SHEREHE KUZIMU (25)

Zephiline F Ezekiel
SHEREHE KUZIMU (25)
Jina: SHEREHE KUZIMU Mtunzi: Frank Silaa SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO ILIPOISHIA... Katika historia ya mganga huyu inasemekana aliwahi kuhamishia mlima Kilimanjaro mkoani kwake kwa muda wa masaa matatu. Ahmedi Juma , ndiyo jina la mganga huyu, japokuwa watu wengi wanamfahamu kwa jina la Kiboko , kutokana na sifa yake ya kutokushindwa na jambo. KAMA SIMULIZI HII UNASOMEA NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI KUPATA VIPANDE VYOTE KWA WAKATI 👉 GUSA HAPA KU-INSTALL 👈 ENDELEA NAYO... Mara baada ya malipo katika nyumba ya wageni ya Kibo guest house iliyopo mjini Moshi , Benedict na mwenzie walijitutumua kubeba mabegi yao hadi kwenye chumba namba 8. Pamoja na kwamba walionekana kuwa na uchovu mwingi wa safari lakini kila mmoja alionyesha hamu ya kumtamani mwenzie kimapenzi. Safari yao ilikuwa ni ya furaha sana. Ucheshi wa Benedict ulisababisha tabasamu na vicheko mwanana visififie katika uso mzuri wa Adela . Baada ya kutua mabegi yao chumbani mule, Adela alishindwa kuendela kukumbatia hisia zake kwahiyo alim…