SHEREHE KUZIMU (30)
Zephiline F Ezekiel
---

Mtunzi: Frank Silaa
SEHEMU YA THELATHINI
ILIPOISHIA...
ILIPOISHIA...
“MGONJWA ALIYECHOMWA KISU AENDELEA KUDUNDA.” Gazeti la Kiu.
Licha ya magazeti mbalimbali kupambwa na habari hiyo lakini pia redio, televisheni, na mitandao ya kijamii iliripoti maendeleo ya Benedict hospitali.
KAMA SIMULIZI HII UNASOMEA NJE YA APP YA CnZ Media IPAKUE ILI KUPATA VIPANDE VYOTE KWA WAKATI
👉GUSA HAPA KU-INSTALL👈
ENDELEA NAYO...
Waungwana walilaani vikali tukio la kutaka kuuwawa kwa mgonjwa huyo. Hata hivyo mashirika binafsi na taasisi mbalimbali zilitoa rai kwa serikali kuhimarisha ulinzi dhidi ya kijana huyo.
Majuma kadhaa mbeleni, daktari mkuu kitengo cha mifupa, alimtembelea Benedict wodini na kukuta hali yake inazidi kuwa njema. Alipendekeza kwa vile fahamu zimemjia basi utaratibu wa kuwasiliana na ndugu zake ufanyike muda wowote kwanzia saa ile. Daktari wa zamu alipewa jukumu hilo la kusimamia zoezi la Benedict kutoa utaratibu wa kuwasiliana na nyumbani kwao.
“Daktari Fransisco, ambaye ndiye aliyepewa jukumu hilo aliahidi kufanya utaratibu haraka iwezekanavyo. Baada ya hapo dokta Fransisco alibaki na Benedict wodini wakati mganga mkuu kitengo cha mifupa kutoka.
“Unakumbukumbu za namba zozote za nyumbani kwenu?” Tabibu Fransisco alihoji.
“Ndiyo.” Benedict alijibu kwa ufupi.
“That’s good, ngoja nikaweke vocha then nakuja sasahivi.” Daktari alisikika akizungumza, ambapo baada ya muda mfupi alibamiza mlango baada ya kutoka.
Alikwenda moja kwa moja hadi kwenye maduka ambayo yalikuwa jirani na hospitali. Kisha akanunua vocha na kuingiza kwenye simu yake. Baada ya kuhakikisha vocha aliyoinunua imeingia kwenye simu, alianza safari ya kuelekea wodini. Dakika sita na ushee hivi, aliwasili wodini kwa mgonjwa ambapo alikuta hali yake imebadilika ghafla. Mgonjwa alionekana yupo katika hatua za mwisho za kukata roho kwani mwili wake ulikuwa umekakaamaa kupita kiasi.
Dokta Fransisco alishtuka sana lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kuanza jitihada za kunusuru uhai wa mgonjwa. Alianza kwa kumfanyia vipimo vya awali ili kubaini tatizo. Hata hivyo jitihada zake za haraka, hazikuzaa matunda kwani mapigo ya moyo ya mgonjwa yalisimama. Baada ya mgonjwa kukata roho uchunguzi ulifanyika kubaini kilichomuuwa mgonjwa. Vipimo vya daktari vilibaini kwamba mgonjwa ameuwawa kwa kuchomwa sindano ya sumu kali iitwayo ‘Phenol.’
********
Adela aliwasili kijijini kwao shinyanga majira ya usiku sana. Alipokelewa na Marwa na kisha wakaongozana hadi nyumbani kwa kina Marwa. Kwa kujiibia Marwa alimuingiza Adela ndani ya chumba chake bila wazazi kufahamu chochote. Usiku wa siku hiyo ulikuwa ni wa furaha sana kwao, kwavile kila mmoja alikuwa anamtamani mwenzie kimapenzi. Mara baada ya Adela kula chipsi kuku alizokwenda kununuliwa gengeni walijitupa kitandani na kuanza kufanya yao.
Baada ya muda fulani Marwa alifanikiwa kuutoa usichana wa Adela. Ilikuwa ni furaha kubwa sana kwake kwasababu hakutarajia kumkuta Adela bado ni msichana ambaye hakuwai kuguswa na mwanaume. Walipomaliza haja zao, usiku wa saa saba, Marwa alimsindikiza Adela hadi kwao ambapo ni jirani sana. Alipofika alimdanganya mama yake kwamba gari alilokuwa amepanda liliaribika zaidi ya mara tatu walipokuwa safarini.
Mama Adela hakufurahia kabisa kitendo cha mwanae kutoroka hospitali kwahiyo alimgombeza kwa kiasi chake.
“Mwanangu nimepata taarifa kuwa umetoroka hospitali, nimesikitika sana kwasababu sikutegemea kwa akili yako unaweza kufanya upuuzi kama huo.”
“Nisamehe mama, nilichoshwa na mazingira ya pale hospitali ndiyo maana.”
“Yaani yule daktari aliponieleza nilipandwa na presha.”
“Naomba unisamehe mamangu.”
“Nimekusamehe, ila usirudie tena.”
“Sawa.”
Maongezi ya Adela na mama yake hayakuwa marefu kwavile ilikuwa ni usiku sana. Kwahiyo Adela alipomaliza kuoga alijitupa kitandani huku akizidi kumuwaza Marwa wake.
Siku iliyofuata haikuwa njema hata kidogo, kwani ilitawaliwa na majonzi pamoja na simanzi kwasababu Marwa alifia usingizini. Adela aliumia sana kutokana na kwamba ndiyo kwanza penzi lake lilikuwa limeanza kuchanua upendo. Alizimia zaidi ya mara kumi pindi alipopata taharifa ya kifo cha mwanaume huyo.
********
Nelson aliwekwa maabusu kutokana na kesi iliyokuwa inamkabili. Alipandishwa mara mbili kizimbani ambapo mara zote alikana kuhusika katika shambulio la kutaka kuuwa. Kifo cha Benedict kilisababisha baba yake azidi kubanwa na jeshi la polisi kwa lengo la kubaini mtandao huo wa wauwaji.
Matukio yote yaliyokuwa yanatoka hospitalini pale yalisababishwa na Vivian katika njia za kichawi. Majini kutoka kuzimu ndiyo walikuwa wanaharibu utaratibu mzima wodini pale. Adhma yao kuu ni kuhakikisha kwamba Benedict anapoteza maisha. Nelson alitegewa mtego ule na majini kusudi asiweze kuwa karibu na mwanae.
Kuzimu ilifurahia juhudi na weledi mkubwa uliokuwa ukionyeshwa na majini waliokuwa wametumwa roho ya Benedict.
Wakati roho ya Benedict ikiendelea kuandamwa na majini, kibuyu cha Vivian kilihitaji damu kwa mara nyingine. Hakuna aliyekuwa akijua kipindi hiki ni zamu ya nani isipokuwa yeye mwenyewe. Haikuchukua muda kupatikana kwa damu ya kibuyu cha kichawi, kwani Frank na Christopha ambao ni watoto wa marehemu mjomba waliweza kupoteza maisha wote katika mazingira ya ajabu. Inasemekana vijana hawa walikuwa wote kwa pamoja katika daladala wakitokea mjini, ghafla walianza kuumwa na kichwa hadi alipopoteza maisha wakiwa ndani ya gari.
Wasamaria wema walichukua simu ya Frank kisha wakatafuta namba moja ya simu ya kuweza kuijulisha taarifa ya muhusika. Kwa bahati nzuri walikutana na namba ya Vivian na kumjulisha yaliyojiri huko barabarani. Haikuumiza sana kichwa cha Vivian kwavile yeye ndiye muhusika wa mauwaji hayo katika njia za giza.
Wiki moja baadaye vijana hao walizikwa wakati Nelson akiwa maabusu gereza la keko dar es saam. Ilikuwa ni simanzi kubwa pale mtaani. Kilichowaumiza watu zaidi ni vijana hao kufa wote kwa pamoja tena kwa ugonjwa mmoja. Sio wanawake wala wanaume kila mmoja alionekana kudondokwa na chozi kutokana na vifo hivyo. Umati mkubwa ulijitokeza kuwasindikiza vijana hao katika safari yao ya mwisho.
Habari za Nelson kuwepo gerezani kwa tuhuma za shambulio la mauwaji lilikuwa likizungumzwa chini kwa chini pale msibani. Hakuna aliyeweza kuamini kwamba Nelson anaweza kuhusika katika tukio kama hilo. Fikra zao ziliwatuma kufikiri kwamba kesi hiyo ni ya kusingiziwa na siyo kweli kabisa. Watumishi wa Mungu waliokuwa wanaendesha shughuli za mazishi waliwasihi watu kuongeza nguvu ya maombi kwaajili ya Nelson na mwanae ambao wapo katika wakati mgumu kiroho.
Nelson kabla ya kuingizwa maabusu aliwasiliana na mke wake na kumjulisha kilichokuwa kimemkuta hospitalini pale. Kwahiyo majirani walipohoji alipo Nelson ndipo mke wake alitoa ufafanuzi huo ambao uliwaumiza kwa kiasi kikubwa.
*******
Marwa alizikwa kijijini kwao. Ndoto zake zilikatishwa na tamaa zilizomsukuma kuingia mapenzini na mwanamke ambaye ukoo wake unateswa na mizimu. Hakuna aliyeweza kufahamu kilichokuwa sababu ya kifo chake. Hata mwili wake ulipopelekwa hospitali kupimwa, vipimo ya daktari vilishindwa kubaini chanzo kilichopelekea kufikwa na umauti.
********
Utaratibu ulifanyika ili Benedict aweze kupelekwa mochwari. Uchunguzi wa kifo chake, ulikamilika mara moja. Hapakuwa na haja ya mwili wa marehemu kuendelea kuwepo wodini, kwahiyo ulichukuliwa na kupelekwa hadi kwenye chumba cha kuhifadhia maiti. Ilibaki kazi kwa waudumu wa mochwari kufanya taratibu zao za awali ili waweze kuuhifadhi mwili.
Wafanyakazi wa mochwari walianza utaratibu wa kuuandaa mwili wa marehemu kama ilivyo kawaida yao. Katika maandalizi hayo mfanyakazi mmoja ajulikanaye kwa jina la Mandipo aligundua moyo wa marahemu unadunda kwa mbali sana. Alishtuka sana baada ya kugundua hilo kwasababu mwili wa Benedict ulikuwa umepoa mithili ya mtu aliyekufa muda mrefu uliyopita.
Aliwashirikisha wafanyakazi wenzake pale mochwari ambao nao walithibitisha kwamba Benedict bado ni mzima. Mandipo alipeleka taarifa hiyo kwa msimamizi mkuu wa shughuli za uhifadhi wa maiti hospitalini hapo bwana Menzimo.
Ilikuwa ni habari ya kushangaza sana, kwavile vipimo vya daktari vilithibitisha kuwa Benedict aliaga dunia. Watu wengi sana walikusanyika nje ya mochwari hiyo ili waweze kushuhudia mtu ambaye anasadikiwa kufufuka akiwa mochwari. Palitokea mafuriko ya waandishi wa habari ambao walikwenda kuandika habari ya maiti kufufukia mochwari.
Pia walifanya mahojiano na daktari aliyethibitisha kifo cha Benedict.
Mwandishi: “Daktari unaweza kutoa ufafanuzi juu ya tukio hili ambalo limeonekana kushangaza dunia?”
Daktari: “Naam, asante ndugu mwandishi. Kwa jina naitwa dokta Fransisco ambaye ndiye niliyethibitisha kifo cha Benedict, ambacho kilisababishwa na kuchomwa sindano ya sumu na watu wasiyojulikana. Kusema kweli hata mimi nimeshangaa sana kwasababu sijawahi kukutana na tukio kama hili tangu nianze kazi miaka thelasini iliyopita. Nilishirikiana na madaktari wenzangu katika kuokoa maisha yake lakini kwa bahati mbaya alifariki wakati tulipokuwa tukijaribu kuokoa maisha yake. Vipimo vilithibitisha ni marehemu na ndipo utaratibu wa kuuhifadhi mwili ulipoanza. Sasa nimeshikwa na butwaa niliposikia na kuthibitisha kuwa ni mzima.”
Mwandishi: “Mmefanikiwa kubaini chanzo cha mgonjwa huyu kuandamwa na matukio ya kutaka kuuwawa hapa hospitali? Kwasababu mara ya kwanza alinusurikaa kufa baada ya kuchomwa na kisu tumboni, mara ya pili ndiyo hii amenusurika kufa kwa kuchomwa sindano ya sumu kali.”
Daktari: “Hapana hatujafanikiwa kugundua chochote, lakini pia ninaomba jambo hili tuliachie vyombo husika waweze kulishughulikia kwa vile ndiyo wenye mamlaka.”
Mwandishi: “Ahsante sana kwa taarifa.”
Daktari: “Hakuna shaka.”
Waandishi wa habari walimaliza mahojiano na mganga huyo na kisha wakaondoka.
Benedict alirudishwa wodini kuendelea na matibabu. Kipindi hiki usalama wake wodini ulihimarishwa kutokana na majaribio mawili ya kutaka kuuwawa.
********
Vivian anakasirika sana baada ya kuona kifo cha Benedict kinachelewa. Kuzimu kunafanyika vikao vingi kwaajili ya kutafakari namna ya kuweza kuongeza nguvu ili zoezi maahususi liweze kutimia. Serikali ya kuzimu inachachamaa katika mipango ya kuhakikisha Benedict anatolewa kafara na mwisho wa siku harusi ifungwe.
Mama Vivian ndiye aliyekabidhiwa jukumu la kuhakikisha kwamba mjukuu wake anafanyika kafara kuzimu. Jukumu hilo lilimuangukia mama huyo, baada ya kuomba aweze kumsaidia binti yake kutekeleza kafara hiyo kwavile imeonekana kumsumbua kichwa kwa muda mrefu.
USIKOSE SEHEMU IJAYO
Ili Kunipa Nguvu ya Kuendelea Kuwaletea Simulizi Share App kwa Wapenzi wa Kusoma Simulizi
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni