Notification
Tidak ada notifikasi baru.

MWANAFUNZI MCHAWI (23)

Mtunzi: Enea Faidy

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU
TULIPOISHIA...
"Daddy! Fanya haraka uje... Kuna mambo mazito sana baba.. " alisema Pamela.

"Nakuja Leo jioni na ndege...."

IKIWA UNASOMA SIMULIZI NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI USIPITWE NA SIMULIZI

TUENDELEE...
"Uje tu baba yangu... Uje haraka.." Alisema Pamela huku akishindwa kuyazuia machozi yake.

Mama yake alibaki kimya huku machozi yakimdondoka. Alishindwa afanyeje.

"Unalia nini na huo uchawi wako?" Alisema Pamela kwa hasira huk

Oy...

.OOH siamini! Siamini kabisa kama sioni nyeti za Eddy" alisema Doreen akiwa amechanganyikiwa sana. Alitazama vizuri kwenye mkoba wake lakini hakuona nyeti za Eddy na hakujua nani amechukua. Kutokana na ulinzi mkali aliokuwa ameuweka ili kulinda vitu vile hakutaka kuamini kama Kweli vimeibiwa.

Doreen alikaa kitandani huku akifikiria kwa muda ndani ya chumba kile cha hoteli. Mawazo yake kila yalipofurika kichwani mwake,jasho jembamba lilimtiririka kwa kasi. "Mbona sielewi hii hali?" Alijiwazia huku akijaribu kutafuta tena nyeti zile ambazo kwake zilikuwa na thamani kubwa kuliko lulu. Doreen alikaa chini kwenye sakafu huku mawazo yakizidi kumuelemea.

Akavua nguo zote kisha akachukua mkoba wake na kuchukua kioo kidogo, akakipaka dawa ya ungaunga kisha akaanza kuomba dua kwa mizimu yake ili iweze kumsaidia katika janga lile gumu lililomkumba. "Mzimu wa Ngotongoto uliomkubwa sana katika ukoo wetu, Mtukufu Tatile na mizimu yako...

Tazama nilivyohangaika na kutafuta zawadi kubwa kama nilivyoagizwa lakini Leo hii sijui ni mzimu gani uliotokea na kutaka kunyang'anya kitu cha thamani kuliko dhahabu... Kafara iliyonzuri kwa mkuu wangu... Nihurumieni mja wenu! Naomba msaada wenu tafadhali.." Doreen alisema maneno Yale kwa hisia Kali huku akiwa ameinamisha kichwa chake chini na mikono yake ikiwa imeshikilia kioo kile. " Ee mizimu yangu tukufu... Nisaidie kumjua mwizi wangu ili nimshughulikie..."

Alisema Doreen na ghafla radi Kali ikapiga kwenye kioo kisha kioo chote kikatapakaa damu. Doreen alishtuka sana akaona hali si shwari maana kioo kile kutapakaa damu kilikuwa na maana ya uwepo wa vita Kali dhidi yake. Hofu ikamtawala sana binti yule, hofu ikamtanda akashindwa kuelewa ni nani adui yake haswaa!. "Doreen! Doreen! Inakubidi kupambana!" Ilisikika sauti nzito yenye mwangwi mkali lakini mzungumzaji hakuonekana. "Doreen! Tumia nguvu zako zote ulizonazo, sisi tuko nyuma yako...

Onesha uwezo wako ili uutwae utukufu.. Uwe malkia uliyetukukaaa!!" Iliisisitiza sauti ile iliyoongea kwa msisitizo wa hali ya juu. Doreen aliogopa sana, akajua tayari mwisho wake umewadia lakini hakuwa na budi kujipa moyo wa ushindi na kuwa na matumaini ya kumbaini mbaya wake. "Nani mpinzani wanguuuu? Nasema nani atampinga Doreen Mbwana mtoto wa kitanga? Kama yupo ajeee!" Alisema Doreen kwa ujasiri wa hali ya juu na kuivua hofu yote aliyokuwa nayo.

Ghafla upepo mkali ukavuma kwa nguvu ndani ya chumba kile cha hoteli. Sauti Kali ya kicheko kilichojaa dharau na jeuri ikasikika na kumfanya Doreen ahamaki sana. Hali ya taharuki ikazuka moyoni mwa Doreen kwani daima hakufikiria kutokewa na mpinzani wa kumpinga mambo yake. "Doreen! Wakati wako umekwisha! Uchawi wako na mateso yako kwa wanadamu wasio na hatia sasa umefika kikomo... Ha ha ha nakwambia Doreen huna nafasi tena!"

