MAMA VANESSA (12)

Zephiline F Ezekiel
0

SEHEMU YA KUMI NA MBILI
ILIPOISHIA...
Lucas lalifurahi sana na kuona msichana huyo alikuwa na uwezo mkumbwa wa kukariri. Aliondoka zake na kurudi nyumbani. Alikaa kwa muda wa siku tatu bila kupokea simu kutoka kwa Mishel. Kila siku alikuwa akipita kwenye ile nyumba ili aweze kuangalia nini kilikuwa kikiendelea na kama anaweza kumuona binti huyo. Haikuwa hivyo hakuweza kabisa kumuona binti huyo.

KAMA SIMULIZI HII UNASOMEA NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI KUPATA VIPANDE VYOTE KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈

ENDELEA NAYO...
Ilikuwa ngumu sana kwake na roho ilimuuma maaana muda wa kufungua shule ulikuwa umefika. Hatimaye aalifungua shule na kuondoa zake. Roho yake ilimuuma sana kwa maana simu shuleni walikuwa wakikatazawa na hata wakituia kwa ujanja uajnja sana sana ni wikiend

Mwezi mzima ulipita kabla ya siku moja kupokea simu ngen kutoka kwa msichana. Sauti hiyo nyororo iliyosisimua masikioni mwake haikuw aya mtu mwingine bali ya Mishel. Mishel alaimweleza kuwa namba zake alikuwa bado anazikumbuka na hakumtafuta kwa sababu siku ile walivyoachana alaianza kuugua na alailaza. Huo ukawa mwanzo wa mawasiliano yao. Mpaka Mishel anamalaiza form four na Lucas anamalaiza form sx watu hawa walikuwa wapenzi wa kwenye simu. Baada ya Mmishel kumalaiza form four alaienda Dar kwa dada zake wengine ambao kipindi hicho walikuwa wameolewa. Na kama bahati vile na Lucas alienda huko huko. Wawili hawa sasa waliweza kukutana.

Lucas mawazo yakaamia siku ya kwanza kabisa kushiriki tendo la ndo na binti huyo. Anakumbuka aaimkuta binti huyo akiwa na bikira kabisa. Anakumbuka jinsi alivyopata tabu kukivunja kikombe cha udongo cha binti huyo. Anakumbuka jinsi alivyoangaika nae kufanikisha hilo. Tangu siku hiyo ukurasa wa mapenzi baina yao ulikuwa umefunguliwa. Mishel alikuwa akimpenda sana nay eye alikua akimpenda sana. Kuna vipindi vigumu walivyopitia na vyote walikuwa wakivikumbuka. Moja ya kipindi kigumu ni pale Mishel mataokeo yake yalivyotoka hayakuwa mazuri hivyo ilimlazimu kubaki Dar kwa dada yake wakati Lucas akaiendelea na chuo.

Huko Dar Mishel alijifunza hizo kozi fupi ndani ya mwaka. Baaada ya hapo sasa aliajiriwa. Uzuri wake ukawa chachu ya kuwavutia wanaume wengi ikiwemo boss. Mishel alibadilika sana na hakumthamini tena Lucas. Mishel jiji lilimkubali sana alikuwa mrembo mara dufu. Hakuwa wa hadhi ya Lucas tena bali alikuwa akitoka na watu wenye fedha zao. Kipindi hicho Lucas alikuwa ameijiunga na masomo kwenye chuo kikuu cha Dar es salaam. Hapo safari ngumu na histori ya uhusiano wa watu hawa ndipo ilipokuwa ndefu. Lucas alikuwa akaimpenda sana bint huyo na hakuweza kabisa kukubaliana na matokeo kuwa aliachwa kwa kigezo kuwa hakuwa na fedha. Roho ilimuuma sana na hakuamini kuwa kama kweli binti huyo amebadilishwa na starehe za jiji. Tukio hili lilimfanya Lucas kumwaga machozi na aliona tabia ni kama ngozi ya mwili huwezi kuibadili.

Maisha ni safari mbwembwe za Mishel ziliishia njiani mara baada ya waliokuwa wakimpa kiburi kuanza kumyanyasa. Walimchoka baada ya kupata walichopata. Mishel alichoka akachakaa hiyo ni mara baada ya kuugua kwa muda mrefu na haikujulikana alikuwa akiumwa nini lakini afya yake ilikuwa imedhoofu mno. Uzuri wake ulifubaa na alififia machoni kwa wanaumme wakwere. Fimbo ya shida za maisha ilimpiga maana hata dada yake aliyekuwa akimpa hifadhi alifariki dunia. Mishel ilimlazimu kurudi kijijini ambapo alikuwa hana mbele wala nyuma. Huko ndipo Lucas alipopata kumuona tena.Alimuonea sana huruma maana binti huyo alianza kuzeeka ingali alikuwa bado mdogo. Mishel alimuomba msamaha Lucas na kumtaka amsamehe tu kwa yote aliyomtendea hata kama hawatakuwa tena wapenzi.

