
Mtunzi: Eliado Tarimo
SEHEMU YA SABA
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
Kulikuwa na ukaribu mkumbwa uliofanywa ili angalau Lucas hasione kuwa dunia ilikuwa imemtenga. Lucas akashindwa kuelewa kwa nini kipindi hicho wanawake walikuwa wakiwa karibu yake sana.
KAMA SIMULIZI HII UNASOMEA NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI KUPATA VIPANDE VYOTE KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA NAYO...
Aliona kama ni bahati na anaweza hata kufanya maamuzi magumu ya kuwa na wasichana wengine wengi maradi kupunguza machungu ya kupokonywa mke wake. Pamoja kuwa alikuwa akitaka kufuata taratibu za sheria za kazi bado alikuwa akiamini na akatamani kuivuruga familia ya boss wake. Alianza kuifuatilia familia hiyo kuwa na habari za ukaribu. Kwanza aliambiwa boss huyo alikuwa na mtoto wa kike ambaye alikuwa mkumbwa na alikuwa akisoma chuo kikuu cha Dar es salaam.
Alifuatilia na kugundua kuwa binti huyo alikuwaa akiitwa Nancy. Alifanikiwa kuzipata mpaka picha zake na roho mbaya ilishamjia kuwa atamuharibia maisha binti huyo. Alipanga kutembea naye na kama yeye akishindwa basi atatumia marafiki zake ili ampate.Nia yake kumbwa ilikuwa kwamba Boss yake apate hayo maaumivu ambayo yeye alikuwa akiyapata. Alijua kabisa dawa ya moto ni moto na mke au mtoto anauma sana. Maumivu aliyopata yalikuwa ni makubwa sana ambayo yalimfanya afikirie unyama. Lakni kwa kuwa mama Vanesaa ameonesha kuwa anataka kuwa na mimi kwa ajli ya kulipiza kisasi basi nitaanza na yeey na mimi nipo tayari kulipa kisasai. Alendele akupanga mikakati yake ambayo aliamini kuwa itafanikiwa. Habari za matoto wa boss wake amabye alikuwa chuo kikuu cha Dar es salaa alikuwa akaizipata kutoka kwa rafiki yake ambaye alaikuwa kifundsiha hapo. Kkwa bahati nzuri kan baadhi ya vipibdi alaikuwa akimfundisha binti huyo. Yaani walikuwa wapo tayai hta kumfelisha mradi tu kulipa kisasi. Ingawa Nancy hakuw ana makosa aliingizwa kweye mango huo.
Siku zilizidi kuyoyoma na hatimaye mama Vanesa alirudi kutoka huko Dar es salaam. Kkw akipindi chote hicho walikuwa wakiwasiliana na mama Vanessa alimsahuri kijana huyo asikimbilie mahakamani au huko idara ya kazi kwa sababau hatofanikiwa. Alimweleza kuwa boss wake anajauna na watu wengi sana na anauwezo wa kununua hata haki. Alimweleza huyo anahitaji kufanyiwa kitu cha kibinadamu amabcho kitauumiza sana. Siku ya tatu tangia watoke Dar es salaam ndio siku amabyo walipanga kukutana. Lucas Manyama alipendekeza kuwa wasikutanie Musoma kwa sababu anahofia usalama wake. Walipanga kukutana Mwanza wakiamaini huko wanaweza kuweka mipango yao. Kinyume na mawazo ya Lucas kuwa mama huyo angekataa la hasha mama huyo hakukataaa na badaa yake alikubali.
Lucas alimshirikisha Kimaro juu ya mipango hiyo na Kimaro akapigilia msumari kuwa hiyo ndo chansi kumbwa sana ya kulipa kisasi.
“Yaaani wewe mwambie aje tena afanye mpango alale huku huku “ Kimaro alisisitiza.
“Sasa nitaanzaje kumwambia kuwa atalala cha msingi mimi naona tufanye kama siku ile. Akija hakuna cha kupanga mipango ni kula bata kwa kwenda mbele alafu baadaye tunampeleka ile hotel kisha tunachukua chumba alale.”
“Sio tunachukua chumba alale bali tunawachukulia chumba mlale. Tena hatutaenda pale pa siku ile tutaenda hotel kabisa yenye hadhi yake.Alafu mimi nitatagesha kamera zangu ukishafanikiwa kufanya nae mapenzi ndo hapo sasa boss atajua kuwa dunia duara na kila binadamu yupo kwenye mzunguko”
Waliweka mikakati yao na Kimaro aliaapa kuwa yupo tayari kutumia gharama yoyote ilimradi tu kukamilisha hilo. Ilikuwa ni faraja kwa Lucas kusikia kuwa kijana huyo atafanya kila awezalo kumsapoti. Basi siku ya kukutana Mwanza ilifika. Mama Vanesaa siku hiyo alikuwa amevaa kisichana na kumfanya aonekane ni mdogo sana tena rika moja na kina Lucas. Alivaa nguo za thamani nguo zilizompendezesha sana , nguo zilizofanya uzuri wake kuonekana.
“Aisee huyu boss wangu ni kiboko yaani hajawahi kukosea. Yaani atakuwa na ugonjwa na watoto wazuri. Yaani sio mke sio michepuko ni alikuwa akichagua wanawake wazuri wenye mvuto kwa kila mwanaume.” Mawazo hayo yaliojawa matamanio na uchu wa ngono yalikuwa yakiwazwa na Lucas akiwa kwenye hotel moja iliyojengwa ndani ya kisiwa kilichopo ndani ya ziwa Victoria.
“Umependeza sana mama Vanesa sasa mbona ulikubali kuwaacha vijana wenzio na kuwa na mzee” Lucas alitupa swali la kizushi.
“Mapenzi alinipenda akanichanganya na pesa zake basi nikajikuta naingia kwenye ndoa na baba mtu mzima”
“Hivi mama Vanessa sio kwamba ulimwacha mpenzi wako saiz yako na kuamua kuwa na huyu baba”
“Aisee una maswali mengi sana lakini usiwe na hofu maana maisha kuna kukosea na kujifunza”.
Muhudumu alikuja na kila mtu aliagiza kinywaji alichopenda. Lucas hakujivunga aliingiza kinywaji kigumu ambacho alijua kabisa kitamlipua kwa muda mfupi na kumfanya aongee vitu vizito. Bila kutarajia na mama Vanesaa alaigiz apombe kali. Alishangaa maana kwa msichana wa namna hiyo lazima angetumia vitu laini.
“Leo nataka nikumbushie enzi zangu maana sijatumia pombe kali tangu nimalize chuo” Mama Vanessa aliongea huku akijimiminia pombe kwenye glass.
Walikunywa na kwa muda mfupi tu mama Vanesa alianza kurembua na kuongea vitu vya ajabu ajabu ishara kuwa alikuwa amelewa.Hii ilimpa chansi Lucas kuanza kucheza na hisia zake ili aweze kujua kama anaweza kulala naye. Alichukua mkono wa Mama Vanesa na kuubusu. Mama Vanesaa akarembua macho zaidi na kusema anatamani kama angembusu mdomoni..
Lucas na yeye hakutaka kufanya makosa alipeleka mdomo wake kwenye kinywa cha mama Vanessa. Alimbusu na kurudisha. Hakuwa na uhakika wa moja kwa moja kwani huyo mwanamke mke wa boss wake ameamua kujiachia na kuonesha yupo tayari kwa lolote. Kwa jinsi alivyokuwa mwanamke wa gharama isingekuwa rahisi hivyo kukubali kukutana na mtu wa chini kama Lucas.
“Nataka kuogelea”mama Vanessa aliropoka mara baaada ya kuangalia kwa muda mrefu maji ya ziwa na jinsi ambavyo watu walikuwa wakiogelea pembezoni mwa kisiwa hicho. Lucas alitafakari kidogo na kumwambia hasiwe na hofu ngoja akachukue boti ya mwendo kasi.
“Wewe mimi boti naogopa”
“Usiogope upo na mimi” Lucas alijibu huku akiondoka na kuelekea sehemu ambapo viboti hivyo vilikuwepo. Hakuwa na wasiwasi maana haikuwa mara yake ya kwanza kula bata eneo hilo.Hili kumuondoa hofu mama Vanessa, Lucas alilipanda kishakuingia ziwani. Aliweza kuliendesha kwa madaha huku akikata mwaimbi ya ziwa mpaka sehemu za mbali kidogo. Alifanya mbwembwe zote kuonesha yeye ni mwanaume ambaye haogopi maji. Mama Vanesaa alitumbua macho na kuona kweli mwanaume huyo ni mtaalamu wa kuchezea maji. Baadaye Lucas alikuja na kumpa mkono ili apande.Mama Vanesa alisita kidogo lakini alipiga moyo konde na kuingia kwenye boti. Walianza kuzunguka ziwa huku wakikata mawimbi.Mama Vanesaa alimshika vilivyo kwenye kiuno ili hasije akaanguka.Walifurahia maji na kwa kweli zile pombe ziliyeyuka. Mama Vanesaa alijihsi yupo dunia ingine kabisa maaana tangu aolewe amekuwa mtu wa kubanwa na hakuwahi kufurahia maisha kwa namna hiyo.
Walirudi sehemu waliyokuwa wamekaa. Wote walikuwa na nguo za mama Vanesa zilikuwa zimelowana. Ujue Lucas alipinguza nguo na kubaki na bukta lakini mama Vanesa yeye hakupnguza kitu. Lucas alikuwa ameliona hilo hivyo alimuuliza kama amekuja na nguo zingine.
“Vipi mama Vanessa umekuja na nguo zingine ili ubadilishe hizo maana naona umelowana.”
“Mwanamke lazima ubebe nguo zingine lakini shida nitabadilishia wapi.”
“Twende kule hotelini kuna chumba nilikuwa nimechukua.”
“Mmmh ulichukua chumba kwani umepanga kulala hapa?. Mimi mwenzio baba Vanesaa ataniua natakiwa nirudi leo nyumbani”
“Hapana mimi sitolala hapa nitaenda kulala kwa rafiki yangu, hicho nimekuchukulia wewe ili ukapumzike kama muda utakuwa umeenda sana. Sasa hivi tayari ni saa kumi na mbili sasa huoni kuwa utachelewa.
“Ni kweli lakini umewezaje kulipia chumba cha ghali hili hali huna kazi maisha yako yao hatariini huna pesa?”
Lilikuwa swali kumbwa ambalo hakulitarajia. Hapo alikosa jibu akanyamaza kimya huku simu yake ikiita na kuangalia alikuwa ni Kimaro akipiga. Alishindwa kuipokea na badala yake alitoa funguo na kumkabidhi mama Vanesa.
“Huko mikono salama nenda chumba namba tano badili nguo then urudi tupange mikakati na muda ukiruhusu basi utarudi”. Lucas safari hii alionekana kubadilika kidogo. Mama Vanesa hakutaka kupingana naye alijinyanyua hapo na kuanza kuelekea huko alipoelekezwa. Hapakuwa mbali sana hivyo alipiga hatua zake za madaha na kumuacha Lucas akimsindikiza kwa macho. Mmacho ya Lucas yaliendelea kukiri kuwa mwanamke huyo ni miongoni mwa wanawake wazuri na warembo huku duniani. Baada ya mama Vanesa kuondoka ilikuwa ni nafasi nzuri kwake kunynyua simu yake na kumpigia Kimaro. Kimaro alimweleza kuwa yupo eneo hilo na yupo na kimwana ..
“Upon a Julieth?Lucas aliuliza kwa kuhamaki.
“ Aaaaaah kwani umeambiwa kimwana ni Julieth tu.”
“Sijamaanisha hivyo ila ukimleta huyo atatuona sisi wote ni Malaya tu na imani yake juu yako itapungua.Lucasa alijaribu kueleza wasiwasi wake.
“ Ebu wacha maneno mengi nishafika hapa naingia umekaa kwa wapi?.
“Huku karibu na ziwa kabisa”
“Sawa dakika sufuri”.
Baaada ya nusu dakikaa Kimaro aliingia eneo hilo huku akiongozana na msichana mwingine ambaye yeye alimwita kimwana. Alikuwa ni mwanamke mrembo kwa maana nachelea kusema ni mzuri sana. Maana uzuri ni tofauti na urembo. Uzuri ni kitu ulichozaliwa nacho ni kutokana na uuumbaji wa Mungu. Urembo ni jinsi ulivyojitengneza kuanzia mwonekano, mavazi na mapozi. Alikuwa ni mwanamke mrembo na alivutia machoni pa Lucas.
“Yani huyu kwa kubadili wanawake kama nguo.. Sasa amempata wapi na huyu?” Lucas aliwaza mara baada ya kuwaona wakiingia kupitia boti ambalo lilikuwa linawavusha watu kutoka nchi kavu na kuwapeleka kwenye kisiwa hicho. Kilikuwa ni kisiwa ambacho hakikuwa mbali sana na nchi kavu na hakikuwa kikumbwa zaidi kilikuwa na hote hiyo na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya utalii.. Aliwapungia mkono na wao walimwona. Hao kwa mwendo wa madaha kama mtu na mpenzi wake walijisogeza eneo hilo. Walifika na kuvuta viti kukaa. Walikuwa wenye furaha na waliochangamka sana. Kwa kuwa viti vilikuwa ni vichacahe n kilea alichokuwa amekalia mama Vanesa kilishatumika ilimlazimu kumwita muhudu ili awasikilize wageni na aongeze kiti kimoja.
Muhudumu aliwasikiliza na kwenda kuchukua vinywaji. Mara Mama Vanesa naye alikuwa akija kutoka kwenye hotel. Alichukua muda mrefu lakini haikuwa tatizo kwa Lucas maana anajua kabisa wasichana linapokuja swala la kubadili nguo lazima waanze kujiremba upya.
USIKOSE SEHEMU IJAYO
Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Share App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi