufananisha na mwanangu" alisema mama Dorice.

"Mwanao? Anaitwa Dorice?"

"Ndio... Umemjuaje?"aliuliza mama Dorice lakini msichana yule alicheka sana kitendo kilichomshangaza mama Dorice.

"Mama we si uliniita Dorice?"

"Eeh ndo jina lake.." Wakati wakiendelea na mazungumzo Yale mjomba wake Dorice alimshangaa sana dada yake.

"Dada mbona unaongea peke yako? Unajibizana na nani?"

******

Mama Pamela alimtazama binti yake na kumsikiliza kwa umakini.

"Niliota nipo hapa sebuleni... Halafu nikakuona wewe ukiwa haujavaa nguo... Ukanifata na kunishika kifuani kwa muda kisha ukaniachia.... Halafu ulikuwa unatisha sana usoni...." Alisema Pamela.

Mama Pamela hakutaka kuamini kile alichokisikia, alipigwa na butwaa sana na kubaki kinywa wazi akimshangaa mwanaye.

"Mimi? Pamela! Mbona sikuelewi?"

"Ndio mama nilikuona wewe ukichukua titi langu.. Mama kwanini umenifanyia hivyo?" Pamela alisema kwa msisitizo huku akilia. Mama Pamela alizidi kuchanganyikiwa maana hakutegemea kusikia maneno Yale kutoka kwa mwanaye.

"Ina maana unataka kusema mimi ni mchawi? Pamela kweli unanisingizia hivyo?" Mama Pamela alikuwa haamini lakini hivyo ndivyo Pamela alivyoota. Kwani wakati Doreen akichukua titi lake, pamela hakuiona sura ya Doreen ila alions sura ya Mama yake hivyo aliamini kuwa mama yake ndiye aliyemfanyia vile.

"Mama! Sikujua kuwa wewe ni mchawi! Kumbe ndivyo ulivyo? Nilikuamini sana mama yangu... Kwanini umenifanyia hivi? Kwanini mama?" Alilalama Doreen na kuonesha ni jinsi gani alivyopoteza uaminifu tena kwa mama yake. Ilikuwa vigumu sana kwa Mama Pamela kumuamisha mwanaye kuwa sio yeye aliyefanya kitendo kile cha ukatili.

"Pamela mwanangu... Wewe ndo mwanangu wa pekee, sina mtoto mwingine zaidi yako Leo hii mimi nikufanyie hivyo? Haiwezekani..." Alijitetea mama Pamela.

"Lakini mama... Ili yote yaishe lazima unirudishie titi langu... Na usipofanya hivyo nampigia simu baba namwambia kila kitu.... Na sio baba tu nawaambia ukoo mzima..."

"Pamela... Sio mimi mwanangu... Nisemeje unielewe?" Mama Pamela alijitahidi kujitetea kadri awezavyo lakini bado ilikuwa vigumu kueleweka. Pamela alilia sana huku akimbebesha mama yake mzigo wa lawama. Alichukua simu na kumpigia baba yake, hofu ikamvaa mama Pamela akiifikiria aibu kubwa ambayo angeipata kwenye ukoo wake na wa mumewe. Mpaka muda ule hakujua kinachoendelea kwa Doreen, kwani alidhani yupo chumbani kwake bila kujua Doreen alishaondoka muda mrefu. Kibaya zaidi kilichompa hofu ni kwamba mumewe angeamini maneno ya Pamela kutokana na jinsi mama Pamela alivyokuwa akimtetea Doreen.

"Lazima aamini... Na atajua ni kweli nimefanya hivyo ndio maana nilimkatalia sana Doreen... Haya majanga ya kupewa uchawi wakati mimi so mchawi!" Aliwaza mama Pamela bila kujua hatma ya tatizo lile.

"Daddy!" Alisema Pamela baada ya simu kupokelewa.

"Yes Pamela... Eti nini kimekupata mwanangu...?" Aliuliza Baba Pamela. Pamela akaongeza kilio huku akimtazama mama yake.

"Daddy! Fanya haraka uje... Kuna mambo mazito sana baba.. " alisema Pamela.

"Nakuja Leo jioni na ndege...."

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)
Mwanafunzi Mchawi Simulizi Z78
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni