SORRY MADAM (54)

0
SEHEMU YA HAMSINI NA NNE
ILIPOISHIA...
Ndege ikagonga sehemu na kusababisha mtikisiko mkubwa na kupinduka kichwa chini miguu juu jambo lililosababisha mikono yangu kushindwa kuhimili kuishikilia siti niliyo kuwa nimeishika na nikajikuta nikiachia na kuanza kuvutwa nyuma na upepo mkali uliochanganyika na moto ambao ni mkali sana

NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU

SASA ENDELEA...
Gafla nikastukia nikidakwa mkono na kuangalia vizuri nikamkuta ni Sheila ambaye amenishika mkono huku na yeye akiwa amekaa kwenye siti yake na kuzuiwa na mkanda alio jifunga na huku mkono mmoja akiwa ameushika kwenye siti iliyopo pembeni.Nikamtazama kwa macho ya huzuni na kumuona akishindwa kuhimili uzito wangu kwani tegemezi lote la mwili wangu ni mkono wake na sikuwa na sehemu yingine ya kushikilia
“Sheila niachie nife”
“Eddy unasemaje?”
“Niachie.”

Nilizungumza huku nikimtazama Sheila machoni ambaye anatumia nguvu nyingi kunizuia nisichomolewe nje ya ndege na mbaya zaidi pembeni yangu hakuna kitu ambacho ninaweza kusema kuwa nitakishika ili kinizuie nisichomolewe nje kwani siti zote za nyuma zimechomoka na watu wake.Ndege ikaendelea kugonga majengo yaliyopo ya hapa uwanja wa ndege hadi ikasimama ndipo Sheila akaniachia mkono na mimi nikaanguka chini na kujigonga mkono wangu wa kushoto kwenye upande wa pili wa ndege.Sheila akaaanza kupata shida ya kujifungua mkanda wa siti yake na mbaya zaidi kwa jinsi ndege ilivyo anguka imemfanya awe kichwa chini miguu juu

Nikaanza kusikia ving’ora vya gari za zimamoto zikija katika eneo la tukio na kuazna kuuzima moto unaoendelea kuiteketeza ndege,moshi mwingi ulio tawala ndani ya ndege ukanifanya nianza kukohoa na taratibu nikaanza kujivuta nje ya ndege huku mkono wangu ukitawaliwa na maumivu makali.Niavutwa nje na waokoaji na gafla mlipuko mkubwa wa ndege ukatokea na kuturusha mbali mimi pamoja na waokoaji na nikajzidi kuuegemea mkono wangu ambao ninahisi unamaumivu
“No Sheila?”

Nikajinyanyua na kuanza kutembea huku nikiyumba na kujitahidi kurudi kwenye ndege ila baadhi ya waaokoaji na askari wakanizuia,Machozi mengi yakaanza kunitawala kwani moja kwa moja ninatambua kuwa Sheila ni miongo mwa walio lipuka na ndege.Wazo la kwamba ninatafutwa na polisi na ninahitajika kurudishwa Afrika kusini kujibu mastaka yangu likanijia kichwani.Nikawatazama askari na waokoaji nikaona kila mmoja yupo na mihangaiko ya kuwaokoa majeruhi wengine na taratibu nikaanza kutembea kwa kujikaza pasipo kutazama pembeni wala nyuma zaidi ya kwenda mbele huku mkono wangu wa kushoto nikiwa nimeushikilia vizuri.Machela moja ikapitishwa kwa haraka pembeni yangu na waokoaji huku wakikimbia kwa kwasi na mtu waliye mmbeba juu ya machela nikamtambua ni Sheila japo mwili wake umeharibika sana kwa moto kitu kilicho nifanya nimtambue kwa haraka ni nguo zake alizo zivaa,wakamuingiza ndani ya gari ya wagonjwa na wakaondoka

Nikabaki nikiwa na mshangao sikujua ni nini nifanye,Nikiwa ninaendelea kushangaa nikwaona askari wawili wakinifwata sehemu niliyo simama.Nikaanza kutembea kwa mwendo wa haraka huku nikigeuza geuza shingo yangu nyuma na kuwatazama askari na kuwoana nao wakiongeza mwendo wa kunifwata.Moto mkali ulio andamwa na upepe mkali ukaanza kushika majengo mengine ya uwanja wa ndege na kuwafanya watu waliopo kweye eneo hili kuaanza kukimbia kimbia ovyo kuyaokoa maisha yao.Nikajichomka katikati ya watu wanaokimbia kuokoa roho zao na nikafanikiwa kutoka nje ya uwanja wa ndege.Nikaendelea kukimbia hadi nikafanikiwa kutoka nje ya uwanja wa ndege na nilipo tizama nyuma yangu sikuweza kuwaona askari wakinifwata.Mauivu ya mkono yakazidi kunitawala na sikuwa na jinsi zaidi ya kujikaza kiume na kuendelea kutembea nisipo pajua na kunyoosha barabara ya lami ambayo nikatembea kwa umbali mkubwa na kukuta kibao kilicho andikwa Athi River na kutokana na uchovu mwingi nikatafuta sehemu nikajipuumzisha pembezoni mwa barabara,Nikapata sehemu nikajipumzisha hadi kulipo pambazuka mida ya saa kumi na moja alfajiri nikasimama barabarani na kuanza kusimamisha magari yanayo pita.Nikafanikiwa kuahatisha gari moja la watalii aina ya Landrover ikasimama

