Mtunzi: Nyemo Chilongani
SEHEMU YA NNE
TULIPOISHIA...
TULIPOISHIA...
Basi baada ya saa kadhaa, mzee Hassani akarudi mahali hapo na kukutana naye. Akanichukua na kuanza kuondoka naye mahali hapo. Kumbuka kwamba kwa kipindi chote tangu nifike Dar es Salaam sikuwa nimetoka ndani ya kituo kile, hivyo kutoka humo ndipo nikaanza kuona mazingira halisi ya jiji hilo.
JE UNAISOMA SIMULIZI HII NJE YA APP YA CnZ Media?
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
IPAKUE ILI KUPATA MWENDELEZO KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
SASA TUENDELEE...
Lilikuwa zuri, lililopendeza machoni mwangu.
Mzee Hassani alifika na gari lake na kulipaki nje. Tulipotoka, tukapanda na kisha kuondoka, tulipoelekea kwa kipindi hicho sikuwa nikipafahamu ila kwa sasa, ninapajua mno, palikuwa ni Bunju.
Njiani tulikuwa tukizungumza mambo mengi, katika kila sentensi aliyoongea ilionyesha alikuwa miongoni mwa watu waliojiamini kwa kila walichokuwa wakikifanya. Sikutakiwa kuwa na hofu hata kidogo.
Tulikwenda mpaka tulipofika sehemu iliyokuwa imeunganishwa na barabara moja ya vumbi, tukaingia nayo, tulikwenda zaidi mpaka tukaanza kuingia sehemu iliyokuwa na miti mingi.
Sikuwa na uhakika kama huko kulikuwa na watu walikuwa wakiishi, kulikuwa kimya sana, hatukusimama, tuliendelea kuifuata barabara hiyo ya vumbi mpaka kufika sehemu ambayo barabara ilifika mwisho, sasa tukaanza kuelekea katika njia ambayo hakukuwa na njia rasmi, nikaanza kushikwa na hofu, nikahisi kuna hatari mbele yangu! Mzee Hassani hakutaka kuzungumza tena, naye alikuwa kimya, macho yake yalikuwa mbele, hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, ila kwangu, nilitamani nirudi. Eti huko ndipo kulipokuwa na utajiri! Nikasubiri nione nini kingetokea.
****
Tuliendelea na safari mpaka tulipofika sehemu fulani ambayo ilikuwa na miti mingi na kwa mbali kulikuwa na nyumba ndogo ya udongo. Nilibaki na mshangao, sikuamini sehemu kama hiyo kungekuwa na mtu anaishi, niliogopa, wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa kwenye sehemu mbaya, yenye kutisha ambayo ingenifanya nitekwe na watu wenye roho mbaya.
“Ila si natafuta utajiri, haina jinsi..” nilijisemea.
Mzee Mudi akaniambia niteremke na tuanze kwenda kule kwenye kile kijumba, wakati natembea, mwili wangu ulikuwa unatetemeka mno na wakati mwingine nilihisi ningeweza hata kuanguka.
“Mbona unatetemeka?” aliniuliza.
“Hakuna kitu.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Japokuwa nilimficha lakini nilikuwa na uhakika kwamba alinigundua. Tuliendelea kusogea mbele mpaka tulipokifikia kijumba kile ambapo akaniambia kwamba hatukutakiwa kuingia moja kwa moja bali tulitakiwa kusubiri nje, tukafanya hivyo.
Baada ya dakika kama mbili, tukasikia sauti ndani ikitukaribisha, tukasimama na kuanza kuingia ndani. Huko, tulimkuta mzee mmoja, kwa kumwangalia harakaharaka, alikuwa na miaka kama sabini ila alikuwa amechoka sana kimaisha.
Kichwa changu kikaanza kujiuliza, je, mzee yule angeweza kunifanya niwe tajiri kama nilivyotaka? Wakati najiuliza hayo, nikashangaa mzee yule akisimama na kunishika kichwa changu.
“Usijiulize swali hilo, nitakufanya kuwa tajiri mkubwa sana,” aliniambia huku akiwa amenikazia macho.
Kwanza nikashtuka, ilikuwaje ajue kile nilichokuwa nikijiuliza, mpaka hapo, nikajua kwamba huyo mzee alikuwa na nguvu za ziada. Nikatulia na kumwangalia usoni. Kwa jinsi chumba kile kilivyokuwa, kiliniogopesha mno, kulikuwa na tunguli kila kona, harufu mbaya ambayo ilinifanya kutamani kuziba pua zangu.
“Unataka kuwa tajiri?” aliniuliza mzee huyo.
“Ndiyo!”
“Una uhakika?” aliniuliza.
“Ndiyo mzee!”
“Utayaweza masharti?” aliniuliza.
“Nitayaweza tu..”
Mzee yule akasimama na kuanza kuimba nyimbo ambazo sikuwa nikizielewa kabisa. Hakuishia kuimba tu bali akaanza kucheza pia. Nilibaki nikimwangalia, sikutaka kuzungumza kitu chochote kile kwani hata nguvu ya kufanya hivyo sikuwa nayo.
Akanisogelea na kunipaka unga fulani machoni mwangu. Ulikuwa na rangi nyeusi, alipoyapaka macho yangu, nikaanza kuhisi hali ya tofauti moyoni mwangu, furaha kubwa ambayo sikuwahi kuipata maisha yangu yote.
“Unajisikiaje?” aliniuliza.
“Najisikia vizuri….”
“Unahitaji utajiri wa aina gani? Wa kuku na mahindi au wa milele?” aliniuliza swali ambalo sikuwa nikilijua kabisa.
“Sijajua upo vipi!”
Mzee Mudi ndiye akachukua nafasi hiyo na kuanza kuniambia tofauti ya utajiri hiyo aliyoniambia mzee huyo. Utajiri wa kuku ulikuwa ni kwamba kuku anatupiwa mahindi chini, anaanza kula, kama akila mahindi matano, basi utajiri wako utakuwa ni wa miaka mitano, kama akila mahindi ishirini, basi utajiri wako utakuwa wa miaka ishirini, baada ya hapo unafilisika na kufa.
“Hapana huo siupendi!” nilimwambia mzee Mudi.
“Kwa nini? Huo ndiyo mzuri!”
“Mimi nautaka huo mwingine.”
“Unaujua upo vipi?”
“Sijui, ila nautaka huohuo!” nilimwambia.
Utajiri niliosema kwamba niliutaka ulikuwa ni wa masharti makubwa. Niliambiwa hilo lakini nikasema kwamba nautaka huohuo na kama ni masharti nitayafanya yote lakini si kukubali ule wa mwanzo wa kuwa tajiri kwa kipindi fulani kisha kufa.
“Huu una masharti makubwa mawili,” aliniambia mganga.
“Yapi?”
“Moja, unatakiwa kuwaua wazazi wako wote wawili,” aliniambia huku akikishika kitunguli kidogo kilichokuwa pembeni yake.
“Kuwaua wazazi wangu?”
“Ndiyo!”
“Na sharti jingine?” niliuliza huku nikionekana kuchanganyikiwa.”
“Kufanya mapenzi na maiti ishirini..” aliniambia.
****
Kwanza nikashtuka, sikuonekana kuamini kile alichoniambia, nikamuuliza mara mbilimbi alisemaje, yeye akaniambia vilevile kwamba nilitakiwa kufanya mapenzi na maiti ishirini kama nilitaka kuwa tajiri, hivyo nilitakiwa kuchagua.
“Umechagua nini?”
“Kati ya nini na nini?”
“Kuwaua wazazi wako au kufanya mapenzi na maiti ishirini?” alinijibu kwa kuniuliza swali.
“Bora nifanye mapenzi na maiti ishirini…” nilimwambia japokuwa niliogopa mno.
Alichokifanya mzee yule ni kuchukua unga mwingine na kunipaka usoni kisha kuniambia nitulie kwa muda. Nilitulia hapohapo, sijui nini kilitokea, ghafla, nikajikuta nikitokea katika hospitali moja kubwa hapa jijini Dar es Salaam, nilishangaa, nilijiuliza nilifikikaje mahali hapo lakini sikuwa na jibu lolote lile.
Kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakiendelea na shughuli zao, wagonjwa waliokuwa wakiingia na kutoka. Ghafla, nikasikia sauti ya yule mzee ikiniambia kwamba nilitakiwa kwenda mochwari, sikujua ilikuwa wapi lakini nikajikuta nikijiongoza mpaka kufika katika mlango ambao uliandikwa MOCHWARI kwa nje.
“Subiri hapo mpaka usiku,” niliisikia sauti hiyo.
Nilifanya kama nilivyoambiwa, nikasubiri mahali hapo. Ilikuwa jioni kama saa kumi na moja hivi. Hakukuwa na mtu aliyeniona, wengi walinipita bila kunisalimia. Ilipofika saa moja usiku, nikasikia sauti ile ikiniambia niende ndani ya mochwari ile, maelekezo mengine angeniambia, nikafanya hivyo na kuanza kuingia humo ambapo kulikuwa na masanduku mengi yaliyokuwa na maiti nyingi. Nikaambiwa nisubiri. Nakuja kutahamaki, eti ilikuwa saa sita usiku. Nikabaki nikitetemeka tu.
*****
Ulikuwa usiku mkubwa, nakiri kwamba hakukuwa na sehemu iliyokuwa inatisha kama ilivyokuwa mochwari. Ndani ya mochwari ile, kulikuwa na majeneza ya maiti ambazo zililetwa humo ndani na nyingine tayari kwa kuchukuliwa lakini pia kulikuwa na masanduku mengi ambayo ndani yake kulikuwa na maiti, baridi lililokuwa humo ndani, lilikuwa kubwa mno.
Humo kulikuwa na walinzi wawili, walikuwa wakilinda, nilijiuliza walipata wapi ujasiri wa kuwa ndani ya chumba kile, tena usiku mzima huku wakionekana kutokuwa na hofu hata kidogo.
Mimi, sikuwa nikionekana, yaani hata niliposogea karibu yao, hawakuwa wakiniona zaidi ya kufanya vitu vyangu. Humo, ndipo nilipojifunza kwamba kulikuwa na mambo mengi yaliyokuwa yakitokea.
Niliwaona watu wakija usiku huohuo, walikuwa wakizungumza na walinzi hao na kuwaambia shida zao, wengine walifika kwa kuwa walihitaji baadhi ya viungo kutoka kwa maiti ili waende kufanya mambo yao ya kishirikina.
Nilimuona mlinzi mmoja akitoka na kwenda kwenye sanduku moja, akalivuta kisha kuanza kuitoa maiti iliyokuwa humo ndani. Mwili wangu ulisisimka mno, sikuamini nilichokuwa nikikiona, hofu ilinijaa moyoni mwangu.
Mlinzi yule akaivua nguo maiti ile, sikujua alichokuwa akikihitaji, yale mambo ambayo nilikuwa nikiyasoma kwenye vitabu vya kusisimua, siku hiyo nilikuwa nikiyaona kwa macho yangu.
Akachukua kisu ambacho alikihifadhi sehemu maalumu, nyuma ya mlango na kisha kuanza kukata kifundo cha mguu cha maiti ile kwani ndicho kilichokuwa kikihitajika kwa hali na mali.
Ninayoyazungumza hapa, niliyashuhudia kwa macho yangu. Mapigo yangu ya moyo yalikuwa juu mno, japokuwa kile kilikuwa kikifanywa kwa maiti lakini niliogopa na kuionea huruma, niliona kama ilikuwa ikionewa.
Alipomaliza, mlinzi akakichukua kifundo cha mguu ule na kisha kumpa mwanaume aliyekuwa amekifuata na kuondoka nacho. Walinzi waligongesheana mikono, kila mmoja alionekana kuwa na furaha.
Wala haukupita muda mrefu, nikaona mlinzi mmoja akitoka nje. Sikutaka kubaki ndani, wakati namsubiria yule mganga, nilitaka kujua ni kitu gani kingine kilichokuwa kikitokea.
Nilimfuata mlinzi, alikwenda moja kwa moja kwenye gari moja ya kifahari, Range SUV nyeusi na kuongea na mtu aliyekuwa humo ndani. Nilisogea kwani nilitaka kuyasikiliza mazungumzo yao.
“Nahitaji maji ya maiti,” alisema mzee aliyekuwa humo ndani ya gari.
“Laki mbili! Hela ipo?” aliuliza mlinzi yule.
“Ipo! Naomba ukaniwekee humu!”
Yule mzee sikuweza kumfahamu kwa kipindi kile lakini sauti yake, hapo baadaye nilimfahamu kwani nilikutana naye mara kwa mara. Baada ya kuzungumza hivyo, akatoa kidumu na kumpa mlinzi yule ambaye akakichukua na kuondoka nacho.
Sikutaka kubaki hapo nje, nikamfuata mlinzi mule mochwari alipokwenda. Nilipoingia, nikakuta akimwambia mwenzake kwamba kulikuwa na dili jingine, kuna mtu alifuata maji ya maiti.
“Hakuna tatizo! Twende kule kwenye maiti za wiki iliyopita!” alisema mlinzi aliyeletewa taarifa.
Wakatoka na kuelekea kwenye moja ya masanduku yaliyokuwa mwisho kabisa ambayo yalikuwa na maiti zilizokuwa na muda mrefu humo mochwari. Wakafungua sanduku moja, wakatoa maiti ya msichana na kuiweka juu ya meza moja kisha kuanza kuiosha huku wakikinga maji na kuyaweka katika sufuria kubwa kabla ya kuyaweka katika kidumu kile.
“Mungu! Kumbe haya ndiyo yanayotokea!” nilijikuta nikisema.
Waliendelea na zoezi lao mpaka walipomaliza na kujaza kile kidumu, yule mlinzi akaelekea nje na kumpa yule mzee, gari likawashwa na kuondoka mahali hapo.
Wakati ikiwa imefika saa nane usiku, hapo ndipo mganga yule akatokea hapo ndani na kunifuata. Kabla ya kuzungumza lolote, akaniangalia machoni, aliiona hofu niliyokuwa nayo.
“Upo sawa?” aliniuliza.
USIKOSE SEHEMU IJAYO
Share CnZ Media App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi Ili Tuwe Wasomaji Wengi