Ilisikika sauti nyembamba na nyororo ikimwambia Doreen. Doreen alishtuka sana kusikia maneno Yale. Kilichomtisha zaidi ni kwamba alishindwa kumuona mtu aliyezungumza. "Kama una uwezo njoo nikuone!" Alisema Doreen. "Ha ha ha! Nitakuja unione wala usiwaze" maneno Yale yalizidi kumchanganya Doreen alibaki kimya akiwa ametumbua mimacho kama vitunguu huku akitazama huku na kule ndani ya chumba lakini bado hakufanikiwa kumuona mtu yule aliyezungumza kwa dharau sana.

"Naongea na huyu binti nilimfananisha na Dorice" alisema mama Dorice na kuwafanya majirani zake wageuke kumtazama Kwa mshangao. Hakujua watu wale wanashangaa nini lakini kilichowashangaza ni kwamba walimsikia mama Dorice akizungumza lakini hawakujua anaongea na nani kwani hawakumuona yule mtu. "Dada upo sawa?" "Nipo sawa ndio! Kwani vipi?" "Muda mrefu sana unaongea peke yako hapa..." "We Majaliwa tuheshimiane....

Nitaongeaje peke yangu kwani Mimi mwehu?" Alisema Mama Dorice kwa ukali kiasi. Abiria ndani ya gari ile walimshangaa sana mama Doreen wakahisi labda hayupo sawa kiakili kwani jirani yake kwenye siti hakuwa mwanamke Bali ni mwanaume mtu mzima mwenye umri kama miaka arobaini na tano.

Na kwa muda wote aliokuwa akizungumza Mama Dorice mwanaume yule alilala usingizi. "Dada hebu mtazame jirani yako vizuri" alisema Majaliwa. Mama Doreen alitamtazama jirani yake kwa makini sana. Ghafla akapatwa na mshtuko wa ghafla Baada ya kuona aliyedhani ni binti anayeendana sana na mwanaye si mwenye siti ile.

Aliyekaa pale ni mtu mwingine tofauti. Mama Dorice alishtuka sana, moyo ukampasuka paah! Hakuamini macho yake. "Kaka Majaliwa!" "Naam dada!" "Mbona sielewi Mimi? Ni mtihani gani huu?" "Labda una malaria dada?" "Sina chochote ila nilikuwa nimekaa na binti Fulani hapa. ." "Mmh! Hapo pagumu.." Mama Dorice alishindwa kuelewa chanzo cha yote hayo ikabidi akae kimya tu.

Macho yake yakatua dirishani na kutulia kwa muda kama aliyetazama kitu kilichomvutia sana. Ghafla akamwona Dorice dirishani( dirisha la gari) akimpungia mkono wa kumuaga kisha akaachia busu la mbali la upendo. Mama Dorice alishtuka sana akabaki ameduwaa tu mpaka Dorice alipopotea ghafla. "Kaka!" Aliita.....

Mama Eddy alitazama juu ili kuona kama kuna chochote lakini hakuona kitu. Ilimbidi atumie nguvu zake za uchawi alizokuwa Nazo ili kujilinda kwani aliziona dalili za kuvamiwa katika mazingira ya kutatanisha.

Mama Eddy ambaye jina lake halisi alijulikana kama Maimuna hakuwa Mtu wa kawaida Bali alitumwa na uongozi mkuu wa himaya aliyotokea Doreen ili kumsaidia kupata vitu alivyovihitaji.

Alitumia mbinu ya kujifanya mke wa Mr Aloyce ili kuweza kumteka vizuri na kumfanya asihangaike sana kuhusu mwanae kwani kulikuwa na uwezekano mkubwa sana wa kuharibu kazi. Maimuna alikuwa ni kijakazi mkongwe wa Bi Tatile na alikuwa akiaminika sana katika himaya ya Wanatatile kwani ni mtu pekee aliyewahi kufanikisha ajali kubwa ya mabasi mawili iliyoua abiria wote kisha wakafanywa kitoweo katika sikukuu ya kumpongeza Bi Tatile kama kiongozi bora wa wachawi wote Afrika Mashariki. Bi Maimuna alikuwa akiaminika sana kwa kila kazi anayoagizwa kwani hakuwahi kufanya makosa zaidi ya tukio moja tu la kuanguka kanisani akiwa katika harakati za kuwanga mchana.

"Maimuna! Maimuna! Hapa sio kwako na Leo ndio mwisho wa ubaya wako kwenye familia hii" ilisikika sauti nyororo isiyo na mkwaruzo hata kidogo huku ikijirudia rudia. Maimuna alibaki na mshangao wa ajabu sana, akataharuki huku akihema kwa nguvu. Akaaangaza macho kila upande pasipo kumuona mtu yeyote.

Akazidi kuchanganyikiwa sana. Ghafla wazo likamjia akilini mwake, bila kuchelewa akaamua kulifanyia kazi. Akanyoosha mkono wake wake wa kulia kisha nguvu nyingi zikamjia kama radi mkononi mwake. Bi Maimuna akaachia tabasamu mwanana akiamini hakuna kitakachomdhuru kwa wakati ule wala wakati mwingine wowote. akatulia kimya akimsubiri adui yake, lakini hakuona chochote zaidi ya ukimya mzito uliokuwa umetawala.