Lucas kama ilivyo imani ya dini yake aliamua kumsamehe binti huyo lakini alisema kuwa kwa sasa watakuwa kama kaka na dada. Lucas akamshauri binti huyo arudie mtihani wa kidato cha nne na akafanikiwa kwenda form five basi yeye atamsomesha. Mishel kwa kuwa hakuwa na mbele wala nyuma alikubaliana na mawazo hayo. Lucas kwa kutumia pesa ya mkopo aliyokuwa akipewa chuoni aliweza kumlipia pesa ya usajili. Lucas alikuwa na moyo wa ajabu sana maana alirudisha moyo wa pendo kwa binti huyo. Akaanza kumuhudumia kwa vitu vingi na hatimaye urembo wa binti huyo ukaanza kuonekana tena. Kadri siku zilivyozidi kwenda walikuta wakitamaniana nakutamani kuvunja ahadi kuwa kwa sasa wataishi kama kaka na dada. Lucas pia alivutiwa na mwenendo wa Mishel maana aliokoka na kuwa mcha Mungu. Mishel alikuwa wa kusali na kuomba yeye na biblia biblia na yeye. Shetani aligeuka kuwa malaika.

Lucas akaamaini sasa Mungu amaembadilisha msichana huyo. Kw kuwa nay eye hakuwa na uhusino mzuri tangia acahane na mwanamke huyo amekuwa wa kupita pita tu alaiamua kumrudia. Kiu ca kwanza lichokifanya ni kumzidishai upendo na kumjali sana. Mpka Misheli akawa anaogopa. Alipewa huduma zote anazostahili kupewa mwanamke.

Siku moja aliamua kumchukua na kwenda naye angaza. Lengo lilikuwa ni kumpima afya. Kwa bahati nzuri binti huyo alikuwa ni mzima. Jambo hili lilikuwa furaha kwa Lucas kwa maana mwanzoni alikuwa na hofu sana akiwaza labda binti huyo alikuwa muathirika wa ukimwi na ndio maana alikonda vile. Awali ni awali hakuna awali mbovu. Kuku wako mwenyewe hakuna haja ya kumshikia manati. Siku moja Lucas alimwomba binti huyo amsindikize mahali ambapo ilikuwa ni mkoa wa jirani. Huko walifanya kilichowapeleka na usiku uliingia na kuwakuta huko. Lucas hakutaka kuuliza hiki wa kile alichukua chumba. Usiku huo ulikuwa usiku wa kukumbushia enzi na kufungua ukurasa mpya wa mapenzi. Mwendo wa uchokozi wa Mishel na madaha ya swaga alizojaliwa zilitosha kabisa kushawishi Lucas kuona anastahili kupata mavuno ya kile alichokipanda.

Alihudumia sana mgodi huo na sasa ilikuwa ni fursa nzuri kwa yeye kupata walau madini kidogo. Walianza kwa kuogeshena. Ile michezo ya kuwaamsha waliolala ilifanyika huko. Na kweli Kiungo mchezeshaji wa Lucas alianza mbwembwe zake za kusimamisha kichwa. Mishel alikuwa kama mwanawali ambaye hakuwahi kushiriki tendo hilo. Miaka miwili ya mateso hakuwahi kabisa kufanya tendo hilo hivyo kumfanya awe mwenye hamu zaidi ya neno lenyewe. Hawakutaka kujua kama waliweka ahadi kuwa ataishi kama kaka na dada. Mioyo yao ilisemezana na kwa pamoja wakashiriki tendo la ndoa. Ilikuwa ni kupeana raha kwa kwenda mbele hakuna aliyechoka siku hiyo. Utamu waliokutana nao ni kama vile hawakuwahi kujuana kabla.Tangu siku hiyo pazia la mapenzi motomoto likafunguliwa baina yao. Wagombanao ndio wapatanao.Wakaseamna kwa vitendo na sasa wakapeana kazi ya kila mmoja kufuta makandokando yote waliyokuwa nayo.

“Kama una mapenzi au ulifikiria kuwa naye kwa sasa itabidi umuache na mimi nitafanya hivyo kwa sasa yalioipita si ndwele tugange ya mbele.Nakupenda sana Mishel na naapa kukoa”

“Kwa sasa mimi nimebadilika sana hata leo sijui imekuwaje nikadhini. Lucas mimi ni mcha Mungu mwili wangu ni hekalu ya bwana.Sina mpenzi na nipo tayari kuolewa na wewe kama itakupendeza.. najua umenirudia kulip akisasi ila tambu akisaasi na hukumu ni vya Mmungu..Nipende tena , nipende tana na nipe nafasi kwenye moyo wako.”

Kila mmoja aliongea maneno ya hisia usiku huo. Na kila baada ya mazungumzo machache nyege zao ziliamka na kuanza tena kupapasana kabla ya kupeana penzi. Walifanya yote na kila wawezalo ili mradi kukata kiu ambayo kila mmoja alikuwa nayo juu ya mwenzake. Walirudi mkoani kwao na kila mmoja aliendelea na ratiba yake. Lucas likizo iliisha na alirudi chuoni.Mishel alisoma kwa bidii sana na baadaye alifanya mtihani wa kidato cha nne. Ilivyo bahati kwa masomo yale ambayo aliyarudia alifaulu kwa kiwango kikumbwa sana. Hili limstaajabisha hata Lucas. Kwa jinsi binti huyo alivyokuwa bize kwa mambo ya dini na Mungu hakuwa na imani kama angeweza kufanya vizuri. Sasa akawa amepeta nafasi za kusoma kidato cha tano. Mishel akamwambia kuwa anataka kusoma masomo ya kidato cha tano na sita kwa mwaka mmoja badala ya miaka miwili. Walibishana lakini Mishel alikomaa na anachokiamini kwa madai kuwa umri wake ulikuwa umeenda sana.

Imani yashinda yote Mishel alifanya kama alivyoamini na Mungu aliendelea kuwa upande wake. Alisoma kama mtumwa huku Lucas akijinyima kwa kila hali kumlipia ada. Mwaka mmoja ukakatika kwa haraka na kipindi hicho Lucas alikuwa ameshamaliza chuo yupo mtaani akirandaranda na bahasha ya kaki kutafuta ajira. Hiki kipindi kilikuwa kigumu sana maana Mishel alihitaji sapoti lakni Lucas hakuwa na uwezo. Hatimaye kwa kuunga unga Mishel alifanikiwa kuuliza form six. Matokeo yalipotoka bado alistaajabisha ulimwengu kwa kufaulu. Safari ya chuo ikaanza na kidogo ilikuwa yenye haueni kwa Mishel alipata mkopo. Alisoma chuo kwa raha mpaka akamaliza. Na ndio ikawa fursa ya wawili hao kuoana.

Kumbukumbu hizi ndizo huwa zinamliza Lucas na kumfanya hata hashindwe kupokea simu ya Mishel. Neno “nimekukumbuka mme wangu” aliyoandika mara baada ya yeye kusita kupokea simu zilimfanya akumbuke mengi sana. Alikumbuka yaletayo furaha na zaidi pia alikumbuka yaletayo huzuni.

“Nimetoka naye mbali sana, nimemlea, nimemtunza lakini bado ameamua kuiacha. Naamini kweli tabia ni kama ngozi ya mwili kuibadili ni shughuli. Si mara yake ya kwanza kunisaliti, amerudia tena na huwa ananiacha kwenye kipindi kigumu. Lakini atanikumbuka na Mungu atanilipa”. Lucas ni kama vile alichanganyikiwa maana maneno hayo alikuwa akiyaongea pake yake. Chumba alichokaa alikiona kidogo. Alisimama na kuzunguka zunguka kama taira.Ni usiku lakini mawazo kuwa apike nini au atakula nini yalimwishia. Akafungulia sabufa yake na kuweka mziki mkumbwa. Mara mlango wake uligongwa. Alishtuka kidogo maana hakutarajia mgeni na wageni wake huwa ni wawili tu mama Vanesa na Kimaro. Alijinyanua kizembe na kwenda kufungua mlango. Macho yalishangaa moyo ulimdunda kupita kiasi mara baada ya kumuona mwanamke ambaye hakujua amafikaje fikaje hapo na nani kamwelekeza.*****Je mwanamke huyo ni nani?

“Upweke ni ugonjwa mbaya sana huku duniani na upweke unaweza kukufanya ukawaza mambo mengi yaliyopita na kujikuta mwenye huzuni. Nimegundua utakuwa mpweke sana usiku huu na nimeona walau nije nikufute machozi yako”

“Kwa sasa sina machozi maana nilishaliia mpaka yakakauka.Umejauje kama nakaa hapa?” alihoji Lucas kwa upole

“Naomba tuzunguzie ndani maana leo mimi ni kama malaika ambaye nimetumwa kukuleta faraja”. Alijubu Juliana.

Haikujulikana Julaina alikuwa ametoka wapi na amejuaje kama mwanaume huyo alikuwa akikaa hapo. Julaina alikuwa na yake moyoni ambayo Lucas hakuyafahamu. Lucas alikubaliana na binti huyo wakaingia ndani.

“Kwa sasa najua kila kinachoendelea kweye maisha yako. Najua unatoka na mke wa boss wako lakini hata hivyo kisasi sio jambo zuri..

USIKOSE SEHEMU IJAYO

Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Share App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)