“Where are you going young boy?”(Unakwenda wapi kijana?)
“Am going Tanzania”(Ninakwenda Tanzania)
“Are you a Tanzanian?”(Wewe ni mtanzania?)
“Yes”(Ndio)
Mama wa kizungu alinihoji maswali hayo kisha akazungumza na mume wake kwa lugha ya kireno,ambaye ni dereva wa gari lao na akanikubalia kupanda ndani ya gari lao na safari ikaanza.Ndani ya gari ukimya ukatawala huku nikiyasikilizia maumivu ya mkono wangu ambao unavuta kwa kiasi kikubwa na sikuhitaji waweze kujua juu ya kuvunjikwa kwangu mkono kwani wangenihoji maswali mengi yasiyo na msingi wowote kwangu

“What’s your name?”(Jina lako ni nani?)
“My name is Eddy”(Jina langu ni Eddy)
“You have a good name as our soon”(Unajina zuri kama mtoto wetu wa kiume)
“Thanks”(Asante)
“My name is Madam Loren we are going Moshi”(Jina langu ni Madam Loren,tunakwenda Moshi)
Sikutaka kujua wanakwenda Moshi kufanya nini kwani mkono wangu unaniuma kupita maelezo,Hadi tunafika Arusha Tanzani mida ya saa sita mchana hatukuweza kusimamishwa na askari njiani na tuliingilia kwa njia ya Monduli hadi tunafika Arusha mjini nikawaomba wanishushe na nikawashukuru kwa masaada wao kisha wakaendelea na safari yao kwani walinieleza wanaelekea Moshi.Nikaanza kupandisha barabara ya Old Moshi na moja kwa moja nikaenda nyumbani kwa Madam Mery.Nikafika nyumbani kwa madam Mery na kukuta mabadiliko kidogo kwani rangi ya ukuta na gati lake vilikuwa vimebadilishwa

Niikaanza kugonga kwa kutumia mkono wa kulia na nikasikia sauti ya kike ikisema inakuja kufungua,Nikasimama kwa dakika kadhaa na gati likafunguliwa na akasimama msichana akiwa amemshika mtoto mdogo mkononi mwake akiwa anasura inayo endana na mimi
“Nikusaidie nini kaka?”
“Ehee madam Mery nimemkuta?”
“Hayupo amekwenda kazini”
“Wapi?”
“Shuleni hapo juu...Karibu ndani”

Nikatazama pande zote za nje kisha nikaingia ndani huku nikimtazama mtoto aliye bebwa na mtoto msichana ambaye ninahisi ni msichana wa kazi na kusema kweli kila kitu ambacho mimi ninacho kwenye sura yangu kipo kwa huyu mtoto mdogo.Binti akatangulia kuingia sebleni na akanikaribisha kwenye masofa mapya niliyo yakuta ndani ya sable hii kidogo nikashusha pumzi,Gafla macho yangu yakagongana na mume wa Madam Mery ambaye siku zote ni adui yangu na mara ya mwisho nakumuka nilimpiga kichwa na akanitolea bastola na jamaa sura yake ikabadilika gafla akanitazama kwa umakini kisha macho yake akayahamishia kwa mtoto aliye bebwa na mfanyakazi wake

“Waooo ni muda sasa sijakuona naona umekuja kuchukua kiumbe chako si ndio?”
Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio huku nikimtazama mume wa Madam Mery na kajasho kembamba kakaanza kunimwagika
“Nipe huyo mtoto”
Mfanyakazi wa ndani akamkabidhi mume wa madam Mery mtoto ambaye tayari nimegundua kuwa ni mwanangu.
“Nenda ndani?”

Mfanyakazi wa ndani akaondoka na kutuacha na mume wa Madam,Japo ninamaumivu ya mkono nikajaribu kunyanyuka ila niweze kujiokoa,mume wa madam Mery akamshika mwanangu kichwa chini miguu juu na kumfanya mtoto kuanza kulia kwa sauti
“Kaa hapo hapo la sivyo huyu paka wako ninamwangamiza mbele ya macho yako”
Nikamangalia jinsi mtoto wangu anavyolia na kujikuta roho ya huruma ikinitawala na nikakaa chini nikimtazama mume wa Madam Mery,Akatoa simu na kuipiga
“Njoo nyum bani”

Jamaa akakata simu na kurudisha mfukoni kisha akaniangalia machoni na kutabasamu.Akamshika mtoto vizuri na kuanza kumbembeleza huku akizunguka huku na huku ndani ya sable.Mlango ukafunguliwa na akaingia Madam Mery akiwaavalia vizuri na ule uzuri wake umezidi kuongezeka na baada ya kunioana akaonekana akistushwa.Akapitiliza hadi kwa mume wake na kumpiga busu la shavu kama ishara ya salamu
“Nenda kakae kule”
“Ehee”
“Nenda kakae kwa mshenzi mwenzako”

Jamaa alizungumza kwa hasira hukua akimsukuma Madam Mery kuja kukaa kwenye sofa ambalo nimekaa
“Jamani Derick mume wangu si tulisha lizungumza na limeisha mbona unataka kuanzisha ugomvi?”
“Nyamaza Malaya mkubwa wewe,hivi unajua uchungu nilio kuwa nao wewe,Au unadhani kukaa siku zote kulea kiumbe kisicho changu hivi unajua ni maumivu gani ambayo ninayo moyoni mwangu”
Derick alizungumza huku machozi yakimwagika na mtoto wetu akiwa amemshika mikononi mwake.Madam Mery machozi yaakanza kuutawala uso wake
“Derick nakuomba unisamehe kwa mara nyingine sito rudia tena kukusaloti mume wangu”
“Ahaaa chagua mawili kati yangu au huyu panya wako?”

Macho yakanitoka nilipomuona Derick akifanya kitendo cha mara ya kwanza cha kumshika mwanangu kichwa chini miguu juu huku akiwa amemuinua kwa mkono mmoja
“Derick nyote ni muhimu sana kwangu ninakuomba mume wangu unisamehe nina kupenda sana mume wangu”
“Wewe manamke ni muuaji,kumbuka mimi ndio nilikufanya kupata elimu yako hadi akawa mwalimu ukaona haitoshi ukanisaliti mara ya kwanza nikakusamehe......Baba yako alifariki mikononi mwangu tukimuwahisha nchini India kwa matibabu na zote zilikuwa gharama zangu senti tano kwenu mulikuwa hamuna nimevunja vibanda vyenu na kuwajengea nyumba nzuri ili nanyi muonekane watu kati ya watu ila bado umeona hatoshi kabla ya ndoa yetu umebeba mimba ambayo si yangu ni ya uyo paka hapo.”
“Ni mara mia ungetembea na mtuu aliye kuzidi umri ila wewe ukachukua Serengeti Boy unadhani atakusaidia nini huyo mwehu wako”

Derick aliendelea kuzungumza kwa hasira huku machozi yakiendelea kumwagika na mwanangu akiendelea kulia kwa maumivu anayo yapata.Madam Mery kapiga magoti na kuanza kuburuzika taratibu akimfwata mumewe sehemu aliyo simama
“Rudi huko huko la sivyo ninamuua huyu paka wenu.”
Madam Mery akaanza kurudi nyuma taratibu huku akiendelea kumwagikwa na machozi mengi.Kelele za mwanangu kulia kwa maumivu zikanifanya nishindwe kuvumilia huku hasira ikinipanda nikanyanyuka huku nikiwa nimeushika mkono nilio vunjika na kupiga hatua mbili mbela za kuikwepa miguu ya madam mery

“Wewe rudisha miguu yako huko la sivyo ninamuachia huyu mtoto”
Derick aliniambia akionekana kutokuwa na huruma kabisa na maumivu anayo yapata mwanangu,nikashindwa kuizuia miguu yangu na kujikuta nikizidi kupiga hatua kwa hasira kali iliyo nitawala mwili mzima.Derick akampiga mwanagu chini kwa nguvu na kumfanya mtoto wangu kunyamaza kimya na kelele kali ikatoka kwa madama Mery pamoja na mfanyakazi wa ndani ambaye alikuwa amejificha kwenye ukuta akishuhudia kila kinacho endelea.

Sikujali kama mkono wangu mmoja umevunjika kwa hasira nikamrukia Derick ambaye akanikwepa na kunisindikiza kwa teke kali la mgongoni na kujigongwa kwenye uso kwenye ukuta na kuangukia pembeni ya miguu ya mfanyakazi wa ndani ambaya mkononi mwake ameshika kisu na kitunguu.

USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA

KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI

KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger

Chapisha Maoni

0Maoni
Chapisha Maoni (0)