"Kumbe unaniogopa eeeh!" Alisema Maimuna.

"Ha ha ha! Sikuogopi Maimuna... Nakuvutia pumzi tu maana sina papara" sauti ile iliyojaa dharau ilisikika. Bi Maimuna hakutushika hata kidogo kwani alikuwa anajiamini kupita kiasi. Ghafla sura yake ikabadilika sana na kuwa sura ya kutisha sana.

Meno yakawa marefu kama mnyama mkali, kucha zikawa ndefu na Kali kama za chui anayemvamia swala, macho yake yakawa meusi huku mboni yake ikiwa nyekundu kama moto. Lengo lake lilikuwa ni kuonesha nguvu zake mbele ya adui yake ambaye hakujua ni nani. Ghafla kicheko kikali cha kutisha kilichojaa dhauri na jeuri kikasikika na kumfanya Maimuna ajione mdogo kama simimizi ilihali hamjui nana aliyemcheka.

Wakati huo huo Mlango ulifunguliwa na Mr Aloyce aliingia sebuleni pale.

"Mamaaaa" Mr Aloyce alipiga ukunga wa nguvu baada ya kumkuta mkewe akiwa na umbile la kutisha sana. Uvumilivu ulimshinda alijikuta anakimbia nje kama chizi huku akihema kwa nguvu. Mlinzi alimshangaa Mr Aloyce bila kuelewa kinachoendelea.

"Vipi bosi?" Aliuliza mlinzi huku akicheka sana. Mr Aloyce alianguka chini kama mzigo huku akihema kama Mtu aliyepanda mlima mrefu kwa kasi. Mlinzi alimsogelea na kumuuliza kilichojiri.

"Kuna maajabu humo ndani"

"Maajabu gani?"

"Mke.. Mke wangu...Ame..."

"Amefanyaje tena?" Aliuliza mlinzi kwa woga kwani alishapewa onto Kali na mwanamke yule kuwa asimfatilie kwa lolote. Lakini kabla hajasema chochote kuna kitu kiliwashtua Mr Aloyce na mlinzi wakabaki wameduwaa kwa mshangao.

******

Mama Pamela hakuwa na la kufanya zaidi ya kulia tu. Muda wote ule hakujua Doreen anaendeleaje ila kilichomshangaza ni kwanini Doreen hakwenda sebuleni kujumuika nao? Alinyanyuka kitini na kwenda chumbani kwake. Lakini ghafla mshangao wa ghafla ulimvaa mwanamama yule baada ya kukuta hali ya chumba ni mbaya sana kila kitu kilikuwa shaghalabaghala tu, ndipo machale yakamcheza, akasogelea droo anayohifadhia pesa.

"Mungu wangu!" Alishtuka mama Pamela baada yakukuta droo IPO wazi lakini haina pesa yoyote zaidi ya stakabadhi ambazo hakuwa na shida nazo wakati ule. Macho yalimtoka kwa mshangao huku akitoatoa vitu ndani ya droo ile bila kuona chochote. Akasimama wima akiwa ameshika mkono kiunoni kwa hasira

"Doreen!" Aliita kwa jazba bila kujua Doreen alikwishaondoka muda mrefu uliopita. Mama Pamela akakugua tena ili kujiridisha kama kweli pesa hazikuwamo lakini bado hakukuta pesa ndani ya droo ile wala eneo lingine chumbani mle.

Mama Pamela alichanganyikiwa sana akatoka ndani ya chumba kile na kupiga hatua za harakaharaka koridoni kuelekea chumbani kwa Doreen.

Alifika mlangoni na kufungua mlango kwa jazba kubwa. Lakini cha ajabu chumba kilikuwa kitupu na hakukuwa na mtu yeyote wala dalili za uwepo wa mtu. Mama Pamela akahamaki, akamwita Doreen kwa sauti kali lakini hakuitikia.

"Mungu wangu ina maana Doreen ametoroka na pesa au?" Alijiuliza Mama Pamela akiwa ameishiwa nguvu kabisa. Hakutaka kuamini kama binti anayemuamini kiasi kile angetenda tukio lililotokea.

Mama Pamela alitoka nje ya nyumba yake ili kumtazama vizuri Doreen. Alimtafuta pale uani na kila upande wa nyumba lakini Doreen hakuwepo.

Naomba Bonyeza Matangazo Kila Unapoyaona ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

JIUNGE KWA UPDATE NA BURUDANI ZAIDI
WhatsApp Channel=> CnZ Media(Follow)
Telegram Channel=> CnZ Media(Join)
Mwanafunzi Mchawi Simulizi Z78
Jiunge kwenye mazungumzo
Chapisha Maoni