SORRY MADAM (106)
Zephiline F Ezekiel
6 min read
SEHEMU YA MIA MOJA NA SITA
ILIPOISHIA...
"Nakupenda mume wangu"
"Nawapenda wote"
Tukaendelea kukumbatiana kwa furaha.
"Eddy muda"
Shamsa alininong'oneza baada ya kuona tunakumbatiana sana.
NIPE SAPOTI KWA KUTAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWANGU
SASA ENDELEA...
Tukanyanyuka, nikambeba Junio wangu ambaye kwa sasa anatarajia kufikisha umri wa miaka mitano.
"Nitakufanyia sherehe kubwa siku ya kuzaliwa kwako"
Nilimuambua Junio, huku tukielekea kwenye ofisi kukamilisha taratibu zote za kuwachukua Phidaya na mwanangu, na kuwa mikononi mwangu.
"Kweli baba"
"Ndio unataka ifanyikie wapi?"
"Mama kule kwa kina yule mchezaji uliye ninunulia mpira wenye jina lake ni wapi?"
"Brazil"
"Ndio, dady nataka huko huko na mimi nikawe mchezaji mpira"
"Usijali mwanangu, unaweza kucheza mpira?"
"Ndio baba nataka niwe kama Ronaldo"
"Sawa mwanangu utakuwa, tena kabla sijasahau, huyu ni Shamsa, mdogo wangu. Kwa sasa atakuwa dada yake Junio"
"Kweli dady?"
"Yeah"
Nikambusu Junio kwenye paji la uso, jambo lililo zidisha furaha kati yetu sote wanne.
***
Kitendo cha ndege kutua kwenye uwanja wa ndege nchini Brazil, likawa ni jambo la kumshukuru Mungu, sote tukafungua mikanda ya siti zetu tulizo kalia, ikiashiria kwamba safari yetu immefika mwisho. Tukatoa mabegi yetu ya nguo, katika sehemu tulipo yaweka. Tukatoka ndani ya ndege kama abiria wengine. Tukafika eneo la kukaguliwa, tukafanikiwa kupita pasipo kusumbuliwa, juu ya hati zetu za kusafiria. Tulizo zikata nchini Kenya tukisaidiwa na rafiki wa Smith, aliye tukutanisha naye kipindi tunatoka Tanzania mimi na Manka, ambaye hadi sasa sijui yupo wapi.
Kwa msaada wa ramani tuliyo pewa na rafiki wa Smith, juu ya miji yote mikuu nchini Brazili, ikatusaidia kutufikisha kwenye hoteli tuliyo kusudua kufikia tangu tukiwa nchini Kenya. Hoteli hii inapatikana pembezoni mwa fukwe za bahari zijulikanazo kwa jina la 'Copar Carban'.x
Sehemu tuliyo chukua kwa ajili ya makazi ya wiki mbili, ina vyumba vitatu, seble, kubwa pamoja na xjiko kubwa. Kila chumba kimejimudu kwa huduma zote muhimu kama choo na bafu.
"Eddy hapa umelipia bei gani?"
Phidaya alizungumza huku akikagua kagua chumba chetu cha kulala, chenye hadhi ya nyota tano.
"Kwa siku ni dola elfu sabini"
"Mmmmm kwa chumba hiki au?"
"Kwa sehemu yote, hii"
"Kweli una pesa ya kuchezea, hii ni birthday ya mwanao mambo ni haya, Je siku ya ndoa yetu itakuaje"
"Ndio ujiulize sasa, nataka kuihakikishia dunia nzima kwamba ninakupenda mke wangu"
Phidaya akanikimbilia, nilipo simama. Akanirukia na kuning'inia kifuani kwangu. Huku miguu yake akiipitisha kiunoni mwangu na kuikutanisha nyuma.
"Wewe ni mwanaume jasiri, i wish wanaume wote wangekua kama wewe. Ninaamini furaha ingepatikana katika ndoa nyingi."
"Ni wachache wenye moyo kama wangu. Ila kikubwa nimekupata wewe na mwanangu, ninaamini furaha itarudi upya"
Phidaya hakusita kuusogeza mdomo wake, karibu na mdomo wangu. Akanitazama kwa muda, kisha kwa haraka akaanza kuunyonya mdomo wangu. Kutokana na nguvu nilizo nazo, sikuweza kutetereka, kwani fujo anazo zifanya Phidaya mdomoni mwangu, huku nikiwa nimembeba, mtu unaweza kuanguka chini.
Nikamlaza kitandani, huku akiendelea kuninyonya lipsi zangu, mikono yangu nikaishusha kifuani mwake, na kuanza kuzichezea chuchu zake. Kwa raha anazo zipata Phidaya, akajikuta akifumba macho yake. Nikazidi kuutadhimini uzuri wa Phidaya. Hapa ndipo nilipo jilaumu, kwa nini nilikua na magubegube, Sheila na Madam Mery. Kwa kupitia kioo kikubwa, kilichopo kwenye kitanda chetu. Nikamuona Junio akiwa amesimama mlangoni huku akiwa ameshika mpira alio nunuliwa na mama yake. Mdomo wake akiwa ameulegeza akishangaa tunacho kifanya.
Nikamuona naye Shamsa, akisimama nyuma ya Junio, wote walikua na safari ya kuingia chumbani kwetu. Shamsa akamfumba macho Junio, aliyeganda akishangaa kama mshumaa wa pasaka. Shamsa akamyanyua Junio taratibu huku akiwa amemfumba macho. Akanikonyeza, na mimi nikamuonyesha ishara ya dole gumba kwa kutumia mkono wa kulia huku mkono wa kushoto akiendelea kuchezea chuchu za Phidaya. Shamsa akatabasamu, taratibu akaurudishia mlango wetu, huku mkono alio mziba macho Junio akiutumia kuufungia mlango, na kumpa fursa Junio kushangaa vya mwisho mwisho.
"Eddy ni nini hicho?"
Phidaya aliniuliza huku akiyafumbua macho, yake kutazama kila kona ya chumba.
"Kitu gani?"
"Kilicho gusa mlango"
"Hakuna kitu bby"
Phidaya akapotezea, na kuendelea na zoezi la kuunyonya mdomo wangu. Huku kila ma}ra akihakikisha ananigusa kila kona ya mwili wangu. Tukavuana nguo tulizo zuvaa, na kubaki kama tulivyo zaliwa.
***
Sote tukajikuta tukiwa tumechoka, kutokana na mechi tuliyo ipiga, saa ya ukutani inatuonyesha ni saa tisa alasiri. Huku mechi tukiwa tumeianza saa sita mchana, uzuri ni kwamba tulifika nchini Brazil, saa kumi na moja alfajiri na hadi tunafika hotelini, ilikua saa sita kasoro.
Phidaya akashuka kitandani huku, akiyumba yumba
"Eheee leo Eddy umenikomoa, hadi miguu imepoteza nertwork. Kweli wewe ni baba Junio. Sikukosea kuzaa na wewe"
"Hata wewe ulinikamia, hapa nina kiu"
"Kiu ya nini tena? Kama ni yakitandani ahaaa usije ukaniua bure"
"Kiu ya maji"
"Ahaa ndio umalizie matamshi yako"
Phidaya akafungua friji, akatoa chupa ya maji, akanirushia kisha yeye akaingia bafuni. Sikuamini kwamba ipo siku nitakuja kumpata mke wangu. Hapa ndipo nilipo tambua, ukijibidiisha kwa kila jambo zuri, mwisho wake nifuraha.
"Eddy Eddy"
Phidaya aliniita kwa sauti ya juu, iliyo nistua. Nikanyanyuka haraka na kukimbilia bafuni. Nikamkuta akiwa amesimama kwenye bomba linalo mwaga maji kwa mfumo wa kama mvua.
"Una nini mke wangu"
"Hahahaaaa, kumbe unanipenda. Nimekuita tuje kuoga."
Phidaya akanivuta karibu yake, na kunikumbatia.
"Kelele nyingine tutakuja kuuana kwa....."
Phidaya akauwahi mdomo wangu kwa kukiwekea kidole chake, ili nisimalize kuzungumza nililo hitaji kuzungumza"
"Shiiii kila mtu na chake. Nisipo kutania wewe nimtanie nani?"
"Ahaa..."
Fhidaya akaniziba mdomo wangu kwa mdomo wake. Busu alilo nipa likanifanya nikae kimya.
"Hii ni siku yetu, sitaki kelele zako"
"Sawa bosi Phidaya"
"Am not your boss"
"But."
"Am your wife, mother of your child"
"Mama Junio"
"Ndio maana yake"
Tukamaliza kuoga, kisha tukarudi chumbani, Phidaya akanichagulia nguo za kuvaa, zinazo endana na mazingira ya kupungia upepo kwenye fukwe. Tukatoka sebleni. Hatukuwakuta Shamsa na Junio, tukatazama kwenye vyumba vyao ila hatukuwaona.
"Watakuwa kwenye fukwe"
"Sasa watakwendaje pasipo kutuaga"
Phidaya alizungumza huku akiwa amekasirika, akafungua mlango na kutoka, nikabaki nikicheka, kutokana hakulishuhudia tukio la Junio na dada yake. Tukafika kwenye fukwe iliyo jaa watu wengi. Tukawakuta wakicheza mpira na watoto wengine, huku, Shamsa akiwa refa wao.
Junio alivyo tuona akakatisha mchezo na kuja tulipo huku akifwatana na Shamsa.
"Mbona mumeondoka bila kutuaga?"
"Mama tuliwaku..."
Shamsa akawahi kumziba mdomo Junio huku akitabasamu. Mimi nikawa nimeielewa maana ya Shamsa kumziba mdomo Junio.
"Wangetuaga saa ngapi mke wangu wakati mlango tulifunga?"
Phidaya akashusha pumzi, akibaki anatushangaa sote.
"Mumeshinda ninyi leo"
Sote tukabaki tukimcheka Phidaya aliye nuna, kisa tu hajaagwa na wanae.
Usiku ukapita salama salmini, kulipo pambazuka tukaanza mizunguko ya kununua vitu kwa ajili ya siku ya kuzaliwa ya Junio, iliyo bakisha siku mbili hadi ifike. Tukazunguka maduka kadhaa, hadi inafika mchana ikatulazimu kuingia kwenye mgahawa mmoja kupata chakula cha mchana.
"Jamani mumesha wahi kula hivyo vyakula mivyo agiza au ndio ushamba. Musije matumbo yakawauma, bado tuna mizunguko mingi"
Nilizungumza kwa kuwatani. Kila mmoja akajibu anauhakika na chakula alicho kiagizia hakita mletea madhara yoyote. Kila mtu akaletewa chakula chake, Phidaya akawa ndio mtaja majina ya vyakula vilivyo wekwa mezani kutokana na kuvifahamu vizuri.
Tukamaliza kula, nikalipa pesa wanayo tudai. Tukatoka na kuvuka barabara upande wa pili, kwenda kwenye duka moja la viatu.
"Dady nimeusahau mpira wangu"
"Wapi?"
"Pale chini ya meza, tuliyo kaa"
"Chagueni viatu, ngoja nikachukue huo mpira.
Nikawaacha mimi nikarudi kwenye mgahawa tulio toka. Nikafika kwenye meza, tuliyo toka kukaa muda si mrefu. Nikaukuta mpira wa Junio anao upenda kuliko kitu chochote. Kitendo cha kunyanyuka, nikamshuhudi Sheila na John wakiingia ndani ya mgahawa huu, wakitafuta sehemu ya kukaa, pasipo wao kuniona.
Nikabaki nikiwa ninawashangaa, hadi wakapata sehemu ya kukaa pasipo wao kuniona. Nafsi moja ikawa inanishawishi kwenda walipo kaa, ila nafsi moja ikawa inanikatiza kufanya ujinga kama huo kwani sehemu nilipo iacha familia yangu si salama kabisa. Na linaweza kuwa kosa kubwa sana la kupotelewa tena na familia yangu. Nikaendelea kuwatazama jinsi wanavyo onekana ni wenye furaha sana. Sheila hakuonyesha dalili yoyote kuwa na ujauzito kutokana na nguo alizo zivaa zimembana sana mwili wake.
Nikapiga hatua hadi mlangoni, nikasimama huku nikifikiria ni nini nimfanyie John kwa yale yote aliyo nitendea kipindi nikiwa mikononi mwake. Jasho lililo changanyika na hisia kali ya asira taratibu likaanza kunimwagika. Huku likiambatana na mapigo ya moyo yalio nifanya nijihisi vibaya. Kwa haraka hali hii ninakumbuka ilinitokea kipindi nikiwa ofisini mwa balozi wa Marekani nchini Afrika Kusini, pale alipo ingia John na Victoria, wakiwa miongoni mwa wageni walio alikwa na balozi huyo.
Nikajikaza na kutoka nje ya mgahawa. Nikatafuta sehemu nikashika nguzo moja kati ya nguzo kadhaa zilizopo pembezoni mwa barabara. Kizunguzungu kilicho nishika gafla taratibu kikaanza kupungua taratibu, huku jasho likiendelea kunimwagika usoni. Kitu kilicho nichanganya ni matone kazaa ya damu, yaliyo anza kutoka puani.
"Ohhh Mungu wangu, nini hichi?"
Nilijisemea huku nikiyatazama matone ya damu yanayo dondoka chini.
"Sir you need help?"(Muheshimiwa unahitaji msaada)
Askari mmoja anayelinda kwenye mgahawa huu, aliniuliza baada ya kunitazama tangu nikiwa ninatoka nje, mpaka ninashikilia nguzo hii ya taa za barabarani.
"I need water"(Nahitaji maji)
Akaingia ndani ya mgahawa, akatoka akiwa ameshika chupa ya maji. Akaifungua, na kunikabidhi. Nikajimwagia kichwani kidogo, kisha nikanawa usoni kutoa damu zilizo churuzika kutoka puani mwangu.
Nikasubiri kama dakika tano, mwili kidogo ukapata nguvu za kutembe. Nikamshukuru mlinzi, nikavuka barabara na kwenda kwenye duka nilipo waagiza Phidaya awachagulie wanae viatu. Nikawakuta wakiendelea kuchagua chagua viatu wanavyo vipenda.
"Mbona umelowa kichwani?"
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA
KWA KUWA NAKUPA SIMULIZI BURE NAOMBA TAZAMA VIDEO HII NDIO MALIPO YAKO KWA KAZI NINAYOIFANYA YA KUKUSOGEZEA SIMULIZI
KWA USHAURI NA MAONI ANDIKA HAPA:
Inbox: Messanger
Email: ZephilineEzekiel@Gmail.Com
Chapisha Maoni
Chapisha Maoni